The Truth of My Hope-Jesus

The Truth of My Hope-Jesus Karibu katika ukurasa huu, tukayajue matendo makuu ya Mungu, kujifunza neno la Mungu, Maombi na Maombezi. 1yoh: 1:5-7.

28/10/2025
13/10/2025
14/05/2024

VITA VYA KI-MIUNGU VILIVYOPO KWA MZALIWA WA KWANZA, K**A LANGO LA WAZALIWA WENGINE
BWANA YESU ASIFIWE WANA WA MUNGU, Namshukuru Mungu sana kwa ajili ya wakati huu mzuri na kwa ajili yako wewe uliyekuwa tayari kusoma fundisho hilo, ambalo baada ya kujifunza hautabaki k**a jinsi ulivyo katika jina la Yesu Kristo.
Wote tunajua tunaposema mzaliwa wa kwanza ni nani, katika familia yako uliyozaliwa kuna mzaliwa wa kwanza yamkini ni wewe unayesoma ujumbe huu, tunasema mzaliwa wa kwanza ni lango kwa sababu anakuwa yeye ndiye wa kwanza kufungua tumbo la mama yake na kuwa lango, kuruhusu wazaliwa wengine kufuatia. Katika ulimwengu wa roho kuna maana kubwa sana na watoto hawa wanakuwa wamebeba Baraka kubwa sana ambazo zinatiririka hadi kwa wazaliwa wanaofuata. Kwa kuwa wamebeba umaana wa Baraka za Mungu. Kitabu cha KUTOKA 13:1-2 “Bwana akasema na Musa, akamwambia Nitakasie mimi wazaliwa wa kwanza wote, kila afunguaye tumbo katika wana wa Israel, wa binadamu na wa mnyama;ni wangu huyo.” Mungu, anasema na Musa awatakase wazaliwa wa kwanza wote, akisema wote hao ni wa kwake, wazaliwa wa kwanza wamebeba umaana mkubwa sana mbele za Mungu kwa sababu kupitia mzaliwa wa kwanza Mungu anapata uhalali wa kutawala familia ile yote.
Kwa nini watoto hawa wanakuwa na vita sana, ni kwa sababu wanapiganiwa/wanatafutwa na pande tatu (3), pande ya kwanza mtoto huyu anapiganiwa na Mungu mwenyewe aliye hai, pande ya pili, anatafutwa na miungu upande wa baba yake, na pande ya tatu anatafutwa na miungu ya upande wa mama yake. Mzaliwa wa kwanza anapitia vita vikubwa kwa sababu amebeba vifuatavyo:- amebeba Nembo ya familia, familia hiyo hutambulishwa kupitia yeye, Ni mteule wa Mungu, amebeba kusudi (Israel), mzaliwa wa kwanza husahihisha makosa ya familia, kuwasaidia wadogo zake, Mungu humpa kipawa cha uongozi, kuwaongoza wanamfuata njia iliyo sahihi, ana neema ya utajiri, ila aweze kuwainua wadogo kimaisha kwa ujumla.
Ukisoma kitabu cha Kutoka 4:22-23 “Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israel ni mwanangu mimi, MZALIWA WA KWANZA WANGU, nami nimekuambia, mpe ruhusa aende ili apate kunitumikia nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako. ‘’ …….kwa Mungu, Israel ni mzaliwa wa kwanza, huyu ndiye aliyebeba ukombozi wa ulimwengu, ukisoma maandika utaona Bwana wetu Yesu Kristo ametoka katika ukoo wa Daudi, ambapo asili ni mzaliwa wa kwanza, Israel. Vita hivi vya mzaliwa wa kwanza havijaanza leo, vipo tokea enzi ya ukombozi wa wana wa Israel. Kiroho, unaweza kuona Farao aling’ang’ana na kuwak**atia wana wa Israel ili wafanyike kuwa watumwa, hapana, alipambana ili kuzuia kusudi la Mungu lililobebwa ndali ya wana wa Israel, katika harakati za ukombozi wa ulimwengu mzima, kupitia Yesu Kristo.
Ukisoma tena, Kumbu. La torati 12:2..”Vunjeni kabisa mahali pale walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki”………..hii ni maadhi ya amri alizokuwa anatoa Bwana kwa wana wa Israel, mzaliwa wa kwanza wake….katika koo nyingi katika maisha ya sasa bado kunakutawaliwa na miungu, miungu hii inaweza ikawa ni ya upande wa baba au wa mama, ambayo bado imebema ile vita ya mzaliwa wa kwanza, miungu inapambana na mzaliwa wa kwanza katika familia kwa sababu amebeba Baraka ambazo zinashuka kwa wanaofuata na familia mzima.
