St. Peter the Apostle Catholic Parish Kikuyu

St. Peter the Apostle Catholic Parish Kikuyu This is the official page of the St Peter the Apostle Parish in Kikuyu.

Its a social platform for evangelisation

Church Location: https://maps.app.goo.gl/AZR599BSsibTp7pz5

07/09/2026

MASOMO YA MISA, SIKUKUU YA KUZALIWA BIKIRA MARIA MTAKATIFU,

SEPTEMBER 8, 2025
RANGI YA KILITURJIA: NYEUPE 🤍

SOMO LA KWANZA
MIKA 5:1—4a

Bwana atawatoa ninyi kwa maadui, mpaka yule mama mwenye mimba awe amejifungua.

Somo katika kitabu cha Nabii Mika

Bwana asema hivi: Lakini wewe, ee Bethlehemu ya Efratha, uliye mdogo kati ya koo za Yuda, kwako wewe atatokea kwa ajili yangu Yule atakayetawala juu ya Israeli; asili yake ni tangu zamani, tangu siku za kale na kale. Ndiyo maana Bwana atawatoa ninyi kwa maadui, mpaka yule mama mwenye mimba awe amejifungua; ndugu zake waliobaki salama watawarudia wana wa Israeli. Hapo Yeye atasimama imara, atachunga kundi lake kwa nguvu ya Bwana, na kwa utukufu wa jina la Bwana Mungu wake. Nao watarudi salama, maana atakuwa mkubwa hata mipaka ya dunia. Yeye atakuwa amani.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

au somo lifuatalo:

SOMO LA KWANZA
WARUMI 8:28—30

"Maana wale aliowajua toka mwanzo, aliwachagua."

Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi

Ndugu: Twajua ya kuwa wale wampendao Mungu hufanikiwa katika yote, ndio wale walioitwa toka mwanzo katika azimio lake. Maana wale aliowajua toka mwanzo, aliwachagua toka mwanzo ili kuwalinganisha na sura ya Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua toka mwanzo aliwaita; nao aliowaita aliwapa uadilifu; nao walioadilishwa aliwapa utukufu wa mbinguni.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 13:6ab, 6cd (K. Isaya 61:10)

K. Ninafurahi sana katika Bwana.

Nami, ee Bwana, nimeitumainia huruma yako,
ujalie moyo wangu furaha wokovu wako. K.

Nitamwimbia Bwana,
kwa maana amekuwa mkarimu kwangu. K.

SHANGILIO LA INJILI

K. Aleluya. W. Aleluya.
K. Umebarikiwa, ewe Bikira Maria, na unastahili sifa zote, kwa maana uliiletea dunia jua la haki, yaani Kristo Mungu wetu.
W. Aleluya.

SOMO LA INJILI
MATHAYO 1:1—16, 18—23

"Amepata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu."

† Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo

Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu. Abrahamu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo alimzaa Yuda na ndugu zake; Yuda alimzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi alimzaa Esromu; Esromu alimzaa Aramu; Aramu alimzaa Aminadabu; Aminadabu alimzaa Nashoni; Nashoni alimzaa Salmoni; Salmoni alimzaa Boazi kwa Rahabu; Boazi alimzaa Obedi kwa Ruthu; Obedi alimzaa Yese; Yese alimzaa mfalme Daudi. Sulemani alimzaa Rehoboamu; Rehoboamu alimzaa Abiya; Abiya alimzaa Asa; Asa alimzaa Yehoshafati; Yehoshafati alimzaa Yoramu; Yoramu alimzaa Uzia; Uzia alimzaa Yothamu; Yothamu alimzaa Ahazi; Ahazi alimzaa Hezekia; Hezekia alimzaa Manase; Manase alimzaa Amoni; Amoni alimzaa Yosia; Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake, wakati wa ule uhamisho wa Babeli. Na baada ya ule uhamisho wa Babeli, Yekonia alimzaa Shealtieli; Shealtieli alimzaa Zerubabeli; Zerubabeli alimzaa Abihudi; Abihudi alimzaa Eliakimu; Eliakimu alimzaa Azori; Azori alimzaa Sadoki; Sadoki alimzaa Akimu; Akimu alimzaa Eliudi; Eliudi alimzaa Eleazari; Eleazari alimzaa Mathani; Mathani alimzaa Yakobo; Yakobo alimzaa Yosefu mumewe Maria aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.

*Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa hivi. Maria, mama yake, alipokuwa ameposwa na Yosefu, kabla hawajakaa pamoja alionekana ana mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Mumewe Yosefu akiwa mtu mwadilifu, hakupenda kumwaibisha hadharani. Basi, akanuia kumwacha kwa Siri. Alipokuwa akifikiria hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea ghafla katika ndoto, akasema, "Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumpokea Maria kuwa mke wako, maana mimba yake ameipata kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Atamzaa mwana, naye utampa jina lake "Yesu." Maana yeye atawaokoa watu wake katika dhambi zao." Hayo yote yametendeka, ili neno alilonena Bwana kwa njia ya nabii litimie, kwamba: "Tazama, bikira atachukua mimba na kumzaa mwana, naye watamwita Emanueli maana yake, "Mungu pamoja nasi."

INJILI YA BWANA... SIFA KWAKO EE KRISTO

07/09/2026

MASOMO YA MISA

SEPTEMBA 7, 2026

JUMATATU YA JUMA LA ISHIRINI NA TATU,

KIPINDI CHA KAWAIDA, MWAKA II,

RANGI YA KILITURJIA: KIJANI KIBICHI 💚

SOMO LA KWANZA
1 WAKORINTHO 5:1—8

"Iondosheni chachu ya zamani, kwa maana mwanakondoo wetu wa pasaka ametolewa sadaka ndiye Kristo."

Somo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Paulo kwa Wakorintho

Ndugu: Habari imeenea ya kuwa kwenu kuna uasherati, tena uasherati wa namna isiyopatikana hata kwa watu wa mataifa, eti mtu anaishi na mke wa baba yake. Na papo hapo mnajitutumua badala ya kusikitika! Mtu aliyetenda hayo sharti aondoshwe katika ushirika wenu. Kwa maana mimi, ijapokuwa nipo mbali kwa mwili, nipo karibu kiroho. Nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, k**a kwamba ningekuwapo. Mnapokutana kwa jina la Bwana wetu Yesu, nami pamoja nanyi kiroho, hapo kwa uwezo wa Bwana wetu Yesu, mtu huyo atolewe kwa Shetani, apatwe na maangamizi ya mwili, ili roho isalimishwe siku ya Bwana. Kujitutumua kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge lote? Basi, iondosheni chachu ya zamani, mpate kuwa donge jipya, ninyi mlio watu msiochachuka. Kwa maana mwanakondoo wetu wa Pasaka ametolewa sadaka, ndiye Kristo. Haya, tuadhimishe sikukuu, si kwa chachu ya zamani, wala kwa chachu ya ubaya na uovu, bali kwa donge lisilochachuka, yaani la unyofu na ukweli.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 5:5—6, 7, 12 (K. 9a)

K. Uniongoze katika haki yako, ee Bwana.

Wewe si Mungu apendezwaye na uovu;
mtu mbaya hatakaa kwako.
Unawadharau watendao maovu;
Wenye majivuno hawatasimama mbele ya macho yako, K.

unawaangamiza wale wasemao uongo.
Watu wenye hila na wenye kumwaga damu,
Bwana anachukizwa nao. K.

Nao wote wanaokukimbilia watafurahi,
na watalia kwa furaha daima.
Unawapa ulinzi wako juu yao; kwako watafurahi,
wale walipendao jina lako. K.

SHANGILIO LA INJILI
YOHANE 10:27

K. Aleluya. W. Aleluya.

K. Kondoo wangu huisikia sauti yangu, asema Bwana; nami nawajua, nao wanifuata.
W. Aleluya.

SOMO LA INJILI
LUKA 6:6—11

"Walimvizia ili waone k**a atamponya mtu siku ya Sabato."

† Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Luka

Ilitokea kwamba Yesu aliingia katika sinagogi siku ya Sabato, akafundisha, humo alikuwamo mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza. Waandishi na Mafarisayo wakamvizia, waone k**a atamponya siku ya Sabato, wapate nafasi ya kumshtaki. Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia mtu mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Akainuka, akasimama. Ndipo Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, je, ni halali siku ya Sabato kutenda mema au kutenda mabaya? Kusalimisha maisha au kuangamiza?" Akawakazia macho wote pande zote, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako." Akaunyosha na mkono wake ukawa mzima tena. Lakini wakajazwa na hasira, wakashauriana wamtendeje Yesu.

