28/03/2026
DOMINIKA YA MATAWI KATIKA MATESO YA BWANA, MACHI 29, 2026
RANGI YA KILITURJIA: NYEKUNDU ♥️
INJILI KABLA YA MAANDAMANO
MATHAYO 21:1—11
Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo
Walipokaribia Yerusalemu na kufika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni, Yesu alituma wafuasi wawili, akawaambia, Nendeni katika kijiji kilichi mbele yenu. Mara mtaona punda amefungwa, na mwanapunda pamoja naye. Wafungueni mniletee. Na k**a mtu akiwauliza sababu, jibuni, ‘Bwana anahitaji.’ Mara atawatoa.” Hayo yalitendeka ili kutimiza neno la nabii aliyesema: “Mwambieni Binti Sioni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mpole, na amekaa juu ya punda, na mwanapunda, mtoto wa punda.’” Basi, wafuasi wakaenda huko, wakafanya k**a Yesu alivyowaagiza. Wakawaleta punda na mwanapunda, wakatandika nguo zao miongoni mwao. Naye akaketi juu yake. Wengi wa umati wakatandaza nguo zao njiani; wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza katika njia. Wengi sana waliomtangulia na kumfuata, walipaza sauti wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi! Mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana! Hosana juu mbinguni!” Alipoingia Yerusalemu, mji wote ukashtuka, wakaulizana, “Huyu ni nani?” Watu wa uamti wakajibu, “Huyu ni Yesu, nabii wa Nazareti ya Galilaya.”
INJILI YA BWANA… SIFA KWAKO EE KRISTO
MASOMO YA MISA
SOMO LA KWANZA
ISAYA 50:4—7
Wala sikuuficha uso wangu, najua ya kwamba sitaaibishwa (Wimbo wa tatu wa Mtumishi wa Bwana).
Somo katika kitabu cha Nabii Isaya
Bwana Mungu amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kumjibu Yule achokaye kwa neno la kumwamsha. Kila asubuhi, yeye huliamsha s**io langu ili nis**ie k**a mwanafunzi; Bwana Mungu amenizibua s**io langu; name sikukataa, sikurudi nyuma. Niliwatolea mgongo wangu wale walionipiga, na mashavu yangu kwa wale walioning’oa ndevu; wala sikuuficha uso wangu ili usifedheheshwe na kutemewa mate. Bwana Mungu ndiye maana nimefanya uso wangu mgumu k**a jiwe, najua ya kwamba sitaaibishwa.
NENO LA BWANA… TUMSHUKURU MUNGU
ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 22:8—9, 17—18a, 19—20, 23—24 (K. 2a)
K. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Wote wanaoniona hunicheka; hunyonga midomo
kwa kunidhihaki; na kutikisa vichwa vyao:
“Alimwamini Bwana, acha amwokoe;
acha amuopoe, kwa kuwa anapendezwa naye.” K.
Kwa maana mbwa wengi wamenizunguka;
kundi la waovu wananisonga.
Wamenitoboa mikono na miguu
naweza kuhesabu mifupa yangu yote. K.
Wanagawanya nguo zangu kati yao;
wanaipigia kura kanzu yangu.
Nawe, ee Bwana, usiwe mbali;
ewe msaada wangu, fanya haraka kunisaidia. K.
Nitawasimulia ndugu zangu jina lako;
katikati ya mkutano nitakusifu:
“Enyi watumishi wa Bwana, msifuni!
Enyi wote, wazao wa Yakobo, mtukuzeni;
enyi wote, wana wa Israeli, mtumikieni!” K.
SOMO LA PILI
WAFILIPI 2:6—11
Alijinyenyekeza mwenyewe, kwa sababu hiyo Mungu alimtukuza.
Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Wafilipi
Kristo Yesu, ijapokuwa alikuwa namna ya Mungu, hakuchukulia kwamba kuwa sawa na Mungu lilikuwa jambo la kushik**ana nalo. Bali alijishusha mwenyewe, akatwaa umbo la mtumishi, akawa ana mfano wa wanadamu, na alipoonekana ana umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza mwenyewe, akawa mtii mpaka mauti, yaani mauti ya msalabani. Kwa sababu hiyo Mungu alimtukuza, akampa jina lipitalo kila jina, ili kwa jina la Yesu wote wapige magoti, wote walioko mbinguni, duniani na kuzimu. Na kila ulimi ukiri kwamba Yesu Kristo ndiye Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
NENO LA BWANA… TUMSHUKURU MUNGU
SHANGILIO LA INJILI
WAFILIPI 2:8b—9
W. Sifa na utukufu kwako, ee Kristo.
K. Kristo alijinyenyekeza mwenyewe, akawa mtii mpaka mauti, yaani mauti ya msalabani. Kwa sababu hiyo Mungu alimtukuza, akampa jina lipitalo kila jina.
W. Sifa na utukufu kwako, ee Kristo.
INJILI (MWAKA A)
MATHAYO 26:14—27:66
Mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo yalivyoandikwa na Mathayo
M. wakati ule: Mmojawapo wa wale Kumi na Wawili jina Yuda Iskariote, aliwaendea makuhani wakuu, akasema,
W. “Mnataka kunipa nini nimtie Yesu mikononi mwenu?”
M. Wakampimia vipande thelathini vya fedha.
Tangu hapo alitafuta nafasi nzuri ya kumtoa.
Siku ya kwanza ya Mikate Isiyotiwa Cgachu, wafuasi wakamwendea Yesu, wakamwambia,
W. “Unataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?”
M. Naye akasema,
†. “Nendeni mjini kwa mtu Fulani, mkamwambie, ‘Mwalimu asema, wakati wangu umewadia; ni nyumbani kwako nitafanya Pasaka pamoja na wafuasi wangu.’”
M. Wafuasi wakafanya k**a Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
Kulipokuwa jioni, aliketi mezani pamoja na wale Kumi na Wawili. Wakati wa kula alisema,
†. “Amin, nawaaambieni, mmoja mmoja wenu atanisaliti.”
M. Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja,
W. “Ati, Bwana, ni mimi?”
M. Naye akawajibu,
†. “Yeye aliyechovya mkono katika sahani pamoja name, ndiye atakayenisaliti.
Basi, Mwana wa Mtu anakwenda zake k**a Maandiko yasemavyo juu yake, lakini ole wake mtu huyu anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalimfaa mtu huyo k**a hangalizaliwa.”
M. Yuda, msaliti wake, akauliza pia,
W. “Ati, Bwana, ni mimi?”
M. Akamwambia,
†. “Wewe umesema.”
M. Pale karamuni Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wafuasi wake akisema,
†. “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
M. Akatwaa kikombe, akashukuru, akawapa akisema,
†. “Inyweni hii ninyi nyote, kwa maana hii ni damu yangu, damu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa maondoleo ya dhambi. Lakini nawaambieni, toka sasa sitakunywa tena uzao wa mzabibu hata siku nitakapokunywa divai mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
M. Baada ya kuimba zaburi, wakatoka wakaenda katika Mlima wa Mizeituni. Halafu Yesu akawaambia,
†. “Ninyi nyote mtakwazwa sababu yangu usiku huu, kwa maana imeandikwa: ‘Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika’; lakini baada ya ufufuko wangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
M. Petro akajibu, akamwambia,
W. “WAkikwazwa wote kwa sababu yako, mimi sitakwazwa hata kidgo.”
M. Yesu akamwambia,
†. “Amin, nakuambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
M. Petro akajibu,
W. “Hata ikinipasa kufa pamoja nawe, sitakukana.”
M. Vivyo hivyo wakasema wafuasi wote. Kasha Yesu akaenda pamoja nao mahali paitwapo Gethsemane. Akawaambia wafuasi,
†. “Kaeni hapa niende kule kusali.”
M. Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo. Akaanza kuhuzunika na kusononeka. Hapo akawaambia,
†. “Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”
M. Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali kwa maneno haya,
†. “Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kinipite, lakini si k**a nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”
M. Akawajia wafuasi, akawakuta wamelala usingizi. Akamwambia Petro,
†. “Je, hata saa moja hamkuweza kukesha pamoja name? Kesheni na kusali msije mkaingia katika kishawishi. Kwa maana roho i tayari, ila mwili ni dhaifu.”
