Neno La Bwana

Neno La Bwana Catholic spirituality, Readings, Reflections, Traditions and Music, News. Christ Day by Day 🙏

*MASOMO YA MISA TAKATIFU YA JUMAPILI, MEI 10, 2026.**DOMINIKA YA SITA YA PASAKA MWAKA A**RANGI YA KILITURJIA: NYEUPE 🤍**...
09/05/2026

*MASOMO YA MISA TAKATIFU YA JUMAPILI, MEI 10, 2026.*

*DOMINIKA YA SITA YA PASAKA MWAKA A*

*RANGI YA KILITURJIA: NYEUPE 🤍*
*ROZARI 📿: MATENDO YA UTUKUFU*

*MADA YA DOMINIKA:*
```AHADI YA ROHO.```

*ANTIFONA YA KUINGIA: Isaya 48: 20*
_Kwa shangwe hubirini, tangazeni neno hili, mlisambaze hata mipaka ya dunia, mseme. Bwana amewakomboa watu wake, aleluya._

*KOLEKTA*
```Ee Mungu mwenyezi, utufanye tuzisherehekee kwa upendo motomoto siku hizi za furaha tunazoadhimisha kwa heshima ya Bwana mfufuka: utujalie, ili hayo tunayoyakumbuka katika liturujia tuyazingatie daima kwa matendo. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...```

*SOMO LA KWANZA*
*MATENDO YA MITUME 8: 5 - 8, 14 - 17*

Waliwawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

*Somo katika kitabu cha Matendo ya Mitume*

Siku zile: Filipo aliingia katika mji wa Samaria, akawahubiri Kristo. Watu wengi wa huko waliyapokea maneno ya Filipo kwa moyo mmoja wakis**iliza na kuona ishara alizozifanya. Kwa maana pepo wachafu walitoka kwa kelele nyingi katika wengi waliopagawa, pia vilema na viwete wengi waliponywa. Kukawa na furaha kubwa katika mji ule. Mitume waliokaa Yerusalemu walipopata habari ya kuwa Wasamaria wamelipokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohane, nao wakaenda, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu, kwa maana alikuwa hajawashukia bado hata mmoja wao; ila walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu. Hapo mitume wakawawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

*Neno la Bwana....*
*Tumshukuru Mungu.*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
*ZABURI 66: 1 - 3a, 4 - 5, 6 - 7a, 16 na 20 (K. 1)*

*KIITIKIO: _Mshangilieni Mungu kwa furaha, ee nchi yote_*

*AU: _Aleluya_*

Mshangilieni Mungu kwa furaha, ee nchi yote:
liimbieni jina lake tukufu:
mtoleeni sifa na heshima.
Mwambieni Mungu, "Matendo yako ni ya ajabu sana!"
*K*

Dunia nzima ikuabudu na kukuimbia,/iliimbie jina lako!
Njoni, tazameni matendo ya Mungu,
amefanya mambo ya kutisha kati ya wanadamu.
*K*

Aligeuza bahari kuwa nchi kavu:
katika mto walivuka kwa miguu.
Hapo ndipo tunamfurahia,
anatawala kwa enzi yake hata milele.
*K.*

Njoni, s**ieni ninyi nyote mnaomcha Mungu,
nami nitawaeleza makuu aliyonitendea.
Asifiwe Mungu asiyekataa maombi yangu,
wala kuniondolea fadhili zake nilizoomba.
*K.*

*SOMO LA PILI*
*1 PETRO 3: 15 - 18*

Aliuawa katika mwilli, akahuishwa katika roho.

*Somo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Petro*

Wapendwa: Mtukuzeni Kristo Bwana mioyoni mwenu. Daima muwe tayari kumjibu kila mtu anayewauliza habari za matumaini mliyo nayo. Lakini kwa upole na kwa heshima, maana mna dhamiri njema. Hapo wale wanaosengenya mwenendo wenu mwema katika Kristo, waaibike kwa sababu ya mashtaka yao ya uongo. Na k**a Mungu akitaka tuvumilie mateso, ni afadhali kuteswa kwa ajili ya kutenda mema kuliko kwa kutenda mabaya. Hata Kristo alikufa mara moja kwa ajili ya dhambi. Mwadilifu alikufa kwa ajili ya wakosefu, ili awapeleke kwa Mungu. Aliuawa katika mwili, akahuishwa katika roho.

*Neno la Bwana....*
*Tumshukuru Mungu.*

*SHANGILIO LA INJILI*
*Yohane 14: 23*

*K. Aleluya. W. Aleluya.*

Mtu akinipenda, atalishika neno langu, asema Bwana; na Baba yangu atampenda, nasi tutakuja kwake na kufanya makao kwake.

*W. Aleluya*

✝️ *INJILI*📖
*YOHANE 14: 15 - 21*

Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine.

*Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Yohane*

Wakati ule: Yesu aliwaambia wafuasi wake, "Mkinipenda, mtashika amri zangu. Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili awepo kwenu hata milele, ndiye Roho wa ukweli, ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa sababu haumwoni wala haumtambui. Bali ninyi mnamtambua, kwa maana anakaa kwenu, na atakuwa ndani yenu. Sitawaacha ninyi k**a yatima; nitakuja kwenu. Bado kitambo kidogo, ulimwengu haunioni tena: bali ninyi mnaniona, kwa kuwa mimi ni hai, nanyi mtakuwa hai. Siku ile mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu. Aliye na amri zangu na kuzishika, ndiye anipendaye. Naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda, na nitajidhihirisha kwake."

*Injili ya Bwana.....*
*Sifa Kwako Ee Kristo.*

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI**DOMINIKA YA TANO YA PASAKA MWAKA A**MEI 3 2026**RANGI YA LITURUJIA: NYEUPE 🤍**MADA YA DOMIN...
02/05/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI*

*DOMINIKA YA TANO YA PASAKA MWAKA A*

*MEI 3 2026*

*RANGI YA LITURUJIA: NYEUPE 🤍*

*MADA YA DOMINIKA:*
```NJIA NYINGI ZA KUJITOLEA MAISHA.```

*_Mada kuu ya masomo ya leo ni "makao mengi" yaliyomo ndani ya nyumba ya Baba, yaani, njia nyingi ambazo tunaweza kusaidiana. Katika Injili Yesu anasema kuwa njia ya kwenda kwa Baba ni huduma tunazotoa kwa wenzetu. Somo la pili linatumia taswira ya jengo jipya na la kwanza linaelezea jinsi jumuiya ya Yerusalemu ilivyosuluhisha tatizo. Masomo haya mawili yanatusaidia kukuza ufahamu wetu katika kuelewa ujumbe._*

*ANTIFONA YA KUINGIA Taz. Zab 98:1-2*
Mwimbieni Bwana wimbo mpya, kwa maana amefanya mambo ya ajabu; mbele ya macho ya mataifa ameifunua haki yake, Aleluya.

*KOLEKTA*
```Ee Mungu mwenyezi wa milele, ulitimize daima fumbo la Pasaka ndani yetu; na hao uliopenda kuwafanya upya kwa njia ya Ubatizo Mtakatifu, uwajalie wazae matunda mengi kwa msaada wa ulinzi wako, na kuzifikia furaha za uzima wa milele. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...```

*SOMO LA KWANZA*
Matendo ya Mitume 6:1-7

_Walichagua miongoni mwao watu saba waliojaa Roho._

*Somo katika kitabu cha Matendo ya Mitume*

Siku zile, idadi ya wafuasi ilipokuwa ikiongezeka sana, Wagiriki waliokuwa wamejiunga na Wayahudi waliwanung'unikia wale wa asili ya Waebrania kwa sababu wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika huduma ya kila siku. Hapo wale Kumi na Wawili waliwaita wafuasi wote, wakasema, "Haifai sisi kuliacha neno la Mungu na kutumikia mezani. Basi ndugu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema na wenye kujaa Roho na hekima, ili tuwakabidhi kazi hiyo, sisi lakini tukazie sala na utume wa neno." Azimio hili likawapendeza wote waliokuwako, wakachagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao, mwongofu wa Antiokia. Hao wakawaweka mbele ya mitume, nao wakasali, wakawawekea mikono juu yao. Neno la Mungu likaenea, na idadi ya wafuasi ikaongezeka sana katika Yerusalemu: pia kundi kubwa la makuhani waliipokea imani.

*Neno la Bwana.*

*ZABUR RI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 33:1-2, 4-5. 18-19 (K 22)

*K. Fadhili, zako zikae nasi, ee Bwana, k**a vile tunavyokutumainia wewe.*

*au: Aleluya.*

Mshangilieni Bwana, enyi wenye haki;
Kusifu kunawafaa watu wanyofu.
Mtukuzeni Bwana kwa kinubi:
Mnigieni kinanda cha nyuzi kumi.
*K.*

Maana neno la Bwana ni la kweli:
matendo yake yote ni maaminifu.
Bwana apenda unyofu na haki
dunia imejaa wema wake.
*K.*

Macho ya Bwana yawaelekea wale wamchao,
wale wanaotumainia wema wake,
ili aziopoe roho zao katika kifo,
na wakati wa njaa awalishe.
*K.*

*SOMO LA PILI*
1 Petro 2:4-9

_Ninyi ni kizazi kiteule, ukuhani wa kifalme._

*Samo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Petro*

Wapendwa: Mjongeeni yeye aliye jiwe lenye uzima lililokataliwa na wanadamu, lakini ni teule, azizi kwa Mungu. Nanyi pia muwe k**a mawe yenye uzima yanayotumiwa kwa kujengea nyumba ya kiroho, ukuhani mtakatifu, unaokubalika na Mungu kwa ujumbe wa Yesu Kristo. Kwa hiyo Maandiko yanasema: "Tazameni, naweka katika Sioni, jiwe kuu la pembeni, teule, azizi. Kila aliaminiye hataaibika." Maana ninyi waamini mmejaliwa heshima hiyo. Lakini kwa wale wasiosadiki: "Jiwe hilo lililokataliwa na waashi ni jiwe la pembeni," ndilo" Jiwe la kujikwaza, na mwamba wa kuangushia watu." Wanajikwaza kwa sababu hawakulisadiki neno. Hii ndiyo ajali yao tangu asili. Bali ninyi ni "kizazi kiteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio mali ya Mungu, mpate kutangaza matendo makuu' ya yule aliyewaita mtoke gizani na kuingia katika mwanga wake wa ajabu.

