NENO La MUNGU Ni Taa

NENO La MUNGU Ni Taa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from NENO La MUNGU Ni Taa, Pentecostal Church, Dzaleka Refugee Camp, Lilongwe.

MISSION UPDATE – SUNDAY, MARCH 28, 2026ADONAI YOUTH MISSIONARIES (ADONAI PENTECOSTAL INTERNATIONAL CHURCH – Dowa) succes...
04/04/2026

MISSION UPDATE – SUNDAY, MARCH 28, 2026

ADONAI YOUTH MISSIONARIES (ADONAI PENTECOSTAL INTERNATIONAL CHURCH – Dowa) successfully carried out an evangelism outreach in Chibwata village.

Led by Missionary Bihembo Ruzimira, alongside Missionary Joe Makutubu, the team shared the Word of God with power. Many people gathered, hearts were touched, and the presence of God was evident throughout the service.

“Go into all the world and preach the gospel to all creation.” — Mark 16:15
However, the mission field still faces many challenges — limited resources, transportation difficulties, and ongoing needs for outreach support.
We believe this work can grow even further with your support.
Your prayers, encouragement, and financial contributions make a real difference in reaching more souls.
If you feel led to support this mission, we welcome you to stand with us. Together, we can extend the Gospel to even more communities.

We sincerely thank all our partners and donors for standing with us.
Glory to God for what He has done — and for what is yet to come.

16/10/2024

16 octobre 2024

Chers amis et bienfaiteurs,

Nous vous écrivons au nom des Adonai Young Missionaries (AYM), un groupe de jeunes passionnés qui se consacrent à partager l'Evangile et à servir leur communauté.

Notre mission est de former et d'équiper les jeunes pour qu'ils deviennent des disciples de Jésus-Christ et des leaders dans leur communauté. Cependant, nous rencontrons un défi important : beaucoup de nos jeunes missionnaires n'ont pas accès à des Bibles.

C'est pourquoi nous lançons un appel à l'aide pour collecter des Bibles et des livres complémentaires pour nos jeunes missionnaires. Votre générosité nous permettra de renforcer leur foi et leur mission.

Les détails de notre demande sont les suivants :

- 30 Bibles (versions Chichewa et Swahili)
- Livres complémentaires : Dictionnaire biblique, Kamusi ya Biblia, Biblia Neno la Uzima Tele, Safari ya Musafiri

Nous vous prions de nous aider à soutenir ces jeunes missionnaires en nous donnant des Bibles et des livres complémentaires. Votre contribution sera un investissement dans leur formation spirituelle et leur mission.

Pour plus d'informations ou pour faire un don, veuillez nous contacter :

Adresse postale : 300 Dowa
Téléphone : +265 885 23 72 48, +265 884 20 97 01
Facebook : Adonai Pentecostal Church International-Dzaleka Adonai pentecostal church Dzaleka (Dzaleka)

Nous vous remercions à l'avance pour votre générosité et votre soutien à notre mission.

Que Dieu vous bénisse !

Cordialement,

ANDRE KABUYAYA GODET André
Représentant des Adonai Young Missionaries

31/08/2024

With JESUS IS COMING – I just got recognized as one of their top fans!

28/07/2024

Dzaleka Adonai International Church
MAHUBIRI YA CHILDREN BIG SUNDAY

Mhubiri: ASANTE KARAUSI MANDRANGA

SOMO: MTOTO NI CHOMBO CHA BWANA
§Mtoto kulijua NENO LA MUNGU

“Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.”
— Isaya 54:13 (Biblia Takatifu)

Wazazi wote wanatarajia watoto wao watembeye katika njia nzuri,lakini wanasahau kuwapeleka machoni pa Bwana,
Mtoto akimtumikia Mungu atakuwa msaada kwa familia na jamii nzima,tusiache watoto waaribikie nyumbani kisha tuanze kuwalaumu kwamba watoto wetu ni wabaya,bila kujua kwamba wangelikua katika njia ya BWANA hawange kua na mwenendo mubaya...
Mtoto ili awe na Amani inaomba awe na Neno la Mungu
Kwa sababu mtoto mwizi,mgonvi hawezi kuwa na Amani hio ni kwa sababu hana maneno ya Mungu,
“Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.”
— Mithali 22:6 (Biblia Takatifu)
Mtoto anafunzwa na kulelewa sehemu tatu

1. WAZAZI
Wazazi wetu wanatufunza tukiwa nyumbani,kazi za nyumbani...
2. MWALIMU
3. NENO LA MUNGU na hapo tunafunzwa njia za Mungu na maadili yake,
Yeremia 1 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.
⁷ Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.

