Efatha Church Namanga

Efatha Church Namanga HEALING AND DELIVERENCE BY BLOOD OF JESUS

10/12/2023
TAREHE 08/12/2023SEMINAKUHANI:DAVID MSHANA   SOMO MAVUNO         K**a unahitaji kupata mavuno Ni lazima ushuhulike Na mb...
09/12/2023

TAREHE 08/12/2023
SEMINA
KUHANI:DAVID MSHANA
SOMO MAVUNO
K**a unahitaji kupata mavuno Ni lazima ushuhulike Na mbwa mwitu wa mazingira yanayo zunguka Na njia zilizojificha ili kuweza Kula vitamu Na vinono (i) Matoleo
(ii)Kuwatunza watumishi

I) Matoleo ni ibada
*K**a huna Matoleo hakuna ibada
*K**a hujafikiria kutoa hujafikiria kuabudu
Palipo Na dhambi Kuna madhabahu
Mungu Ni Matoleo Na uhitaji wa Mungu Ni uumbaji, ibada pasipo Matoleo ni Sawa na bure Kwa maana ibada huambatana na Matoleo

II) Kuwatunza watumishi
Luka 10 : 4-7
Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani.
Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu;
na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu.
Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.

TAREHE 07/12/2023SEMINA KUHANI ;DAVID MSHANA     SOMO: NGUVU YA MUNGU  (LUKA 10:1 ...)    (Kutoka 20 : 4-6)Usijifanyie s...
08/12/2023

TAREHE 07/12/2023
SEMINA
KUHANI ;DAVID MSHANA
SOMO: NGUVU YA MUNGU
(LUKA 10:1 ...)
(Kutoka 20 : 4-6)

Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

Yesu anapenda kufurahi Na kinacho mfurahisha Ni kumzalia matunda
Mungu anapenda watoto wa kiroho wachukue Na kuvuna watoto wa kimwili Na kuwasababisha wapate kibali mbele zake;Basi utakuwa umemfurahisha Mungu.
Furaha Na Kula vinono Ni matokeo ya nguvu. Na nguvu Ni matokeo ya kumfurahisha bwana
Kwahio kituvkikubwa Na cha msingi Ni kumfurahisha bwana maana nguvu anazo yeye
Ukipungukiwana Na nguvu hakuna kitu utaweza kufanya Wala kuongeza kitu kwenye Maisha yako
Ifanye furaha yako ya kumfurahisha Mungu ikuinue Na ikupe nguvu ya kusimama katika Maisha
(Luka 15 : 7-10)

Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.
Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione?
Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.
Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.

IBADA YA JUMAPILI3/12/2023MCH: WINNIE ROSE     SOMO;UPENDO         Mungu anakupenda vile ulivyo; kwanini unakata tamaa h...
03/12/2023

IBADA YA JUMAPILI
3/12/2023
MCH: WINNIE ROSE
SOMO;UPENDO
Mungu anakupenda vile ulivyo; kwanini unakata tamaa hatak**a uko kwenye majaribu, upo kwenye shida Na taabu usirudi nyuma Mungu anakupenda
Inawezekana mke wako au mume wako anakusukuma lakini Mungu anakutangazia kuwa alikupenda tangia ulipokuwa tumboni mwa mamayako : kunamahali Mungu anakupitisha kwenye wakati mgumu ili ujue namna ya kuomba Na kuongea Na Mungu
Mtu mwenye Pendo la Mungu Hana chuki Na kitu chochote Wala mtu yeyote ukiona kunamtu humpendi hata kuwe Na sababi za chuki basi ujue wewe huna Pendo la Mungu
Usikimbie kwenye nyumba ya Mungu kwasababu ya kunyooshewa vidole Kwa kuwa Mungu anakupenda hivo ulivyo ndo maana akamtoa mwanae wapekee ili kila amwaminie asipotee Bali awe Na uzima wamilele
Kristo akikupa Pendo la kumjua Mungu kamwe usije ukaliacha

IBADA YA MAOMBIMT: GERVAS  (ZABURI 51)  Muombe Mungu kwasababa haujui ilikiwaje kutoka vizazi vyako vyote vilivyo pita k...
03/12/2023

IBADA YA MAOMBI
MT: GERVAS
(ZABURI 51)
Muombe Mungu kwasababa haujui ilikiwaje kutoka vizazi vyako vyote vilivyo pita kuanzia mababu Na mababu vizazi Na vizazi had vizazi
Je, Ni marangapi roho mtakatifu amekuacha , Na hujui kuwa amekuacha?
Mtume Daud anamwambia Mungu"Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani"

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA Kuna mambo unayofanya na matokeo yake unamsababisha Mungu aseme na kufanya  jambo...
26/11/2023

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Kuna mambo unayofanya na matokeo yake unamsababisha Mungu aseme na kufanya jambo kwako. Isaya 65:24 “Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Hii ina maana gani? Mungu hajibu kwa sababu umesema, Bali ni kwa sababu umefanya jambo ndipo unamsababisha Yeye aseme au atende kwako. Kumsababisha Mungu asimame kwa ajili yako lazima umchokoze kwanza, mfanye Yeye atende kwako kwa kufanya jambo katika ufalme wake.

Mungu anasikia maombi ya wengi wakiomba lakini anawajibu wachache, kwa nini? Kwa sababu kuna mambo ambayo unapaswa kufanya.

K**a unataka kumgusa Mungu na kumfanya atende kwa ajili yako unapaswa kufanya yafuatayo:-

1. Utoaji wa kupitiliza matarajio au kilichotarajiwa.
Kwa nini malkia wa sheba utoaji wake unakumbukwa mpaka leo? Kwa sababu alitoa kuliko matarajio yaliyotarajiwa. Utoaji wa ziada ndio unaomchokonoa Mungu na humsababisha akuulize unataka nikutendee nini? Kuna mambo mengine unaweza kuomba sana lakini Mungu hatajitokeza mpaka utoe zaidi ndipo utamsababisha ajitokeze kwako na kukuuliza unataka nikutendee nini?
• 2 Nyakati 1:7-13 “Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, Omba utakalo nikupe. Sulemani akamwambia Mungu, Umemfanyia baba yangu Daudi fadhili kuu, nawe umenimilikisha mimi badala yake. Basi sasa, Ee Bwana Mungu, na limyakinie baba yangu Daudi neno lako; maana umenitawaza niwe mfalme juu ya watu wengi k**a mavumbi ya nchi..........”

Suleiman alitoa zaidi na hata akaugusa moyo wa Mungu ndipo Mungu akauliza unataka nikufanyie nini? Usimtolee Mungu kwa sababu unacho cha kutoa bali toa zaidi ili kuugusa moyo wa Mungu na kusababisha Mungu atende kwa ajili yako.

2. Unapoijenga nyumba ya Bwana Mungu wako utukufu unakuwa ni wa kwako. 2 Mambo ya Nyakati 7:1-3 “ Basi Sulemani alipokwisha maombi hayo, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; utukufu wa Bwana ukaijaza nyumba. Wala makuhani hawakuweza kuingia nyumbani mwa Bwana

Address

Namanga
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Namanga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Namanga:

Share