28/11/2025
Makala.
(UGAIDI TATIZO SUGU)
Katika ulimwengu wa leo neno (Gaidi) au (Ugaidi) limeenea sana na mara nyingi ukiskia neno hili basi wanaokusudiwa ni waislamu.
Sasa jee Ugaidi ni nini na ni nani Gaidi ?
Ugaidi ni kuwatishia watu amani na kuwaua kinyume cha haki bila ya sababu , kwa maana hii Gaidi anaweza kua mtu yeyote.
Jee Uislamu unahamasisha (Ugaidi)
Uislamu unakataza na kupinga na kukemea ugaidi kwa maana zake zote , hata katika Uislamu wakati wa vita jeshi la kiislamu hawaruhusiwi kuaa na kuwatishia watu ovyo ovyo ukisoma katika Qur'an ALLAH anasema : ((Na piganeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanao kupigeni, wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui.)) Qur'an 2:190 , katika Aya hii waislamu katika vita wanaambiwa wasifanye uadui.
Pili : Aya zote katika Qur'an zinazungumzia wasiokua waislamu hazisema "Wauweni makafiri" Aya zote zinasema "Piganeni na makafiri" na katika vita huwezi kujiacha uuwawe lazima ujitetee.
Tatu : Mtume Muhammad alikua akituma jeshi la kiislamu alikua anawapa maelekezo na amri za wazi alikua anawaambia :
Musikate miti , musimuue mwanamke au mtoto , musiwasumbue watu walio katika nyumba zao za ibada , musibomoe nyumba , musiue wanyama .
Nne : Vita alivyopigana mtume Muhammad ni vita 27 katika vita hivyo watu waliouwawa katika miaka kumi ni watu hata hawafiki 2000 bali ni 1018 katika pande zote mbili , na hakuna katika vita hivyo mwanamke aliyeuwawa wala mtoto wala mzee ukilinganisha na vita vya leo kwa mfano vita vya (Gaza) katika miaka miwili tu wameuwawa watu zaidi ya elfu sitini 60,000 hapo kuna watoto na wanawake.
Tano : Mtume Muhammad ambae anatuhumiwa ni muuaji na mpenda vita katika maisha yake amemuua mtu mmoja tu kwa mkono wake bas .
Sita : ALLAH anasema katika Qur'an : ((Mwenyezi Mungu hakukatazini kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao uadilifu.)) Qur'an sura ya 60 Aya ya 8 katika Aya hii Waislamu tunaambiwa tuwatendee wema wasiokua waislamu maadamu hawajatupiga vita na kututoa makwetu.
Saba : Ugaidi hauna Dini , Rangi , Wala Kabila hata Waislamu wenyewe wanauwawa na magaidi wa dini tofauti kwa mfano k**a vile huko (Palestina) waislamu kila siku wanauwawa , huko (India) wahindu kila siku wanauwafanyia uadui waislamu bila ya kusahau tukio la mskiti wa (Christ Church) huko (New Zealand) mwaka wa 2019 ambapo waislamu waliuwawa msiktini kinyama.
Nikimalizia nasema makundi ya kigaidi yanayonasibishwa na Uislamu k**a vile (Al Shabab) , (Al Qaeeda) , (Islamic State) , (Boko Haram) ni makudi potofu ambayo yako kinyume na dini na wengi wa wafuasi wa makundi haya ni watu wajinga ambao hata dini hawajasoma sisi tunawapinga na kuwakemea na sio katika sisi.