M. Akaenda mara ya pili, akasali tena akisema,
†. “Baba yangu, isipowezekana kikombe hiki kinipite bila kukinywa, mapenzi yako yatimizwe.”
M. Akaja tena, akawakuta wamelala usingizi, maana macho yao yalikuwa mazito. Akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yale yale. Kasha akawajia wafuasi, akawaambia,
†. “Je, bado mnalala na kupumzika? Tazameni saa imewadia, na Mwana wa Mtu anatiwa mikononi mwa wakosefu. Simanmeni! Twende zetu. Tazameni, mtu wa kunisaliti amekaribia.”
M. Alipokuwa akisema bado, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, alikuja, na pamoja naye kundi kubwana la watu waliochukua panga na rungu, walikuja kwa amri ya makuhani wakuu na wazee wa baraza. Msaliti alikuwa amepatana nao ishara. Alisema,
W. “Nitakayembusu ndiye, mk**ateni.”
M. Mara akamjongea Yesu, akasema,
W. “Salamu, Rabbi!”
M. Na akambusu. Yesu akamwaambia,
†. “Rafiki, fanya ulilolijia.”
M. Baada ya hayo wakaja wakanyosha mikono, wakamk**ata Yesu. Papo hapo, mmoja wa waliokuwa na Yesu akanyosha mkono, akachomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa kuhani mkuu na kumkata s**io. Yesu akamwambia,
†. “Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote wachukuao upanga wataangamia kwa upanga. Je, wadhani nisingeliweza kumwomba Baba yangu, aniletee sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na wawili ya malaika? Lakini hapo yangelitimiaje Maandiko yasemayo kwamba hayo sharti yatendeke?”
M. Saa ile Yesu akawaambia makundi,
†. “Mmekuja na panga na rungu kunik**ata mimi k**a kumk**ata mnyang’anyi? Kila siku nilikaa hekaluni nikifundisha, huko hamkunik**ata. Lakini hapo yote yametendeka, ili Maandiko ya manabii yatimie.”
M. Hapo wafuasi wote wakamwacha, wakakimbia. Nao waliomkata Yesu walimpeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu. Huko walikuwa wamekusanyika Waandishi na wazee. Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akakaa pamoja na watumishi apate kuona mwisho. Makuhani wakuu na baraza lote walitafuta ushuhuda wa uongo, wapate kumwua, wasiupate, ingwa mashahidi wengi wa uongo walitokea. Mwisho wawili wakaja, wakasema,
W. “Huyu alisema, ‘Naweza kulibomoa hekalu la Mungu, na kulijenga upya kwa siku tatu.’”
M. Kisha kuhani mkuu akasimama, akamwuliza,
W. “Je, hujibu neno kwa mashtaka wanayokushuhudia hawa?”
M. Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani mkuu akamwambia,
W. “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie k**a wewe ndiwe Kristo. Mwana wa Mungu.”
M. Yesu akamwambia,
†. “Wewe umesema. Juu ya hayo nawaambieni: Toka sasa mtamwona ‘Mwana wa mtu amekaa kulia kwa Mwenyezi’ na ‘akija juu ya mawingu ya mbinguni.’”