*Neno la Bwana.*

*SHANGILIO LA INJILI*
Yohane 14: 6

*Aleluya. Aleluya*
Mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima, asema Bwana. Hakuna ajaye kwa Baba, ila kwa njia yangu mimi
*Aleluya.*

*INJILI*
Yohane l4:1-12

_Mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima._

*Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Yohane*

Siku zile: Yesu aliwaambia wafuasi wake, Mioyo yenu isihangaike. Mnasadiki Mungu; nisadikini mimi pia. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi. K**a sivyo, je, ningaliwaambia kwamba ninakwenda kuwaandalia mahali?Baada ya kwenda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwachukue kwangu, mpate kuwapo nilipo mimi. Na mmeijua njia ya niendako." Tomaso akamwambia, "Bwana, hata uendako hatujui; basi, twaijuaje njia?"" Yesu akamwambia, "Mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima. Hakuna ajaye kwa Baba, ila kwa njia yangu mimi. K**a mngalinijua mimi, mngalimjua Baba yangu pia. Toka sasa mnamjua, na mmemwona." Filipo akamwambia, "Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha." Yesu akamwambia, "Muda mwingi hivi nimekaa kwenu, Filipo, nawe je, hujanitambua? Aliyeniona mimi amemwona Baba. Sasa wasemaje, Utuonyeshe Baba'? Je, husadiki ya kuwa mimi niko ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu?Maneno ninayowaambia mimi siyasemi kwa amri yangu. Lakini Baba akaaye ndani yangu azitenda kazi zake. Mnisadiki ya kuwa mimi niko ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu, k**a sivyo, sadikini walau kwa sababu ya kazi zilizotendeka. Amin, amin, nawaambieni, anisadikiye mimi, atafanya mwenyewe kazi k**a mimi, na hata kubwa zaidi atafanya, kwa maana naenda kwa Baba,"

*Injili ya Bwana*

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI**DOMINIKA YA HURUMA YA MUNGU/ DOMINIKA YA PILI YA PASAKA**12/4/2026**RANGI YA LITURUJIA: NYE...
12/04/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI*

*DOMINIKA YA HURUMA YA MUNGU/ DOMINIKA YA PILI YA PASAKA*

*12/4/2026*

*RANGI YA LITURUJIA: NYEUPE 🤍*

*MADA YA DOMINIKA:*

```"HERI WALE AMBAO HAWAJAONA."```

*_Maneno haya ya Bwana Mfufuka yanaelekezwa kwa wafuasi wote. Tunakutana na Bwana aliyefufuka katika mkusanyiko wa jumuiya siku ya Dominika. Hii ndio mada ya Injili ambayo inaungana na somo la pili, hasa kifungu cha mwisho. Ikiwa hatuwezi kumwona Bwana Mfufuka, kuna jambo lingine tunaweza kuona: jumuiya ambayo, kupitia maisha yake, ni ushahidi kwamba Kristo yu hai na yupo nasi (somo la kwanza)._*

*ANTIFONA YA KUINGIA: 1 Petro 2:2*
K**a watoto wachanga waliozaliwa sasa, mtamani maziwa halisi ya kiroho, mpate kukua katika wokovu, aleluya.

*KOLEKTA*
``` Ee Mungu wa rehema ya milele, wewe unaamsha imani ya taifa lako takatifu katika kurudia kila mwaka kwa sikukuu ya Pasaka; tunakuomba uongeze neema uliyolijalia, ili wote watambue kwa uelewa sahihi thamani kuu ya Ubatizo uliowatakasa, ya Roho aliyewazaa upya na ya damu iliyowakomboa. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao..```

*SOMO LA KWANZA*
Matendo ya Mitume 2:42-47

_Wote waliopokea imani walikuwa jamii moja na wakashirikiana vitu vyote._

*Somo katika kitabu cha Matendo ya Mitume*

[Ndugu wote] walilishikilia fundisho la mitume, kuishi pamoja kindugu, kumega mkate na kusali. Kila mtu akaingiwa na hofu, kwa maana miujiza na ishara nyingi zilifanywa na mitume. Wote walioipokea imani walikuwa jamii moja na wakashirikiana vitu vyote; wakauza mashamba na mali zao na kuwagawia watu wote, kila mtu kadiri ya mahitaji yake. Siku kwa siku walikutana hekaluni na walimega mkate nyumba kwa nyumba, wakala pamoja kwa furaha na unyofu wa moyo. Walimtukuza Mungu na kupendwa na watu wote. Na kila siku Bwana aliwaongeza wale waliokuwa wakiokolewa.

