12/08/2022
Somo la Agosti 13, 2022 (Av 16, 5782)
KUKOMBOLEWA KWA MWANADAMU
Somo Kuu: Warumi 5
Fungu La Kukariri: Wagal. 3:15 -18.
1. Tulipokuwa katika hali ya kuanguka
tulikombolewaje? Waefeso. 2: 1; Wagal. 3:13.
2. Je! Hii iliwezekanaje wakati hukumu ya kifo ilipitishwa kwa wanadamu wote? Yohana 3:16; Warumi 5:15.
3. Je, watu wote watajiwakilisha kwa ukombozi huu? Mathayo. 7:13, 14; Luka 13:23, 24.
4. Je, watu wote watapata fursa ya kukubali wokovu huu wa ajabu? 1 Yohana 2: 2; 1 Tim. 2: 3, 4.
Maelezo. - K**a vile sisi ni maskini wa mambo ya kiroho, Yahshua alitukomboa, baada
ya kuwa jamaa yetu kwa njia ya kibinadamu, kwa kumwaga damu Yake ya thamani. Tunaona hii inapatikana kwa kila mtu ambaye alitaka kuwa huru kutoka kwenye mateka ya ulimwengu huu mbaya wa dhambi, Masihi ni mkombozi wa kila mtu. - Wagalatia. 1: 3, 4.
5. Pamoja na ukombozi ni jambo gani lingine Masihi hufanya? Tito 2:12, 14.
Maelezo. Yahshua Masihi hakomboi tu, bali damu yake pia huwatakasa watakatifu
ambao huenenda kwa njia ya unyenyekevu mbele yake.
6. WaMasihi wanapaswa kufanya nini kila wakati ili wakae katika ukombozi na kuwa safi?
Ayubu 11:14, 15; Luka 11: 4; Zab. 34:18.
7. Mtume Paulo aliuliza nini kwa WaMasihi walioishi Korintho? 2 Wakor. 7: 9-10.
8. Ni kweli kwamba ukombozi ni zawadi ya bure kutoka kwa Elohim. - Waefeso. 2: 4-7.
9. Paulo alimtukuzaje Elohim kwa upendo uliotolewa bure wakati alipokuwa mwenye
dhambi? 1 Tim. 1: 14-18.
Maelezo. - Ukombozi huathiri mtu aliyeanguka. Ukombozi humuinua mtu kwa kiwango cha juu ambapo anaweza kufahamu upendo wa ajabu wa Elohim. Ili kuthibitisha kuwa mtu huyo anapokea ukombozi uliotolewa, anabatizwa katika maji, akawa kiumbe kipya
katika Masihi Yahshua, akiendelea kutafuta mambo yaliyo juu.