Yesu ndiye njia

Yesu ndiye njia JESUS IS GOD
Helping the Thinker Believe. Helping
the Believer Think.

05/01/2026

Quran inataja Arshi ya ALLAH mara nyingi, hasa kuhusiana na mamlaka yake au ukuu wake juu ya viumbe:

QURAN 57:4-5

هُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۚ يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنْزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا ۖ وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنْتُمْ ۚ وَاللَّهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ

Al-Barwani

Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita; kisha akakaa vyema juu ya enzi. Anayajua yanayo ingia katika ardhi na yanayo toka humo, na yanayo teremka kutoka mbinguni, na yanayo panda humo. Naye yu pamoja nanyi popote mlipo. Na ALLAH ni Mwenye kuyaona mnayo yatenda.

� New to streaming or looking to level up? Check out StreamYard and get $10 discount! �

30/11/2025

The Arab dilemma

23/10/2025

Kuna nini imefichwa?
Anasimulia Zaid Bin Thabit, Abubakar aliniita wakati watu wa Yamamah walipouwawa, nilikwenda kwake na nilimkuta Umar bin Khattab r.a amekaa naye. Abubakar aliniambia kwamba, Umar alikuja kwangu na kuniambia, 'Wahifadhi (Quraa) Quran wengi wamefariki dunia siku ya vita vya Yamamah ninachelea wengi wao wanaweza kuwa mashahidi katika vita vingine na sehemu kubwa ya Quran kupotea. Kwa hiyo nakushauri wewe Abubakar utoe amri Quraan ikusanywe. Nilimwambia Umar; Unawezaje kufanya jambo ambalo mjumbe wa Allah hakulifanya? Umar akajibu 'Wallah hili ni jambo zuri la kufanywa, Umar aliendelea kunishawishi nikubali pendekezo lake mpaka Allah alipofungua kifua changu na kuanza kuona uzuri wa rai ya Umar. Kisha Abubakar aliniambia, wewe ni kijana mwerevu, na hatuna mashaka nawe. Ulikuwa ukiandika wahyi kwa zama za Mjumbe wa Allah s.a.w kwa hiyo tafuta maandiko ya Quraan na yakusanye yawe kitabu kimoja."
Wa llahi! K**a wangeniamuru kuhamisha moja ya milima isingelikuwa mizito k**a.ombi ili la kukusanya Quran. Kisha nikamwambia Abubakar, 'Unafanyaje jambo ambalo mtume s.a.w halilifanya? Abubakar aliendelea kunishawishi nikubaliane na rai yake mpaka Allah alipofunua kifua changu kwa vile alichofunua kifua cha Abubakar na Umar. Kwa hiyo nilianza kuitafuta Quraan na kuikusanya kutokana na yale yaliyoandikiwa juu yake, makuti ya mitende, mawe meupe membamba na kutoka kwa watu walioijua kwa moyo, mpaka nilipoipata ayah ya mwisho ya Suratul al Tawbah kwa Abi Khuzaimah Al Ansari, na Ayah hiyo niliikuta kwake tu. Ayah yenyewe ni hii; "
Hakika amekwisha kujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa waumini ni mpole na mwenye huruma. Basi wakigeuka wewe sema: Allaah ananitosheleza. Hapana mungu isipokuwa yeye tu. Mimi namtegemea yeye na yeye ndiye Mola mlezi wa Kiti kikuu cha enzi. Quran 9:128-129.