Hapo MUNGU aliona utumishi ndani yetu sisi watoto,na hapo YEREMIA alikua na miaka 8,na MUNGU akampa nguvu ili aongoze watu wazima,naye akaongoza taifa vizuri

“Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.”
— Mathayo 18:10 (Biblia Takatifu)
Wapendwa,
Musiwazarau watoto wadogo kwasababu munamkwaza saana Mungu,kwasababu Mungu anatarajia uamsho wa Injili kubwa ya kesho,

Tunawasii sana wazazi wetu muendelee kutuimiza sisi watoto na pia wachungaji wetu waendelee kuimarisha wazazi wetu waendelee kututuma kanisani.

Mhubiri:
Mwandishi: Mr. Prince Malipo Gedeon Prima
Mads Nielsen

14/07/2024

Kanisa la Adonai Pentecostal Church International-Dzaleka Adonai pentecostal church Dzaleka

NENO LA LEO 14-07-2024

Mhubiri: Ev. K**ALEBO

Nehemia 1 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni,


⁶ tega sikio lako, macho yako yakafumbuke, upate kuyasikiliza maombi ya mtumishi wako, ninayoomba mbele zako wakati huu, mchana na usiku, kwa ajili ya wana wa Israeli, watumishi wako; hapo ninapoziungama dhambi za wana wa Israeli, tulizozifanya juu yako; naam, mimi na nyumba ya baba yangu tumefanya dhambi.

NENO:

Nehemia alikuwa Muyahudi ambaye alikwenda utumwani huko BABELI,Wana wa Israeli walitenda zambi mbele za Mungu naye Mungu akawaazibu nakumtuma Mfalme Nebukandeneza huko Babeli naye akawapiga nakuwapeleka watu huko Babeli.

ZERUBABELI
Baada ya miaka 60 kundi la pili likatoka kuongozwa na mtumishi wa Mungu EZDRA

Baada ya miaka 80 chini ya mfalme ALTASHASTA kundi la tatu likaongozwa na mtumishi wa Mungu NEHEMIA mnamo mwaka wa 4444

Aliyelijenga Hekalu la Yerusalemu ni kundi lile la pili la EZDRA
NEHEMIA naye huko alikua na mnywesha mfalme divai ama kinywaji,
Sasa akiwa huko Shushani watu wakutoka Yerusalem naye Nehemia akawauliza habari na hali za Yerusalem,naye HANANI akamjibu NEHEMIA kwamba mji uko katika hali ya mateso na Yerusalem iko katika hali mbaya saana,ukuta ama ulinzi wa Yerusalem umebomolewa na kwamba malango yake yamechomwa na moto.
Ukuta huo ulikuwa ni ulinzi juu ya mji mkubwa,hata adui hakuwa na njia yakupitia lakini ulipobomolewa kila adui alikua naingia mara kwa mara,
Alipoambiwa habari hio,NEHEMIA akauguwa rohoni,akakosa amani,Biblia inasema kwamba
NENO: ISHI MAONO ULIYO YABEBA, ISHI MALENGO
K**a vile maneno ya Mungu inasema Tusiyasikie tuh maneno bali tuyatende
NEHEMIA akaomba Mungu
Hio ilikuwa hatuwa ya kwanza,na maombi yake hayakukuwa ya kawaida,alitubu zambi zake,zambi zamababu zake...
Siku ya pili alipoenda kwa Mfalme kumnywesha naye Mfalme akamuona Nehemia akaona kwamba hali yake sio nzuri,
“Basi mfalme akaniambia, Mbona umesikitika uso wako, nawe huna ugonjwa? Nini hii, isipokuwa ni huzuni ya moyo? Ndipo nikaogopa sana.”
— Nehemia 2:2 (Biblia Takatifu)
SWALI: KWANINI NEHEMIA ALIHUZUNIKA KWA AJILI YA YERUSALEM?
Kwasababu ndani yake mulikua Upendo na Huruma ndani yake,
Sio sisi wakristo mwenzako anapopatwa na shida wewe unafurahia,mwenzenu anateseka wewe unacheka.
2. WIVU WA KAZI YA MUNGU: Wengine hawana wivu wa kazi ya Mungu,kwamfano wewe ni muimbaji hauwezi furahia uimbaji unaenda vibaya,
3. HAKUA MUBINAFSI: hakujifungia ako kazi yote hio
4. ALIKUWA ALIBEBA MISINGI YA YERUSALEM NDANI YAKE: Kiukweli kulikuwa watu wenye nguvu nyingi,wenye pesa,ma injenia mafundi wakubwa lakini misingi hio ilikua nabebwa na NEHEMIA,
MPENDWA acha nikuambie kwamba wewe sio wakawaida,Nehemia hakukua fundi,hakukua nanguvu zakuijenga Yerusalem

