30/12/2024
*VUKA MWAKA NA NGUVU KWA NENO NA KWA MAOMBI YA SIKU 40*
LEO TUKIWA SIKU YA 18(Tarehe 30 Disemba
Wacha Tujifunze
Kuhusiana
Na UTII.
*SOMO:SIRI YA UTII*
Dokezola Utii “Naye Samweli akasema, Je! BWANA huzipenda sadaka za kutekeketezwa na dhabihu sawasawa na kutii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya bebeeru.” 1 Samweli 15:22 Ukimuwekea Mungu machaguo mawili ili achague mojawapo kati ya hayo; upande mmoja uweke sadaka na upande mwingine uweke utii. Uwe na uhakika Mungu huchagua utii. Hata hivyo, ni heri ukijua ya kwamba sadaka ni udhihirisho wa utii wetu kwa BWANA.Sadakayoyote inayowasilishwanje ya kigezo cha utii, Mungu huiona k**a “hela” tu! Haisemi chochote mbele zake. K**a utii ni muhimu kiasi cha mvutia Mungu hivyo, utii ni nini basi? Utiini kukubali na kutendea kazi maelekezo ya Mungubila kuyatilia mashaka.
Namna tunavyohusiana na Mungu na kumwendea ni kwa utii. Hii ni kwa sababu kwenye mahusiano hayo, Mungu hutoa maelekezo na si mapendekezo. Mapendekezo hupokelewa kwa majadiliano. Wakati maelekezo hupokelewa kwa utii tu na si pungufu ya hapo. NenonamaelekezoyaMunguhupokelewakwa utii na si kwauchaguzi.“NenolaMungunikwa ajili ya utekelezaji na si uchambuzi.” Dr. Sam Adeyemi Upendeleo ya kiungu uko ng’ambo ya pili ya barabara ya utii unakusubiri. Je, utavuka mwaka 2024 ukiwa na hali yako ya kiburi na majivuno?
Ngazi nne za Utii: 1. Utiikuyaelekeamaandikomatakatifu(Biblia). “2. Katika mwaka wa kwanzawa kumiliki kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka,ambayoenolaBWANAlilimjiaYeremianabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini. 3. Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguozamagunia namajivu,” Danieli 9:2-3 Kile alichokisoma Danieli kinapatikana kwenye vitabu vifuatavyo: Yeremia 25:11-12; 29:10; Ezra 1:1; 2 Nyakati 36:21. Angeweza kusoma k**a machapisho tu au vitabu vya historia ya taifa lake au masimulizi kutoka kwa waandishi wazuri na wema wa taifa lake zuri la Israeli. Lakini aliuvuka huo mtego. Aliposoma, alichukua kile alichokisoma kwa uzito na heshima ya hali ya juu sana. Alijua ya kwamba anachokisoma ni neno la BWANA.
Mwitikio wake juu ya kile alichokisoma unatuambia hali nya moyo wake kuyaelekea maandiko matakatifu, “…Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi…” . Hii ni heshima na mwitikio wa hali ya juu sana kwa neno la Mungu. Halikuwa neno lililoishia kumpa taarifa tu, bali liliyakunja magoti yake. Hakuna mahali kwenye unabii huo ambapo Danieli alitajwa kwa jina ya kwamba ana wajibu wa kuomba au kutenda chochote ili litokee na kuwa halisi kwenye maisha ya watu wake. Kilichoyakunja magoti yake, ni hali ya utii uliokuwa ndani yake kuliekea neno la Mungu. Iko hivi, kila ukisoma maandiko matakatifu ukagundua yanamuhusu kila mmoja isipokuwa wewe, ujue kuna upungufu wa utii ndani yako kuyaelekea maandiko. Kabla haujaanza kutafuta kusikia sauti ya Roho Mtakatifu, hakikisha umemaliza kuisikia iliyomo ndani ya neno lake; na k**a unapenda sana unabii,
hakikisha umeupokea unabii wako wote tena uliokwisha kutimilizwa uliomo ndani ya maandiko matakatifu. 2. NenolaMungulililovuviwa “31. Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, kusema, 32. “Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka , na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu bali wa walio hai.” Mathayo 22:31-32 (SUV). Ukisoma andiko hilo kutokea tafsiri ya NENO utagundua kuna msisitizo tofauti, “Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamkusoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,” Utaona si tu kwambaMungualisema ujumbe ukaenda hewani, bali alikuwa anasema na hawa ndugu waliokuwa wanaongea na Bwana Yesu. Tafsiri nyingi za lugha ya kiingereza zinakubaliana kabisa na wazo hili ya kwamba si tu Mungu alisema ujumbe bali alisema na watu hawahuuujumbe. “But about the resurrection of the dead– have you not read what Godsaidto you,” (NIV)
