10/06/2024
AKILI NA UJINGA HAVIENDANI KABISA..
"" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "" "
Iko hivi..!!! Unakumbuka Kundi lilelile lililomchukua MDOGO wao, (Nabii YUSUF a.s), kwa BABA yao kwa ahadi ya kumlinda lakini likaishia kumtumbukiza KISIMANI kwa NIA OVU (MBAYA)... Na ndio kundi hilohilo lilirudi kwa mara ya PILI kumomba tena BABA yao watoke na BENJAMIN (Yaani MDOGO wake NABII YUSUF a.s)
Sasa, soma sentensi mbili zifuatazo za majibu ya NABII YAQUBU (Mzee Yakub a.s) ambaye ni BABA yao juu ya maombi yao hayo.
1-..NABII YAQUBU Alisema hivi : “Je, NIKUAMININI kwa huyu k**a NILIVYOKUAMININI kwa nduguye zamani?”
2-...Jibhu la pili “Lakini M/MUNGU ndie mbora wa KULINDA, naye ndiye mbora wa KULEHEM kuliko wenye KUREHEMU wote”
Kwenye sentensi (JIBU) ya kwanza M/MUNGU anatuonyesha UDHAIFU wa BINADAMU kwamba ni kiumbe mwenye MASHAKA sana katika mambo yake mengi..
Na sentensi ya pili M/MUNGU pia anatufundisha kwamba penye kila UDHAIFU muweke YEYE pekee. Kwani YEYE pekee ndiye NGUVU kwenye UDHAIFU wako. (Elewa neno UDHAIFU)
VIJANA wenzangu siku zote M/MUNGU anapotusimulia simulizi k**a hizi, huwa sio kwaajili ya KUTUBURUDISHA hapana. Ni MAZINGATIO kwa WATU wenye AKILI timamu k**a ukiwa na AKILI hizo...
.By ✍️✍️✍️