09/01/2026
Faida 7 za kuwa mtu wa maombi
1:Kujenga mahusiano mazuri na Mungu
Maombi ni mawasiliano kati ya mtu na Mungu
Kadri unavyokuwa mtu wa maombi ndivyo ambavyo unatengeneza mahusiano mazuri na Mungu sababu kila muda unapoomba unawasiliana naye na kuzidi kuwa karibu naye
Zaburi 105:4
2:Maombi hubadili tabia
Unavyoongea na Mungu mara kwa mara utaanza kuona kuna tabia zinabadilika sababu unakuwa na mahusiano mazuri na Mungu ,Inakuwa ni rahisi Roho Mtakatifu kusema na wewe na ukamsikia
Hivyo tabia inapojitokeza ambayo sio nzuri Roho Mtakatifu hukuonya mapema na wewe kujirekebisha haraka sababu unaijua sauti ya Mungu
3:Kukua Kiroho
Maisha ya kuomba huchaji ukiroho wetu kila siku ,Unapokuwa mwamini na huna maombi ni sawa na simu ambayo haina chaji
Hutaweza kufanya kazi za kiroho unakuwa umekufa ,Mungu ni Roho nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Sababu Mungu ni Roho na wewe unatakiwa maisha yako ya rohoni yawe vizuri ili uweze kumsikia vizuri
Yohana 4:24
4:Maombi hukupa nguvu na kukuepusha na majaribu
Unapokuwa mtu wa maombi ni rahisi kutambua kuwa jambo fulani ni jaribu kwako na ukaweza kuliepuka sababu
Taa yako ya rohoni inakuwa inawaka
Na Mungu anasema na wewe unasikia
Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu ,Mathayo 26:41
5:Maombi hukufanya kutembea katika mapenzi ya Mungu na kukubali kutembea katika mapenzi hayo
Unapokuwa mtu maombi ,Mungu husema na wewe na kukusaidia kutembea katika mapenzi yake
Unifundishe kuyatenda mapenzi yako,
Kwa maana ndiwe Mungu wangu;
Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa,Zaburi 143:10
6:Maombi huondoa woga na kukupa kujiamini kwa sababu unatambua kuwa hakuna jambo lolote gumu kwake lolote napaswa kuomba
Hupaswi kuwa na woga juu ya maisha bali lolote lipeleke kwa Mungu
Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.Wafilipi 4:6
7:Maombi ni namna pekee ya kuwasilisha mahitaji yetu mbele za Mungu
Mwambie Mungu nini kinakusibu nini unahitaji,Usikae na mambo yanakulemea na una Mungu ,Mtwishe yote naye atafanya kwako , Hicho ambacho kinakuogopesha mwambie Mungu naye atafanya
Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;
Kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
Mathayo 7:7-8
Kila mwezi kwa mwaka 2026 tunafunga siku 7 kila tar 1 hadi 7
Kujiunga na programu yetu tuma neno MAOMBI kwenda Whatsp 0737172299
Karibu sana