Muswada kamili ulibaki kwa Abubakar mpaka alipofariki dunia, kisha ukawa kwa Umar r.a mpaka alipofariki dunia, kisha kwa Hafsa Binti ya Umar (Mke wa Mtume). Al Bukhari Hadith Na 4986.
Sahih al-Bukhari 4986
حَدَّثَنَا مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ، عَنْ إِبْرَاهِيمَ بْنِ سَعْدٍ، حَدَّثَنَا ابْنُ شِهَابٍ، عَنْ عُبَيْدِ بْنِ السَّبَّاقِ، أَنَّ زَيْدَ بْنَ ثَابِتٍ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ أَرْسَلَ إِلَىَّ أَبُو بَكْرٍ مَقْتَلَ أَهْلِ الْيَمَامَةِ فَإِذَا عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ عِنْدَهُ قَالَ أَبُو بَكْرٍ ـ رضى الله عنه ـ إِنَّ عُمَرَ أَتَانِي فَقَالَ إِنَّ الْقَتْلَ قَدِ اسْتَحَرَّ يَوْمَ الْيَمَامَةِ بِقُرَّاءِ الْقُرْآنِ وَإِنِّي أَخْشَى أَنْ يَسْتَحِرَّ الْقَتْلُ بِالْقُرَّاءِ بِالْمَوَاطِنِ، فَيَذْهَبَ كَثِيرٌ مِنَ الْقُرْآنِ وَإِنِّي أَرَى أَنْ تَأْمُرَ بِجَمْعِ الْقُرْآنِ‏.‏ قُلْتُ لِعُمَرَ كَيْفَ تَفْعَلُ شَيْئًا لَمْ يَفْعَلْهُ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ عُمَرُ هَذَا وَاللَّهِ خَيْرٌ‏.‏ فَلَمْ يَزَلْ عُمَرُ يُرَاجِعُنِي حَتَّى شَرَحَ اللَّهُ صَدْرِي لِذَلِكَ، وَرَأَيْتُ فِي ذَلِكَ الَّذِي رَأَى عُمَرُ‏.‏ قَالَ زَيْدٌ قَالَ أَبُو بَكْرٍ إِنَّكَ رَجُلٌ شَابٌّ عَاقِلٌ لاَ نَتَّهِمُكَ، وَقَدْ كُنْتَ تَكْتُبُ الْوَحْىَ لِرَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَتَتَبَّعِ الْقُرْآنَ فَاجْمَعْهُ فَوَاللَّهِ لَوْ كَلَّفُونِي نَقْلَ جَبَلٍ مِنَ الْجِبَالِ مَا كَانَ أَثْقَلَ عَلَىَّ مِمَّا أَمَرَنِي مِنْ جَمْعِ الْقُرْآنِ قُلْتُ كَيْفَ تَفْعَلُونَ شَيْئًا لَمْ يَفْعَلْهُ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ هُوَ وَاللَّهِ خَيْرٌ فَلَمْ يَزَلْ أَبُو بَكْرٍ يُرَاجِعُنِي حَتَّى شَرَحَ اللَّهُ صَدْرِي لِلَّذِي شَرَحَ لَهُ صَدْرَ أَبِي بَكْرٍ وَعُمَرَ ـ رضى الله عنهما ـ فَتَتَبَّعْتُ الْقُرْآنَ أَجْمَعُهُ مِنَ الْعُسُبِ وَاللِّخَافِ وَصُدُورِ الرِّجَالِ حَتَّى وَجَدْتُ آخِرَ سُورَةِ التَّوْبَةِ مَعَ أَبِي خُزَيْمَةَ الأَنْصَارِيِّ لَمْ أَجِدْهَا مَعَ أَحَدٍ غَيْرَهُ ‏{‏لَقَدْ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مِنْ أَنْفُسِكُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِتُّمْ‏}‏ حَتَّى خَاتِمَةِ بَرَاءَةَ، فَكَانَتِ الصُّحُفُ عِنْدَ أَبِي بَكْرٍ حَتَّى تَوَفَّاهُ اللَّهُ ثُمَّ عِنْدَ عُمَرَ حَيَاتَهُ ثُمَّ عِنْدَ حَفْصَةَ بِنْتِ عُمَرَ ـ رضى الله عنه ـ‏.‏
Reference : Sahih al-Bukhari 4986
In-book reference : Book 66, Hadith 8
USC-MSA web (English) reference : Vol. 6, Book 61, Hadith 509

YESU NDIYE NJIAMwalimu wa Sunday School alikuwa anafundisha darasa lake aya ya kumbukumbu: "Yesu akamwambia, Mimi ndimi ...
28/07/2025

YESU NDIYE NJIA

Mwalimu wa Sunday School alikuwa anafundisha darasa lake aya ya kumbukumbu: "Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima." (Yohana 14:6.)

