Neno La Bwana

Neno La Bwana Catholic spirituality, Readings, Reflections, Traditions and Music, News. Christ Day by Day πŸ™

15/08/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI*

*DOMINIKA YA ISHIRINI KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A*

*AGOSTI 16 2026*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANIπŸ’š*

*ANTIFONA YA KUINGIA*
Ee Mungu uliye ngao yetu, uangalie, utazame uso wa mpakwa wako. Kweli, siku moja katika nyua zako ni bora kuliko zingine elfu.

*KOLEKTA*
```Ee Mungu, umewaandalia wakupendao mema yasiyoonekana; uwashe mioyoni mwetu moto wa upendo wako, ili, kwa kukupenda wewe katika yote na kuliko yote, tuzifikie ahadi zako zinazopita hamu zote. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao....```

*MADA YA DOMINIKA*
```"KANISA KATOLIKI" LINAMAANISHA NINI?``

*SOMO LA KWANZA*
Isaya 56: 1, 6-7

_Nao wageni nitawaongoza mpaka mlima wangu mtakatifu_

*Somo katika kitabu cha Nabii Isaya*

Bwana asema hivi: "Shikeni sheria, tendeni haki, kwani wokovu wangu uko karibu kuja, na haki yangu iko karibu kufunuliwa. Nao wageni wanaoandamana na Bwana ili kumtumikia, na kulipenda jina la Bwana, -- kusudi wawe watumishi wake -- nao wote wanaotunza Sabato bila kuivunja, na kulishika agano langu, hao nitawaongoza mpaka mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala. Sadaka zao na matoleo yao vitakubaliwa juu ya altare yangu, kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote."

*Neno la Bwana*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 67: 2 - 3, 5, 6 na 8 (K. 4 )

*K. Watu na wakutukuze ee Mungu, watu wote na wakutukuze.*

Mungu na aturehemu na kutubariki;
Atuangazie uso wake. /Njia yake itambulike duniani,
Na wokovu wake katika mataifa yote..
*K*

Mataifa na wafurahi na kushangilia;
Kwa kuwa unawatawala kwa haki,
Na kuwaongoza mataifa ya dunia.
*K*

Watu na wakutukuze, ee Mungu;
Watu wote na wakutukuze!/ Mungu atatubariki sisi;
Na miisho yote ya dunia itamcha Mungu wetu.
*K*

*SOMO LA PILI*
Warumi 11: 13 -15, 29 - 32

_Kwa maana Mungu akiwajalia watu neema zake na kuwaita, hajuti tena._

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi*

Ndugu zangu: Ninyi watu wa mataifa, nawaambieni: Mimi niliye mtume wa watu wa mataifa, nakuza huduma yangu nikitumaini kuchochea wivu wa wenzangu wa damu moja, na hivyo kuwaokoa walau baadhi yao. Kwa kuwa kukataliwa kwao kumeiletea dunia upatanisho, kupokewa kwao kutazidi kuwa uzima baada ya kufa. Kwa maana Mungu akiwajalia watu neema zake na kuwaita,hajuti tena. K**a vile ninyi zamani mlivyomkaidi Mungu, sasa lakini mmesamehewa kutokana na ukaidi wao. Vivyo hivyo wale wamekaidi kwa ajili ya msamaha mliyojaliwa ninyi, ili sasa wao pia wasamehewe. Kwa maana Mungu amewatia wote katika ukaidi wao, ili awasamehe wote.

*Neno la Bwana*

*SHANGILIO LA INJILI*
Mathayo 4: 23

*Aleluya. Aleluya.*
Yesu alitangaza Injili ya ufalme akiponya kila namna ya magonjwa na maradhi kati ya watu.
*Aleluya*

*INJILI*
Mathayo 15: 21 - 28

_Mama, imani yako ni kubwa!_

✝️ *Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo*

Wakati ule: Yesu aliondoka huko akaenda sehemu za Tiro na Sidoni. Hapo Mwanamke Mkananayo alikuja kutoka eneo lile akaita kwa sauti kubwa, " unihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi. Binti yangu anasumbuliwa sana na pepo mbaya." Lakini hakumjibu neno, wafuasi wake Wakamwendea, wakamwomba wakisema, "Mwache aende zake, kwa maana anatufuata kwa kelele. " Akajibu, " Nimetumwa kwa kondoo wapotevu wa nyumba ya Israeli tu." Naye akaja,akamsujudia, akasema, " Bwana, unisaidie, " Akamjibu, " Si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. " Naye akasema, "Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo katika meza za Bwana wao." Hapo Yesu akajibu, akamwambia, "Mama, imani yako ni kubwa! Utendewe k**a utakavyo. " Tangu saa ile binti yake akawa mzima.