MFALME AKAMUULIZA,NIFANYE NINI? NEHEMIA hakuishia kuomba tuh lakini alifanya hatua
“Ndipo mfalme akaniambia, Una haja gani unayotaka kuniomba? Basi nikamwomba Mungu wa mbinguni.”
— Nehemia 2:4 (Biblia Takatifu)
ALIMUOMBA MFALME RUHUSA NA MFALME AKAMPA VITU VILIVYOKUA NA ITAJIKA...
Tumesikiya habari za ujenzi wa Yerusalem,nasi mioyo yetu imeharibika,familia zetu zimeharibika,kuna watu wanaoishi katika nyumba moja,katika kanisa moja lakini hawaongeyi,hawana mahusiano ya sawa,Leo nisiku ya kujenga familia zetu,leo nisiku yakujenga kanisa zetu,
Nehemia alimweka Mungu mbele na hata mfalme akamsaidia Mpendwa,wakati unamuweka Mungu Mbele anatumikisha hata adui yako ili akusaidie katika mambo unayoyafanya.
KUNA MAOMBI YAKIPEKEE AMBAYO UNAITAJIKA KUOMBEWA ILI UJUWE MAONO ULIYOYABEBA, NA UISHI MALENGO UWE K**A NEHEMIA.

Muhubiri: **alebo
Mwandishi: Prince Malipo Gedeon Prima

Kanisa lako la Dzaleka Adonai International Church MAHUBIRI YA LEO 03-03-2024Mhubiri: BISHOP MORRIS BANDANENO: KATIKA MA...
03/03/2024

Kanisa lako la Dzaleka Adonai International Church

MAHUBIRI YA LEO 03-03-2024

Mhubiri: BISHOP MORRIS BANDA
NENO: KATIKA MAISHA YA KIROHO KUNA VITA TUNAPASWA KUPIGA

Waefeso 6 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁰ Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.


¹⁸ kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

Tunapaswa kujua k**a sisi wakristo tuko katika vita, ndiomana Paulo alisema kuusu vita ambavyo sio vya kimwili bali ni vya kiroho, ambavyo vilianza hapo kale Shetani alipoasi Mungu alianzisha vita na kuonza vita zidi ya MUNGU, na MUNGU Alipomshusha hakushuka mwenyewe, lakini alishuka na serikali yake, na hao wote wanapigana vita vya ajabu sana, na aliposhushwa, Shetani hapigani tena na Mungu bali anapigana na wana wa MUNGU, shetani sasa yeye anatumia system yakupigana na hapiganishi wapagani na wasio amini, lakini anaandaa tena vita visivyokua vya kawaida, kwahio hatupaswi kusinzia na ```MUNGU Alipoona vita ivyo akaandaa silaha ya kupambana na vita ivyo```
Na vita ivyo sio vya damu na nyama inamaanisha Shetani ndie adui yetu, na Paulo akaona uwezekano wakushinda vita kwakuonyesha silaha ambazo MUNGU aliziweka ni SILAHA SABA AMBAZO MTU ANAPOZIVAA NA ANASHINDA VITA

1⃣ KUVAA MKABA WA KWELI NA HAKI
“Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,”
— Waefeso 6:14 (Biblia Takatifu)
Unapokua na kweli ndani yako unakua na NENO LA MUNGU
“Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.”
— Yohana 17:17 (Biblia Takatifu)
Ukikosa ukweli ndani yako utakuwa mtu wakushindwa,