Alitaka watoto waelewe vizuri, akawauliza: "Watoto, ina maana gani tunaposema Yesu ndiye njia?"

Juma, mtoto mcheshi wa darasani, akainua mkono kwa haraka.
Mwalimu akasema kwa tabasamu, “Ndiyo Juma?”

Akasimama na kusema kwa ujasiri:
"Ina maana ukiwa hujui unaenda wapi, fuata tu Yesu, maana mara ya mwisho tulipopotea njiani, mama alimwambia baba, ‘Hujui njia kabisa. Basi mwache Yesu ashike usukani!’" 😄

Darasa zima likavunjika kwa kicheko… hata mwalimu alicheka sana.

Umewahi kumwachia Yesu ashike usukani wa maisha yako, au bado unaendesha bila ramani?

29/05/2025

Ungana nami tunapo barikiwa pamoja kwa kusikia jinsi MUNGU alivyomwokoa kaka Abel kutoka katika minyororo ya Uislamu

12/12/2024

JE TAMKO ILI ALLAH LINA MAANA GANI? JE MAANA YAKE NI MWENYEZI MUNGU? JE TAMKO ILI LINA WINGI WAKE K**A VILE MUNGU- MIUNGU AU JINSI YAKE YA K**E K**A WALIVYOKUWA NA MUNGU WA K**E WAARABU WA ZAMA ZA UJAHILLIYA YAANI WAKAWA NA ALLAH NA ALLAT? IKIWA ALLAH MAANA YAKE MWENYEZI MUNGU BASI JE JINA LA MUNGU ANAYEABUDIWA MSIKITINI NI LIPI?

21/11/2024

QURAN 33:56. Hakika ALLAH na Malaika wake wanamsalia Nabii. Enyi mlio amini! Msalieni na mumsalimu kwa salamu.

08/05/2024

Yesu Kristo - Mwana wa Mungu Anayejua Yote
Katika somo ili, nitakuwa nikinukuu maandiko kutoka katika maandishi ya Agano Jipya ili kuthibitisha kwamba Bwana Yesu Kristo anajua mambo yote k**a vile kujua mioyo ya watu wote, ambayo ni mojawapo ya sifa muhimu za Mungu. Kusudi la kuandaa orodha hii ya marejeo ni kufidia mwito unaorudiwa na wapinga Utatu kwenye vifungu ambapo Yesu anaelezwa kutojua mambo yote au kukua katika hekima na kimo (rej. Marko 13:32; Luka 2:40, 52) ), huku wakipuuza ushuhuda wa Biblia wa wazi wa Kristo kujua yote. Ukweli rahisi ni kwamba kulingana na Maandiko yaliyovuviwa BWANA YESU alikuwa MUNGU KWELI kutoka kwa MUNGU na katika uungu huo Yesu anajua kila kitu. LAKINI huku pia akiwa hajui mambo yote kuhusiana na ufahamu wake wa kibinadamu ambao anao kutokana na asili yake ya kibinadamu TANGU PALE ALIPOZALIWA KWA MARIAMU. Huenda tusiweze kuelewa hili au kueleza jinsi hii inavyofanyika, lakini ukweli rahisi wa mambo ni kwamba hiki ndicho Biblia Takatifu inafundisha.
katika somo la pili baada ya ushahidi huu nitatazama maandiko k**a vile Mathayo 24:36, Luka 2:52 nakadhalika, ili kujibu swali je Bwana Yesu anayajua majira ya Kurudi kwake?
Zaidi ya hayo, baadhi ya mistari hii pia inajumuisha kauli nyingine wazi zinazo shuhudia Uungu wa Kristo, k**a vile Yesu kudai kuwa Bwana wa Sabato au kuwa na uwezo wa kusamehe dhambi, ambayo inatia nguvu ukweli wa Kristo kuwa mjuzi wa yote. Ni wazi kuwa, ikiwa Kristo anaelezewa k**a Mungu katika mwili basi lazima awe mjuzi wa yote kwa kuwa hii ni sifa muhimu ya Uungu.