*Injili ya Bwana*

08/08/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI*

*DOMINIKA YA KUMI NA TISA KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A*

*AGOSTI 9 2026*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANI πŸ’š*

*MADA YA DOMINIKA*

```UDHIHIRISHO WA MUNGU NA UDHIHIRISHO WA KRISTO ```

*ANTIFONA YA KUINGIA: Zab 74:20,19,22,23*
Ee Bwana, uangalie agano, usiyasahau milele maisha ya watu wako walioonewa. Simama, ee Mungu, ukajitetee, usisahau kelele za washindani wako.

*KOLEKTA*
```Ee Mungu Mwenyezi wa milele, kwa kufundishwa na Roho Mtakatifu tunathubutu kukuita Baba; uikamilishe mioyoni mwetu roho ya kuwa wana,ili tustahili kuingia katika urithi tulioahidiwa. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao....```

*SOMO LA KWANZA*
1 Wafalme 19: 9a, 11 - 13a

_Ukasimame mlimani mbele ya Bwana_

*Somo katika kitabu cha kwanza cha Wafalme*

Siku zile: Eliya alifika [ Horebu, mlima wa Mungu], akaingia pango na kulala ndani yake. Hapo neno la Bwana likamjia. Bwana akamwambia: " Toka nje, ukasimame mlimani mbele ya Bwana "; na tazama, Bwana akapita. Upepo mwingi wenye nguvu ukaitikisa na kuipasua miamba, lakini Bwana hakuwapo katika upepo ule. Baada ya upepo,likaja tetemeko la nchi, lakini Bwana hakuwamo katika tetemeko lile la nchi; na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto,lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; baada ya moto, kukawa na sauti na upepo mtulivu. Eliya aliposikia sauti hiyo, akaufunika uso wake kwa nguo zake,akatoka na kusimama kwenye lango la pango.

*Neno la Bwana*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 85: 9ab -10, 11 - 12, 13 - 14( K. 😎

*K. Utuonyeshe wema wako, ee Bwana;*
*Utuletee wokovu wako.*

Ninasikia anayosema Bwana Mungu,
Hakika, anasema maneno ya amani.
Wokovu wake ni karibu nao wenye kumcha;
Utukufu wake utakaa katika nchi yetu.
*K*

Wema na uaminifu zitakutana;
/haki na amani zitabusiana.
Uaminifu utachipuka katika nchi;
Na haki itachungulia kutoka mbinguni.
*K*

Naye Bwana atatoa yaliyo mema,
Na nchi yetu itatoa mazao.
Haki itatangulia mbele ya Bwana,
Wokovu utafuata nyayo zake.
*K*

*SOMO LA PILI*
Warumi 9: 1 - 5

_Ningependa kulaaniwa k**a ingekuwa msaada kwa ndugu yangu_

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi*

Ndugu zangu: Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo. Shahidi wangu ni dhamiri yangu inayoongozwa na Roho Mtakatifu: nina huzuni nyingi, na moyo wangu una maumivu daima. Ningependa kulaaniwa na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu wenye damu moja nami k**a ingewafaa. Hao ni Waisraeli. Kwa hiyo wamejaliwa kuasiliwa, utukufu, agano, kupewa sheria, ibada na ahadi. Mababu ni wao, na hata Kristo ametokea kwao kadiri alivyo mwanadamu, ndiye yeye aliye juu ya yote, Mungu, na kutukuzwa milele. Amina.

*Neno la Bwana*

*SHANGILIO LA INJILI*
Zaburi 130:5

*_Aleluya. Aleluya._*
Ninamngoja Bwana, roho yangu inamngoja ,na ninalitumainia neno lake.
*_Aleluya._*

