09/09/2020
Ezekiel 18:14- 19 “Na k**a yeye huyo akizaa mwana, naye ameona dhambi zote za Baba yake alizozitenda, akaogopa, asifanye neno lolote k**a hayo. Hakula juu ya milima wala hakuviinulia macho vinyago vya nyumba ya Israeli wala hakumtia najisi wa jirani yake wala hakumdhulumu mtu wala hakutwaa kitu kiwekwe rehani wala hakumnyanganya mtu mali yake kwa nguvu bali amewapa wenye njaa chakula chake, na kuwafunuka nguo walio uchi”
Ni kweli Baba zetu walitenda uovu lakini tumetambua na kuukimbia uovu na utumishi wetu utaishi na uhai utatangazwa. Uhai wako na uhai wa maisha yako utatangazwa juu yako maana umeijua sheria ya Mungu.
Sasa ili kutoka kwenye utumwa wa nchi na utumwa wa nyumba ya Baba yako kuna kutoka na hapo ndipo kunako kutoka katika utumwa wa nchi. Mwanzo 12:1 Sasa anza kuomba kutoka katika utumwa wa nchi au kijiji ukitoka omba kutoka katika utmwa wa nyumba ya baba yako kisha ombkuijua sheria ya Bwana.
Warumi 8:15 “kwakuwa hamkukmpokea tena Roho wa utumwa wa utumwa iletayo hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hio twalia, Aba, Yaani Baba”
Tunapopiga hizi roho za utumwa wa nchi pamoja na utumwa wa nyumba ya Baba yako pia omba kupokea roho ya Baba.
1samwel 16:12-15
Basi akatuma, naye akamleta kwao, naye alikuwa mwekundu mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza, Bwana akasema, ondoka, umtuie nmafuta; maana huyu ndiye”
Sasa roho ya Baba ilitoka kwa samweli na kuwa juu yake na leo roho ya baba inaenda na mtu mmoja kwa maana mafuta katika pembe yalimiminika juu yangu nami leo naiachilia juu yako.