Baada ya kusema hayo kwenye utangulizi sasa tunaendelea na ushahidi wa maandiko.

Marko 2:5 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako. 6Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao, 7 Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu? 8Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu? 9Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende? 10Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza), 11Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako. 12Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Hatujawahi kuona jambo k**a hili kamwe. Tazama pia Mathayo 9:4; Luka 5:22

Mathayo 12:25Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yoyote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

Luka 6:5Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

6 Ikawa siku ya sabato nyingine aliingia katika sinagogi akafundisha; na mlikuwamo mtu ambaye mkono wake wa kulia umepooza. 7 Na Waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimvizia, ili waone k**a ataponya siku ya sabato; kusudi wapate neno la kumsh*takia. 8Lakini yeye akayatambua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, Ondoka, simama katikati; akaondoka akasimama. 9Ndipo Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, Je! Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya; kuponya roho au kuangamiza? 10Akawakazia macho wote pande zote, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena. 11Wakajawa na uchungu, wakashauriana wao kwa wao wamtendeje Yesu.

Luka 9:46 Wakaanza kuhojiana, ni nani atakayekuwa mkubwa miongoni mwao. 47Naye Yesu alipotambua mawazo ya mioyo yao, alitwaa mtoto mdogo akamweka karibu naye, 48 akawaambia, Yeyote atakayempokea mtoto huyu kwa jina langu anipokea mimi; na yeyote atakayenipokea mimi ampokea yeye aliyenituma. Kwa kuwa aliye mdogo miongoni mwenu nyote huyo ndiye mkubwa.

Luke 11:16 Wengine walimjaribu, wakimtaka afanye ishara itokayo mbinguni. 17Naye akajua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme uliofitinika wenyewe kwa wenyewe hufanyika ukiwa; na nyumba juu ya nyumba huanguka.

Yohana 2:23Hata alipokuwapo Yerusalemu kwenye sikukuu wakati wa Pasaka, watu wengi waliamini jina lake, walipoziona ishara zake alizozifanya. 24Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; 25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.

Yohana 6:64 Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti.

Yohana16:16 Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni; na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona. 17Basi baadhi ya wanafunzi wake wakasemezana, Neno gani hilo asemalo, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona? Na hilo, Kwa sababu naenda zangu kwa Baba? 18Basi walisema, Neno gani hilo asemalo; hilo, Bado kitambo kidogo? Hatujui asemalo. 19Yesu alifahamu ya kwamba wanataka kumwuliza, akawaambia, Ndilo hilo mnaloulizana, ya kuwa nilisema, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona?

Yohana 16:25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa inakuja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba. 26Na siku ile mtaomba kwa jina langu, wala siwaambii ya kwamba mimi nitawaombea kwa Baba; 27 kwa maana Baba mwenyewe awapenda kwa kuwa ninyi mmenipenda mimi, na kusadiki ya kwamba mimi nilitoka kwa Baba. 28Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja hapa ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu; na kwenda kwa Baba. 29 Basi wanafunzi wake wakasema, Tazama, sasa wasema waziwazi, wala huneni mithali yoyote. 30 Sasa tumejua ya kuwa wewe wafahamu mambo yote, wala huna haja ya mtu akuulize; kwa hiyo twasadiki ya kwamba ulitoka kwa Mungu. 31Yesu akawajibu, Je! Mnasadiki sasa? 32 Tazama, saa inakuja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; lakini mimi siko peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami. 33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

Yohana 21:17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.