*INJILI*
Mathayo 14: 22 - 33

_Niamuru nije kwako juu ya maji_

✝️ *_Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo_*

[Baada ya watu kushiba,] Yesu aliwahimiza wafuasi wake wapande mashua na kumtangulia kuvuka hadi ng'ambo, yeye akiwaaga watu. Baada ya kuwaaga watu,alipanda mlimani peke yake kusali. Kukawa jioni, naye alikuwako huko peke yake. Wakati huo chombo kilikuwa maili kadhaa mbali na pwani, kikisongwa na mawimbi, kwa maana upepo ulikipiga. Wakati wa zamu ya nne ya usiku, aliwakaribia akitembea juu ya bahari. Wafuasi walipomwona anatembea baharini, walifadhaika ,wakasema, "Ni kivuli." Wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu akawaambia, "Tulieni, ni mimi msiogope." Petro akamjibu, akasema, "Bwana ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji." Naye akasema, " Njoo. " Petro akashuka mashuani,akamjongea Yesu akitembea juu ya maji. Lakini alipoona uvumi wa upepo, aliogopa, akaanza kuzama. Akapiga yowe, akaita, "Bwana, uniokoe." Mara Yesu akanyosha mkono, akamshika, akamwambia, "Ewe mwenye imani haba, Mbona uliona shaka?" Nao walipopanda chomboni, upepo ulitulia. Watu waliokuwa chomboni wakamsujudia, wakisema, "Hakika, wewe u Mwana wa Mungu."

*Injili ya Bwana*

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, AGOSTI 2, 2026**DOMINIKA YA KUMI NA NANE KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A**RANGI YA LITUR...
01/08/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, AGOSTI 2, 2026*

*DOMINIKA YA KUMI NA NANE KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANI πŸ’š*

*MADA YA DOMINIKA:*
```KRISTO ANATULIZA NJAA YETU.

*ANTIFONA YA KUINGIA: zab 70:2, 6*
Ee Mungu, uniopoe; ee Bwana, fanya haraka, unisaidie. Wewe ni msaada wangu na mwokozi wangu, ee Bwana, usikawie.

*KOLEKTA*
```Ee Bwana, uwe karibu na watumishi wako, na uwaonyeshe wema wako wa milele hao wakuombao; na kwa hao wanaojisifia kwamba wewe ndiwe Mwumba na mtawala wao, utengeneze upya vilivyoumbwa, na kuvihifadhi vilivyotengenezwa. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...```

*SOMO LA KWANZA*
Isaya 55:1-3

_Njoni mle._

*Somo katika kitabu cha Nabii Isaya*

Bwana asema hivi: "Enyi wote wenye kiu, njoni penye maji! Hata msipokuwa na fedha, njoni: njoni mnunue nafaka na kula: njoni mnywe divai na maziwa, bila fedha na bila kulipa. Kwa nini mnatoa fedha mpate kitu kisicho mkate, kwa nini mnatoa mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha? Nisikilizeni mimi, mtakula vitamu, na kufurahishwa kwa vyakula vitamu. Tegeni sikio, njoni kwangu; sikilizeni, na roho zenu zitaishi. Nitafanya nanyi agano la milele, nitasimika wema wa milele niliyomwahidia Daudi.'"

*Neno la Bwana.*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 145:8-9, 15-16, 17-18

*K. Wewe waufumbua mkono wako, ee Bwana, na kutushibisha.*

Bwana ni mwenye huruma na mpole,
si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili.
Bwana ni mwema kwa wote,
na huruma yake i juu ya viumbe vyake vyote.
*K.*

Macho ya wote yanakuelekea wewe;
nawe huwapa chakula chao wakati wake.
Wewe waufumbua mkono wako
na kukidhi hamu ya kila kilicho hai.
*K.*

Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote.
na mwema kwa kazi zake zote.
Bwana yu karibu na wote wakuitao,
wote wakuitao kwa uaminifu.
*K.*

*SOMO LA PILI*
Warumi 8:35, 37-39

_Hakuna kiumbe chochote kinachoweza kututenganisha na upendo wa Mungu uliomo katika Kristo Yesu._

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi*

Ndugu zangu: Ni nani anayeweza kututenga na upendo wa Kristo? Je, ni matatizo au shida, au dhuluma, au njaa, au kukosa nguo, au hatari, au upanga? Lakini katika mambo hayo yote twashinda kupita kiasi kwa msaada wake yeye anayetupenda. Kwa maana najua hakika kwamba wala mauti, wala uzima, wala malaika wenye enzi, wala wenye utawala, wala mambo ya sasa wala mambo yajayo, wala kimo wala kina, wala kiumbe chochote, hakiwezi kututenganisha na upendo wa Mungu uliomo katika Kristo Yesu, Bwana wetu.

