02/06/2026
Second Swahili Service
Mada; Vazi la Upendo
Mnenaji; Mtume Alex Lwamba
Maandiko;
1 Wakorintho 13:13
Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.
1 Yohana 4:7-17
Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.
Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.
Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.
Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake.
Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu.
Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.
Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, k**a yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.
Mathayo 22:37-39
Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako k**a nafsi yako.
1 Wakorintho 13:1-3
Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, k**a sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, k**a sina upendo, mimi si kitu.
Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, k**a sina upendo, hainifaidi kitu.
Kumbuka;
✔️ Hakuna vile kanisa la Bwana linaweza kujengwa na likawa na msingi dhabiti pasipo kusimama kwa msingi wa upendo.
✔️ Pasipo upendo unaweza sema maneno yote kuhusu Mungu lakini mbingu haikujui.
✔️ Hakuna mtu anayependa pasipo ishara.
✔️ Upendo dhabiti ni upendo wa matendo.
✔️ Kanisa linaweza kuwa na ishara kubwa lakini watu wanakaa na chuki katika nyumba ya bwana.
✔️ Roho wa upendo huzalisha upendo ndani mwako.