13/03/2026
Bilingual Bible. Philippians 4:4-8
[4]Rejoice in the Lord alway: and again I say, Rejoice.
Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
[5]Let your moderation be known unto all men. The Lord is at hand.
Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
[6]Be careful for nothing; but in every thing by prayer and supplication with thanksgiving let your requests be made known unto God.
Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
[7]And the peace of God, which passeth all understanding, shall keep your hearts and minds through Christ Jesus.
Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
[8]Finally, brethren, whatsoever things are true, whatsoever things are honest, whatsoever things are just, whatsoever things are pure, whatsoever things are lovely, whatsoever things are of good report; if there be any virtue, and if there be any praise, think on these things.
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.