*Neno la Bwana.*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 118:2-4, 13-15ab, 22-24 (K. 1)

*K. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, kwa maana wema wake ni wa milele.*

Israeli na aseme sasa: / wema wake ni wa milele.
Nyumba ya Haruni iseme: / wema wake ni wa milele.
Wamchao Bwana waseme: / wema wake ni wa milele
*K.*

Nilisukumwa, nilisukumizwa nianguke,
lakini Bwana amenisaidia.
Bwana ni nguvu na uhodari wangu,
yeye amekuwa wokovu wangu.
Sauti ya shangwe na ya ushindi imo katika hema za watu waadilifu.
*K.*

Jiwe walilolikataa waashi /limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Jambo hili alilifanya Bwana; / nalo ni la ajabu machoni petu.
Hil ndiyo siku aliyoifanya Bwana; / tuishangilie na kuifurahia.
*K.*

*SOMO LA PILI*
1 Petro 1:3-9

_Ametuzaa upya kwa huruna yake kubwa, tupate tumaini hai kwa ufufuko wa Yesu Kristo katika wafu._

*Somo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Petro*

Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Huyo Baba ametuzaa upya kwa huruma yake kubwa, tupate tumaini hai kwa ufufuko wa Yesu Kristo katika wafu: pia tupate urithi usioharibika, wala kuchafuka, wala kufifia, mliowekewa mbinguni. Nguvu ya Mungu inawahifadhi kwa sababu ya imani yenu, hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho. Hapo mtashangilia, ijapo sasa imewapasa kuhuzunika kwa kitambo kidogo katika majaribio kadha wa kadha. Wakati wa kufunuliwa Yesu Kristo, imani yenu - iliyojaribiwa k**a dhahabu iliyosafishwa kwa moto- ionekane ni bora zaidi kuliko dhahabu hafifu, mpate sifa na utukufu na heshima. Mwampenda Kristo, ijapo hamjamwona bado, na bila kumwona sasa, mnamsadiki. Mtamshangilia kwa furaha tukufu isiyosemekana, yaani wakati mtakapokuwa mmefikia upeo wa imani yenu, ndio wokovu wa roho zenu.

*Neno la Bwana.*

*SHANGILIO LA INJILI*
Yohane 20:29

*Aleluya. Aleluya.*
Kwa kuwa umeniona, Tomaso, umesadiki, asema Bwana. Wenye heri wale wasioona na wakasadiki.
*Aleluya*


*INJILI*
Yohane 20:19-31

_Baada ya siku nane, alikuja Yesu._

*+ Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa a na Yohane*

Jioni ya siku ile ya kwanza ya Juma, alikuja Yesu, akasimama katikati, ingawa milango ya chumba walimokaa wafuasi ilikuwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi, akawaambia, "Amani iwe nanyi. Baada ya maneno hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wafuasi wakafurahi walipomwona Bwana. Yesu akawaambia mara ya pili, "Amani iwe nanyi. K**a Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi." Baada ya maneno hayo, akawapulizia, akawaambia, "Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa. Na wowote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa." Lakini Tomaso, aitwaye Pacha, mmoja wa wale Kumi na Wawili, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. Basi, wafuasi wengine wakamwambia, "Tumemwona Bwana." Yeye lakini akawajibu, Nisipoona matundu ya misumari mikononi mwake, na kutia kidole changu sehemu za misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, sisadiki hata kidogo." Baada ya siku nane, wafuasi wake walikuwamo tena chumbani, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, ingawa milango ilikuwa imefungwa, akasimama kati yao, akasema, "Amani iwe nanyi." Kisha akamwambia Tomaso, tia kidole chako humu, tazama mikono yangu, lete mkono wako na kuutia katika ubavu wangu na usikose imani, bali uwe anayeamini." Tomaso akajibu akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu!" Yesu akamwambia, "Kwa kuwva umeniona, umesadiki? Wenye heri wale wasioona na wakasadiki." Sasa Yesu alifanya ishara nyingine nyingi mbele ya wafuasi wake zisizoandikwa katika kitabu hiki. Lakini hizi zimeandikwa, mpate kusadiki ya kuwa Yesu ni Masiya, Mwana wa Mungu, tena kwa kusadiki mpate kuwa na uzima kwa jina lake.

*Injili ya Bwana.*

DOMINIKA YA MATAWI KATIKA MATESO YA BWANA, MACHI 29, 2026RANGI YA KILITURJIA: NYEKUNDU ♥️INJILI KABLA YA MAANDAMANOMATHA...
28/03/2026

