08/05/2024
Yesu Kristo - Mwana wa Mungu Anayejua Yote
Katika somo ili, nitakuwa nikinukuu maandiko kutoka katika maandishi ya Agano Jipya ili kuthibitisha kwamba Bwana Yesu Kristo anajua mambo yote k**a vile kujua mioyo ya watu wote, ambayo ni mojawapo ya sifa muhimu za Mungu. Kusudi la kuandaa orodha hii ya marejeo ni kufidia mwito unaorudiwa na wapinga Utatu kwenye vifungu ambapo Yesu anaelezwa kutojua mambo yote au kukua katika hekima na kimo (rej. Marko 13:32; Luka 2:40, 52) ), huku wakipuuza ushuhuda wa Biblia wa wazi wa Kristo kujua yote. Ukweli rahisi ni kwamba kulingana na Maandiko yaliyovuviwa BWANA YESU alikuwa MUNGU KWELI kutoka kwa MUNGU na katika uungu huo Yesu anajua kila kitu. LAKINI huku pia akiwa hajui mambo yote kuhusiana na ufahamu wake wa kibinadamu ambao anao kutokana na asili yake ya kibinadamu TANGU PALE ALIPOZALIWA KWA MARIAMU. Huenda tusiweze kuelewa hili au kueleza jinsi hii inavyofanyika, lakini ukweli rahisi wa mambo ni kwamba hiki ndicho Biblia Takatifu inafundisha.
katika somo la pili baada ya ushahidi huu nitatazama maandiko k**a vile Mathayo 24:36, Luka 2:52 nakadhalika, ili kujibu swali je Bwana Yesu anayajua majira ya Kurudi kwake?
Zaidi ya hayo, baadhi ya mistari hii pia inajumuisha kauli nyingine wazi zinazo shuhudia Uungu wa Kristo, k**a vile Yesu kudai kuwa Bwana wa Sabato au kuwa na uwezo wa kusamehe dhambi, ambayo inatia nguvu ukweli wa Kristo kuwa mjuzi wa yote. Ni wazi kuwa, ikiwa Kristo anaelezewa k**a Mungu katika mwili basi lazima awe mjuzi wa yote kwa kuwa hii ni sifa muhimu ya Uungu.
Baada ya kusema hayo kwenye utangulizi sasa tunaendelea na ushahidi wa maandiko.
Marko 2:5 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako. 6Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao, 7 Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu? 8Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu? 9Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende? 10Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza), 11Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako. 12Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Hatujawahi kuona jambo k**a hili kamwe. Tazama pia Mathayo 9:4; Luka 5:22
Mathayo 12:25Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yoyote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.
Luka 6:5Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
6 Ikawa siku ya sabato nyingine aliingia katika sinagogi akafundisha; na mlikuwamo mtu ambaye mkono wake wa kulia umepooza. 7 Na Waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimvizia, ili waone k**a ataponya siku ya sabato; kusudi wapate neno la kumsh*takia. 8Lakini yeye akayatambua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, Ondoka, simama katikati; akaondoka akasimama. 9Ndipo Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, Je! Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya; kuponya roho au kuangamiza? 10Akawakazia macho wote pande zote, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena. 11Wakajawa na uchungu, wakashauriana wao kwa wao wamtendeje Yesu.
Luka 9:46 Wakaanza kuhojiana, ni nani atakayekuwa mkubwa miongoni mwao. 47Naye Yesu alipotambua mawazo ya mioyo yao, alitwaa mtoto mdogo akamweka karibu naye, 48 akawaambia, Yeyote atakayempokea mtoto huyu kwa jina langu anipokea mimi; na yeyote atakayenipokea mimi ampokea yeye aliyenituma. Kwa kuwa aliye mdogo miongoni mwenu nyote huyo ndiye mkubwa.
Luke 11:16 Wengine walimjaribu, wakimtaka afanye ishara itokayo mbinguni. 17Naye akajua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme uliofitinika wenyewe kwa wenyewe hufanyika ukiwa; na nyumba juu ya nyumba huanguka.
Yohana 2:23Hata alipokuwapo Yerusalemu kwenye sikukuu wakati wa Pasaka, watu wengi waliamini jina lake, walipoziona ishara zake alizozifanya. 24Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; 25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.
Yohana 6:64 Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti.
Yohana16:16 Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni; na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona. 17Basi baadhi ya wanafunzi wake wakasemezana, Neno gani hilo asemalo, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona? Na hilo, Kwa sababu naenda zangu kwa Baba? 18Basi walisema, Neno gani hilo asemalo; hilo, Bado kitambo kidogo? Hatujui asemalo. 19Yesu alifahamu ya kwamba wanataka kumwuliza, akawaambia, Ndilo hilo mnaloulizana, ya kuwa nilisema, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona?