Kuna baadhi ya familia, wazaliwa wao wa kwanza wanapitia katika changamoto kubwa za kimaisha, maisha yake hayaeleweki, hana kinachoendelea katika maisha yake, na wengine hata kuachia shule njiani, wengine wamesoma lakini hawana wanachojivunia, wengine ni maprofesa kabisa lakn ukiangalia maisha wanayoishi huoni k**a vinaendana, wengine wamek**atwa kwenye uzizi, wengine kwenye magonjwa, wengine kwenye mitala, kwenye pombe kupita kiasi, umasikini, utasa, nk. Kuna watoto Mungu ameachilia Baraka kubwa katika kuzibeba familia zao, kuzisaidia, lakini maisha ya huyo mtu yameshikiliwa na kuruhusu familia kubaki masikini, kuna watu ni wakubwa sana katika nchi hii, yamkini kwenye siasa, biashara, kwenye huduma, kazi, nk. lkn huoni wakiishi maisha yale Mungu amekusudia kuishi.
Mzaliwa huyu wa kwanza, anakuwa amek**atwa na miungu, kwa sababu akik**atwa yeye familia nzima inakuwa imek**atwa ili kuharibu lile kusudi la Mungu lilibebwa na familia husika. Mtoto huyu akifunguliwa, basi wote wanaofuta wanakuwa wemefunguliwa hata wale wa uzao wake. Wakati mwingine wadogo wanamuangalia mkubwa wao mzaliwa wa kwanza, wanaiga maisha yake, hivyo k**a anaishi maisha ya Baraka, hivyo wadogo wanarithi matendo ya mkubwa wao, ikitokea sasa maisha anayoishi ya hovyo, wadogo nao yamkini wakafuta hivyo, kwa sababu ya ile roho ya laana aliyeachiwa mzaliwa wa kwanza. je,? ulishawahi kuona mzazi anaishi maisha ya mitala, na watoto wanaishi maisha hayohayo?
Nini ufanye, fanya maombi ya kuita damu ya Yesu ipite kila mahali uliposhikiliwa, ita damu ya yesu ikutenganishe wewe na nguvu za kimiungu zilizokushikilia, Wakolosai 1:19-20 “kwa kuwa katika yeye (Yesu) ilipendeza utimilifu wote ukae, na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiishakufanya amani kwa DAMU ya msalaba”, Damu ya yesu Kristo hutengeneza agano jipya kati yako na Mungu, ukiisha kufanya agano kwa damu ya Yesu, miuungu haitakuwa na uhalali tena katika maisha yako..kitabu cha Marko 14:24 “akawaambia, hii ndiyo DAMU yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi”…….maombi yako yaambatane na kutoa SADAKA, toa sadaka kwa ajili ya ukombozi wako, k**a wewe nimzaliwa wa kwanza, pia unaweza kutoa sadaka kwa ajili ya mwanao ambaye ni mzaliwa wa kwanza…soma KUTOKA 13:13 “kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana- kondoo, na kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu katika wanao utamkomboa”. Unadhani kwa nini Mungu alisema haya? Mungu anajua mzaliwa wa kwanza amebeba uthamani gani kwake yeye Mungu kwanza lakini pia kwa familia kwa ujumla. Soma pia. Kumbu. 21:16,17
Nikurudishe katika neno hili KUTOKA 13:1-2 “Bwana akasema na Musa, akamwambia Nitakasie mimi wazaliwa wa kwanza wote, kila afunguaye tumbo katika wana wa Israel, wa binadamu na wa mnyama;ni wangu huyo.”…hapa mnyama ametajwa katika mzaliwa wa kwanza, mnyama hapa anaweza pia kuwa kiwakilishi cha mali zako zote unazozianzisha kwa mara ya kwanza, mfano unataka kufungua biashara, biashara inaweza kuwa mzaliwa wa kwanza katika maisha yako, je, unatoa sadaka ya ukombozi kwa ajili ya hiyo biashara? Inaweza ikawa ni biashara, kazi, ndoa yako, mifugo nk. Hivyo, katika kuomba sio tu unaomba kwa ajili ya binadamu, omba na toa sadaka kwa ajili ya dhughuli zako unazozianzisha.
MUNGU AKUBARIKI MWANA WA MUNGU.
SOMO LINALOFUATA, VITA VYA ROHONI VILIVYOPO JUU YA MTU ANAYEPATA NEEMA YA WOKOVU NA NINI AFANYE ILI KUSHINDA VITA HIVYO. Usiapange kukosa.
HAULE JP-0767 565834

