27/11/2022
Ayubu 5:
Job
8 Lakini mimi ningemtafuta Mungu, Ningemwekea Mungu daawa yangu;
8 "But as for me, I would seek God, And to God I would commit my cause--
9 Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana; Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;
9 Who does great things, and unsearchable, Marvelous things without number.
10 Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, Na kuyapeleka maji mashambani;
10 He gives rain on the earth, And sends waters on the fields.
11 Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.
11 He sets on high those who are lowly, And those who mourn are lifted to safety.
12 Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu, Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.
12 He frustrates the devices of the crafty, So that their hands cannot carry out their plans.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe; Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.
13 He catches the wise in their own craftiness, And the counsel of the cunning comes quickly upon them.
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, Hupapasa mchana vilevile k**a usiku.
14 They meet with darkness in the daytime, And grope at noontime as in the night.
15 Lakini yeye huokoa na upanga wa kinywa chao, Hata kumwokoa mhitaji na mkono wake aliye hodari.
15 But He saves the needy from the sword, From the mouth of the mighty, And from their hand.
16 Basi hivi huyo maskini ana matumaini, Na uovu hufumba kinywa chake.
16 So the poor have hope, And injustice shuts her mouth.
17 Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.
17 "Behold, happy is the man whom God corrects; Therefore do not despise the chastening of the Almighty.
18 Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza; Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.
18 For He bruises, but He binds up; He wounds, but His hands make whole.
19 Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa...