Efatha Church Taveta

Efatha Church Taveta Efatha church...Healing and deliverance by the blood of Jesus

Karibu Mwezi JuniKwa sababu ya Agano la Damu ya Yesu, Mwezi huu Mpya, Wewe ni kiumbe KIPYA, ya kale yamepita tazama umek...
01/06/2024

Karibu Mwezi Juni

Kwa sababu ya Agano la Damu ya Yesu, Mwezi huu Mpya, Wewe ni kiumbe KIPYA, ya kale yamepita tazama umekuwa MPYA; Hivyo Shangwe hazitakoma Kwako.

Usiangalie mambo ya kale maana ya kale kamwe hayawezi kukustawisha, Wewe sio wa kale bali ni Mpya; hivyo zingatia Mapya©...
05/04/2024

Usiangalie mambo ya kale maana ya kale kamwe hayawezi kukustawisha, Wewe sio wa kale bali ni Mpya; hivyo zingatia Mapya

© Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

Vita yako haipo dhidi yako na shetani bali ipo dhidi yako mwenyewe katika AKILI yako© Mtume na Nabii Josephat Elias
15/03/2024

Vita yako haipo dhidi yako na shetani bali ipo dhidi yako mwenyewe katika AKILI yako

© Mtume na Nabii Josephat Elias

NAIBARIKI JUMAMOSI YANGU.BWANA ni Wokovu wangu na Ngome  ya Uzima wangu; mabaya HAYATANIPATA Mimi.Haleluya, YESU Nakupen...
09/03/2024

NAIBARIKI JUMAMOSI YANGU.

BWANA ni Wokovu wangu na Ngome ya Uzima wangu; mabaya HAYATANIPATA Mimi.

Haleluya, YESU Nakupenda.

NENO LASIKU Na, Mama Eliakunda Mwingira- Kanisa la EfathaTarehe 08/03/2024SOMO: BWANA NIUMBIE TABIA YAKO KATIKA MAISHA Y...
08/03/2024

NENO LASIKU

Na, Mama Eliakunda Mwingira- Kanisa la Efatha

Tarehe 08/03/2024

SOMO: BWANA NIUMBIE TABIA YAKO KATIKA MAISHA YANGU

Zaburi 20:1-9 “Bwana akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni. Azikumbuke sadaka zako zote, Na kuzitakabali dhabihu zako. Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote. Na tuushangilie wokovu wako, Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. Bwana akutimizie matakwa yako yote……..”

Bwana akaonekane katika maisha yako, wewe uliyekuwa umeinama ukainuke na Bwana akakupelekee msaada wakati unaohitaji, maana ni ahadi na mpango wake kwamba yeyote anayemkimbilia anamshika mkono na kumtegemeza.

UKIRI:
•Bwana nipe kutii sheria na maagizo yako maana ndipo utatii yale ninayokuomba, niondolee tabia ya maswali maswali na uniumbie tabia ya utii.

•Baba yangu wa mbinguni niumbie tabia ya uaminifu katika kukupenda wewe, uaminifu katika matoleo yangu, utumishi wangu na katika maisha yangu kwa ujumla. Umba tabia ya uaminifu ndani yangu na iwe ndio maisha yangu maana hivi ndivyo ulivyo wewe BABA yangu, k**a alivyo baba ndivyo alivyo mwana nipe kufanana na wewe Bwana.

•Eeh! BABA nipe kujitoa kwa ajili ya utukufu wa Jina lako, umeonesha mfano kwangu pale ulipomtoa mwanao wa pekee Yesu akafa msalabani kwa ajili yangu mimi niliyekuwa nimepote na leo nimepatikana, tabia hii iwe ya kwangu. Nipe kujitoa kwa ajili ya kazi yako na kwa ajili ya wengine, kutoa nguvu, mali zangu na kila nilichonacho kwa maana kila nilichonacho ni cha kwako, wewe umenipa ili nivitunze nakubali BWANA kuvitoa kwako wakati unaofaa na usiofaa.

NAIBARIKI IJUMAA YANGU.K**a BWANA alivyoushinda Ulimwengu, Mimi nami NIMESHINDA, na Hakuna cha Kunishinda kamwe, Mimi ni...
08/03/2024

NAIBARIKI IJUMAA YANGU.

