13/05/2026
Disemba 17, 2024 Mwenyekiti wa Vijana KKKT Bw. Anania J. Ndondole alitembelea Wilaya ya Kilwa(Mkoa wa Lindi) iliyopo katika Dayosisi ya Kusini Mashariki kwaajili ya kuangalia kazi kubwa iliyofanyika katika ujereshaji wa misitu ya mikoko (Restoration ya Mangrove Forests).
Video hii akielezea kazi kubwa iliyofanyika katika mradi huo ambao Dawati la Vijana KKKT iliuandaa kwa kushirikiana na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani ambao walifadhili mradi huo.
KKKT imekuwa mstari wa mbele katika utunzaji wa mazingira na kukabiliana na changamoto ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa.
Video hii ilirekodiwa na Bw. ambaye alikuwa ndiye mratibishaji wa program hiyo.