M. Hapo kuhani mkuu akararua mavazi yake, aksema,
W. “Amekufuru. Kwanini tunahitaji bado mashahidi? Sasa hivi mmes**ia kufuru. Mwaonaje?”
M. Nao wakajibu,
W. “Amestahili kufa.”
M. Baada ya hayo, wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi; wengine wakampiga kwa fimbo wakisema,
W. “Ewe Masiya, utufumbulie ni nani aliyekupiga?”
M. Wakati huo Petro alikaa nje uani.
Mjakazi mmoja akamjongea, akasema,
W. “Nawe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
M. Naye akakana mbele ya wote akisema,
W. “Sijui usemalo!”
M. Lakini alipopita mlangoni aende nje, mjakazi mwingine akamwona, akawaambia watu pale,
W. “Na huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
M. Akakana tena akiapa,
W. “Simjui mtu huyu!”
M. Punde kidogo, watu waliosimama pale, wakamjongea Petro, wakamwambia,
W. “Hakika, nawe ni mmoja wao, kwa maana hata usemi wako wakutambulisha.”
M. Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema,
W. “Simjui mtu huyu.”
M. Mara hapo jogoo akawika. Petro akalikumbuka neno la Yesu, yaani, “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Akaenda nje, akalia machozi uchungu. Asubuhi yake, makuhani wakuu wote na wazee wa baraza wakashauriana juu ya Yesu kusudi la kumwua. Wakamfunga, wakampeleka na kumtoa kwa Ponsio Pilato, gavana. Hapo Yuda, msaliti wake, a;opoona ya kuwa amehukumiwa, alijuta. Akawarudishia makuhani wakuu na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema,
W. “Nimekosa, maana nimesaliti damu isiyo na hatia.’
M. Wakajibu,
W. “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.”
M. Akavitupa vipande vya fedha hekaluni, akaondoka, akaenda, akajinyonga. Makuhani wakuu wakavitwaa vipande vya fedha,
W. “Si halali kuviweka katika hazina, kwa maana ni fedha ya damu.”
M. Wakashauriana, wakavitumia kwa kununua shamba la mfinyanzi kwa kuwazika wageni. Kwa hiyo shamba hilo huitwa Shamba la Damu mpaka siku ya leo. Hivyo yakatimia maneno ya nabii Yeremia aliyesema, “Walivitwaa vipande thelathini vya fedha, yaani bei, ambayo wana wa Israeli walimpimia yuke waliyempimia bei, wakavitumia kwa kununua shamba la mfinyanzi, k**a Bwana alivyoagiza.”
* Yesu alisimama mbele ya Pilato. Pilato akamwuliza,
W. “Wewe u mfalme wa Wayahudi?”
M. Yesu akamjibu,
†. “Wewe wasema.”
M. Aliposhtakiwa na makuhani wakuu na wazee, hakujibu neno. Pilato akamwambia,
W. “Je, huyas**ii yale wanayokushuhudia?”
M. Lakini hakumjibu neno lolote, hata Pilato akashangaa sana. Basi ilikuwa desturi kwa sikukuu ya Pasaka, gavana kuwafungulia watu mfungwa mmoja waliyemtaka wenyewe. Siku zile palikuwa na mfungwa mwenye sifa mbaya sana, jina lake Baraba. Basi, Pilato akawauliza watu wa mkutano,
W. “Mnataka niwafungulie nani: Baraba au Yesu aitwaye Kristo?”
M. Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda. Alipokaa katika kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea habari hii, “Usijitie katika shauri la mwadilifu huyu kwa maana leo nimeteswa sana katika ndoto kwa ajili yake.” Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashauri watu wamtake Baraba na kumwangamiza Yesu. Basi, gavana alipowauliza tena,
W. “Mwataka niwafungulie nani kati ya hawa wawili?”
M. Wakajibu,
W. “Baraba.”
M. Pilato akawauliza,
W. “Nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?”
M. Wakasema,
W. “Asulibiwe.”
M. Akajibu,
W. “Je, amefanya ubaya gani?”
M. Nao wakazidi kupaza sauti,
W. “Asulibiwe.”
M. Pilato akaona ya kwamba hafaulu kitu, isipokuwa ghasia inazidi tu. Basi akatwaa maji, akanwa mikono mbele ya umati akasema,