DOMINIKA YA MATAWI KATIKA MATESO YA BWANA, MACHI 29, 2026
RANGI YA KILITURJIA: NYEKUNDU ♥️

INJILI KABLA YA MAANDAMANO
MATHAYO 21:1—11

Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo

Walipokaribia Yerusalemu na kufika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni, Yesu alituma wafuasi wawili, akawaambia, Nendeni katika kijiji kilichi mbele yenu. Mara mtaona punda amefungwa, na mwanapunda pamoja naye. Wafungueni mniletee. Na k**a mtu akiwauliza sababu, jibuni, ‘Bwana anahitaji.’ Mara atawatoa.” Hayo yalitendeka ili kutimiza neno la nabii aliyesema: “Mwambieni Binti Sioni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mpole, na amekaa juu ya punda, na mwanapunda, mtoto wa punda.’” Basi, wafuasi wakaenda huko, wakafanya k**a Yesu alivyowaagiza. Wakawaleta punda na mwanapunda, wakatandika nguo zao miongoni mwao. Naye akaketi juu yake. Wengi wa umati wakatandaza nguo zao njiani; wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza katika njia. Wengi sana waliomtangulia na kumfuata, walipaza sauti wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi! Mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana! Hosana juu mbinguni!” Alipoingia Yerusalemu, mji wote ukashtuka, wakaulizana, “Huyu ni nani?” Watu wa uamti wakajibu, “Huyu ni Yesu, nabii wa Nazareti ya Galilaya.”

INJILI YA BWANA… SIFA KWAKO EE KRISTO

MASOMO YA MISA

SOMO LA KWANZA
ISAYA 50:4—7

Wala sikuuficha uso wangu, najua ya kwamba sitaaibishwa (Wimbo wa tatu wa Mtumishi wa Bwana).

Somo katika kitabu cha Nabii Isaya

Bwana Mungu amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kumjibu Yule achokaye kwa neno la kumwamsha. Kila asubuhi, yeye huliamsha s**io langu ili nis**ie k**a mwanafunzi; Bwana Mungu amenizibua s**io langu; name sikukataa, sikurudi nyuma. Niliwatolea mgongo wangu wale walionipiga, na mashavu yangu kwa wale walioning’oa ndevu; wala sikuuficha uso wangu ili usifedheheshwe na kutemewa mate. Bwana Mungu ndiye maana nimefanya uso wangu mgumu k**a jiwe, najua ya kwamba sitaaibishwa.

NENO LA BWANA… TUMSHUKURU MUNGU

ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 22:8—9, 17—18a, 19—20, 23—24 (K. 2a)

K. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Wote wanaoniona hunicheka; hunyonga midomo
kwa kunidhihaki; na kutikisa vichwa vyao:
“Alimwamini Bwana, acha amwokoe;
acha amuopoe, kwa kuwa anapendezwa naye.” K.

Kwa maana mbwa wengi wamenizunguka;
kundi la waovu wananisonga.
Wamenitoboa mikono na miguu
naweza kuhesabu mifupa yangu yote. K.

Wanagawanya nguo zangu kati yao;
wanaipigia kura kanzu yangu.
Nawe, ee Bwana, usiwe mbali;
ewe msaada wangu, fanya haraka kunisaidia. K.

Nitawasimulia ndugu zangu jina lako;
katikati ya mkutano nitakusifu:
“Enyi watumishi wa Bwana, msifuni!
Enyi wote, wazao wa Yakobo, mtukuzeni;
enyi wote, wana wa Israeli, mtumikieni!” K.

SOMO LA PILI
WAFILIPI 2:6—11

Alijinyenyekeza mwenyewe, kwa sababu hiyo Mungu alimtukuza.

Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Wafilipi

Kristo Yesu, ijapokuwa alikuwa namna ya Mungu, hakuchukulia kwamba kuwa sawa na Mungu lilikuwa jambo la kushik**ana nalo. Bali alijishusha mwenyewe, akatwaa umbo la mtumishi, akawa ana mfano wa wanadamu, na alipoonekana ana umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza mwenyewe, akawa mtii mpaka mauti, yaani mauti ya msalabani. Kwa sababu hiyo Mungu alimtukuza, akampa jina lipitalo kila jina, ili kwa jina la Yesu wote wapige magoti, wote walioko mbinguni, duniani na kuzimu. Na kila ulimi ukiri kwamba Yesu Kristo ndiye Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

NENO LA BWANA… TUMSHUKURU MUNGU

SHANGILIO LA INJILI
WAFILIPI 2:8b—9

W. Sifa na utukufu kwako, ee Kristo.
K. Kristo alijinyenyekeza mwenyewe, akawa mtii mpaka mauti, yaani mauti ya msalabani. Kwa sababu hiyo Mungu alimtukuza, akampa jina lipitalo kila jina.
W. Sifa na utukufu kwako, ee Kristo.

