21/07/2026
SOMO: KUSUDI MAALUM LA MWANADAMU
Warumi 8:30
"Na wale aliowachagua tangu mwanzo, hao pia aliwaita..."
Mimi na wewe tumechaguliwa kabla ya kuumbwa kwa dunia. Mungu alikuwa na kusudi na maisha yetu tangu mwanzo.
Mwanzo 1:26–27
"Na Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu..."
Mimi na wewe tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Pia tumeumbwa kwa kusudi la Mungu. Sisi ni miungu wadogo, mbona sasa tunakata tamaa? Huku kuvunjika moyo kunatoka wapi?
Viumbe vyote alivitamka vikawa, lakini sisi Mungu alitufinyanga, akatupulizia pumzi ya uhai. Uhai wetu na wa wanyama haufanani, maana sisi tuna pumzi ya Mungu.
Kwa ajili ya kuumbwa na kufinyangwa, tuna kazi ya kufanya. Tunapotoka hapa, tutoke tukiwa hatujioni wadogo tena. Tamka: “Nimebarikiwa.”
Mungu alipotuumba alitubariki na akasema tuzae, tuongezeke. Tulipewa kuijaza nchi na kuitiisha. Chochote unachokitaja kiko chini ya uweza wako.
Tumepewa kutawala viumbe vyote vya angani na majini. Tuna mamlaka ya kila kitu: kuumba, kuharibu na kutengeneza. Tambua kuwa una kazi ya kumwakilisha.
Ambia moyo wako kwamba ni lazima uende sawasawa na kusudi la Mungu, maana tumepewa vyote. Mungu anangoja mimi na wewe tujitambue kuwa tunaweza.
Mungu hampi mtu jaribu asiloliweza. K**a ulijaribu kufanya vitu vikashindikana, usife moyo; endelea mbele. Hakuna mwenye kusudi la Mungu ambaye hapitii mapito.
1 Wakorintho 10:13
"Jaribu halikuwapata isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu... lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea..."
Kila jaribu, mlima au changamoto, jua kwamba haiko pale kukumaliza. Iko pale ili upate ushuhuda na Mungu ajitukuze.
Katika hali ya kushindwa, usichoke; ng’ang’ana mpaka utoboze. Chochote ambacho ni mlima, kisambaratishwe kwa maombi.
Kila jaribu lina mlango wa kupitia. Usikate tamaa mpaka siku ile mlango utakapotokea. Usichoke kuomba, kufanya ibada na kutumika.
Ili uweze kukitunza ulichopokea, ni lazima uombe. Chochote kigumu unachopitia, tengeneza toolbox, ukiweke ndani na umpige Ibilisi.
Esta 4:11–16
"...Na ni nani ajuaye k**a hukufikilia ufalme kwa wakati k**a huu?"
Popote ulipo, tambua una kazi ya kufanya. Mungu hakupi kazi kwa sababu anaweza, bali kwa sababu yeye anafanya ndani yako na kukuwezesha. Kile ambacho unakiona hakiwezekani, kifanye.
MAMBO UNAYOHITAJI KATIKA WITO
1. Uwe mtu wa maombi.
Elisha alikaa katika nafasi ya maombi hadi akajibiwa. Mngoje Bwana kwenye maombi.
2. Tengeneza watu wanaofanana na wewe.
Esta alitengeneza watu wa kufunga pamoja naye.
3. Soma Neno.
Nguvu ya maombi itakuja yenyewe.
4. Vua roho ya uoga, vaa roho ya mamlaka.
IBADA YA JUMAPILI
©️ASKOFU: DINA ADUO
Efatha Ministry Ukunda