2⃣HAKI AMA UTAKATIFU
Kuvaa utakatifu kifuani mwako,
Sababu Biblia inasema LINDA SANA MOYO WAKO KULIKO YOTE UULINDAO
3⃣MIGUU AMBAYO ILIO TAYARI KWAKUHUBIRI INJILI YA KWELI
“Tena wahubirije, wasipopelekwa? K**a ilivyoandikwa, Ni mizuri k**a nini miguu yao wahubirio habari ya mema!”
— Warumi 10:15 (Biblia Takatifu)
Unapopeleka ujumbe na kumshuhudia KRISTO,
Popote unaposhuhudia Kristo mahali popote iwe
Katika familia yako,
Iwe kazini mwako,
Iwe jamiini kwako
4⃣KUVAA NGAO YA IMANI
“zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.”
— Waefeso 6:16 (Biblia Takatifu)
Yaani silaha hio ndio ngao kubwa inayozuia miyali ya shetani, unapomwamini Mungu saana unatumia Imani, wakati YESU alikua naponya watu alikua nawaambia kwamba imani yao imewaponya “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.”
— Waebrania 11:1 (Biblia Takatifu)
Imani ni kitu ambacho kinakutoa woga na mashaka sababu mtu anakua na uhakika katika hali yote.
Imani inatulinda na woga,
Inatukinga na mashaka
Inatukinga na kutufanya tustarehe, ndiomana sisi Wakristo tunaishi kwa furaha haijalishi matatizo wanayoyapitia lakini wanajua yakwamba MUNGU Atabadilisha kwa mda wowote.

5⃣. KUPOKEA CHAPEO YA WOKOVU
Kichwa chetu kijazwe na wokovu, sababu kichwa njo
“Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;”
— Waefeso 6:17 (Biblia Takatifu)
“Akajivika haki k**a deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu k**a joho.”
— Isaya 59:17 (Biblia Takatifu)
6⃣KWA SALA
MKRISTO yeyote anapaswa kuwa imara kwa kusoma Biblia, sababu Biblia inasema kwamba Maneno ya Mungu iwe Taa ya miguu yetu, sasa Biblia ni jambo Muhimu saana kwa Mkristo, sio k**a kumiliki Biblia tuh ndani ya nyumba yako lakini kuisoma mara kwa mara

7⃣KWA MAOMBI
Maombi ni silaha kubwa sana, kuomba kuusu mambo yote, kuwaombea watakatifu, wagonjwa na ulinzi, ukingo,..
Silaha zote izo zinatumika kwa kushirikiana k**a vile uniform ya shule, mwanafunzi hata awe tajiri wala maskini anatakiwa kuvaa uniform ya shule ili aweze kuingia shuleni.
Shetani ananguruma k**a mbwa mwitu, lakini hata angurume namna gani hawezi kukushinda k**a unavaa silaha.

Maombi yako ya leo:
Baba yetu wa Mbinguni;nimejikuta kwamba sivai silaha zote, ninauzaifu katika hali ya kiroho, uzaifu wakuomba, uzaifu wa kusoma Biblia, ... Naomba univike tena SILAHA ZA VITA VYA ROHO.

Mhubiri: BISHOP H.E
Mwandishi: Mr Prince Malipo Gideon Prince Malipo Gedeon Prima

Dzaleka Adonai International ChurchNENO La MUNGU Ni TaaPrince Malipo Gideon  20-01-2024Neno:  “Bali wote waliompokea ali...
20/01/2024

Dzaleka Adonai International Church
NENO La MUNGU Ni Taa
Prince Malipo Gideon
20-01-2024

Neno:

“Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”
— Yohana 1:12 (Biblia Takatifu)

