02/09/2026
MASOMO YA MISA, ALHAMISI YA JUMA LA ISHIRINI NA MBILI, KIPINDI CHA KAWAIDA, MWAKA II, KUMBUKUMBU YA MT. GREGORI MKUU, PAPA NA MWALIMU WA KANISA, SEPTEMBA 3, 2026
RANGI YA KILITURJIA: NYEUPE 🤍
SOMO LA KWANZA
1 WAKORINTHO 3:18—23
"Mambo yote ni yenu, nanyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu."
Somo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Paulo kwa Wakorintho
Ndugu: Mtu asijidanganye mwenyewe: k**a mmoja wenu akijiona ni mtu wa hekima nyakati hizi, awe kwanza mjinga, apate kuwa mwenye hekima. Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni ujinga mbele ya Mungu, kwani imeandikwa: Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao." Na tena, "Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima, maana ni ya bure." Basi, mtu asijisifie wanadamu. Kwa maana yote ni yenu: Paulo, Apolo au Kefa, ulimwengu au uzima au mauti; mambo ya sasa au ya baadaye, yote ni yenu. Nanyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu.
NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU
ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 24:1—2, 3—4ab, 5—6 (K. 1a)
K. Nchi ni yake Bwana na vyote vinavyoijaza.
dunia yote na wakaaji waliomo. Maana Mungu ameweka
misingi yake juu ya bahari; ameisimika juu ya mito ya maji. K.
Nchi ni yake Bwana na vyote vinavyoijaza,
Ni nani atakayeupanda mlima wa Bwana?
Ni nani atakayesimama mahali pake patakatifu?
Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe,
asiyeuinua moyo wake kwa mambo ya miungu. K.
Huyo atapata baraka kutoka kwa Bwana.
na tuzo ya Mungu Mwokozi wake.
Hiki ni kizazi cha wenye kumtafuta,
cha wenye kuutafuta uso wako, ee Mungu wa Yakobo. K.
SHANGILIO LA INJILI
MATHAYO 4:19
K. Aleluya. W. Alelya.
K. Njoni mnifuate, asema Bwana, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
W. Aleluya.
SOMO LA INJILI
LUKA 5:1—11
"Waliacha vyote wakamjuata."
† Somo la Injili takatifu ilivyoan dikwa na Luka
Wakati ule: Watu wengi walimsonga wapate kulisikiliza neno la Mungu, [Yesu] alikuwa amesimama kando ya Ziwa la Genesareti. Akaona vyombo viwili vimepwelewa pwani; wavuvi wame shuka, wanaosha nyavu. Akapanda chombo kimoja, ndicho cha Simoni, akamwomba akitenge kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makundi toka chomboni. Baada ya mafundisho, akamwambia Simoni, “Rudisha chombo baharini, shusheni nyavu zenu kwa kuvua samaki." Simoni akajibu, akamwambia, "Bwana, tumejitahidi sana usiku mzima tusipate kitu, lakini kwa neno lako nitashusha nyavu." Walipofanya hivyo, walinasa samaki wengi mno, hata nyavu zao zikaanza kukatika. Wakawaashiria wenzao waliokuwako katika chombo kingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili hata karibu ya kuzama. Simoni Petro alipoona hayo, alimwangukia Yesu magotini pake, akasema, “Ondoka kwangu, ewe Bwana, kwa maana mimi ni mtu mkosefu."" Maana mshangao ulimshika yeye na wote waliokuwa pamoja naye kwa sababu ya wingi wa samaki waliowanasa, kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, ndio washiriki wa Simoni. Yesu akamwambia Simoni, "Usiogope; tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu." Walipoviegesha vyombo pwani, wakaacha vyote, wakamfuata.
INJILI YA BWANA... SIFA KWAKO EE KRISTO