*Neno la Bwana.*

*SHANGILIO LA INJILI*
Mathayo 4:4b

*Aleluya. Aleluya.*
Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo
kinywani mwa Mungu.
*Aleluya*

*INJILI*
Mathayo 14:13-21

_Wote wakala, wakashiba._

*+ Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo*

Wakati ule: Yesu aliposikia [kuhusu kifo chake Yohane Mbatizaji, alipanda mashua, akaondoka huko, akaenda mahali pa ukiwa ili awe peke yake. Watu walipopata habari, wakatoka mijini, wakamfuatia kwa miguu. Aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu. Akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao. Kulipokuchwa, wafuasi walimwendea, wakasema, "Mahali hapa ni pa ukiwa, na saa imepita. Afadhali uwaage umati huu, waende viijini kujinunulia chakula." Lakini Yesu akawaambia, Hawana sababu ya kwenda. Wapeni ninyi chakula." Wakamjibu, Hapa hatuna kitu ila mikate mitano na samaki wawili." Akasema, "Nileteeni hapa." Akishawaamuru watu kuketi kwenye majani, akaitwaa mikate mitano na samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akashukuru, akaimega, akawapa wafuasi mikate, na wakawapa watu. Wote wakala, wakashiba. Wakayaokota makombo ya mikate yaliyosalia, yakajaa vikapu kumi na viwili. Nao waliokula walikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuwahesabu wanawake na watoto.

*Injili ya Bwana.*

✝️WHY DOES THE BISHOP REMOVE HIS ZUCCETTO DURING THE EUCHARISTIC PRAYER__________________If you have ever watched a bish...
27/07/2026

✝️WHY DOES THE BISHOP REMOVE HIS ZUCCETTO DURING THE EUCHARISTIC PRAYER
__________________
If you have ever watched a bishop celebrate Mass, you may have noticed something curious:

He wears his purple zucchetto (skullcap)…
until the Eucharistic Prayer begins.

Then suddenly,
he removes it
and keeps his head bare
until after Communion.

Many Catholics see this every Sunday
but do not know why.

The real reason is beautiful, ancient, and deeply theological.

Let’s break it down.

✝️1. BECAUSE NO ONE β€œCOVERS HIS HEAD” BEFORE THE REAL PRESENCE

By ancient Christian tradition,
no cleric, bishop, priest, or deacon,
may cover his head
before the Eucharistic Mystery.

Once the Eucharistic Prayer begins,
the bread and wine are being prepared
to become the Body and Blood of Christ.

Every head must be uncovered
as a sign of:

humility,

reverence,

and total submission before God.

The zucchetto is a sign of office…
but the Eucharist is the presence of God Himself.

Office bows before Sacrament.

✝️2. BECAUSE AT THIS MOMENT THE BISHOP IS NO LONGER β€œLEADER”—HE IS β€œSERVANT AT THE ALTAR”

Wearing the zucchetto shows:

dignity of office,

authority,

responsibility as shepherd.

But during the Eucharistic Prayer,
the bishop stands at the altar
not as a ruler,
but as a servant of the Mystery.

He removes the sign of authority
to show that HE is now being overshadowed
by the One he represents.

It is a silent declaration:

β€œThis is no longer about me.
Only Christ is acting now.”

✝️3. BECAUSE CHRIST THE HIGH PRIEST IS NOW TAKING OVER

During the Eucharistic Prayer,
the priest or bishop is not merely prayingβ€”
he is acting in persona Christi,
in the very place of Jesus.

At this point, the bishop sets aside the zucchetto
because Christ the High Priest
is now the invisible celebrant.

The Church teaches:
At the altar, the bishop disappears
so that Christ may be seen.

The uncovered head shows:

surrender,

obedience,

and the overshadowing of human authority
by divine authority.

✝

24/07/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, JULAI 26, 2026*

*DOMINIKA YA KUMI NA SABA KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANIπŸ’š*
*ROZARI πŸ“Ώ: MATENDO YA UTUKUFU*

*MADA YA DOMINIKA.*
```UJASIRI

*ANTIFONIA YA KUINGIA.*
_Zab 68:6-7.36_
_Mungu yu katika makao yake matakatifu; walio pweke,Mungu huwapatia boma; yeye huwapa watu wake uwezo na nguvu._

*KOLEKTA.*
```Ee Mungu, wewe ndiwe ngao yao wote wanaokukimbilia, pasipo wewe hapana kilicho dhabiti wala kitakatifu; utuzidishie rehema yako, ili kwa mamlaka na maongozi yako, tupate kuzitumia mali za muda huu kwa namna inayotuwezesha kuambatana na zile zinazodumu milele. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao....```

*SOMO LA KWANZA.*
1 Wafalme 3: 5, 7 - 12.

