Ministère MPA

Ministère MPA Nous sommes déterminé pour proclamer la bonne nouvelle du Royaume Mathieu 24:14, Éphésiens 2:20-21

07/27/2026
06/23/2026

SOMO LA LEO: MOYO WENYE SHUKRANI HUMPENDEZA MUNGU
1 Wathesalonike 5:18"Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu."

NENO KUU: Shukrani kwa Mungu.
WAZO KUU: Mungu hufurahishwa na watu wanaojua kutambua wema wake na kumshukuru katika kila hali ya maisha.
SHABAHA: Kukuhimiza wewe muumini kuwa na moyo wa shukrani kila siku, ukitambua kwamba kila jambo jema hutoka kwa Mungu.

UTANGULIZI
Ni rahisi kumshukuru Mungu wakati mambo yanakwenda vizuri. Tunapopata kazi, tunapopona ugonjwa, tunapofanikiwa katika biashara au tunapopokea baraka tulizoziomba, shukrani hutoka kwa urahisi. Lakini mtume Paulo anasema:"Shukuruni kwa kila jambo." Hakusema shukuruni kwa mambo mazuri pekee. Alisema kwa kila jambo. Hii haimaanishi kufurahia mateso au majaribu, bali kutambua kwamba hata katikati ya hali ngumu, Mungu bado anatawala na ana kusudi jema kwa maisha yetu.

1. SHUKRANI HUONYESHA KWAMBA TUNAMTAMBUA MUNGU
Yakobo 1:17"Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga." Watu wengi hupokea baraka lakini husahau chanzo chake. Mtu anapata afya nzuri, lakini hasemi asante. Anapata kazi, lakini hamkumbuki Mungu. Anapata familia nzuri, lakini hana muda wa kumshukuru Mungu. Moyo wenye shukrani hutambua kwamba kila tulicho nacho ni zawadi kutoka kwa Mungu.

Fundisho:
Kadiri tunavyotambua wema wa Mungu, ndivyo shukrani zetu zinavyoongezeka.

2. SHUKRANI HUFUKUZA MANUN'UNIKO
Wafilipi 2:14 "Yatendeni yote pasipo manung'uniko."
Waisraeli waliona miujiza mingi jangwani, lakini mara nyingi walilalamika.
Badala ya kuhesabu baraka walizopokea, walikazia macho matatizo yao.
Matokeo yake, walikosa furaha na amani. Mtu mwenye moyo wa shukrani huona kile Mungu amefanya badala ya kuangalia tu kile ambacho bado hajapata.

FundishoManung'uniko humfanya mtu asione baraka zake, lakini shukrani humfanya azione hata zilizo ndogo.

3. SHUKRANI HULETA AMANI MOYONI
Wafilipi 4:6-7"Katika kila neno kwa kusali na kuomba pamoja na kushukuru..."
Paulo anaunganisha maombi na shukrani. Tunapomshukuru Mungu, mioyo yetu hujazwa amani.
Badala ya kuishi katika wasiwasi, tunaanza kukumbuka jinsi Mungu alivyotutunza zamani. Na k**a alitusaidia jana, atatusaidia tena leo.
Fundisho: Moyo wa shukrani hujenga imani na kuondoa hofu.

4. YESU ALITUACHIA MFANO WA SHUKRANI
Luka 22:19. Kabla ya kula mkate katika karamu ya mwisho, Yesu alishukuru. Hata kabla ya kumfufua Lazaro, Yesu alimshukuru Baba. Yesu alionyesha kwamba shukrani si jambo la kufanya baada ya kupata kila kitu tunachotaka, bali ni mtindo wa maisha.

Fundisho: Ikiwa Yesu mwenyewe alikuwa na moyo wa shukrani, sisi pia tunapaswa kuishi kwa shukrani.

5. MUNGU HUFURAHISHWA NA WATU WENYE SHUKRANI
Luka 17:15-18 Yesu aliwaponya watu kumi wenye ukoma. Lakini mmoja tu alirudi kumshukuru. Yesu akauliza: "Je! hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wako wapi?"Mungu anathamini moyo unaorudi kutoa shukrani.

Fundisho: Usiwe mtu anayepokea baraka na kuondoka kimya kimya. Jifunze kurudi na kusema, "Asante Bwana."

HITIMISHO
Leo ukiangalia maisha yako, utagundua kwamba Mungu amekufanyia mengi. Amekupa pumzi ya uhai. Amekulinda katika hatari nyingi usizoziona. Amekupa nguvu za kuendelea. Amekupa neema ya kufika leo. Huenda bado kuna maombi ambayo yanasubiri majibu. Lakini bado unayo sababu nyingi za kumshukuru Mungu.Kwa hiyo, usisubiri mpaka kila tatizo liishe ndipo umshukuru Mungu.Mshukuru sasa. Mshukuru kila siku.Mshukuru katika furaha na katika majaribu. Kwa sababu moyo wenye shukrani humpendeza Mungu.

TUOMBE:
Baba yetu wa mbinguni, ninakushukuru kwa wema wako, rehema zako na upendo wako usio na mwisho. Asante kwa pumzi ya uhai, kwa ulinzi wako, kwa chakula, kwa familia, na kwa neema zako ambazo naziona na hata nisizoziona. Nisamehe pale ambapo nimekuwa nikilalamika badala ya kushukuru. Nifundishe kuwa na moyo wa shukrani katika kila hali ya maisha. Nijalie kuona wema wako kila siku na nikutumike kwa furaha na unyenyekevu. Na maisha yangu yawe sadaka ya shukrani mbele zako siku zote. Naomba haya kwa Jina la Yesu Kristo. Amina.