Matendo ya Mitume 1:1 Kitabu kile cha kwanza nilikiandika, Theofilo, kuhusu mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, 2 hadi siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; 6 Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? 7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. 21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, 24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuoneshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

Warumi 2:16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na Injili yangu, kwa Kristo Yesu.

1Wakorintho 4:4 Maana sijui sababu ya kujish*taki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana. 5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulika yaliyositirika katika giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.

Wakolosai 2:2 ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo; 3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Ufunuo wa Yohana 2:18 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo anenayo Mwana wa Mungu, yeye aliye na macho yake k**a muali wa moto, na miguu yake mfano wa shaba iliyosuguliwa sana. 19Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.

23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye fikira na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.

Ufunuo 22:12 Tazama, naja upesi, na malipo yangu yako pamoja nami, kumlipa kila mtu k**a kazi yake ilivyo. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, ili wawe na haki ya kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake 20Yeye ayashuhudiaye haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu. 21Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.

Sasa ili kufahamu kikamilifu kauli hizi na uzito wake zilinganishe na yale ambayo maandiko yafuatayo yanasema kuhusiana na ujuzi wa Mungu:

1Yohana 3:20ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.

Zaburi 44:21 Je! Mungu hangegundua jambo hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.

1Wafalme 8:39 basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote);

1Mambo ya Nyakati 28: 9 Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele

ISAYA 40: 10 Tazameni, Bwana Mungu atakuja k**a shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia;Tazameni, thawabu yake i pamoja naye,

Na fidia yake i mbele zake. 11 Atalilisha kundi lake k**a mchungaji,

Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole

ISAYA 62:11 Tazama, BWANA ametangaza habari mpaka mwisho wa dunia, Mwambieni binti Sayuni, Tazama, wokovu wako unakuja; Tazama, thawabu yake iko pamoja naye, Na malipo yake yako mbele zake.

YEREMIA 17; 10 Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake. Tazama pia 11:20; 29:23; Zaburi 62:12; Methali 24:12



Kwa kuzingatia Ushahidi huu wa maandiko, ni wazi kabisa kwamba Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanatangaza kwamba Yesu Kristo anajua yote. Bila shaka anayajua mambo yote, hasa mawazo na makusudio ya kila moyo wa mwanadamu. Waandishi waliovuviwa wanafikia hata kuchukua na kuiga lugha ile ile ambayo baadhi ya vifungu vya Biblia hutumia kuelezea ujuzi wa Yehova na kuihusisha kwa Kristo! Linganisha, kwa mfano Mathayo 16:27, Ufunuo 2:23, na 22:12 na Isaya 40:10 na Yeremia 17:10.



Haya yote yanathibitisha kwa uthabiti kwamba Yesu Kristo ndiye Mungu-Mwanadamu kulingana na Maandiko yenye pumzi ya Mungu. Kwa hivyo, Kristo hakujua mambo yote kuhusiana na ufahamu wake wa kibinadamu, ila katika asili yake ya kimungu yeye ni Bwana wa utukufu na udhihilisho kamili wa Mungu asiyeeleweka na asiyeweza kueleweka kwani mungu amezidi Mawazo yetu ya kiutu:



Luka 10:21 Saa ile ile alishangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza. 22 Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia. Tazama Mathayo 11:25-27



Yohana 1:18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.

Yohana 6:44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenituma; nami nitamfufua siku ya mwisho. 45 Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu. 46 Si kwamba mtu amemwona Baba, ila yeye atokaye kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.

Yohana 12: 44 Naye Yesu akapaza sauti, akasema, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenituma. 45 Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenituma. 46 Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.

Yohana 14:6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. 7K**a mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. 8Filipo akamwambia, Bwana, utuoneshe Baba, yatutosha. 9 Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuoneshe Baba? 10 Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. 11 Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. 12 Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. 13 Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. 14 Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.