INJILI YA BWANA... SIFA KWAKO EE KRISTO

06/09/2026

Monday of the Twenty-third Week in Ordinary Time
7th September 2026

Reading 1
1 Corinthians 5:1-8
Brothers and sisters:
It is widely reported that there is immorality among you,
and immorality of a kind not found even among pagans–
a man living with his father’s wife.
And you are inflated with pride.
Should you not rather have been sorrowful?
The one who did this deed should be expelled from your midst.
I, for my part, although absent in body but present in spirit,
have already, as if present,
pronounced judgment on the one who has committed this deed,
in the name of our Lord Jesus:
when you have gathered together and I am with you in spirit
with the power of the Lord Jesus,
you are to deliver this man to Satan
for the destruction of his flesh,
so that his spirit may be saved on the day of the Lord.

Your boasting is not appropriate.
Do you not know that a little yeast leavens all the dough?
Clear out the old yeast, so that you may become a fresh batch of dough,
inasmuch as you are unleavened.
For our Paschal Lamb, Christ, has been sacrificed.
Therefore, let us celebrate the feast,
not with the old yeast, the yeast of malice and wickedness,
but with the unleavened bread of sincerity and truth.

Responsorial Psalm
Psalm 5:5-6, 7, 12
R. Lead me in your justice, Lord.
For you, O God, delight not in wickedness;
no evil man remains with you;
the arrogant may not stand in your sight.
You hate all evildoers.
R. Lead me in your justice, Lord.
You destroy all who speak falsehood;
The bloodthirsty and the deceitful
the LORD abhors.
R. Lead me in your justice, Lord.
But let all who take refuge in you
be glad and exult forever.
Protect them, that you may be the joy
of those who love your name.
R. Lead me in your justice, Lord.

Alleluia
John 10:27
R. Alleluia, alleluia.
My sheep hear my voice, says the Lord;
I know them, and they follow me.
R. Alleluia, alleluia.

Gospel
Luke 6:6-11
On a certain sabbath Jesus went into the synagogue and taught,
and there was a man there whose right hand was withered.
The scribes and the Pharisees watched him closely
to see if he would cure on the sabbath
so that they might discover a reason to accuse him.
But he realized their intentions
and said to the man with the withered hand,
"Come up and stand before us."
And he rose and stood there.
Then Jesus said to them,
"I ask you, is it lawful to do good on the sabbath
rather than to do evil,
to save life rather than to destroy it?"
Looking around at them all, he then said to him,
"Stretch out your hand."
He did so and his hand was restored.
But they became enraged
and discussed together what they might do to Jesu

05/09/2026

MASOMO YA MISA,

JUMAPILI, SEPTEMBA 6, 2026

JUMA LA 23 LA MWAKA
________

MWANZO
Zab. 119:137, 124

Ee Bwana, wewe ndiwe mwenye haki, na hukumu zako ni za adili. K**a zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako.
________

SOMO I
Eze. 33:7-9

Basi wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli; basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu. Nimwambiapo mtu mbaya, Ewe mtu mbaya, hakika utakufa, nawe husemi neno la kumwonya mtu huyo, aiache njia yake, mtu mbaya huyo atakufa katika uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako. Walakini ukimwonya mtu mbaya kwa sababu ya njia yake, kusudi aiache; wala yeye asiiache; atakufa huyo katika uovu wake, lakini wewe umejiokoa roho yako.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 95:1-2, 6-9 (K) 7-8

(K) Ingekuwa heri leo tusikie sauti yake!

Tusifanye migumu mioyo yetu.
Njoni tumwimbie Bwana,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele yake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi. (K)

Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.
Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake. (K)

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu;
K**a vile huko Meriba;
K**a siku ile ya Masa jangwani,
Hapo waliponijaribu baba zetu;
Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)
________

SOMO 2
Rum. 13:8-10

Msiwiwe na mtu chochote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sharia. Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani, na ikiwapo amri nyingine yoyote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako k**a nafsi yako. Pendo halimfanyii jirani neno baya, basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________

SHANGILIO
Yn. 14:23

Aleluya, aleluya,
Mtu akinipenda, atalishika neno langu;
Na baba yangu atampenda; Nasi tutakuja kwake.
Aleluya.
________

INJILI
Mt. 18:15-20

Siku ile Yesu aliwaambia wafuasi wake: Ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo. La, k**a hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike. Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako k**a mtu wa mataifa na mtoza ushuru. Amin, nawaambieni, yoyote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yoyote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.
Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lolote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.