Hii ni Injili ya YOHANA ambayo alikua akimuelezea NENO, ambaye ni YESU KRISTU aliyeshuka kutoka mbinguni na kuuacha utukufu wa BABA nakujifanya kuwa mtu, ambaye hakukuwa wa kawaida, ALIKUA NI MUNGU MZIMA, kwasababu Yeye ni mtakatifu zaidi sana, hangelimsogelea mtu(Sisi wenye zambi) ikabidi avae mwili ili aje atukomboe, Sasa yeye ni muumbaji wa kila kitu biblia inasema kila kitu kilifanyika kwaajili yake YOHANA 1:1-
Sasa Neno huyo akaonekana k**a NURU na UPENDO lakini nuru hio haikupenya katika dunia Sababu aliowajia walimkataa (Wayahudi) basi naye akawaendea mataifa ambao ni sisi na ```AKAJA NA UWEZO WAKUWAWEKA WATU WOTE WAMUAMINIO WAWE WANA WA MUNGU.```
Nikuulize neno Mpendwa:
🔹Wewe unamuamini nani?
Watu wengi huwa wanawaamini watu, na wana uhodari wakusema hawawezi kuishi bila watu hao, wengine madawa ya kienyeji na hao hujilinda na vitu mbalimbali k**a Hirizi, uchawi na hapo wanajisifia kuwa ni wana wa Mungu, lakini BIBLIA yangu inasema yakwamba wote waliompokea YESU KRISTU walipewa uwezo wakufanyika kuwa wana wa MUNGU na hao wanaliamini jina lake, Sijuwi wewe unaliamini jina gani mpendwa,
🔸je unawaamini wakuu wa majeshi ili upatwapo na shida watakusimamia? Ama unawaamini ndugu zako ma daktari uuguwapo watakuponya haraka?
Mimi nina YULE AMBAYE alipofika mbele ya kipofu akamponya: Marko 10 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁴⁶ Wakafika Yeriko; hata alipokuwa akishika njia kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano mkubwa, mwana wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa ameketi kando ya njia.


⁵² Yesu akamwambia, Enenda zako, imani yako imekuponya. Mara akapata kuona; akamfuata njiani.

Yule Bartimayo alimwamini YESU na kumuita naye Yesu akamfanya apate kuona.
Ndiomana nakusii mpendwa uweze kumpokea _YESU AWE BWANA NA MWOKOZI WAKO ILI UFANYIWE KUWA MWANA WA MUNGU._
Usiwategemee watu wala uchawi, wala mambo ya dunia hii wala wakuu wa nchi,
®Mungu yupo na anakuambia atatuweka kuwa huru kweli-kweli,
®K**a wewe ni mgonjwa atakuponya kweli-kweli,
®Mwenye zambi atakutakasa kweli-kweli,
Paulo na Sila walipokua gerezani walimwita na milango ya gereza ikafunguka.
BASI MPENDWA
Mpokeye YESU akuweke kuwa huru, akufanye kuwa mwana wa MUNGU.

JE UMEZALIWA MARA YA PILI: Omba ivi
*Bwana YESU mimi ni mwenye dhambi, naomba unisamee na nimekubali na kukupokea kuwa wewe ni Bwana na Mwokozi wangu na nitakutumikia siku zote za maisha yangu.*
Amen

Mnenaji: Mr. Prima Premier

Dzaleka Adonai International Church MAFUNDISHO YA JUMATANO 10-01-2024NENO: *KUTAMBUA BARAKA NAKUZILINDA*Mwalimu: *Rev. P...
10/01/2024