2Wakorintho 4:4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, wasiione nuru ya Injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. 5 Kwa maana hatujihubiri wenyewe, bali Kristo Yesu ya kuwa ni Bwana; na sisi wenyewe kuwa tu watumishi wenu kwa ajili ya Yesu. 6 Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.

07/05/2024

Mtumishi Aketiye kwenye kiti cha enzi cha YEHOVA

Chaka Wa Musa:

Nabii Isaya anatangaza kwamba Mtumishi huyu angeinuliwa sana na kutukuzwa baada ya kutoa uhai wake kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi:

ISAYA 52: 13 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.

Kinachofanya jambo hili kuwa la kustaajabisha zaidi ni kwamba Nabii Isaya anatumia maneno yaleyale kuelezea kuinuliwa kwa Mtumishi ambayo anayatumia anapozungumza juu ya hadhi ya juu ya Yehova ya kutawazwa juu ya uumbaji!

Zingatia mifano ifuatayo:

ISAYA 6:1 Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. 2. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. 3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake. 4 Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. 5Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, BWANA wa majeshi. 6 Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; 7akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.

8 Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.

Na:

ISAYA 57:15 Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

Isaya anamwona Yehova ameketi juu ya kiti cha enzi kilichoinuka sana kwa kuwa yeye ndiye Mtakatifu akaaye mahali pa juu. Tena:

ISAYA 33:5 BWANA/YEHOVA ametukuka; kwa maana anakaa juu; amejaza Sayuni hukumu na haki.

10 Basi, sasa nitasimama; asema BWANA/YEHOVA; sasa nitajiinua, sasa nitajitukuza. Mungu akaaye juu atainuka ili atukuzwe na kuinuliwa.

Kinachofanya kutukuzwa na kuinuliwa kwa Mtumishi kushtua sana ni kwamba Isaya alitangaza wazi kwamba Yehova peke yake ndiye atakayeinuliwa, na kila mtu atanyenyekezwa mbele zake:

ISAYA 2:11 Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye BWANA/YEHOVA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo. 12Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA/ YEHOVA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini. 13Na juu ya mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu na kuinuka, na juu ya mialoni yote ya Bashani; 14na juu ya milima mirefu yote, na juu ya vilima vyote vilivyoinuka; 15na juu ya kila mnara mrefu, na juu ya kila ukuta ulio na boma; 16na juu ya merikebu zote za Tarshishi, na juu ya kila taswira ipendezayo. 17Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA/YEHOVA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.

Vile vile jambo la kushtua ni namna ambayo Mtume Petro anatumia maneno yaleyale ambayo Isaya anafanya katika maandiko haya kueleza Yesu akiinuliwa na kuinuliwa kuketi kwenye kiti cha enzi kwenye mkono wa kuume wa Mungu wa mbinguni k**a Bwana Mwenye Enzi Kuu!

MATENDO YA MITUME 2:29 Wanaume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo. 30 Basi kwa kuwa ni Nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa wazawa wake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi; 31 yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu. 32Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake. 33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hadi mkono wa kulia wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia. 34 Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,

Bwana alimwambia Bwana wangu,

Keti upande wa mkono wangu wa kulia.

35Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

36 Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulubisha kuwa Bwana na Kristo.

Petro hata anazungumza juu ya Mungu kuwa amemtukuza Yesu ambaye Wayahudi walimwua, ingawa yeye ndiye Mtakatifu na Mwenye Haki ambaye ndiye Mwanzilishi wa Uzima:

MATENDO YA MITUME 3:13 Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe. 14 Bali ninyi mlimkana yule Mtakatifu, yule Mwenye haki, mkataka mpewe mwuaji; 15 mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambaye Mungu amemfufua katika wafu; na sisi tu mashahidi wake. 16Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

It is obvious that Peter is not only alluding to Isaiah 52:13 but also to the Isaiah 53:11 where the Servant is called the Righteous or Just One:

Ni dhahiri kwamba Petro hazungumzii Isaya 52:13 tu bali pia Isaya 53:11 ambapo Mtumishi anaitwa Mwenye Haki au mwadilifu:

ISAYA 52:13 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.