_Umeomba hekima._

*Somo katika kitabu cha kwanza cha Wafalme.*

Siku zile: Bwana alimtokea Sulemani katika ndoto. Mungu akamwambia: "omba kitu utakacho nikupe." Sulemani akajibu, "Ee Bwana Mungu wangu, umenifanya mimi mtumishi wako kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yangu; ila mimi ni kijana tu, sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia. Naye mtumishi wako yupo katikati ya taifa lako uliloliteua, taifa la watu wengi wasioweza kuhesabika, wala jumla yao kufahamiwa kwa sababu ni wengi mno. Basi umpe mtumishi wako moyo wa hekima nipate kuwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya. Maana ni nani awezaye kuwatawala hawa watu wako walio wengi hivi?" Bwana akapendezwa na ombi hili la Sulemani. Mungu akamwambia: "kwa kuwa umeomba jambo hili-- wala hukujitakia maisha marefu, wala hukujitakia utajiri, wala hukuomba roho za adui zako-- bali umeomba hekima ya kujua kuhukumu - basi, tazama, ninatenda k**a ulivyosema. Ninakupa moyo wa hekima na akili, hata kabla yako hakupatikana mtu k**a wewe, na wala baada yako hatainuka mtu k**a wewe."

*Neno la Bwana.*

*ZABURI YA KUITIKIZANA.*
Zab 119: 57 na 72, 76-77, 127-128, 129-130( *K* 97a)

*K. Jinsi gani naipenda sheria yako, ee Bwana!*

Nimesema, ee Bwana, u sehemu yangu;
Naahidi kushika maneno yako.
Sheria ya kinywa chako ina thamani kwangu zaidi
Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.
*(K)*

Wema wako unifariji,
Sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
Rehema zako zinifikie nipate kuishi,
Kwani sheria yako ni furaha yangu.
*(K)*

Ndiyo maana nayapenda maagizo yako,
Kuliko dhahabu, hata dhahabu safi.
Na kwa sababu naziona amri zako zote kuwa adili;
Naichukia kila njia potovu.
*(K)*

Mafundisho yako ni ya ajabu;
Ndiyo maana roho yangu inayashika.
Ufafanuzi wa maneno yako huleta mwanga,
Huwapa ufahamu wajinga.
*(K)*

*SOMO LA PILI.*
Warumi 8: 28 - 30.

_Alituchagua toka mwanzo ili kutulinganisha na sura ya mwana wake._

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi.*

Ndugu zangu: twajua ya kuwa wale wampendao Mungu hufanikiwa yote, ndio wale walioitwa toka mwanzo katika azimio lake. Maana wale aliowajua toka mwanzo, aliwachagua toka mwanzo ili kuwalinganisha na sura ya mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua toka mwanzo aliwaita ; nao aliowaita aliwapa uadilifu; nao walioadilishwa aliwapa pia utukufu wa mbinguni.

*Neno la Bwana.*

*SHANGILIO LA INJILI.*
Mathayo 11:25.

*Aleluya, Aleluya.*

Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewafunulia watoto wadogo mafumbo ya ufalme wako.
*Aleluya.*

*INJILI.*
Mathayo 13: 44 - 52.

_Akauza mali yake yote akalinunua lile shamba._

✝️ *Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo.*

*β˜†* Wakati ule: Yesu aliuambia umati: "Ufalme wa mbingu umefanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu alipoigundua, aliificha tena, kwa furaha juu yake akaenda, akauza mali yake yote, akalinunua lile shamba. Tena Ufalme wa mbingu umefanana na mfanya biashara atafutaye lulu nzuri. Alipoiona moja ya thamani kubwa, alikwenda, akauza mali yake yote, akainunua.*β˜†* Tena Ufalme wa mbingu umefanana na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina. Ulipojaa, [wavuvi] waliuvuta pwani, wakaketi, wakawakusanya Samaki wazuri katika vyombo, bali wabovu waliwatupa. Ndivyo itakavyokuwa mwisho wa dunia. Malaika watakwenda kuwatenga waovu na waadilifu. Wakiwatupa waovu katika tanuri ya moto. Humo mtakuwamo kulia na kusaga meno. Mmeelewa hayo yote?" Wakamwambia, " "Ndiyo, tumeelewa." Akajibu, "Kwa hiyo kila mwandishi apataye kuwa mfuasi wa ufalme wa mbingu anafanana na mkuu wa familia atoaye mapya na ya kale katika hazina yake."

*Injili ya Bwana.*

_Somo fupi:Mathayo 13: 44- 46. Soma kati ya *β˜†*_

23/07/2026

πŸ“– *Masomo ya Misa
(Ijumaa, Julai 24, 2026)*

*Somo la kwanza*
Yer 3:14–17
Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; maana mimi ni mume wenu; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni; nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu. Kisha itakuwa mtakapoongezeka na kuwa wengi katika nchi hiyo, asema Bwana, siku zile hawatasema tena, Sanduku la agano la Bwana; wala halitaingia moyoni; wala hayatafanyika hayo tena. Wakati ule watauita Yerusalemu kiti cha enzi cha Bwana; na mataifa yote watakusanyika huko Yerusalemu, kwa ajili ya jina la Bwana; wala hawatakwenda tena kwa ukaidi wa moyo wao mbaya.