INJILI (MWAKA A)
MATHAYO 26:14—27:66

Mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo yalivyoandikwa na Mathayo

M. wakati ule: Mmojawapo wa wale Kumi na Wawili jina Yuda Iskariote, aliwaendea makuhani wakuu, akasema,
W. “Mnataka kunipa nini nimtie Yesu mikononi mwenu?”
M. Wakampimia vipande thelathini vya fedha.
Tangu hapo alitafuta nafasi nzuri ya kumtoa.
Siku ya kwanza ya Mikate Isiyotiwa Cgachu, wafuasi wakamwendea Yesu, wakamwambia,
W. “Unataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?”
M. Naye akasema,
†. “Nendeni mjini kwa mtu Fulani, mkamwambie, ‘Mwalimu asema, wakati wangu umewadia; ni nyumbani kwako nitafanya Pasaka pamoja na wafuasi wangu.’”
M. Wafuasi wakafanya k**a Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
Kulipokuwa jioni, aliketi mezani pamoja na wale Kumi na Wawili. Wakati wa kula alisema,
†. “Amin, nawaaambieni, mmoja mmoja wenu atanisaliti.”
M. Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja,
W. “Ati, Bwana, ni mimi?”
M. Naye akawajibu,
†. “Yeye aliyechovya mkono katika sahani pamoja name, ndiye atakayenisaliti.
Basi, Mwana wa Mtu anakwenda zake k**a Maandiko yasemavyo juu yake, lakini ole wake mtu huyu anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalimfaa mtu huyo k**a hangalizaliwa.”
M. Yuda, msaliti wake, akauliza pia,
W. “Ati, Bwana, ni mimi?”
M. Akamwambia,
†. “Wewe umesema.”
M. Pale karamuni Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wafuasi wake akisema,
†. “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
M. Akatwaa kikombe, akashukuru, akawapa akisema,
†. “Inyweni hii ninyi nyote, kwa maana hii ni damu yangu, damu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa maondoleo ya dhambi. Lakini nawaambieni, toka sasa sitakunywa tena uzao wa mzabibu hata siku nitakapokunywa divai mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
M. Baada ya kuimba zaburi, wakatoka wakaenda katika Mlima wa Mizeituni. Halafu Yesu akawaambia,
†. “Ninyi nyote mtakwazwa sababu yangu usiku huu, kwa maana imeandikwa: ‘Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika’; lakini baada ya ufufuko wangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
M. Petro akajibu, akamwambia,
W. “WAkikwazwa wote kwa sababu yako, mimi sitakwazwa hata kidgo.”
M. Yesu akamwambia,
†. “Amin, nakuambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
M. Petro akajibu,
W. “Hata ikinipasa kufa pamoja nawe, sitakukana.”
M. Vivyo hivyo wakasema wafuasi wote. Kasha Yesu akaenda pamoja nao mahali paitwapo Gethsemane. Akawaambia wafuasi,
†. “Kaeni hapa niende kule kusali.”
M. Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo. Akaanza kuhuzunika na kusononeka. Hapo akawaambia,
†. “Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”
M. Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali kwa maneno haya,
†. “Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kinipite, lakini si k**a nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”
M. Akawajia wafuasi, akawakuta wamelala usingizi. Akamwambia Petro,
†. “Je, hata saa moja hamkuweza kukesha pamoja name? Kesheni na kusali msije mkaingia katika kishawishi. Kwa maana roho i tayari, ila mwili ni dhaifu.”
M. Akaenda mara ya pili, akasali tena akisema,
†. “Baba yangu, isipowezekana kikombe hiki kinipite bila kukinywa, mapenzi yako yatimizwe.”
M. Akaja tena, akawakuta wamelala usingizi, maana macho yao yalikuwa mazito. Akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yale yale. Kasha akawajia wafuasi, akawaambia,
†. “Je, bado mnalala na kupumzika? Tazameni saa imewadia, na Mwana wa Mtu anatiwa mikononi mwa wakosefu. Simanmeni! Twende zetu. Tazameni, mtu wa kunisaliti amekaribia.”
M. Alipokuwa akisema bado, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, alikuja, na pamoja naye kundi kubwana la watu waliochukua panga na rungu, walikuja kwa amri ya makuhani wakuu na wazee wa baraza. Msaliti alikuwa amepatana nao ishara. Alisema,
W. “Nitakayembusu ndiye, mk**ateni.”
M. Mara akamjongea Yesu, akasema,
W. “Salamu, Rabbi!”
M. Na akambusu. Yesu akamwaambia,
†. “Rafiki, fanya ulilolijia.”
M. Baada ya hayo wakaja wakanyosha mikono, wakamk**ata Yesu. Papo hapo, mmoja wa waliokuwa na Yesu akanyosha mkono, akachomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa kuhani mkuu na kumkata s**io. Yesu akamwambia,
†. “Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote wachukuao upanga wataangamia kwa upanga. Je, wadhani nisingeliweza kumwomba Baba yangu, aniletee sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na wawili ya malaika? Lakini hapo yangelitimiaje Maandiko yasemayo kwamba hayo sharti yatendeke?”