ISAYA 53: 10 Lakini BWANA aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi,Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya BWANA/YEHOVA yatafanikiwa mkononi mwake;

11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika.

Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki

Atawafanya wengi kuwa wenye haki;

Naye atayachukua maovu yao.

Hii inachoonyesha ni kwamba Yesu kwa Petro hakuwa tu Mtumishi wa Mungu tu, bali pia Bwana Mungu ambaye amefufuka kutoka kwa wafu ili kujitukuza na kujiinua sana juu ya uumbaji!

Mtumishi aliye Mkono wa Yehova

Nabii Isaya anatumia neno “Mkono wa Yehova” kurejelea nguvu ambazo Mungu hutumia anapoamua kufanya jambo fulani peke yake. Hapa kuna mifano michache:

ISAYA 30:30 Naye BWANA/YEHOVA atawasikizisha watu sauti yake ya utukufu, naye atawaonesha jinsi mkono wake ushukavyo, na ghadhabu ya hasira yake, na mwako wa moto uangamizao, pamoja na dhoruba, na tufani, na mvua ya mawe ya barafu.

ISAYA 51:5 Haki yangu i karibu, wokovu wangu umekuwa wazi, na mkono Wangu Utawahukumu makabila ya watu; visiwa vitaningoja, navyo vitautumainia mkono wangu.

9 Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana/YEHOVA;

Amka k**a katika siku zile za kale, Katika vizazi vile vya zamani.

10 Si wewe uliyemkatakata Rahabu? Uliyemchoma yule joka? Si wewe uliyeikausha bahari,

Na maji ya vilindi vikuu; Uliyevifanya vilindi kuwa njia, Ili wapite watu waliokombolewa?

ISAYA 63:1 Ni nani huyu atokaye Edomu, Atokaye Bosra akiwa na mavazi yenye madoa mekundu?

Huyu aliye na nguo za fahari, Anayekwenda katika ukuu wa uweza wake?

Ndimi nisemaye kwa haki, Niliye hodari wa kuokoa. 2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu,

Na nguo zako k**a za mtu akanyagaye zabibu? 3 Nilikanyaga shinikizoni peke yangu;

Wala katika watu hakuwapo mtu pamoja nami; Naam, niliwakanyaga kwa hasira yangu,

Niliwaponda kwa ghadhabu yangu; Na mavazi yangu yametiwa madoa kwa damu yao,

Nami nimezichafua nguo zangu zote. 4Maana siku ya kisasi ilikuwamo moyoni mwangu,

Na mwaka wao niliowakomboa umewadia. 5 Nikatazama, wala hapakuwa na wa kunisaidia;

Nikashangaa kwa kuwa hakuna mwenye kutegemeza; Basi, mkono wangu mwenyewe uliniletea wokovu, Ghadhabu yangu ndiyo iliyonitegemeza. 6 Nikayakanyaga makabila ya watu kwa hasira yangu, Nikawalevya kwa ghadhabu yangu, Nami nikaimwaga damu yao chini.

ISAYA 59: 15Naam, kweli imepunguka kabisa, na yeye auachaye uovu ajifanya kuwa mateka; naye BWANA akaona hayo, akachukizwa kwa kuwa hapana hukumu ya haki. 16 Akaona ya kuwa hapana mtu, akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi; basi, mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu; na haki yake ndiyo iliyomsaidia. 17 Akajivika haki k**a deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu k**a joho. 18Kadiri ya matendo yao, kwa kadiri iyo hiyo atawalipa, ukali kwao wampingao, malipo kwa adui zake; naye atavirudishia visiwa malipo. 19 Basi, wataliogopa jina la BWANA/YEHOVA toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja k**a mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya BWANA. 20 Na Mkombozi atakuja Sayuni, kwa wao wa Yakobo waachao maasi yao, asema BWANA. 21 Tena kuhusu habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema BWANA; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema BWANA, tangu leo na hata milele.

