Masjid Aisha Sigona

Masjid Aisha Sigona In the name of Allah the Almighty. This is a community of Muslims who worship at Sigona Mosque. Alhamdullilah for the blessing of being Muslims.

29/03/2026
Bismillahi rrahmani rrahim.Naandika makala haya kwa lengo la kuwaelimisha wasiokua Waislamu (Wakristo) na wengineo.Jana ...
02/03/2026

Bismillahi rrahmani rrahim.
Naandika makala haya kwa lengo la kuwaelimisha wasiokua Waislamu (Wakristo) na wengineo.
Jana katika wa Austin huko Texas Marekani mtu mmoja anaejinasibisha na Uislamu amewapiga risasi na kuwaua watu wasio na hatia kwa kigezo kwamba sio waislamu nataka kusema yafwatayo :-
1- Uislamu haukubaliana na Ugaidi wala kuwaua wasio na hatia bila ya sababu , aya zote zinazozungumzia kuua katika Qur'an zinazungumzia vita nitanukuu aya mbili .
ALLAH anasema : {Na piganeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanao kupigeni, wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui.} Quran sura ya 2 aya ya 190.
{Mwenyezi Mungu hakukatazini kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao uadilifu.} Qur'an 60:8

2- Makundi yote ya kigaidi k**a (Al Shabaab), (Al Qaeeda) , (Boko Haram) na kadhalika ni makundi hayauwakilishi Uislamu matendo yao maovu ni yao wala sio mafunzo ya dini yote wanayoyafanya ni ugaidi na hatia na sisi tunayapinga haya makundi.

3- Uislamu unaamrisha kuwafanyia wema hata wanyama na wadudu Mtume Muhammad anasema : {Mwanamke mmoja aliingia motoni (jahanamu) kwa sababu ya paka hakumlisha wala hakumuacha huru akatafute chakula mpaka akafa} k**a kumuua paka mtu anaenda motoni itakuaje kumuua mtu bila hatia.

4- Watu lazima watofautishe kati ya (Muislamu) mtu na (Uislamu) dini , Waislamu wako waovu wahuni walevi washenzi magaidi majambazi na kadhalika , lakini Uislamu haufunzi tabia hizo wala hauamrishi ugaidi na ujambazi , Soma uujue Uislamu sio waislamu.

5- Neno (Ugaidi) lina maana pana na sio waislamu tu wanafanya ugaidi , Waislamu India kila siku wanateswa na kuuwawa , Waislamu Palestina kila siku wanateswa na kuuwawa , Mbona wakiua watu wengine hakuna tatizo lakini akiua Muislamu dunia yote itasimama . Ugaidi huna rangi wala kabila wala dini.

ASSALAMU ALYKUM.NI NINI MAANA YA KUFUNGA  KATIKA MWEZI WA RAMADHAN ?KUFUNGA NI MTU KUJIZUIA NA KULA KUNYWA NA TENDO LA N...
14/02/2026

ASSALAMU ALYKUM.
NI NINI MAANA YA KUFUNGA KATIKA MWEZI WA RAMADHAN ?

KUFUNGA NI MTU KUJIZUIA NA KULA KUNYWA NA TENDO LA NDOA .

SWAUM AU KUFUNGA KATIKA MWEZI WA RAMADHAN INAANZA SAA NGAPI NA INAISHA SAA NGAPI ?

SWAUM INAANZA AL FAJIRI K**A SAA 05:00 AM HIVI MPAKA JIONI MAGHARINI K**A SAA 06:30 PM HIVI KWA SAA ZA AFRIKA MASHARIKI , AU IKIADHINIWA ADHANA YA MAGHARIBI NDIO MWISHO WA KUFUNGA.

JEE WATU HULA SAA NGAPI KATIKA RAMADHAN ?

KATIKA MWEZI WA RAMADHAN WAISLAMU HULA MARA MBILI , CHAKULA CHA KWANZA KINAITWA (DAKU) KINALIWA SAA KUMI USIKU KABLA YA AL FAJIRI ,

NA CHAKULA CHA PILI KINAITWA (FUTARI) KINALIWA JIONI MAGHARIBI BAADA YA SWALA YA MAGHARIBI.

KUFUNGA NI MCHANA JEE USIKU WA RAMADHAN MTU ANAWEZA KUFANYA YALE AMBAYO ALIKUA HAWEZI KUFANYA MCHANA ?

NDIO IKISHAFIKA MAGHARIBI YA RAMADHAN KWANZIA HAPO NA USIKU MZIMA MPAKA AL FAJIRI MTU ANARUHUSIWA KULA , KUNYWA , NA HATA KULALA NA MKE WAKE. YAANI KUFUNGA NI MCHANA USIKU HAKUNA KUFUNGA.

Address

Zambezi, On Nairobi Nakuru Highwayp
Kikuyu

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Masjid Aisha Sigona posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share