M. Saa ile Yesu akawaambia makundi,
†. “Mmekuja na panga na rungu kunik**ata mimi k**a kumk**ata mnyang’anyi? Kila siku nilikaa hekaluni nikifundisha, huko hamkunik**ata. Lakini hapo yote yametendeka, ili Maandiko ya manabii yatimie.”
M. Hapo wafuasi wote wakamwacha, wakakimbia. Nao waliomkata Yesu walimpeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu. Huko walikuwa wamekusanyika Waandishi na wazee. Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akakaa pamoja na watumishi apate kuona mwisho. Makuhani wakuu na baraza lote walitafuta ushuhuda wa uongo, wapate kumwua, wasiupate, ingwa mashahidi wengi wa uongo walitokea. Mwisho wawili wakaja, wakasema,
W. “Huyu alisema, ‘Naweza kulibomoa hekalu la Mungu, na kulijenga upya kwa siku tatu.’”
M. Kisha kuhani mkuu akasimama, akamwuliza,
W. “Je, hujibu neno kwa mashtaka wanayokushuhudia hawa?”
M. Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani mkuu akamwambia,
W. “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie k**a wewe ndiwe Kristo. Mwana wa Mungu.”
M. Yesu akamwambia,
†. “Wewe umesema. Juu ya hayo nawaambieni: Toka sasa mtamwona ‘Mwana wa mtu amekaa kulia kwa Mwenyezi’ na ‘akija juu ya mawingu ya mbinguni.’”
M. Hapo kuhani mkuu akararua mavazi yake, aksema,
W. “Amekufuru. Kwanini tunahitaji bado mashahidi? Sasa hivi mmes**ia kufuru. Mwaonaje?”
M. Nao wakajibu,
W. “Amestahili kufa.”
M. Baada ya hayo, wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi; wengine wakampiga kwa fimbo wakisema,
W. “Ewe Masiya, utufumbulie ni nani aliyekupiga?”
M. Wakati huo Petro alikaa nje uani.
Mjakazi mmoja akamjongea, akasema,
W. “Nawe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
M. Naye akakana mbele ya wote akisema,
W. “Sijui usemalo!”
M. Lakini alipopita mlangoni aende nje, mjakazi mwingine akamwona, akawaambia watu pale,
W. “Na huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
M. Akakana tena akiapa,
W. “Simjui mtu huyu!”
M. Punde kidogo, watu waliosimama pale, wakamjongea Petro, wakamwambia,
W. “Hakika, nawe ni mmoja wao, kwa maana hata usemi wako wakutambulisha.”
M. Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema,
W. “Simjui mtu huyu.”
M. Mara hapo jogoo akawika. Petro akalikumbuka neno la Yesu, yaani, “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Akaenda nje, akalia machozi uchungu. Asubuhi yake, makuhani wakuu wote na wazee wa baraza wakashauriana juu ya Yesu kusudi la kumwua. Wakamfunga, wakampeleka na kumtoa kwa Ponsio Pilato, gavana. Hapo Yuda, msaliti wake, a;opoona ya kuwa amehukumiwa, alijuta. Akawarudishia makuhani wakuu na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema,
W. “Nimekosa, maana nimesaliti damu isiyo na hatia.’
M. Wakajibu,
W. “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.”
M. Akavitupa vipande vya fedha hekaluni, akaondoka, akaenda, akajinyonga. Makuhani wakuu wakavitwaa vipande vya fedha,
W. “Si halali kuviweka katika hazina, kwa maana ni fedha ya damu.”
M. Wakashauriana, wakavitumia kwa kununua shamba la mfinyanzi kwa kuwazika wageni. Kwa hiyo shamba hilo huitwa Shamba la Damu mpaka siku ya leo. Hivyo yakatimia maneno ya nabii Yeremia aliyesema, “Walivitwaa vipande thelathini vya fedha, yaani bei, ambayo wana wa Israeli walimpimia yuke waliyempimia bei, wakavitumia kwa kununua shamba la mfinyanzi, k**a Bwana alivyoagiza.”
* Yesu alisimama mbele ya Pilato. Pilato akamwuliza,
W. “Wewe u mfalme wa Wayahudi?”
M. Yesu akamjibu,
†. “Wewe wasema.”
M. Aliposhtakiwa na makuhani wakuu na wazee, hakujibu neno. Pilato akamwambia,
W. “Je, huyas**ii yale wanayokushuhudia?”
M. Lakini hakumjibu neno lolote, hata Pilato akashangaa sana. Basi ilikuwa desturi kwa sikukuu ya Pasaka, gavana kuwafungulia watu mfungwa mmoja waliyemtaka wenyewe. Siku zile palikuwa na mfungwa mwenye sifa mbaya sana, jina lake Baraba. Basi, Pilato akawauliza watu wa mkutano,
W. “Mnataka niwafungulie nani: Baraba au Yesu aitwaye Kristo?”
M. Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda. Alipokaa katika kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea habari hii, “Usijitie katika shauri la mwadilifu huyu kwa maana leo nimeteswa sana katika ndoto kwa ajili yake.” Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashauri watu wamtake Baraba na kumwangamiza Yesu. Basi, gavana alipowauliza tena,
W. “Mwataka niwafungulie nani kati ya hawa wawili?”
M. Wakajibu,
W. “Baraba.”
M. Pilato akawauliza,
W. “Nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?”
M. Wakasema,
W. “Asulibiwe.”
M. Akajibu,
W. “Je, amefanya ubaya gani?”
M. Nao wakazidi kupaza sauti,
