Kkkt_umojawavijana

Kkkt_umojawavijana Ni kundi la Umoja wa vijana KKKT Taifa lenye lengo la kupeana taarifa mbalimbali za vijana ndani ya

Mratibu wa Vijana KKKT Mchg Frank Mexon Mng'ong'o amewakilisha ujumbe wa Vijana kutoka KKKT wanaoshiriki Maadhimisho ya ...
12/08/2026

Mratibu wa Vijana KKKT Mchg Frank Mexon Mng'ong'o amewakilisha ujumbe wa Vijana kutoka KKKT wanaoshiriki Maadhimisho ya Siku ya Vijana Kitamaifa ambayo kwa Tanzania inaadhimishwa Jijini Dodoma ikiwa na kauli mbiu "Mazingira Tofauti, Fursa sawa kwa Vijana".

Ushiriki huu ni kupitia Mwaliko wa Mh. JOEL NANAUKA Waziri wa Maendeo ya Vijana nchini Tanzania aliposhiriki na kuhitimisha Kongamano la Vijana KKKT Kitaifa.

Mratibu wa Vijana ameambatana na Bw. Augustine Mkungile kutoka Dayosisi ya Kati, Bw. Charles John Silayo kutoka Dayosisi ya Dodoma ambaye pia ni Katibu wa 'Jukwaa la Vijana wa KKKT wafanyabiashara na wajasirimali', pamoja na Bi Fadhila Mjengy kutoka Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha). Dawati la Vijana KKKT tunathamini mwaliko wa Mh. Joel Nanauka Waziri wa Maendeo ya Vijana nchini. Heri ya Siku ya Vijana Kimataifa.

Tunakila sababu ya kumshukuriu Mungu kwa wema na fadhili zake za kila siku. Kongamano limefana na limefana tena. * Neno ...
09/08/2026

Tunakila sababu ya kumshukuriu Mungu kwa wema na fadhili zake za kila siku. Kongamano limefana na limefana tena.

* Neno Safi
* Masomo Safi
* Maombi Safi
*Chakula Safi

Hakika Mungu ni mkuu sana sana.

Tunawatakia heri vijana wote Tanzania Nzima.

Mh. JOEL NANAUKA WAZIRI WA MAENDELEO YA VIJANA ASHIRIKI KATIKA KUHITIMISHA KONGAMANO LA SABA LA VIJANA KKKT KITAIFAKatik...
09/08/2026

Mh. JOEL NANAUKA WAZIRI WA MAENDELEO YA VIJANA ASHIRIKI KATIKA KUHITIMISHA KONGAMANO LA SABA LA VIJANA KKKT KITAIFA

Katika kuhitimisha Kongamano la Saba la Vijana KKKT Kitaifa, lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) tar 05-09 AGOSTI 2026 tumepata neema na heshima ya kipekee ya kuwa na Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Joel Nanauka, Waziri wa Maendeleo ya Vijana.

Katika hotuba yake, Mheshimiwa Nanauka alizungumza na vijana na kusisitiza umuhimu wa vijana kuamka, kuchangamkia fursa na kujiandaa kuzitafuta na kuzitumia fursa zinazopatikana kwa ajili ya kujenga maisha yao na mustakabali wa taifa.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa vijana kuwa na fikra chanya, kujiamini, kuthubutu na kuwa na mtazamo wa matumaini katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha.

Kwa namna ya kipekee, Mheshimiwa Nanauka alihitimisha kwa kuwaombea vijana na washiriki wote wa Kongamano, akimwomba Mungu awape hekima, nguvu, ujasiri na kuwaongoza katika safari yao ya maisha na katika kulitumikia Kanisa na Taifa.

Tunamshukuru sana Mheshimiwa Waziri Joel Nanauka kwa muda wake, ujumbe wake wenye kujenga na kwa baraka ya maombi aliyotuachia. Hakika, ujumbe wake utaendelea kuwa chachu ya kuwahamasisha vijana kuchangamkia fursa, kuwa na fikra chanya na kujenga maisha yenye tija kwao, Kanisa na Taifa.

“Kanisa Msingi wa Malezi Bora.”

08/08/2026

Umemfahamu Mchungaji nani hapa?

08/08/2026

Baba Askofu Jackson Sostenes

07/08/2026

Matayarisho kabla ya Group Photo katika Kongamano la Vijana KKKT linaloendelea Dodoma

Mkuu wa KKKT Ask. Dkt. Alex Gehazi Malasusa amewasili katika KONGAMANO LA VIJANA KKKT TAIFA.Awahaasisha Vijana kuendelea...
07/08/2026

Mkuu wa KKKT Ask. Dkt. Alex Gehazi Malasusa amewasili katika KONGAMANO LA VIJANA KKKT TAIFA.

Awahaasisha Vijana kuendelea kufanyika kuwa Chachu ya Maendeleo na kutambua Fursa zilizopo katika jamii.

06/08/2026

Kongamano la Vijana KKKT Taifa linaendelea hapa Chuo Kikuu cha Dodoma.

Vijana na viongozi mbalimbali wa kanisa wamehudhuria kwa wingi na Mwenyeji wetu Askofu Dr. Ndossa ameshawasili katika ukumbi wetu kuanza shughuli mbalimbali za Kongamano la Vijana KKKT Taifa.


Mungu anatuvusha hatua
06/08/2026

Mungu anatuvusha hatua

Neno la Ufunguzi.....
06/08/2026

Neno la Ufunguzi.....

Address

Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kkkt_umojawavijana posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kkkt_umojawavijana:

Shortcuts

Share