Masjid Aisha Sigona

Masjid Aisha Sigona In the name of Allah the Almighty. This is a community of Muslims who worship at Sigona Mosque. Alhamdullilah for the blessing of being Muslims.

29/03/2026
Bismillahi rrahmani rrahim.Naandika makala haya kwa lengo la kuwaelimisha wasiokua Waislamu (Wakristo) na wengineo.Jana ...
02/03/2026

Bismillahi rrahmani rrahim.
Naandika makala haya kwa lengo la kuwaelimisha wasiokua Waislamu (Wakristo) na wengineo.
Jana katika wa Austin huko Texas Marekani mtu mmoja anaejinasibisha na Uislamu amewapiga risasi na kuwaua watu wasio na hatia kwa kigezo kwamba sio waislamu nataka kusema yafwatayo :-
1- Uislamu haukubaliana na Ugaidi wala kuwaua wasio na hatia bila ya sababu , aya zote zinazozungumzia kuua katika Qur'an zinazungumzia vita nitanukuu aya mbili .
ALLAH anasema : {Na piganeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanao kupigeni, wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui.} Quran sura ya 2 aya ya 190.
{Mwenyezi Mungu hakukatazini kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao uadilifu.} Qur'an 60:8

2- Makundi yote ya kigaidi k**a (Al Shabaab), (Al Qaeeda) , (Boko Haram) na kadhalika ni makundi hayauwakilishi Uislamu matendo yao maovu ni yao wala sio mafunzo ya dini yote wanayoyafanya ni ugaidi na hatia na sisi tunayapinga haya makundi.

3- Uislamu unaamrisha kuwafanyia wema hata wanyama na wadudu Mtume Muhammad anasema : {Mwanamke mmoja aliingia motoni (jahanamu) kwa sababu ya paka hakumlisha wala hakumuacha huru akatafute chakula mpaka akafa} k**a kumuua paka mtu anaenda motoni itakuaje kumuua mtu bila hatia.

4- Watu lazima watofautishe kati ya (Muislamu) mtu na (Uislamu) dini , Waislamu wako waovu wahuni walevi washenzi magaidi majambazi na kadhalika , lakini Uislamu haufunzi tabia hizo wala hauamrishi ugaidi na ujambazi , Soma uujue Uislamu sio waislamu.

5- Neno (Ugaidi) lina maana pana na sio waislamu tu wanafanya ugaidi , Waislamu India kila siku wanateswa na kuuwawa , Waislamu Palestina kila siku wanateswa na kuuwawa , Mbona wakiua watu wengine hakuna tatizo lakini akiua Muislamu dunia yote itasimama . Ugaidi huna rangi wala kabila wala dini.

ASSALAMU ALYKUM.NI NINI MAANA YA KUFUNGA  KATIKA MWEZI WA RAMADHAN ?KUFUNGA NI MTU KUJIZUIA NA KULA KUNYWA NA TENDO LA N...
14/02/2026

ASSALAMU ALYKUM.
NI NINI MAANA YA KUFUNGA KATIKA MWEZI WA RAMADHAN ?

KUFUNGA NI MTU KUJIZUIA NA KULA KUNYWA NA TENDO LA NDOA .

SWAUM AU KUFUNGA KATIKA MWEZI WA RAMADHAN INAANZA SAA NGAPI NA INAISHA SAA NGAPI ?

SWAUM INAANZA AL FAJIRI K**A SAA 05:00 AM HIVI MPAKA JIONI MAGHARINI K**A SAA 06:30 PM HIVI KWA SAA ZA AFRIKA MASHARIKI , AU IKIADHINIWA ADHANA YA MAGHARIBI NDIO MWISHO WA KUFUNGA.

JEE WATU HULA SAA NGAPI KATIKA RAMADHAN ?

KATIKA MWEZI WA RAMADHAN WAISLAMU HULA MARA MBILI , CHAKULA CHA KWANZA KINAITWA (DAKU) KINALIWA SAA KUMI USIKU KABLA YA AL FAJIRI ,

NA CHAKULA CHA PILI KINAITWA (FUTARI) KINALIWA JIONI MAGHARIBI BAADA YA SWALA YA MAGHARIBI.

KUFUNGA NI MCHANA JEE USIKU WA RAMADHAN MTU ANAWEZA KUFANYA YALE AMBAYO ALIKUA HAWEZI KUFANYA MCHANA ?

NDIO IKISHAFIKA MAGHARIBI YA RAMADHAN KWANZIA HAPO NA USIKU MZIMA MPAKA AL FAJIRI MTU ANARUHUSIWA KULA , KUNYWA , NA HATA KULALA NA MKE WAKE. YAANI KUFUNGA NI MCHANA USIKU HAKUNA KUFUNGA.