03/04/2024

FAIDA ZILIZOPO NDANI YA UZIMA WA MILELE
UZIMA WA MILELE NINI ?
Uzima wa milele ni ZAWADI anayotoa Mungu kwa wanadamu wanaoamini katika Yesu Kristo. Nikisema kwa wanaoamini, inamaanisha kuwa wanadamu wasioamini katika Yesu Kristo hawawezi kupokea zawadi hii. Yoh. 3:36. “Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele, asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.”

Mara nyingi watu wanafananisha Uzima na Afya, Uzima unaozungumzwa katika maandiko matakatifu ni zaidi ya afya na kinyume na mauti. Neno Milele, tuite umilele, hauhusiani na miaka mingi, wakati ujao, uzima wa milele unafanya kazi zaidi ya muda au nyakati. Unapompokea Yesu Kristo tayari uzima wa milele unanza kufanya kazi muda huo huo, inamaana mtu anayeamini anao uzima huo, yaani muda huo huo.

Binadamu anaweza akawa ana afya nzuri sana lakini asiwe na uzima wa milele, uzima wa milele ni KITU cha kiroho kinachoachiliwa na Mungu kupitia Yesu Kristo. Yoh. 6:36 “Amin, amin, nawaambia, yeye aaminiye yuna uzima wa wa milele.” Uzima huu, utaupata pale ambapo utampokea Yesu Kuwa Bwana na Mwokozi wako, ukimjua Mungu. Yohana 17:3 “Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”

1 Petro 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye UZIMA kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu.” Kuzaliwa mara ya pili maana yake ni nini? Ni swali muhimu kwa sababu jibu lake ni chanzo pia cha binadamu kuwa na uzima wa milele, (soma Yoh. 3: 3-6) imeandikwa, kilichozaliwa kwa mwili ni mwili na kilichozaliwa kwa Roho ni roho, kuzaliwa kwa katika Roho huko ndiko kuzaliwa mara ya pili, ni pale ambapo Binadamu anapo TUBU DHAMBI na kumpokea Yesu Kristo Kuwa Ni Bwana na Mwokozi wake, kwa kufanya hivyo UZIMA unaingia ndani yake.

Mwanadamu anaishi katika maeneo mawili, anaishi katika
ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili, na tukumbuke asilimia kubwa ya maisha yetu yapo katika ulimwengu wa roho. Maisha yako ya rohonni ndiyo yanayojulisha Uzima wako wa milele upoje na wala sio maisha yako ya mwilini. Mungu ni Roho na Anafanya kazi kwa jinsi ya rohoni.