*Wimbo wa Katikati*
Yer 31:10–13
Lisikieni neno la Bwana, enyi mataifa,
Litangazeni visiwani mbali,
Mkaseme: Aliyemtawanya Israeli atamkusanya,
Na kumlinda k**a mchungaji alindavyo kundi lake.
(K) Bwana anatulinda k**a mchungaji alindavyo kundi lake.

Kwa maana Bwana amemweka huru Yakobo,
Amemkomboa mkononi mwake aliyekuwa hodari kuliko yeye.
Nao watakuja na kuimba katika mlima Sayuni,
Wataukimbilia wema wa Bwana, nafaka, na divai,
Na mafuta, na wachanga wa kondoo na wa ng’ombe.
(K) Bwana anatulinda k**a mchungaji alindavyo kundi lake.

Ndipo bikira atafurahi katika kucheza,
Na vijana na wazee pamoja,
Maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha,
Nami nitawafariji
Na kuwafurahisha waache huzuni yao.
(K) Bwana anatulinda k**a mchungaji alindavyo kundi lake.

*Shangilio*
Mt 11:25
Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya.

*Injili*
Mt 13:18–23
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi. Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia. Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea mara kwa furaha; lakini hana mizizi ndani yake bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa, naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai. Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.

21/07/2026

MASOMO YA MISA, SIKUKUU YA MTAKATIFU MARIA MAGDALENA, JULAI 22, 2026
RANGI YA KILITURJIA: NYEUPE 🀍

SOMO LA KWANZA
WIMBO ULIO BORA 3:1β€”4a

"Nilipata kumwona mpendwa wa moyo wangu."

Somo katika Wimbo ulio Bora

Bibi harusi anasema: Usiku nilipokuwa nimelala kitandani, nilimtafuta mpendwa wa moyo wangu β€” nilimtafuta, sikumpata. "Basi, nitaondoka, nitazunguka mjini, katika njia na viwanja nimtafute mpendwa wa moyo wangu." Nilimtafuta na sikumpata. Nikakutana na walinzi, waliouzunguka mji. "Je, mmepata kumwona yule mpendwa wa moyo wangu?" Nilipokuwa nimewaacha kitambo kidogo, nikapata kumwona mpendwa wa moyo wangu.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

au somo lifuatalo:

SOMO LA KWANZA
2 WAKORINTHO 5:14β€”17

Hatumtambui tena Kristo kwa kadiri ya ubinadamu wake peke yake.

Somo katika barua ya pili ya Mtakatifu Paulo kwa Wakorintho

Ndugu: Upendo wa Kristo unatusonga tuking'amua: mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi wote wamekufa. Naam, alikufa kwa ajili ya wote, kusudi wenye kuishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali waishi kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka. Kwa hiyo, kutoka sasa hatuwajui watu kadiri ya ubinadamu wao tu. Zamani tulimwona hata Kristo katika utu wake tu. Lakini sasa maoni yetu ni tofauti. Basi, mtu akiwa katika Kristo ni kiumbe kipya. Ya kale yamepita, mapya yamefika.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 63:2, 3β€”4, 5β€”6, 8β€”9 (K. 2b)

K. Roho yangu inakuonea kiu, ee Bwana, Mungu wangu.

Ee Mungu, Mungu wangu, ninakutafuta kwa dhati!
Roho yangu inakuonea kiu;
mwili wangu unakuonea shauku,
k**a nchi kavu, yenye kiu, isiyo na maji. K.

Hivyo nilikutazama katika patakatifu,,
nione enzi yako na utukufu wako.
Fadhili zako ni bora kuliko maisha;
kwa hiyo midomo yangu itakutukuza! K.

Nitakusifu ningali hai;
kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
Roho yangu itakinai k**a kwa kushiba mafuta na vinono,
kwa midomo ya furaha, kinywa changu kitakusifu! K.

SHANGILIO LA INJILI

K. Aleluya. W. Aleluya.
K. Utuambie Maria, uliona nini njiani. Niliona kaburi la Kristo aliye hai na utukufu wake Yeye aliyefufuka.
W. Aleluya.

SOMO LA INJILI
YOHANE 20:1β€”2, 11β€”18

"Mwanamke, unalia nini? Unamtafuta nani?"

† Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Yohane

Siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalena alifika kwenye kaburi asubuhi sana, kungali giza bado, na akaliona jiwe limeondoshwa kaburini. Basi akapiga mbio, akafika kwa Simoni Petro na yule mfuasi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, "Wamemwondoa Bwana kaburini, na sisi hatujui walikomweka." Maria alisimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi akaona malaika wawili, wamevaa mavazi meupe, wameketi mahali palipolazwa kwanza mwili wa Yesu, mmoja alikaa kichwani na mmoja miguuni. Nao wakamwambia, "Mwanamke, unalia nini?" Akawaambia, "Kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, nami sijui walikomweka. "Baada ya maneno hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama huko, lakini hakutambua ya kuwa ni Yesu. Yesu akamwambia, "Mwanamke, unalia nini? Unamtafuta nani?" Naye akadhani ni mtunza bustani, akamwambia, "Bwana, k**a ni wewe uliyemwondoa, uniambie ulipomweka, nami nitamchukua." Yesu akamwambia, "Maria!" Naye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, "Rabbouni," maana yake mwalimu wangu. Yesu akamwambia, "Usinishike, kwa maana sijapaa bado kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu, ukawaambie, 'Ninapaa juu kwa Baba yangu na Baba yenu, kwa Mungu wangu na Mungu wenu.'" Maria Magdalena akaenda, akawapasha wafuasi habari, "Nimemwona Bwana," na yale aliyomwambia.

INJILI YA BWANA... SIFA KWAKO EE KRISTO

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, JULAI 19, 2026* *DOMINIKA YA KUMI NA SITA KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A*  *RANGI YA LI...
18/07/2026

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, JULAI 19, 2026*

*DOMINIKA YA KUMI NA SITA KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA A*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANI πŸ’š*
*ROZARI πŸ“Ώ: MATENDO YA UTUKUFU*

*MADA YA DOMINIKA*
```UVUMILIVU WA MUNGU NA UKOSEFU WETU WA UVUMILIVU```

*_Sisi kiasili hujitenga wenyewe katika wema na ubaya, marafiki na maadui. Matokeo ya tofauti hiyo ni kukosa Uvumilivu na kuwa na tamaa ya kutatua mara moja mvutano wowote unaotokea kutokana na hayo. Wengine humwomba Mungu aingilie kati ili awahukumu na kuwaadhibu wengine. Masomo ya leo yanatuambia kuwa Mungu hafanyi mambo k**a hayo. Somo la Kwanza linatufundisha kuwa yeye hutumia nguvu zake sio kutuadhibu bali kutuokoa; anataka sisi sote tufanye vivyo hivyo. Injili inatuambia kuwa tukubali kwa akili tulivu na amani uwepo wa uovu ulimwenguni, na inatualika kutambua magugu mioyoni mwetu. Inatuhakikishia kwamba siku moja upendo wa Mungu utauangamiza. Somo la pili linazungumzia juu ya Roho anayetuombea, akimsihi Baba aondoe uovu wote. Hakika sala hii itasikika._*

*ANTIFONIA YA KUINGIA*
_Tazama, Mungu ananisaidia, Bwana ananitegemeza mimi. Kwa moyo mkujufu nitakutolea sadaka, nitalisifu jina lako, ee Bwana, maana ni jema._

*KOLEKTA*
```Ee Bwana, uwabariki watumishi wako, na uwaongezee kwa huruma vipaji vya neema yako, ili wakiwa na ari katika matumaini, imani na mapendo, wadumu daima katika kuzishika kiaminifu amri zako. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...```

*SOMO LA KWANZA*
Hekima ya Sulemani. 12 :13.16-19

_Nawe huwajalia kutubu juu ya dhambi zao._

*Somo katika kitabu cha Hekima ya Sulemani*

Hakuna Mungu mwingine ila Wewe, ambaye unavijali vitu vyote, hata utakiwe kumwonyesha kwamba hukuhukumu pasipo haki; maana, nguvu zako ni chanzo cha haki; na utawala wako juu ya vyote, unakufanya uwe ukivuhurumia vyote. Naam, huwaonyesha nguvu wasiouamini uwezo wako mkamilifu; na kuulaumu ujasiri wao waujuao. Lakini wewe, mtawala wa nguvu, ukuhukumu kwa upole, na kutuongoza kwa huruma nyingi; maana uwezo unao wa kutenda utakalo wakati wowote. Kwa njia ya kutenda hivyo, uliwafundisha watu wako, kwamba mtu mwenye haki lazima awe mpenda watu; nawe ukawafanya watoto wako kuwa na tumaini jema, kwa sababu huwajalia kutubu juu ya dhambi zao.