W. “Mimi sina hatia katika kumwaga damu ya mwadilifu huyu, shauri lenu wenyewe.”
M. Watu wote wakajibu na kusema,
W “Damu yake iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
M. Hapo akawafungulia Baraba. Na Yesu akisha kupigwa mijeledi, Pilato alimtoa kusudi asulibiwe. Kisha askari wa gavana wakamchukua Yesu ukumbini, wakamkusanyikia kikosi kizima. Baada ya kumvua nguo, wakamvika joho jekundu. Wakasuka taji la miiba na kumvika kichwani. Wakamshikisha mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakampigia maggot wakisema kwa dhihaka,
W. “Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
M. Wakamtemea mate, wakautwaa mwanzi wakampigapiga kichwani. Baada ya kumdhihaki, wakamvua joho, wakamvika tena mavazi yake na wakampeleka kumsulibisha. Walipotoka nje, walikutana na mtu wa Kirene, jina lake Simoni, wakamshurutisha achukue msalaba wake. Wakafika mahali paitwapo Golgotha, (maana yake, Mahali pa Fuvu la Kichwa). Wakampa divai iliyochanganyika na nyongo anywe. Akaionja lakini akakataa kunywa. Baada ya kumsulibisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura. Wakaketi, wakamlinda huko. Juu ya kichwa chake wakaweka hati iliyokitaja kisa cha hukumu yake: “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.” Pamoja naye wakasulibiwa wanyang’anyi wawili, mmoja kulia kwake, mmoja kushoto kwake. Watu waliopita njiani walimtukana, wakatikisa vichwa vyao na kusem,
W. “Ewe uwezaye kulibomoa hekalu na kulijenga upya kwa siku tatu, ujiokoe mwenyewe. Ukuwa wewe ni Mwana wa Mungu, shuka msalabani”
M. Kadhalika, makuhani wakuu pamoja na Waandishi na wazee, wakamdhihaki, wakisema,
W. “Aliwaokoa wengine, kujiokoa mwenyewe hawezi. K**a ni mfalme wa Israeli, basi ashuke sasa msalabani, nasi tutamsadiki. Amemtegemea Mungu, basi amwokoe sasa k**a anampenda, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’”
M. Kadhalika wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimtukana vile vile. Toka saa sita giza lilifunika nchi yote mpaka saa sita. Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kuu,
†. “Eli, Eli, lema sabakthani?”
M. Mana yake,
†. “Mungu wangu, Mungu wangu, kwanini umeniacha?”
M. Baadhi ya wale waliosimama pale na kus**ia, wakasema,
W. “Huyu anamwita Eliya.”
M. Mara mmoja wao akaenda hima, akatwaa sifongo, akaijaza s**i, akaitia juu ya mwanzi, akampa anywe. Wengine wakasema,
W. “Acha tuone k**a ELiya atakuja kumwokoa.”
M. Yesu akalia tena kwa sauti kuu, akakta roho.
M. Hapo pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Nchi ikatetemeka, na miamba ikapasuka. Makaburi yakafunuka, na miili mingi ya watakatifu waliolala humo usingizi wa mauti ikafufuka. Na baada ya ufufuko wake, wakatoka makaburini, wakaingia mji mtakatifu wakawatokea watu wengi. Wakati akida na wale waliokuwa naye wakimlinda Yesu, walipoona tetemeko la nchi na matukio hayo, waliogopa sana. Wakasema,
W. “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu!” *
M. Pale palikuwa na wanawake wengi waliotazama kutoka mbali. Hao walikuwa wamemfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. Miongoni mwao walikuwamo Maria Magdalena, na Maria mama wa Yakobo na Yosefu, na mama wa wana wa Zebedayo. Jioni akaja mtu tajiri wa Arimathea, jina lake Yosefu. Naye pia alikuwa mfuasi wa Yesu. Huyo alimwendea Pilato, akamwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe. Yosefu akautwaa mwili, akauzungushia sanda ya kitani safi. Akauweka katika kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga mwambani. Akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaondoka. Pia Maria Magdalena na Maria mwingine walikuwa pale, wameketi kulielekea kaburi.
Siku ya pili, ndiyo iliyofuata maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo wakakutana kwa Pilato. Wakasema,
W. “Bwana, tumekumbuka ya kuwa Yule mdanganyifu alipoishi bado alisema, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’ Basi, uamru kulilinda kaburi mpaka siku ya tatu, wsije wafuasi wake wakamwiba na kuwambia watu, ‘Amefufuka katika wafu.’ Hivyo udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya zaidi kuliko wa kwanza.’
M. Pilato akawaambia,
W. “Mna walinzi. Basi, nendeni mkalilinde kadiri mnavyojua.”
M. Nao wakaenda, wakalifanyia usalama kaburi kwa kutia muhuir jiweni na kuwaweka walinzi.