Yesu anasisitiza, atakayemuamini ndiye atakayepokea uzima wa milele, hapa anamaanisha Mungu ana kundi lake ambalo ni teule kupokea uzima, ni yeyote aliye tayari kumuamini yeye na kuokoka, huyo atapokea. Mungu kwa kutupenda kupitia Bwana wetu Yesu Kristo aliweka uzima huo ili tuzidi kumjua yeye, pia kuna faida ambazo mtu anayemwamini Yesu na kumpokea anazipata kutokana na ule uzima wa milele; faida zipo nyingi leo tuziangalie hizi chache….
1. UNAPATA ULINZI. Mungu anakupa ulinzi kwenye maisha yako ya kila siku. Yeremia 15: 20 “Nami nitakufanya kuwa k**a ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa, nao watapigana nawe, lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema Bwana” Mungu anakupa ulinzi kwenye kila kilichopo katika maisha yako, afya, uchumi, familia, ndoa nk.
2. KUPOKEA BARAKA. Ukiwa na uzima wa milele, baada ya kumpokea Yesu, utaanza kuona Baraka za Mungu zinakuijilia. Waefefo 1:3. “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa Baraka zote za rohono, katika ulimwengu war oho, ndani yake Kristo;………..Mungu ataanza kukupa Baraka, maisha yako yanaanza kufunguka, kubadirika, kiuchumi, afya nk.
3. KUKUSHINDIA MAJARIBU, Unapokuwa Na uzima ndani yako, Unaweza kushinda majaribu hata yale unayoyaona ni magumu MUngu anakushindia. Yesu alijaribiwa na shetani, tena amejaribiwa baada tu ya kutoka kufanya maombi ya kufunga pale mlimani, wewe na mimi ni nani hata tusijaribiwe? Lkn katika kumpokea Yesu, Uzima unakaa ndani yako na hakuna jaribu lolote litakalo kupata. 2 Wakorinto 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo la wanadamu, ila Mungu ni mwaminifu, ambaye hataawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea. Ili mweze lustahimili”.
4. UNAKUWA NA MAMLAKA YA KIKUHANI. Luka 10: 19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za Yule adui , wala hakuna kitu kitakachowadhuru 20. Lakini wala msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni”…Unajua, kazi ya kufukuza pepo sio kazi ya mchungaji tu, hata wewe unayesoma ujumbe huu, lakini utaweza pale tu utakapompokea Yesu kristo na kumuweka kuwa Bwana na mwokozi wako katika maisha na kuisha maisha matakatifu, jina lako linaandikwa mbinguni unakuwa mteule. Mungu anakupa mamlaka ya kutawala, kumiliki.
5. KUWA HURU. Ukimpokea Yesu, Uzima ukiwa ndani yako, utaijua KWELI, na hiyo kweli itakuweka kuwa huru. Yohana 8. 31 “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli, 32. Tena MTAIFAHAMU KWELI, NA HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.” Ukimuamini Yesu Katina neno lake Uzima utakuwa juu yako, utaweza kuifahamu KWELI, na hiyo kweli itakuweka HURU…Mungu atakupa ufahamu wa rohoni, atakupa maarifa, atakupa hekima, macho ya mioyo yako yatatiwa nuru utaweza kuona visivyoonekana kwa macho ya kwaida, pia, utaweza kusijimamia katika masuala ya kiroho na sio kuwategemea wanadamu.

Leo, tumeweza kuangalia faida hizo tano, lakini zipo nyingi sana, ninakuombea UZIMA uwe juu yako, maisha yako yawe ya kumtegemea MUNGU na sio mwanadamu au mazingiza yaliyokuzunguka. Uzima ukikaa ndani yako utaweza kutawala mazingira yaliyokuzunguka, usiruhusu mazingira kukutawala wewe…hii ni kanuni. Mungu alimpa Adamu kuitawala bustani ya Edeni sio Bustani kumtawala Adamu na Hawa. Mwisho, nakuombea usishiriki au kufanya jambo kwa Ushabiki, au kusema nitaonekanaje nisipoenda au nisipofanya, hii kuna watu wengi wamepita katika changamoto pasipo kujua, UZIMA uwe juu yako ili Roho Mtakatifu apate nafasi ya kukujulisha, kukuepusha na kila mitego unayotegewa iwe kupitia vyakula, vinywaji au kwa namna yoyote ile. Mungu akubari sana.
SOMO LIJALO: VITA VYA KI-MIUNGU VILIVYOPO KWA MZALIWA WA KWANZA KWENYE FAMILIA K**A LANGO, KIATU CHA URITHI, KINAVYOWEZA KUHARIBU AU KUSTAWISHA MAISHA YA WATU. LANGO NI NINI? KIATU CHA URITHI NI NINI? JE; KWENYE FAMILIA YAKO MZALIWA WA KWANZA ANA HALI GANI YA KIMAISHA KWA UJUMLA? KWA NINI MIUNGU INAPAMBANA NA MZALIWA WA KWANZA? TUONANE KATIKA SOMO HILI, Usipange kukosa, Mungu Aliye Hai Akubariki Sana.
HAULE JP. 0767565834