*Neno la Bwana*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 86: 5 - 6, 9 - 10, 15 - 16a (K. 5a )

*K. Wewe, ee Bwana, ni mwema na mwenye huruma.*

Wewe, ee Bwana, ni mwema na mpole,
Umejaa huruma kwa wote wanaokuomba.
Usikie, ee Bwana, sala yangu;
Uielekee sauti ya maombi yangu.
*(K)*

Mataifa yote uliyofanya watakuja, ee Bwana,
Watakuabudu wewe, watalitukuza jina lako.
Kwani wewe ni mkuu na mfanya miujiza;
Ndiwe Mungu peke yako.
*(K)*

Lakini Wewe, ee Bwana,
Ni Mungu mwenye huruma na mpole,
Mvumilivu, mwenye wema na uaminifu mwingi.
Unielekezee macho, unihurumie.
*(K)*

*SOMO LA PILI*
Warumi 8 : 26 - 27

_Roho mwenye anatuombea kwa maombi yasiyosemeka._

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi*

Ndugu zangu: Roho anasaidia udhaifu wetu. Hatujui jinsi inavyotubidi kuomba. Roho mwenyewe anatuombea sisi kwa maombi yasiyosemeka. Lakini Mungu achunguzaye mioyo ajua nia ya Roho anayewaombea watakatifu kwa Mungu.

*Neno la Bwana*

*SHANGILIO LA INJILI*
Mathayo 11: 25

*Aleluya. Aleluya.*
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewafunulia watoto wadogo mafumbo ya ufalme.
*Aleluya.*

*INJILI*
Mathayo. 13: 24 - 43

_Acheni mbegu zote mbili zikue pamoja mpaka wakati wa mavuno._

✝️ *Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo*

*β˜†* Wakati ule: Yesu aliwasimulia mfano mwingine akisema, "Ufalme wa mbingu umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika shamba lake. Lakini watu walipolala usingizi, adui yake akaja, akapanda magugu kati ya ngano, akaenda zake. Miche ilipomea na kuchanua, magugu pia yakaonekana. Hapo watumishi wa mwenye shamba wakamwendea na kumwambia, 'Bwana, hukupanda mbegu njema katika shamba lako? Basi limepataje magugu?' Akawaambia, 'Adui amefanya haya.' Watumishi wakamwuliza , 'Je, wataka twende tukayakusanye?' Akasema, 'La, sivyo, msije mkang’oa ngano pamoja na magugu mnayotaka kukusanya. Acheni mbegu zote mbili zikue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Na wakati wa mavuno, nitawaambia wavunaji, "Kusanyeni kwanza magugu, mkayafunge matita matita na kuyachoma moto. Na kisha hapo kusanyeni ngano ghalani mwangu.'" *β˜†* Akawasimulia mfano mwingine akisema, :Ufalme wa mbingu umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake. Nayo ni ndogo kuliko mbegu zote. Lakini ikiisha kumea huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata ndege wa angani huja na kukaa katika matawi yake." Akawaambia mfano mwingine: "Ufalme wa mbingu umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaichanganya na pishi tatu za unga, hata wote ukachacha. Hayo yote Yesu aliyasema kwa makundi ya watu kwa mifano. Pasipo mifano hakusema nao. Ilikuwa hivyo ili litimie lile lililosemwa na nabii, "Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, nitatangaza yaliyofichika tangu mwanzo wa dunia." Kisha Yesu akayaaga makundi ya watu, akaenda nyumbani. Huko wafuasi wake wakamwendea, wakasema, "Tufafanulie ule mfano wa magugu ya shambani." Akajibu akisema, "Mtu apandaye mbegu njema ni Mwana wa Mtu. Shamba ni dunia. Mbegu njema ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa mwovu. Adui aliyeyapanda ni Shetani. Mavuno ni mwisho wa dunia. Wavunaji ni malaika. Basi, k**a magugu yanavyokusanywa na kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwisho wa dunia. Mwana wa Mtu atawatuma malaika wake. Nao watakusanya katika ufalme wake makwazo yote, na watenda maovu, na kuwa-tupa katika tanuru ya moto. Humo mtakuwamo kulia na kusaga meno. Hapo waadilifu watang’aa k**a jua katika ufalme wa Baba yao. Aliye na masikio, na asikie."

*Injili ya Bwana*

Address

Nairobi
Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno La Bwana posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Neno La Bwana:

Shortcuts

Share