07/08/2022
SOMO: MLINZI WA MJI
*UTANGULIZI*
• Kila mji una mlizi na kila mji una mamlaka yake
• katika ulimwengu wa roho kunakua kuna ukuta wa kuingia mkoa fulani mfano Arusha ina malango yake ya kuingia na kutoka Arusha na malango hayo yanakua na walinzi wake
• kila mlinzi wa mjui kuna vitu anataka mji uwe vipi au mkoa uwe vipi eitha kielimu/kiuchumi/kiafya n.k mfano mlinzi wa mji anaweza akaamua mji fulani uwe na wasomi kiasi gani na hali yao ya uchumi ikae vipi
• walinzi wa mji wanaweza wakakaa ndani ya baba/mama au mlezi ili kuilinda familia yake au uzao wake usitoke hata k**a kwenye familia kuna mtoto wa k**e na wakiume ambae umri wake umefika wa kuoa au kuolewa lakini bado yupo nyumbani na hana sababu yoyote.
zaburi 127:1 imeandikwa “1 Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure.
• nyumba inajengwa na mji unalindwa
• ikiwa Mungu hausiki kwenye ujenzi wako anaelinda inakua ni bure, hivyo basi kwenye nyumba yako Mungu anatakiwa awe mlinzi mkuu
isaya 21:8 imeandikwa “8 Ndipo akalia k**a simba, Ee Bwana, mimi nasimama daima juu ya mnara wakati wa mchana, na kila usiku ninakaa katika zamu ya ulinzi wangu.
Mwanzo 19:1 imeandikwa “1 Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi.
2 Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha.
3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala.
4 Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote.
5 Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua.
6 Lutu akawatokea mlangoni, akafunga mlango nyuma yake.
7 Akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi.
8 Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu mume, nawasihi nitawatolea kwenu mkawafanyie vilivyo vyema machoni penu, ila watu hawa msiwatende neno, kwa kuwa wamekuja chini ya dari yangu.
9 Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango.
10 Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango.
11 Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango.
12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa;
13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za Bwana; naye Bwana ametupeleka tupaharibu.
14 Lutu akatoka akasema na wakweze, waliowaposa binti zake, akasema, Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu Bwana atauharibu mji huu. Lakini akawa k**a achezaye machoni pa wakweze.
• Lutu alikua na kuhani wake ambae ni ibrahimu
• Kuna vitu vinatokea ila hatujui k**a Mungu ndo kasababisha vitokee
• Kuna namna unapoingia kwenye mji wale wenyeji wanaweza wakawahi kukumiliki na kukufanya vile watakavyo
• Ili uweze kufanikiwa kwenye mji uliohamia lazima uwamilki wao kwanza
Mathayo 12:29 imeandikwa “29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake.
• Mwenye nguvu akiweza kukuteka anaweza akauza kila ulichonacho mfano anaweza akauza akili/ mikono ya biashara au nyota ya biashara sasa ili kuweza kurudisha vitu hivyo lazima uwe na nguvu za kuuteka mji huo
Marko 3:27 imeandikwa “27 Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.
• Mtu hawezi kuingia kwenye nyumba ya mtu bila kumteka Yule alindaye mji
Luka 11:21-22 imeandikwa “21 Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama;
22 lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyang'anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea, na kuyagawanya mateka yake.
• Mtu anaweza kua na nguvu lakini asilinde pia anaweza akawa na silaha lakini asilinde na kumpa nafasi adui ya kumshambulia
UKIRI
Bwana Yesu ninakushukurun kwa ajiliya siku ya leo ambayo bwana umeifanya kwa kusudi lako na utukufu wako maana umeikusudia siku hii mimi na watu wa nyumbani mwangu nishiriki ibada hii ni nikaisikia sauti yako maana leo ni siku ya tofauti kwangu maana umenipa neema ya kulisikia neno lako kwa habari ya walizi wa mji na namna wanavyofanya kazi leo Bwana umeniweka mimi ili niwe baraka kwa wengine kupitia vitu ambavyo nimevitoa kwa ajili ya wengine maana Mungu umesema nikimvika mtu asie na mavazi nawe utanivika mimi asante mungu kwa ajili ya kibari chako ambacho umekiachilia kwangu.Bwana Yesu leo ninakuja mbele zako nianafanya vita na kila walinzi wa kipepo waliosimama kwenye mji wangu kwa mamlaka ya jina la Yesu leo ninawaamuru kila walinzi waliotumwa kulinda mji wangu teketea kwa jina la Yesu wachawi wote wasoma nyota wote waganga washirikina waliowatuma walinzi ili kuilinda hatua yangu, elimu yangu biashara yangu leo ninawateketeza wote kwa moto ulao. Leo ninawapiga walinzi wa mji wote imeandikwa “mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama;
leo natangaza mimi ni mwenye nguvu zaidi yao na mimi ni mtawala na mmiliki maana nmepewa neema nimiliki na nitawale na chochote walichoiba wakauza hazina na mafanikio leo wanaachia kwa damu Yesu leo kila ngome ya wakuu wa mji walionishikilia na kunifunga kwa nmna yoyote leo napiga ngome yao kwa jina la Yesu na kila ngome iliozuia huduma na mafanikio yangu leo ninaibomoa sasa hivi kwa damu ya Yesu kila walinzi wa mtaa wanaolinda hatma yangu maana wamejua Mungu ameweka nini ndani yangu leo ninawateketeza kwa jina la Yesu. kila waliponishikilia leo wananiachia kwa mamlaka ya jina la Yesu. Ewe mlinzi ulieshikilia hatma yangu na mafanikio yangu ninakuteketeza kwa jina la Yesu. Leo Bwana ninaifungua mipaka yangu ya kumiliki na kutawala kwa jina Yesu na leo ninamshambulia yule mlinzi wa mji alietumwa ili kuilinda hatma yangu na leo naweka ulinzi mkali kwenye mipaka ya mji wangu na Mipaka ya watu wa nyumbani mwangu kwa jina la Yesu .