19/02/2026
NIFUNGE NINI KWARESMA.?
โข Hili ni swali tunalojiuliza wengi, ila majibu yake ni k**a ifuatavyo:
1. Funga dhambi upate utakatifu.
2. Funga huzuni upate furaha.
3. Funga majivuno upate utukufu.
4. Funga wivu upate baraka.
5. Funga kinyongo upate faraja.
6. Funga uchoyo upate neema.
7. Funga dharau upate heshima.
8. Funga hofu upate imani.
9. Funga kiburi upate unyenyekevu.
10. Funga hasira upate upole.
11. Funga ujinga upate hekima.
12. Funga umbea upate amani.
13. Funga matusi upate uchaji.
14. Funga aibu upate ujasiri.
15. Funga chuki upate marafiki.
16. Funga uvivu upate mafanikio.
17. Funga ulevi upate afya.
18. Funga uzinzi upate wongofu.
19. Funga roho mbaya upate upendo.
20. Funga starehe upate muda wa sala.
โข Mpendwa! Yatupasa kipindi hiki cha Kwaresima tufunge yote yaliyo mabaya, ili tupate mema tusiyoyatarajia kutoka kwa Muumba wetu. Hivyo Kwaresima ya mwaka huu, ikawe ya tofauti sana maishani mwetu.
NAWATAKIA MAANDALIZI MEMA YA KWARESMA.