Injili Takatifu...Sifa kwako, ee Kristo
________

04/09/2026

MASOMO YA MISA

JUMAMOSI, SEPTEMBA 5, 2026

JUMA LA 22 LA MWAKA

SOMO 1
1Kor. 4:6 – 15

Ndugu zangu, mambo hayo nimeyafanya kuwa mfano wa mimi na Apolo kwa ajili yenu, ili kwamba kwa mfano wetu mpate kujifunza kutokupita yale yaliyoandikwa; ili mmoja wenu asijivune kwa ajili ya huyu, kinyume cha mwenziwe. Maana ni nani anayekupambanua na mwingine? Nawe una nini usichokipokea? Lakini iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea? Mmekwisha kushiba, mmekwisha kupata utajiri, mmemiliki pasipo sisi. Naam, laity mngemiliki, ili sisi nasi tumiliki pamoja nanyi! Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, k**a watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu tumekuwa tamasha kwa dunia; kwa malaika na wanadamu.

Sisi tu wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye akili katika Kristo; sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu; ninyi mna utukufu, lakini sisi hatupati heshima. Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tu uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao; kasha twataabika tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa twabariki, tukiudhiwa twastahimili; tukisingiziwa twasihi; tumefanywa k**a takataka za dunia, na tama ya vitu vyote hata sasa.

Siyaandiki hayo ili kuwatahayarisha; bali kuwaonya k**a watoto niwapendao. Kwa kuwa ijapokuwa mna waalimu kumi elfu katika Kristo, walakini hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 145:17 – 21 (K0 18

(K) Bwana yu karibu na wote wamwitao.

Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote,
Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Bwana yu karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa uaminifu. (K)

Atawafanyia wamchao matakwa yao,
Nay atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
Bwana huwahifadhi wote wammpendao,
Na wote wasio haki atawaangamiza. (K)

Kinywa change kitazinena sifa za Bwana;
Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu
Milele na milele. (K)

SHANGILIO
Zab. 119:18

Aleluya, aleluya,
Unifumbue macho yangu niyatazame
maajabu yatokayo katika sharia yako.
Aleluya.

INJILI
Lk. 6:1 – 5

Ilikuwa siku ya sabato moja Yesu alikuwa akipita katika mashamba, wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke na kuyala, wakiyapukusa-pukusa mikononi mwao. Basi baadhi ya Mafarisayo wakawaambia, Mbona mnafanya lisilo halali siku ya sabato? Yesu akawajibu akawaambia, Hamkulisoma, hata hilo alilolifanya Daudi, alipokuwa na njaa, nay eye na wale aliokuwa nao? Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akaitwaa mikate ile ya Wonyesho, akaila akawapa na hao wenziwe, ambayo si halali kuila ila kwa makuhani peke yao. Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

Injili takatifu...Sifa kwako, ee Kristo

FRIDAY NIGHT VIGIL DAY :           04/09/2026TIME:          8:00 PMVENUE:       ST. PETER THE APOSTLE CENTRE KIKUYUProgr...
04/09/2026

FRIDAY NIGHT VIGIL

DAY : 04/09/2026
TIME: 8:00 PM
VENUE: ST. PETER THE APOSTLE CENTRE KIKUYU

Programme

CONFESSIONS

MASS IN HONOUR OF THE SACRED HEART OF JESUS

Praise
Rosary + Litanies
Adoration
Reparation
Way of the Cross

MASS AT DAWN IN HONOUR OF THE IMMACULATE HEART OF THE BLESSED VIRGIN MARY

Most Sacred Heart of Jesus, have mercy on us.

Join us this Sunday 6th September, 12 pm mass (4th Mass) as we launch our parish anthem video 🥳🥳
04/09/2026

Join us this Sunday 6th September, 12 pm mass (4th Mass) as we launch our parish anthem video 🥳🥳

Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

04/09/2026

Friday of the Twenty-second Week in Ordinary Time
4th September 2026

Reading 1
1 Corinthians 4:1-5
Brothers and sisters:
Thus should one regard us: as servants of Christ
and stewards of the mysteries of God.
Now it is of course required of stewards
that they be found trustworthy.
It does not concern me in the least
that I be judged by you or any human tribunal;
I do not even pass judgment on myself;
I am not conscious of anything against me,
but I do not thereby stand acquitted;
the one who judges me is the Lord.
Therefore, do not make any judgment before the appointed time,
until the Lord comes,
for he will bring to light what is hidden in darkness
and will manifest the motives of our hearts,
and then everyone will receive praise from God.