BAADHI YA AGENDA KUU ZA MUNGU KWA WANADAMU.1. UTAKATIFU, KUACHA DHAMBI2. KUWA NA UTAJIRI3. KUWA NA AFYA NA UZIMALeo tugu...
23/03/2024

BAADHI YA AGENDA KUU ZA MUNGU KWA WANADAMU.

1. UTAKATIFU, KUACHA DHAMBI
2. KUWA NA UTAJIRI
3. KUWA NA AFYA NA UZIMA
Leo tugusue kidogo tu kuhusu utajiri, afya na Uzima. Mungu hajakuumba ili uwe masikini, ili uteseke, ili uwe na afya mbovu, ili usiwe na Uzima, Mungu ametutengeneza na kutufinyanga ktk mwili na roho ili tubarikiwe katika kila eneo..

2 Wakorintho 8: 9
(2 Corinthians)
9. Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
---------------
Kwa umasikini wa Yesu,kwa kuteswa kwake, wewe umekuwa tajiri, tunaposema tajiri waza baraka kwenye kila eneo la maisha yako, ktk familia, ndoa, kazi, huduma, watoto, elimu, biashara, shambani kila eneo, wewe ni tajiri.

3 Yohana 1:
(3 John)
2. Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo.
---------------
Afya ni haki yako, ni ahadi kutoka kwa Mungu Baba, ingawa tunafundishwa pia, ukitaka KUWA na afya kunywa maji, chukua mazoezi, zingatia mlo wako nk. Lkn Bado kiroho Afya ni ahadi Mungu ameweka, kuna wanaofanya hayo yote kulinda afya zao lakini Bado hawana afya.

Sasa, kwa ujumbe huu mfupi sana, jaribu kutafakari ndani ya moyo wako, jiulize k**a ni AHADI kutoka kwa Mungu kwa nini huoni hizo baraka? maendeleo, mafanikio, afya njema, Uzima, amani, furaha, utajiri nk. Ni kwa nini upo katika hali hiyo hiyo? ( unachokitamani kiwe, hakiwi) Ndugu yangu, nikukumbushe Leo haya yote yanapatikana ndani ya Yesu Kristo aliye hai, ndani ya Yesu kuna Uzima, kuna afya, Kuna utajiri, kuna kila kitu unachokitamani ktk maisha.

AMUA LEO KUMPOKEA YESU KRISTO AWE BWANA NA MKOMBOZI WAKO. YEYE YESU ATAINGILIA KATI MAISHA YAKO, ATAKAA NDANI YA MOYO WAKO, ATAKUFINYANGA NA KUKUTENGENEZA KWA UPYA, UNACHOPASWA KUFANYA NI KUWA NA IMANI TU. Unaweza kuwepo kanisani masaa mengi lkn hujampokea Kristo Yesu hayupo ndani yako bado, lazima kujua, huyu Yesu yupo ndani yangu? Je, anatenda sawasawa na ahadi zake?

Pengine kuna maswali mengi ya kujiuliza, nakushauri tenga muda wako mzuri, kaa faragha jitenge, baki wewe na Yesu wako tu, ongea naye , mwambie Mungu natamani kukuona na kukujua katika maisha YANGU, Muombe Roho Mtakatifu akusaidie, katika hiyo tafakari KUU (Meditation) yenye ukimya Mkuu, Roho atasema nawe, anza kuchukua hatua kile utakachosemeshwa, utaona giza lililokuwa ndani yako, ambalo lilikuwa linasababisha hata usijue kesho yako, usijue dira ya maisha yako, usijue hatima ya afya yako, UTAANZA kuona NURU ya Yesu Kristo inaanza kuingia na kukusaidia,

Yohana 8:
(John)

12. Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
---------------
K**a Bado hujampokea Yesu na unatamani Yesu aanze kutawala maisha yako...omba sala hiii....