Yohana 16:25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa inakuja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba. 26Na siku ile mtaomba kwa jina langu, wala siwaambii ya kwamba mimi nitawaombea kwa Baba; 27 kwa maana Baba mwenyewe awapenda kwa kuwa ninyi mmenipenda mimi, na kusadiki ya kwamba mimi nilitoka kwa Baba. 28Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja hapa ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu; na kwenda kwa Baba. 29 Basi wanafunzi wake wakasema, Tazama, sasa wasema waziwazi, wala huneni mithali yoyote. 30 Sasa tumejua ya kuwa wewe wafahamu mambo yote, wala huna haja ya mtu akuulize; kwa hiyo twasadiki ya kwamba ulitoka kwa Mungu. 31Yesu akawajibu, Je! Mnasadiki sasa? 32 Tazama, saa inakuja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; lakini mimi siko peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami. 33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.
Yohana 21:17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
Matendo ya Mitume 1:1 Kitabu kile cha kwanza nilikiandika, Theofilo, kuhusu mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, 2 hadi siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; 6 Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? 7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. 21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, 24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuoneshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,
Warumi 2:16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na Injili yangu, kwa Kristo Yesu.
1Wakorintho 4:4 Maana sijui sababu ya kujish*taki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana. 5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulika yaliyositirika katika giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.
Wakolosai 2:2 ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo; 3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
Ufunuo wa Yohana 2:18 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo anenayo Mwana wa Mungu, yeye aliye na macho yake k**a muali wa moto, na miguu yake mfano wa shaba iliyosuguliwa sana. 19Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.
23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye fikira na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
Ufunuo 22:12 Tazama, naja upesi, na malipo yangu yako pamoja nami, kumlipa kila mtu k**a kazi yake ilivyo. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, ili wawe na haki ya kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake 20Yeye ayashuhudiaye haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu. 21Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.
Sasa ili kufahamu kikamilifu kauli hizi na uzito wake zilinganishe na yale ambayo maandiko yafuatayo yanasema kuhusiana na ujuzi wa Mungu:
1Yohana 3:20ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.
Zaburi 44:21 Je! Mungu hangegundua jambo hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.
1Wafalme 8:39 basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote);
1Mambo ya Nyakati 28: 9 Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele
ISAYA 40: 10 Tazameni, Bwana Mungu atakuja k**a shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia;Tazameni, thawabu yake i pamoja naye,
Na fidia yake i mbele zake. 11 Atalilisha kundi lake k**a mchungaji,
Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole
ISAYA 62:11 Tazama, BWANA ametangaza habari mpaka mwisho wa dunia, Mwambieni binti Sayuni, Tazama, wokovu wako unakuja; Tazama, thawabu yake iko pamoja naye, Na malipo yake yako mbele zake.
YEREMIA 17; 10 Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake. Tazama pia 11:20; 29:23; Zaburi 62:12; Methali 24:12
Kwa kuzingatia Ushahidi huu wa maandiko, ni wazi kabisa kwamba Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanatangaza kwamba Yesu Kristo anajua yote. Bila shaka anayajua mambo yote, hasa mawazo na makusudio ya kila moyo wa mwanadamu. Waandishi waliovuviwa wanafikia hata kuchukua na kuiga lugha ile ile ambayo baadhi ya vifungu vya Biblia hutumia kuelezea ujuzi wa Yehova na kuihusisha kwa Kristo! Linganisha, kwa mfano Mathayo 16:27, Ufunuo 2:23, na 22:12 na Isaya 40:10 na Yeremia 17:10.
Haya yote yanathibitisha kwa uthabiti kwamba Yesu Kristo ndiye Mungu-Mwanadamu kulingana na Maandiko yenye pumzi ya Mungu. Kwa hivyo, Kristo hakujua mambo yote kuhusiana na ufahamu wake wa kibinadamu, ila katika asili yake ya kimungu yeye ni Bwana wa utukufu na udhihilisho kamili wa Mungu asiyeeleweka na asiyeweza kueleweka kwani mungu amezidi Mawazo yetu ya kiutu:
Luka 10:21 Saa ile ile alishangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza. 22 Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia. Tazama Mathayo 11:25-27
Yohana 1:18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
Yohana 6:44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenituma; nami nitamfufua siku ya mwisho. 45 Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu. 46 Si kwamba mtu amemwona Baba, ila yeye atokaye kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
Yohana 12: 44 Naye Yesu akapaza sauti, akasema, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenituma. 45 Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenituma. 46 Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.
Yohana 14:6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. 7K**a mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. 8Filipo akamwambia, Bwana, utuoneshe Baba, yatutosha. 9 Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuoneshe Baba? 10 Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. 11 Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. 12 Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. 13 Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. 14 Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.
2Wakorintho 4:4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, wasiione nuru ya Injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. 5 Kwa maana hatujihubiri wenyewe, bali Kristo Yesu ya kuwa ni Bwana; na sisi wenyewe kuwa tu watumishi wenu kwa ajili ya Yesu. 6 Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.