“But as touching the resurrection of the dead, have ye not read that which was spoken unto you by God saying,” (ASV) “And as for whether the dead are resurrected, haven’t you read what Godsaidtoyou,” (CJB) Kwa msingi huo basi, twaweza kufikia hitimisho ya kwamba ndani ya neno la Mungu lililoandikwa kulikuwa na ujumbe ulimwendea Musa k**a msikiaji wa awali. Hata hivyo halikuishia hapo, bali limebeba pumzi ya kukihudumia na kukifaa kizazi kilichokuwa kimesimama mbele ya Yesu… na halikuishia hapo, linasema hata hivi leo. Kwahiyo, unaposomamaandikomatakatifu, kumbuka kuizingatia pumzi na sauti iliyo nyuma na maandiko hayo. Utagundua waliyoandikiwa ya kwamba maandiko Wakorintho, Wathesalonike, Wagalatia, Waebrania na wengineo yanakufaa wewe mtanzania (na mtu mwingine yeyote) hivileo! “Maana Neno la Munguli hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena
lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” Waebrania 4:12 Kila wakati unapofungua maandiko matakatifu kuyasoma, huwa yamefunuka kukusoma wewe. Huo ni uthibitisho wa pumzi iliyomo ndani ya neno. Usisome maandiko k**a kitabu cha historia, bali ni pumzi hai ya Munguhatahivi leo! 3. MaongoziyaRohoMtakatifu “Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, haondio wanawaMungu.” Warumi8:14 “Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.” Wagalatia 5:18 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.” Yohana 16:13
Nimekusudia uone ya kwamba moja wapo ya kiashairia cha uana wa Mungu ni kuongozwa na Roho waMunguaambayeameachiliwakwaajili hiyo. Kumbuka neno linamtambulisha Roho Mtakatifu k**a msaidizi na si mlazimishaji. Kwa hiyo, namna yake ya kuongoza ni ile ya kutusaidia kuliko kutulazimisha zaidi. Nafasi hii ya “msaidizi” ndiyo mtegowenyewe.Unahitajikautii wa haliyajuusana ili kuongozwanamsaidizi! 4. Mamlakahalalijuuyangu: Katika kuyaongoza na kuyaratibu maisha ya mwanadamu hapa duniani, Mungu ameyaweka chini ya mamlaka. Kunamamlakanyingiambazozikojuuya maisha yako. Hata hivyo, kwa minajiri ya kitabu, ninatambulisha kwako mamlaka nne ambazo unapaswakuzitii. a) Wazazi wa kimwili: Hawa si tu kwamba ni watu waliokuleta duniani na kukupatia utambulisho wa kibaiolojia/vinasaba na kukupaukoo. Hawanimamlaka!
Tazama ni kwa namna gani maandiko yamewaambatanisha na aina fulani ya uheri. “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.” Wakolosai3:21 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki 2. Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, 3. Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.” Waefeso 6:13 Kutotii mamlaka hii ya wazazi wa kibaiolojia ni kuchagua kutopokea thawabu iliyoambatanishwa pamoja nao. b) Wazaziwakiroho “Kwa kuwa nakuamini kutii kwako ndiyo maana nimekuandikia, nikijua ya kuwa utafanya zaidi ya hayo nisemayo.” Filemoni 1:21
Moja ya mifano ya mahusiano ya mzazi wa kiroho na mtoto wake na swala la utii ni katika ya mtume Paulo k**a baba kwa upande mmoja; na Filemoni k**a mwanakwaupandewapili. Kwenye waraka huu wenye sura moja, utaona malekezo ya baba kwamwanae: Kumpokea Onesimo k**a ndugu yake katika Kristo. Hapo awali Onesimo alikuwa ni mtumwa wa Filemoni na inaonekanaaliotoroka naaliiba sehemuya mali ya bwanawake(Filemoni 1:16) Kufuta madeni yote ya mali yaliyopita juu ya Onesimo. Lakini ikiwa ni muhimu sana kuendelea kuyadai, basi amdai baba yake, yaani mtumePaulo (Filemoni 1:18) Amuandalie baba yake mahali pa kukaa ambapo atafikia baada tu ya kumaliza kifungo chake gerezani (Filemoni 1:22) Tahadhari: Filemoni anakumbushwa na baba yake ya kwamba yeye anadaiwa nafsi
yake kabisa, siyo hata fedha au mali. Hii ni kwa sababu ya uwekezaji wa kiroho wa Paulo kwa mwanae(Filemoni 1:19b) Sasa, ni vizuri uelewe ya kwamba ujasiri wa kutoa malekezo alionao Paulo kwa mwanae Filemoni ni kwa sababu ya kiwango cha utii wake si tu kwa sababu ya mamlakayakiroho ya Paulo. “Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maanawaowanakeshakwaajili yarohozenu, k**a watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.” Waebrania 13:17 Mwitikio wetu kwa wanaotuongoza ni utii na unyenyekevu. Kwenye andiko hili, wanaoongoza ni wale wanaokesha kwa ajili ya roho zetu na wenye wajibu wa kutoa hesabu juu ya maisha yetu. Ni nani mwingine afanye hivyo ispokuwa mzazi wako wa kiroho? Unadhani kuna mtu mahali fulani anaweza kukesha kwa ajili yako? Unadhani kuna mtu mahali fulanianawezakujiwekakwenyejukumulakujakutoa