W. “Asulibiwe.”
M. Pilato akaona ya kwamba hafaulu kitu, isipokuwa ghasia inazidi tu. Basi akatwaa maji, akanwa mikono mbele ya umati akasema,
W. “Mimi sina hatia katika kumwaga damu ya mwadilifu huyu, shauri lenu wenyewe.”
M. Watu wote wakajibu na kusema,
W “Damu yake iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
M. Hapo akawafungulia Baraba. Na Yesu akisha kupigwa mijeledi, Pilato alimtoa kusudi asulibiwe. Kisha askari wa gavana wakamchukua Yesu ukumbini, wakamkusanyikia kikosi kizima. Baada ya kumvua nguo, wakamvika joho jekundu. Wakasuka taji la miiba na kumvika kichwani. Wakamshikisha mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakampigia maggot wakisema kwa dhihaka,
W. “Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
M. Wakamtemea mate, wakautwaa mwanzi wakampigapiga kichwani. Baada ya kumdhihaki, wakamvua joho, wakamvika tena mavazi yake na wakampeleka kumsulibisha. Walipotoka nje, walikutana na mtu wa Kirene, jina lake Simoni, wakamshurutisha achukue msalaba wake. Wakafika mahali paitwapo Golgotha, (maana yake, Mahali pa Fuvu la Kichwa). Wakampa divai iliyochanganyika na nyongo anywe. Akaionja lakini akakataa kunywa. Baada ya kumsulibisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura. Wakaketi, wakamlinda huko. Juu ya kichwa chake wakaweka hati iliyokitaja kisa cha hukumu yake: “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.” Pamoja naye wakasulibiwa wanyang’anyi wawili, mmoja kulia kwake, mmoja kushoto kwake. Watu waliopita njiani walimtukana, wakatikisa vichwa vyao na kusem,
W. “Ewe uwezaye kulibomoa hekalu na kulijenga upya kwa siku tatu, ujiokoe mwenyewe. Ukuwa wewe ni Mwana wa Mungu, shuka msalabani”
M. Kadhalika, makuhani wakuu pamoja na Waandishi na wazee, wakamdhihaki, wakisema,
W. “Aliwaokoa wengine, kujiokoa mwenyewe hawezi. K**a ni mfalme wa Israeli, basi ashuke sasa msalabani, nasi tutamsadiki. Amemtegemea Mungu, basi amwokoe sasa k**a anampenda, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’”
M. Kadhalika wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimtukana vile vile. Toka saa sita giza lilifunika nchi yote mpaka saa sita. Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kuu,
†. “Eli, Eli, lema sabakthani?”
M. Mana yake,
†. “Mungu wangu, Mungu wangu, kwanini umeniacha?”
M. Baadhi ya wale waliosimama pale na kus**ia, wakasema,
W. “Huyu anamwita Eliya.”
M. Mara mmoja wao akaenda hima, akatwaa sifongo, akaijaza s**i, akaitia juu ya mwanzi, akampa anywe. Wengine wakasema,
W. “Acha tuone k**a ELiya atakuja kumwokoa.”
M. Yesu akalia tena kwa sauti kuu, akakta roho.
M. Hapo pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Nchi ikatetemeka, na miamba ikapasuka. Makaburi yakafunuka, na miili mingi ya watakatifu waliolala humo usingizi wa mauti ikafufuka. Na baada ya ufufuko wake, wakatoka makaburini, wakaingia mji mtakatifu wakawatokea watu wengi. Wakati akida na wale waliokuwa naye wakimlinda Yesu, walipoona tetemeko la nchi na matukio hayo, waliogopa sana. Wakasema,
W. “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu!” *
M. Pale palikuwa na wanawake wengi waliotazama kutoka mbali. Hao walikuwa wamemfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. Miongoni mwao walikuwamo Maria Magdalena, na Maria mama wa Yakobo na Yosefu, na mama wa wana wa Zebedayo. Jioni akaja mtu tajiri wa Arimathea, jina lake Yosefu. Naye pia alikuwa mfuasi wa Yesu. Huyo alimwendea Pilato, akamwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe. Yosefu akautwaa mwili, akauzungushia sanda ya kitani safi. Akauweka katika kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga mwambani. Akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaondoka. Pia Maria Magdalena na Maria mwingine walikuwa pale, wameketi kulielekea kaburi.
Siku ya pili, ndiyo iliyofuata maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo wakakutana kwa Pilato. Wakasema,
W. “Bwana, tumekumbuka ya kuwa Yule mdanganyifu alipoishi bado alisema, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’ Basi, uamru kulilinda kaburi mpaka siku ya tatu, wsije wafuasi wake wakamwiba na kuwambia watu, ‘Amefufuka katika wafu.’ Hivyo udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya zaidi kuliko wa kwanza.’
M. Pilato akawaambia,
W. “Mna walinzi. Basi, nendeni mkalilinde kadiri mnavyojua.”
M. Nao wakaenda, wakalifanyia usalama kaburi kwa kutia muhuir jiweni na kuwaweka walinzi.

Address

Nairobi
Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno La Bwana posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Neno La Bwana:

Share