Dzaleka Adonai International Church
MAFUNDISHO YA JUMATANO 10-01-2024

NENO: *KUTAMBUA BARAKA NAKUZILINDA*

Mwalimu: *Rev. Pastor CHARLES KAYUMBA*

Mwanzo 1 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
²⁷ Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
²⁸ Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

```“Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?”```
— Mathayo 5:46 (Biblia Takatifu)

*“Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo.”*
— Mithali 10:22 (Biblia Takatifu)

BARAKA: BARAKA NI MAMLAKA NA UWEZO AMBAO MUNGU ANAMPATIA MTU KWAKUTIMIZA KITU FULANI

Kabla Mungu hajamubariki IBRAHIM alikua tajiri, alikua na kila kitu, lakini Mungu alimpatia MAMLAKA ambayo kila kitu kitakua chini ya mamlaka ya MUNGU CHINI YA ULINZI WA MUNGU ndiomana wakati Farao alimtamani Mke wa Ibrahim Biblia inasema kwamba MUNGU alimjia Farao kumkanya amwache Sara ili asije akaingia hatarini.

Baraka sio vitu tuonavyo wala tunavyogusa, Baraka ni kitu ambacho MUNGU anaweka ndani ya mtu kisichoonekana. Mfano wa AYUBU alipopoteza mali zake, wana wake na wanyama wake wote alikua anajua tuh k**a yeye ANA BARAKA NDANI MWAKE, hakumwacha MUNGU sababu alijua kwamba yeye ni njomana tunapaswa tofautisha Mafanikio na baraka.

🔷MAFANIKIO: Ni vitu ambavyo mtu hua anajishugulisha ili ajibu maitaji yake: pesa, mali, magari, utajiri...
🔷BARAKA: Ni kitu ambacho hakionekani kwa macho, lakini ni mamlaka ama uwezo ambao Mungu anawapatia watu ili afanye kitu chochote

Nazaidi ya yote tunapaswa kujua BARAKA ni kukua chini ya Ulinzi wa Mungu sababu adui zako wanapambana na Mungu,
Atakaye kunenea mabaya mabaya yake yanamrudilia, na akikutakia mema, mema nayo yanamrudilia.
Mtu akiwa CHINI YA NEEMA AMA WINGU WA MUNGU anakuaka na uwezo tele na mwisho wa baraka ni UZIMA WA MILELE.

Mwalimu: *Rev. Pastor
Mwandishi: *Mr. Prima Premier
LLike Page yetu NENO La MUNGU Ni Taa

NENO LA MUNGU NI TAA YA MIGUU YETU                    Zaburi: 119:105Mhubiri PRINCE MALIPO GEDEONNENI: LEO NI SIKU YAKOL...
31/12/2023

NENO LA MUNGU NI TAA YA MIGUU YETU
Zaburi: 119:105

Mhubiri PRINCE MALIPO GEDEON
NENI: LEO NI SIKU YAKO
Luka 19 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
² Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.

⁹ Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.

Hii ni Habari ya Zakayo, mtozahushuru katika mji was Yeriko, mtozahushuru ni mtumishi wa serikali yaani (analipisha kodi na pesa ya soko)
Sasa MTU huyo alikua mnyanganyi was hali ya juu, alikua akipewa pesa ya kodi ya watu kumi hakua nafikisha yote kwenye azina ya serikali, nahio ni shida kubwa ambayo watoza ushuru wengi wao wanaibia serikali katika masoko, mipaka na ma Barabara...
Biblia yangu inasema kwamba MTU huyo aliposikia k**a YESU anapita tajiri huyo alikua akijiuliza HUYO YESU NI MTU WA NAMNA GANI? Sasa kwasababu MTU huyo alikua mfupi wa kimo asingeliona YESU kwa sababu ya umati wa watu akaamua kupanda kwenye mti
Mpendwa:
🔥Je unataka kumuona YESU? Umefanya hatua gani? Zakayo alipanda kwenye mti nahio inamaanisha kua alikua na shauku yakumwona YESU...
YESU alipomwona Zakayo akamwita na Biblia inasema k**a Zakayo alishuka haraka na kamkaribisha kwa furaha...
🔥Nawe pia mpendwa
Mkaribishe YESU kwa furaha ili aingie maishani mwako, k**a Zakayo hakuangalia yeye ni tajiri was namna gani lakini aliangalia umuhimu was YESU MAISHANI MWAKE
Walipoingia nyumbani mwa ZAKAYO Biblia inasema alifanya mambo mawili
1️⃣ Aligawa Mali yake nakuwasaidia wakosaji
2️⃣ Aliwarudishia Mara NNE wale wote aliowanyanganya,
HIO ilionyesha kutubu zambi nakuonyesha alama upendo na kutubu zambi sake
Mpendwa YESU anapoingia maishani mwako kila hali mbaya inabadilika, jifunze kubadili mwenendo ili YESU aketi nakustarehe maishani mwako
Na hapo hapo YESU AKAMWAMBIA ZAKAYO : WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI MWAKO

Leo ni siku yako Mpendwa! Tafuta umwone YESU na umkaribishe nyumbani kwako kwakuzitubu zambi zako nakuziungama najua k**a wokovu utaingia maishani mwako na hapo YESU ATAKUA NDANI YAKO NAWE UTAKUA NDANI YAKE... Usiangalie cheo ulionayo, utajiri wako ama nguvu na urembo wako Fanya hatua YESU anasema Leo ni siku yako wokovu utaingia maishani mwako...
Karibu sana Mpendwa na MUNGU AKUBARIKI.
AMEN
Mhubiri: Prima Premier

Address

Dzaleka Refugee Camp
Lilongwe

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NENO La MUNGU Ni Taa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share