heshabu kwa ajili yako? Ni kwa nini ajiingine kwenye majukumumazitohivyo? c) Mume Mume ni mamlaka kwa mke wake! K**a mke atatambua hivyo, atachukua neno la Mungu k**a lilivyo na atatekeleza neno basi atavuna thawabu ya kutii kwake. Maandiko yanasema hivi kuhusu mamlakahii. “22. Enyi wake, watiini waume zenu k**a kumtii Bwana wetu. 23. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe,k**aKristo nayeni kichwachakanisa; naye ni mwokozi wa mwili 24. Lakini k**a vile kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.” Waefeso 5:22-24 Kwenye kitabu kiitwacho NYWILA nimefundisha kwa upana wake sana msukumo wa kiungu nyuma ya utii wa mwanamke kumuelekea mumewe. Mwanamke ameaminiwa Mungu kumfundisha mume wake utii kwa kuwa kilelezo cha huo utii wenyewe. Na mume, ambaye ni sehemu ya kanisa la Kristo, atatenda
inavyotarajiwa awapo kwenye nafasi yake ya bibi arusi wa Kristo. Hata hivyo, ni vizuri kujua ya kwamba Mungu ndiye aliyeweka mtiririko huo wa kimamlaka si kwa ajili ya hasara au kutuonea bali ni kwa faida na ustawi wetu. Hili ni jambo ambalo linabishaniwa sana miongoni mwa tamaduni na mapokeo kiasi kwamba mtu anayeamini katika njia hii anaonekana kuwa ni wa kizamani na amepitwa na wakati. Atukuzwe Mungu kwambavitu vyotevitapita, neno litasimama! “Ninyi wake, watiini waume zenu, k**a ipendezavyo katika Bwana.” Wakolosai 3:18 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi. Ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendowawakezao,pasipolile Neno.” 1Petro 3:1 d) Kiongoziwakazi Kuelewa muktadha kidogo, ni kwamba wakati wa kanisa la mwanzoni kulikuwa kuna uatamaduni wa utumwa kwenye jamii za wakati huo. Lilikuwa ni jambo la kawaida kabisa. Ikafikia wakati ambapo watumwa wanaiamini injili na wanaokoka… wanfunguliwa kutoka katika utumwawadhambi(siyo utumwa wa kazi). Wengine walianza kuhoji ya kwamba, maadamu wamewekwa huru na Kristo kuna umuhimu gani tena wakuendelea kuwa chini ya utumwa wa bwana zao? Sasa ikumbukwe ya kwamba utumwa ndiyo ulikuwa mfumo wa kiuchumia wa uzalishaji (means of production)– ni k**a ilivyo ajira kwa zama zetu. Kulikuwa na utaratibu na miongozo ya namna ya kukombolewa (kulipiwa deni au kujilipia deni la kutoka utumwani) au kuachilia huru kwa utashi wa bwana. Tofauti na hapo ilionekana kuwa ni uasi na athari zake zingekuwa kubwa. Maandiko yanaelekeza ya kwamba watumwa wawaone bwana zao k**a mamlaka ambayo hata k**aumeokokaunapaswakuiitikia kwautii. “Ninyi watumwa, watiini hao ambao kwa mwili ni bwanazenu, katika mambo yote, si kwa utumwa wa macho, k**a wajipendekezao kwa wanadamu, bali
kwa unyofu wa moyo, mkimcha Bwana.” Wakolosai 3:22 “Enyi watumishi, watiini bwana zenu kwa hofu nyingi, sio walio wema na wenye upole tu, bali nao walio wakali.” 1 Petro 2:18 Ni sawa na zama hizi baada tu ya kuokoka usemi ya kwamba hupendi kuwa chini ya mtu, hupendi maelekezo yake, hupendi kubanwa… unataka umtii Kristo tu na neno lake! Hiyo siyo sawasawa. Ukiokoka, hakikisha viongozi wako wanauona mwenendo wako mwema kiasi cha kuwavuta kwa Yesu Kristo.
**************************************
NAOMBA TUENDELEE NA SOMO HILI KESHO.
JITAHIDI KUTII.
SOMA NENO
OMBA
FUNGA
TOA SADAKA.
USIPOVUKA MWAKA NA NGUVU YA KUMILIKI UJUE MUNGU NINAYE MTUMIKIA SIO MUNGU WA KWELI.
---------------------------------------------
Zaburi50:23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.-"*
Kwa iyo
Ikiwa Unayo sadaka.
*Tuma kwa namba 0719123504.
Jina: Charles John Chazya*
*Au Airtel Lipa namba. 0088881.
Jina: Jukwaa la Maombi Tz*
Naomba Ubarikiwe ikiwa utasimama kwa Uaminifu katika yote Hayo
*_NENO_*
*_MAOMBI_*
*_SADAKA_*
Waweza pia share link hii kwa wtu wengine na utakua umehubiri Injili pamoja nasi.
https://whatsapp.com/channel/0029VaDFjlC1CYoQJaAeA40T
Group letu
https://chat.whatsapp.com/E6mbIkETWaMK7JTIoMIU9G
______________________________________________