Ni wazi kutokana na vifungu hivi kwamba Mkono wa YEHOVA unamrejelea Mungu mwenyewe akifanya kitendo maalum kwa uwezo wake mwenyewe bila msaada wa kiumbe chochote. Kwa hiyo inashangaza kumkuta Isaya akimrejelea Mtumishi kuwa ndiye Mkono wa Yehova unaoleta wokovu kwa mataifa!

ISAYA 52: 7 Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima Miguu yake aletaye habari njema, Yeye aitangazaye amani,

Aletaye habari njema ya mambo mema, Yeye autangazaye wokovu, Auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki! 8 Sauti ya walinzi wako! Wanapaza sauti zao, wanaimba pamoja; Maana wataona jicho kwa jicho, Jinsi BWANA arejeavyo Sayuni.

9Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja, Enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa; Kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake, Ameukomboa Yerusalemu.

10 BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu Machoni pa mataifa yote; Na ncha zote za dunia

Zitauona wokovu wa Mungu wetu. 11 Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA. 12 Maana hamtatoka kwa haraka, wala hamtakwenda kwa kukimbia, kwa sababu BWANA atawatangulia; na Mungu wa Israeli atawafuata nyuma; awalinde.

13 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana. 14 K**a vile wengi walivyokustaajabia, (uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu yeyote, na umbo lake zaidi ya wanadamu), 15 ndivyo atakavyowastusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu.

ISAYA 53: 1 Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?

2 Maana alikuwa mbele zake k**a mche mwororo, Na k**a mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.

Hapa twaona Mtumishi huyu akitambulishwa kuwa Mkono uleule ambao Yehova hubeba kwa mataifa yote kumtazama, Yule anayekua mbele za Yehova k**a mche mwororo na anayeleta wokovu wa Mungu hadi miisho ya dunia.

Kwa kustaajabisha, kitabu cha Ufunuo wa Yohana kinatoa taswira ya Isaya 63:1-6, ambapo Yehova anaelezewa kuwa amevaa vazi lililochovywa katika damu ya adui zake ambalo yeye peke yake alilikanyaga chini ya miguu yake katika shinikizo la mvinyo la ghadhabu yake, na kulitumia kwa Bwana Yesu Kristo!

UFUNUO WA YOHANA 19: 11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. 12 Na macho yake yalikuwa k**a muali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. 13 Naye amevikwa vazi lililoloweshwa katika damu, na jina lake anaitwa, Neno la Mungu. 14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. 15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili kwa upanga huo awapige mataifa. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. 16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.

17 Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njooni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu; 18mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.

19 Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake. 20 Yule mnyama akak**atwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao hao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wakiwa hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti; 21 na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.

Lakini njia pekee ambayo Mtumishi huyu anaweza kuitwa Mkono wa Yehova mwenyewe ni ikiwa Nabii Isaya aliamini kwamba huyu Mtumishi alikuwa tofauti na bado, wakati huo huo, sawa na Mungu. Kwa maneno mengine, Mtumishi k**a Mkono wa Yehova lazima awe sehemu ya ndani ya Utu wa Yehova mwenyewe, na kwa hivyo lazima awe na asili ya Mungu kikamilifu. Vinginevyo, Mtumishi huyu hangeweza kamwe kujulikana k**a Mkono wa Yehova.

Sasa njia pekee ambayo mwandishi Yohana aliyevuviwa angeweza kumwelezea Yesu kwa namna hii ni k**a aliamini kwamba Bwana aliyefufuka ni Mkono wa Yehova, na kwa hiyo Yehova Mungu aliyedhihishwa kwenye Mwili!

Ndimi ndugu yenu katika utumishi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi nyote.

Chaka wa Musa

Address

Valley Road
Nairobi
00100

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Yesu ndiye njia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Yesu ndiye njia:

Share