K**a BWANA alivyoushinda Ulimwengu, Mimi nami NIMESHINDA, na Hakuna cha Kunishinda kamwe, Mimi ni MSHINDI.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

NENO LA SIKUNa, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la EfathaTarehe 07/03/2024SOMO: JIFUNZE KUVUMILIA CHANGAM...
07/03/2024

NENO LA SIKU

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha

Tarehe 07/03/2024

SOMO: JIFUNZE KUVUMILIA CHANGAMOTO UKIWA NDANI YA YESU

Zaburi 126:5-6 “Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha. Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Walio na hofu ya Mungu mara zote watafanya kwa ajili ya Mungu, wanafanya kwa machozi na maumivu kwa kumpenda Mungu wao na ndio hao watakao vuna kwa kelele za furaha. Kwa sababu hiyo, Mungu anakuwa msaada wao na kamwe hawata kaa wapungukiwe na chochote kwa sababu wanalia kwa ajili ya wengine waokolewe. Wanataka kuona vitu vikisonga mbele na wanataka kuona watu wakiponywa na kubarikiwa.

K**a unataka kufurahia maisha yako hapa duniani;-
• Mpende Mungu kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote,
• Usilie kwa sababu mke wako au mume wako amekukosea bali lia kwa sababu unataka kuona watu walioumbwa kwa sura na mfano wa Mungu wakimjua Muumbaji wao.

Hutakaa uyabadilishe maisha yako k**a hujaelewa mapenzi ya Mungu kwako. Maumivu ndiyo njia ya kukupeleka kwenye ukuu wako, hivyo jifunze kuvumilia hayo maumivu katika Yesu.

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU.Nyumbani kwangu Kuna UTELE; Vyakula Vizuri, Mavazi Mazuri, Mazingira Mazuri, Usafiri Mzuri, maa...
07/03/2024

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU.

Nyumbani kwangu Kuna UTELE; Vyakula Vizuri, Mavazi Mazuri, Mazingira Mazuri, Usafiri Mzuri, maana Mimi ni MMILIKI wa Yale Yatamanikayo.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

NAIBARIKI JUMATANO YANGU.Nafurahi katika BWANA maana MIMI ni MMILIKI na MTAWALA.Haleluya, YESU Nakupenda.
06/03/2024

NAIBARIKI JUMATANO YANGU.

Nafurahi katika BWANA maana MIMI ni MMILIKI na MTAWALA.

Haleluya, YESU Nakupenda.

NENO LA SIKU.Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha.Tarehe: 05/03/2024.SOMO: ANZA NDOA YAKO NA BWA...
05/03/2024

NENO LA SIKU.

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha.

Tarehe: 05/03/2024.

SOMO: ANZA NDOA YAKO NA BWANA.

Mwanzo 2:18 "BWANA Mungu akasema, si vema huyu mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye."

Mungu hazuii mtu kuolewa au kuoa mwenzi anayemtaka lakini sio kila Mume au Mke mtu amepewa na Bwana. Watu wanaofuata utaratibu wa Kiungu katika ndoa hata wakikosana hawata achana kwa sababu Bwana ataleta suluhisho.

Mkianza ndoa kwa Utakatifu mtamaliza kwa Utakatifu na ndoa za aina hii hata k**a wanaanza bila kitu Watastawi na kuacha Baraka kwa uzao wao. Siri ya kuishi maisha Matakatifu ni Ustawi na hakuna Kuzeeka bali kuna kuhuishwa kwani ni ahadi ya Mungu.

Hata hivyo ukianza ndoa vibaya unadhulumiwa haki yako ya kustawi, kwa hiyo usianze uchumba kwa kuzini huo ni ujinga na dhambi ambayo huzeesha. Ni vizuri ukaanza ndoa yako na Bwana.

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.Familia yangu ni NZURI na BORA, Mke / Mume wangu ni MZURI na BORA, Watoto Wangu ni WAZURI na BOR...
05/03/2024

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.

Familia yangu ni NZURI na BORA, Mke / Mume wangu ni MZURI na BORA, Watoto Wangu ni WAZURI na BORA na Ndoa yangu ni NZURI na BORA. Mimi ni MMILIKI.

Haleluya, YESU Tunakupenda.

Address

Chachewa
Taveta
80302

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Taveta posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share