Makala.(UGAIDI TATIZO SUGU)Katika ulimwengu wa leo neno (Gaidi) au (Ugaidi) limeenea sana na mara nyingi ukiskia neno hi...
28/11/2025

Makala.
(UGAIDI TATIZO SUGU)

Katika ulimwengu wa leo neno (Gaidi) au (Ugaidi) limeenea sana na mara nyingi ukiskia neno hili basi wanaokusudiwa ni waislamu.

Sasa jee Ugaidi ni nini na ni nani Gaidi ?
Ugaidi ni kuwatishia watu amani na kuwaua kinyume cha haki bila ya sababu , kwa maana hii Gaidi anaweza kua mtu yeyote.

Jee Uislamu unahamasisha (Ugaidi)
Uislamu unakataza na kupinga na kukemea ugaidi kwa maana zake zote , hata katika Uislamu wakati wa vita jeshi la kiislamu hawaruhusiwi kuaa na kuwatishia watu ovyo ovyo ukisoma katika Qur'an ALLAH anasema : ((Na piganeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanao kupigeni, wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui.)) Qur'an 2:190 , katika Aya hii waislamu katika vita wanaambiwa wasifanye uadui.

Pili : Aya zote katika Qur'an zinazungumzia wasiokua waislamu hazisema "Wauweni makafiri" Aya zote zinasema "Piganeni na makafiri" na katika vita huwezi kujiacha uuwawe lazima ujitetee.

Tatu : Mtume Muhammad alikua akituma jeshi la kiislamu alikua anawapa maelekezo na amri za wazi alikua anawaambia :
Musikate miti , musimuue mwanamke au mtoto , musiwasumbue watu walio katika nyumba zao za ibada , musibomoe nyumba , musiue wanyama .

Nne : Vita alivyopigana mtume Muhammad ni vita 27 katika vita hivyo watu waliouwawa katika miaka kumi ni watu hata hawafiki 2000 bali ni 1018 katika pande zote mbili , na hakuna katika vita hivyo mwanamke aliyeuwawa wala mtoto wala mzee ukilinganisha na vita vya leo kwa mfano vita vya (Gaza) katika miaka miwili tu wameuwawa watu zaidi ya elfu sitini 60,000 hapo kuna watoto na wanawake.

Tano : Mtume Muhammad ambae anatuhumiwa ni muuaji na mpenda vita katika maisha yake amemuua mtu mmoja tu kwa mkono wake bas .

Sita : ALLAH anasema katika Qur'an : ((Mwenyezi Mungu hakukatazini kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao uadilifu.)) Qur'an sura ya 60 Aya ya 8 katika Aya hii Waislamu tunaambiwa tuwatendee wema wasiokua waislamu maadamu hawajatupiga vita na kututoa makwetu.

Saba : Ugaidi hauna Dini , Rangi , Wala Kabila hata Waislamu wenyewe wanauwawa na magaidi wa dini tofauti kwa mfano k**a vile huko (Palestina) waislamu kila siku wanauwawa , huko (India) wahindu kila siku wanauwafanyia uadui waislamu bila ya kusahau tukio la mskiti wa (Christ Church) huko (New Zealand) mwaka wa 2019 ambapo waislamu waliuwawa msiktini kinyama.
Nikimalizia nasema makundi ya kigaidi yanayonasibishwa na Uislamu k**a vile (Al Shabab) , (Al Qaeeda) , (Islamic State) , (Boko Haram) ni makudi potofu ambayo yako kinyume na dini na wengi wa wafuasi wa makundi haya ni watu wajinga ambao hata dini hawajasoma sisi tunawapinga na kuwakemea na sio katika sisi.

Khutba ya ijumaa ya leo kutoka katika msikiti mtukufu wa Makkah imetolewa na Dr.Sheikh (Yasir Al Dowsary) na  haya ni ba...
14/11/2025

Khutba ya ijumaa ya leo kutoka katika msikiti mtukufu wa Makkah imetolewa na Dr.Sheikh (Yasir Al Dowsary) na haya ni baadhi ya aliyoyasema.

"Katika uzuri wa Uislamu na na katika fadhila zake na katika matendo ambayo mtu atajikirubisha nayo kwa ALLAH ni kuwatendendea wema Wazazi wawili jambo hili ni katika ibada kubwa mno , ALLAH ameunganisha utajo wake na utajo wa wazazi na ameunganisha haki yake na haki ya mzazi na shukrani yake na shukrani ya mzazi amesema ALLAH : ((Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema.)) na Mtume Muhammad amesema : {{Radhi za Mola zipo katika radhi za wazazi wawili na hasira zake zipo katika hasira za wazazi wawili}}".

03/11/2025

Chukia tabia sio mwenye tabia

Mtume Muhammad Anasema :-Chakula cha wawili kinawatosha watu watatu , na Chakula cha watu watatu kinawatosha watu wanne.
03/11/2025

Mtume Muhammad Anasema :-

Chakula cha wawili kinawatosha watu watatu , na Chakula cha watu watatu kinawatosha watu wanne.

Address

Zambezi, On Nairobi Nakuru Highwayp
Kikuyu

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Masjid Aisha Sigona posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share