Ee BWANA YESU, MIMI FULANI....(taja jina) NINAKUJA MBELE ZAKO, NINAOMBA UNISAMEHE MAOVU YANGU YOTE, DHAMBI ZANGU ZOTE, NILIZOFANYA SEHEMU ZA SIRI NA SEHEMU ZA WAZI KWA DAMU YA YESU, NINAOMBA UNIOSHE NA KUNITAKASA KWA DAMU YAKO YENYE THAMANI, ULIONDOE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU NA ULIWEKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA KWA JINA LA YESU, Ee BWANA YESU KAA NDANI YANGU, TAWALA MAISHA YANGU, ROHO MTAKATIFU UNISAIDIE KWA JINA JINA LA YESU NA KWA DAMU YA YESU. AMINA.

Baada ya hii sala Mshukuru Mungu, amini kabisa Tayari umempokea Yesu Kristo. HAKIKA UTAANZA KUONA NGUVU MPYA INAINGIA NDANI YAKO.

AMINA.
*************************

# # SOMO LIJALO, ni Kuhusu AFYA na UZIMA...NI VITU VINAVYOFANANA ILA ROHONI VIPO TOFAUTI,

Mtu anaweza kuwa na AFYA ila asiwe na UZIMA, Anaweza akawa na UZIMA ila asiwe na AFYA. (Tumeweza kushuhudia, tunayemuona ana afya akapoza maisha haraka kuliko tunayemuona mgonjwa). UZIMA NI NINI? UZIMA NI NINI? UZIMA NI NINI? majibu utayapata katika somo LIJALO.

UBARIKIWE MTU WA MUNGU.
Haule JP. 0767565834
# # # # # # # # # # # # # # # # # #

06/01/2024

ABOUT 2024
Prophetess Evelyn TB Joshua -SCOAN
IS THE YEAR OF A NEW NAME ..GENESIS 17:5

Chief Prophet Nicolaus Suguye- WRM
IS THE YEAR OF BIENG CROWNED WITH GOODNESS...Psalms 65:11

Man of God Joel Haule (......)
IS THE YEAR OF RESTORATION..Joel 2:25-27

12/09/2023

Hekima na Busara

Nini?
Kwa nani?
Wakati gani?
Wapi?
Na Kwa nini?
Nakuombea kila ukifanyacho uongozwe na Roho Mtakatifu, Busara na Hekima, vitawale katika maisha yako.

19/08/2023

"Kila unapokaribia kubarikiwa ndivyo shetani anavyozidisha vita..."

Usikate tamaa, endelea kusimama, hapo unapoona pagumu ndipo mpenyo wako ulipo, endelee kuomba, omba, omba, omba...

Wagalatia 5:1
Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.

03/08/2023

Luka 9:23-24
[23]Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

[24]Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

# # tayari kutukanwa kwa ajili ya Yesu, kuwa tayari kutengwa na binadamu kwa ajili ya Bwana Yesu, ukiona kila unapokaribia kumpata Yesu, halafu kuna binadamu wanainuka kukukatisha tamaa, ujue ushindi wako umekaribia, usiache mk**atie Bwana Yesu kisawasawa.

NINAKUOMBEA WIKI INAYOANZA LEO, MILANGO YA BARAKA KATIKA UCHUMI, AFYA, FAMILIA, KAZI, NDOA KWENYE MAISHA YAKO, IKAFUNGUK...
20/03/2023

NINAKUOMBEA WIKI INAYOANZA LEO, MILANGO YA BARAKA KATIKA UCHUMI, AFYA, FAMILIA, KAZI, NDOA KWENYE MAISHA YAKO, IKAFUNGUKE KWA JINA LA YESU!

Address

Guangzhou

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Truth of My Hope-Jesus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to The Truth of My Hope-Jesus:

Share