30/08/2022
REMAIN PURE-Baki Msafi.
Bwana Yesu asifiwe,na ongera sana kwa majukumu yako ya kila siku,wote twastahili kulitukuza jina la Bwana wakati wote kwasababu yeye ndiye anaetuwezesha kuwa hivi tulivyo leo.
Kwakweli inafurahisha sana Taifa lenye mtu,au watu wanaomtumikia Mungu kwa mioyo yao yote wakitenda yale ambayo Bwana wao ataka wayatende.Ongera sana ikiwa wewe huu miongoni mwao.
Karibu sana kwenye somo letu la leo.Remain Pure ( Baki Msafi).
Katika hali ya kawaida kila mtu hupenda usafi iwe kwenye nyumba yake mwenyewe,mwili wake,mazingira yake n.k,yaani kuna watu kwa mambo ya mwili tu ni wasafi kweli kweli,ongera yako katika wewe ikiwa ni msafi katika mambo hayo ya mwilini,lakini somo letu zaidi limelenga usafi katika mambo yote.
Remain Pure,au Baki msafi,kisafi chochote huwa kinapendwa kwasababu ya kupendwa kinaganganiwa na katika kuganganiwa kule chaweza kuchafuliwa muda wowote na watakaosema hakifai tena ni wale waliokuwa wakikigangania,.
Leo hii kwa sababu ya maarifa kuibuka mengi,kuna maji tunayokunywa leo lakini chimbuko lake siyo kwenye chemichemi bali yanatolewa kwenye madimbwi mabaya alafu yanafanyiwa mchujo kupitia vifaa maalum na hatimae yanakuwa maji safi yanayostahili kunyweka.
Biblia inasema najua asili ya imani yako,manake Bwana anakutambua kuwa wewe ni wake ijapokuwa upo katikati ya watu waliokuchafua,yaani kuna watu unakaa nao lakini hawakuthamini tena,kwa maana ya kwamba wewe siyo wa muhimu kwao lakini mko pamoja,pengine ni aina yako ya maisha unayoishi,kuvaa kwako,wamezoe maneno yako,ahaadi zako,n.k.
Sasa anapokuja yule wa sirini atambue kuwa wewe ni safi,ili akufanye uwe safi Bwana Yesu anasema atakupitisha kwenye moto k**a mtu apitishavyo dhahabu kwenye moto,manake ataanza kusafisha nafsi yako na akikwisha kamilisha hivyo atakutambulisha katika jamii na watu watakuona unafaa kwa ajili ya kesho zao.
Sasa Bwana akikwisha kufanya msafi,usifikili wenye nia ya kukuchafua watakoma,sikiliza,Yesu katika wanafunzi wake kumi na mbili alikuwepo mmoja ambae yeye licha ya mambo yote aliyokuwa anayashuhudia kwa macho yake kutoka kwa Bwana Yesu bado ndani mwake nia yake haikuwa njema huyo ni Yuda Eskariot,hii ni kumaanisha kwamba yeyote uliyekaribu nawe anaweza kutumika kwamba kila ulifanyalo yeye anaona ni baya tu,kuna wanawake wameolewa kila analolifanya kwa mme wake bado mmewe maneno ya kejeli yatatoka kinywani mwake tu,au kila mwanaume analolifanya bado mwanamke haoni k**a mmewe ni shujaa kwake,ili uwepushwe na watu wa aina hii,kazi yako siyo kuugeuza moyo wako k**a watakavyo wao bali jukumu lako ni kuendelea kuwa safi moyoni mwako.
Kuna watu wamechafuliwa na wamekubali kujiona kuwa wao ni wachafu,wamekuwa na hisia za kujiona si kitu kwenye maisha,wameishia kujichafua moja kwa moja,wamefuta uaminifu wao kwa kila mtu,hawapendi tena,hawafanyi kazi kwa bidii tena,hawavai vizuri tena,hawasaidii watu tena,k**a ni kujukumika vizuri kwenye tendo la ndoa hawawezi tena n.k.
Ninachotaka nikwambie Yesu alitambua mapema sana nia ya Yuda eskariot kuwa ni mpinzani wake,yaani ni k**a mfano umeoa unakuja kutambua mkeo au mmeo hayuko upande wa maono yako ya shughuli zako,licha ya kwamba shughuli hiyo unayoifanya sasa,inamlisha,inamvisha nk lakini huwezi kusikia maneno mazuri kutoka kwa mkeo au meo akikupongeza,sasa ukiona hivyo usije ukaanza kudanganywa na watu wa nje unaokutana nao mfano katika shughuli zako unakutana na mdada yaani kuongea kwake kutenda kwake unaona angefaa kuwa mkeo au unakutana na mkaka anasema anakukubali sana kwenye kujituma kwako lakini neno hilo hujawai kulisikia kwa meo,usikulupuke kuanza mahusiano ya siri kati ya aina ya watu hao wawili kwasababu nia ya ibilisi ni kukuondoa kwenye kusudi nyuma ya mtu.
Jitahidi sana kudumisha nia njema kwa huyo mtu akupingae,asiyethamini uwepo wako,kuna vitu vingine Mungu uruhusu viwepo ili ajitwalie utukufu katika hayo,atakapomwondoa huyo mtu usiangalie nyuma tena,na kuingiza huruma zako za kijinga,Mungu atamleta mtu aliyekwisha guswa moyo kwa ajili ya kusudi lake mwenyewe,usije ukaangalia macho ya watu watakuonaje wewe songa mbele na timiza wajibu uliokwisha pewa.
Kwenye kitabu cha Samweli biblia inasema waliomchukia Sauli baada kupakwa mafuta teule ya kifalme wakaonekana si kitu,Mungu akamwinulia Sauli watu walioguswa moyo kuambatana na Sauli.
Ngoja nikwambie kitu baadhi ya vitu au taratibu zilizowekwa na wanadamu ili katika taratibu hizo kusudi la Mungu lizuiliwe kwa urahisi kabisa ni taratibu za kufunga ndoa kanisani,sikiliza kuna watu wanataka kuagwa vizuri nyumbani kwao ili waende kufanana k**a mama zao au baba zao huko wanakoenda,wengine wanataka tu waonekane wamevaa shera yaani hawana haja na kusudi ndani ya ndoa wanazoziendea,sasa usije ukatishwa na mtu awaye yote pale ambapo Mungu atakutaka ufanye maamuzi kwa ajili ya kusudi lake,kitakachokufanya ubaki salama dhidi ya maneno yao na vita yao ni kwasababu Mungu hakuona hatia juu yako.
Nihitimishe kwa kusema hivi,kubambwa kwa Yesu msalabani hakukutokana na kisasi cha adui zake walio mpinga,bali Mungu aliluhusu kwa ajili ya mimi na wewe tukombolewe,weka hofu pembeni muweke Mungu awe mtetezi wako kwenye kila hatua unayoikabili,.
God bless you.
Geofrey Julius-Jesus power ministry Tz