Responsorial Psalm
Psalm 37:3-4, 5-6, 27-28, 39-40
R. (39a) The salvation of the just comes from the Lord.
Trust in the LORD and do good,
that you may dwell in the land and be fed in security.
Take delight in the LORD,
and he will grant you your heart’s requests.
R. The salvation of the just comes from the Lord.
Commit to the LORD your way;
trust in him, and he will act.
He will make justice dawn for you like the light;
bright as the noonday shall be your vindication.
R. The salvation of the just comes from the Lord.
Turn from evil and do good,
that you may abide forever;
For the LORD loves what is right,
and forsakes not his faithful ones.
Criminals are destroyed
and the posterity of the wicked is cut off.
R. The salvation of the just comes from the Lord.
The salvation of the just is from the LORD;
he is their refuge in time of distress.
And the LORD helps them and delivers them;
he delivers them from the wicked and saves them,
because they take refuge in him.
R. The salvation of the just comes from the Lord.

Alleluia
John 8:12
R. Alleluia, alleluia.
I am the light of the world, says the Lord;
whoever follows me will have the light of life.
R. Alleluia, alleluia.

Gospel
Luke 5:33-39
The scribes and Pharisees said to Jesus,
“The disciples of John the Baptist fast often and offer prayers,
and the disciples of the Pharisees do the same;
but yours eat and drink.”
Jesus answered them, “Can you make the wedding guests fast
while the bridegroom is with them?
But the days will come, and when the bridegroom is taken away from them,
then they will fast in those days.”
And he also told them a parable.
“No one tears a piece from a new cloak to patch an old one.
Otherwise, he will tear the new
and the piece from it will not match the old cloak.
Likewise, no one pours new wine into old wineskins.
Otherwise, the new wine will burst the skins,
and it will be spilled, and the skins will be ruined.
Rather, new wine must be poured into fresh wineskins.
And no one who has been drinking old wine desires new,
for he says, ‘The old is good.’”

03/09/2026

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 4, 2026

IJUMAA, JUMA LA 22 LA MWAKA

SOMO 1
1Kor. 4:1 – 5

Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu. Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu. Maana sijui sababu ya kujish*taki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana. Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 37:3 – 6, 27, 28, 39 – 40 (K) 39

(K) Wokovu wa wenye haki una Bwana.

Umkabishi Bwana njia yako,
Pia umtumaini, naye atafanya.
Atajitokeza haki yako k**a nuru,
Na hukumu yako k**a adhuhuri. (K)

Umtumaini Bwan aukatende mema,
Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.
Nawe utajifurahisha kwa Bwana,
Naye atakupa haja za moyo wako. (K)

Jiepue na uovu, utende mema,
Na kukaa hata milele.
Kwa kuwa Bwana hupenda haki,
Wala hawaachi watauwa wake. (K)

Na wokovu wa wenye haki una Bwana;
Yeye ni ngome yao wakati wa taabu.
Naye Bwana huwasaidia na kuwaopoa;
Huwaopoa na wasio haki na kuwaokoa;
Kwa kuwa wamemtumaini Yeye. (K)

SHANGILIO
Zab. 25:4, 5

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako.
Aleluya.

INJILI
Lk. 5:33 – 39

Mafarisayo na waandishi walimwambia Yesu, Wanafunzi wa Yohane hufunga mara nyingi, na kuomba dua; na kadhalika wanafunzi wa Mafarisayo; lakini wanafunzi wako hula na kunywa! Lakini Yesu akawaambia, Je! Mwaweza kuwafanya wafunge walioalikwa arusini, akiwapo bwana arusi pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi, ndipo watakapofunga siku zile. Akawaambia na mithali, Hakuna akataye kiraka cha vazi jipya na kukitia katika vazi kuukuu; na k**a akitia, amelikata lile jipya, na kile kiraka cha vazi jipya hakilingani na lile vazi kuukuu.

Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; na k**a akitia, ile divai mpya itavipasua vile viriba, divai yenyewe itamwgika, na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya sharti kutiwa katika viriba vipya. Wala hakuna anyway divai ya kale akatamani divai mpya; kwa kuwa asema, Ile ya kale ndiyo iliyo njema.

Injili takatifu… Sifa kwako Ee Kristo.

Address

Kikuyu

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when St. Peter the Apostle Catholic Parish Kikuyu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share