Kkkt_umojawavijana

Kkkt_umojawavijana Ni kundi la Umoja wa vijana KKKT Taifa lenye lengo la kupeana taarifa mbalimbali za vijana ndani ya

13/05/2026

Disemba 17, 2024 Mwenyekiti wa Vijana KKKT Bw. Anania J. Ndondole alitembelea Wilaya ya Kilwa(Mkoa wa Lindi) iliyopo katika Dayosisi ya Kusini Mashariki kwaajili ya kuangalia kazi kubwa iliyofanyika katika ujereshaji wa misitu ya mikoko (Restoration ya Mangrove Forests).

Video hii akielezea kazi kubwa iliyofanyika katika mradi huo ambao Dawati la Vijana KKKT iliuandaa kwa kushirikiana na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani ambao walifadhili mradi huo.

KKKT imekuwa mstari wa mbele katika utunzaji wa mazingira na kukabiliana na changamoto ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa.

Video hii ilirekodiwa na Bw. ambaye alikuwa ndiye mratibishaji wa program hiyo.

12/05/2026

Sehemu ya Salamu za Katibu Mkuu wa KKKT Bw. Rogath Mollel kwa washarika wa Dayosisi ya Magharibi Kati-Tabora.

Agusia Katiba ya KKKT, KKKT Digital na Fursa kwa Vijana kuhusu teknolojia.

Vijana VijanaKKKT Dayosisi ya Mwanga baada ya kuhitimisha Semina ya Viongozi wa Vijana kutoka katika madhehebu mbalimbal...
12/05/2026

Vijana Vijana

KKKT Dayosisi ya Mwanga baada ya kuhitimisha Semina ya Viongozi wa Vijana kutoka katika madhehebu mbalimbali.

Picha ya Pamoja ya Viongozi wa Vijana walioshiriki Semina ya Viongozi iliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi za KKKT Dayosi...
12/05/2026

Picha ya Pamoja ya Viongozi wa Vijana walioshiriki Semina ya Viongozi iliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi za KKKT Dayosisi ya Mwanga.
Katika picha hii alikuwepo pia Mwenyekiti wa Vijana KKKT na Mratibu wa Vijana KKKT .frank_mexon

Naibu Katibu Mkuu Huduma za Jamii na Mkurugenzi wa Afya KKKT Dkt. Paul Mmbando akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada y...
11/05/2026

Naibu Katibu Mkuu Huduma za Jamii na Mkurugenzi wa Afya KKKT Dkt. Paul Mmbando akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya kuwahudumia watu wenye magonjwa ya kusendeka inayofanyika kwa siku tatu jijini Arusha.

Washiriki wa mafunzo hayo ni Madaktari, wauguzi, wafamasia, maafisa ustawi wa jamii n.k wanaotokea katika Hospitali na vituo vya Afya vya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).

Source: elcthq

Morning Family...[26]...Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.(Yohana 12:26)*Mafafanuzi:* Yesu Kristo Katika aya hii; ...
11/05/2026

Morning Family...
[26]...Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
(Yohana 12:26)

*Mafafanuzi:* Yesu Kristo Katika aya hii; anatoa wajibu wa kumfuata kwanza Yeye; kisha heshima kwa Yeyote atakaye mtumikia.

Kila mtu amewekwa kutumika mahali. Popote ulipo; wewe ni mtumishi wa Mungu.

Tumika kwa moyo, bidii na unyenyekevu wote. Gusa mioyo ya watu kwa utumishi wako; na Mungu atakubariki sana.

Ikiwa ni Mtumishi wa Madhabahuni; Mwalimu, Daktari, Mwanasheria, Askari, Mfanya biashara, Mzee wa Kanisa au yeyote yule.

Ulimwengu hauwezi kukulipa ipasavyo; Mungu ndiye ajuaye.

Heshima na malipo ya Mungu hayataishia kwako tu; bali kwa kizazi chako chote.

Usichoke; tumika kwa uaminifu wote.

Nikutakie Jumatatu njema na Ubarikiwe.

Rev. Frank Kimambo
*KKKT-DMP*

Mkuu wa KKKT Baba Askofu Dkt Alex Gehaz Malasusa akiwa pamoja na ugeni kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Bavaria (U...
11/05/2026

Mkuu wa KKKT Baba Askofu Dkt Alex Gehaz Malasusa akiwa pamoja na ugeni kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Bavaria (Ujerumani) pamoja na Maaskofu na Viongozi wa Makanisa ya Kilutheri kutoka nchi za Kenya, Liberia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Msumbiji. Ni katika Mkutano uliofanyika nchini Tanzania na kukutanisha Makanisa rafiki na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Bavaria (KKKB)

KKKT ina urafiki wa muda mrefu na KKKB.

11/05/2026

"Wewe kijana uufurahie ujana wako..."

Mratibu wa Vijana KKKT .frank_mexon akisoma neno la Mungu mbele ya Vijana wa Usharika wa Kanisa Kuu-Dayosisi ya Mwanga mara baada ya Ibada ya pili.

Mchezo wa Draft Vijana wakicheza. Ni katika Centre ya Vijana KKKT Dayosisi ya Mwanga. Mwenyekiti wa Vijana KKKT na kijan...
11/05/2026

Mchezo wa Draft Vijana wakicheza. Ni katika Centre ya Vijana KKKT Dayosisi ya Mwanga. Mwenyekiti wa Vijana KKKT na kijana wake

Mwenyekiti wa Vijana KKKT Dayosisi ya Mwanga Bw. Joseph Mrutu akiongea na Washarika katika Ibada ya Usharika wa Kanisa K...
10/05/2026

Mwenyekiti wa Vijana KKKT Dayosisi ya Mwanga Bw. Joseph Mrutu akiongea na Washarika katika Ibada ya Usharika wa Kanisa Kuu Mwanga.

Aidha, aliwakaribisha pia M/kiti na Mratibu wa Vijana KKKT ambao nao walishiriki Ibada hiyo.

Bw. Joseph Mrutu pia ni Diwani na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga.

Semina Maalumu  ya Vijana KKKT Usharika wa Nakapanya.Ni tarehe 15 Juni 2026
10/05/2026

Semina Maalumu ya Vijana KKKT Usharika wa Nakapanya.

Ni tarehe 15 Juni 2026

Address

Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kkkt_umojawavijana posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kkkt_umojawavijana:

Share