Comments, shares na likes ni mojawapo ya njia ya kushirikiana nasi katika kuwafikia wengi iwezekanavyo. MUNGU akubarik

Avec Magical sports  – Je fais désormais partie de ses super fans ! 🎉
04/20/2026

Avec Magical sports – Je fais désormais partie de ses super fans ! 🎉

Avec Saviour A, k,a Sparrow  – Je fais désormais partie de ses super fans ! 🎉
04/20/2026

Avec Saviour A, k,a Sparrow – Je fais désormais partie de ses super fans ! 🎉

04/08/2026

THÈME: DIEU EST LA FORCE ET LA PROTECTION DE TA VIE
VERSET CLÉ: (Psaume 28:7) « L'Éternel est ma force et mon bouclier ; mon cœur s'est confié en lui, et j'ai été secouru. Aussi mon cœur est dans la joie, et je le louerai par mes cantiques. »

Ce verset est le témoignage de David après avoir traversé la peur et les combats. Il a découvert que la vraie force et la sécurité dans la vie ne s'obtiennent pas par la puissance humaine, mais en s'appuyant sur Dieu. Ce message touche toute personne qui se sent faible, craintive, ou incertaine du lendemain.

1. L'ÊTRE HUMAIN VIT EN CHERCHANT FORCE ET PROTECTION
Chacun cherche un refuge :

A) certains s'appuient sur l'argent,
B) d'autres s'appuient sur les hommes,
C) d'autres encore s'appuient sur le savoir ou le pouvoir.

Mais la vie montre que toutes les choses de ce monde ont des limites.
La peur demeure :

a) la peur du lendemain,
b) la peur de l'échec,
c) la peur de la mort,
d) la peur de la solitude.

👉 Au fond du cœur humain se trouve un besoin de vraie protection.

2. « L'ÉTERNEL EST MA FORCE »
David n'a pas dit « j'ai de la force », mais il a dit : L'Éternel est ma force. Cela signifie que :

a) la vraie force vient de Dieu,
b) l'être humain seul se fatigue,
c) le cœur de l'homme perd espoir sans Dieu.

📖 Ésaïe 40:29 — Il donne de la force à celui qui est épuisé.
Beaucoup de gens semblent solides en apparence, mais intérieurement ils sont épuisés.
C'est Jésus qui donne la force intérieure.

3. « ET MON BOUCLIER » — LA VRAIE PROTECTION
Le bouclier est un instrument de guerre qui arrête les flèches de l'ennemi. Spirituellement, ces flèches sont :

a) le péché,
b) la peur,
c) les attaques de la vie,
d) la condamnation de la conscience.

L'être humain ne peut pas se protéger seul contre les combats spirituels. Mais Dieu devient le bouclier de celui qui se réfugie en Lui. 📖 Psaume 91:4 — Sa fidélité est un bouclier et une cuirasse.

4. LE SECRET DU CHANGEMENT : « MON CŒUR S'EST CONFIÉ EN LUI »Le changement s'est produit lorsque David a mis sa confiance en Dieu.

Le problème de l'être humain n'est pas l'absence d'aide — c'est le manque de confiance en Dieu. La Bible dit : 📖 Jérémie 17:5 — Maudit soit l'homme qui se confie en l'homme. Mais celui qui croit en Dieu reçoit une aide véritable.

5. JÉSUS EST LA FORCE ET LA PROTECTION DE L'ÊTRE HUMAIN
Dieu a envoyé Jésus pour être notre salut. Pourquoi ? Parce que le plus grand ennemi de l'être humain est le péché. 📖 Romains 6:23 — Le salaire du péché, c'est la mort. Mais grâce à Jésus :

a) le péché est pardonné,
b) le cœur trouve la paix,
c) la vie reçoit une protection éternelle.
📖 Jean 10:28 — Personne ne les arrachera de ma main.

6. LES FRUITS DE LA RÉCEPTION DU CHRIST
David a dit : « Mon cœur est dans la joie… »
Celui qui reçoit Christ reçoit :

✅ la paix à la place de la peur
✅ l'espérance à la place du désespoir
✅ la force à la place de la faiblesse
✅ la joie intérieure. La vraie joie commence lorsque l'on rencontre Dieu.

7. L'APPEL DE DIEU POUR TOI
Aujourd'hui, tu te fies peut-être à toi-même, mais ton cœur a encore peur. Jésus t'invite aujourd'hui :

a) à Le recevoir comme ta force,
b) à Le laisser être la protection de ta vie,
c) à recevoir une vie nouvelle.
Il n'y a pas de vraie sécurité en dehors du Christ.

🔥 CONCLUSION DE MESSAGE
Le Psaume 28:7 nous enseigne :
👉 Dieu est une force qui ne s'épuise jamais.
👉 Dieu est une protection qui ne faillit pas.
👉 Et celui qui croit en Christ reçoit une aide véritable.
Ne vis pas sans bouclier alors que Dieu veut être la protection de ta vie.

SI CE MESSAGE T'A TOUCHÉ, JE T'INVITE À PRIER AVEC MOI POUR RECEVOIR LE SALUT, COMME SUIT:

Seigneur DIEU, je reconnais que j'ai essayé de vivre par mes propres forces. Aujourd'hui, je me confie en Toi. Pardonne mes péchés, sois ma force et le bouclier de ma vie. Entre dans mon cœur et guides-moi à partir d'aujourd'hui. Au nom de Jésus-Christ je prie, Amen.

03/24/2026

TOPIC: NI NINI KINACHOKUCHELEWESHA?

Sababu moja inayokuchelewesha ni hii:
Unajua unachopaswa kufanya…lakini hufanyi.

Si kwamba hujui.
Ni kwamba tu hujachukua hatua.

Maisha yatabadilika utakapoanza kutii kile unachojua tayari.
Usisahau kulike, share na comment kwa maarifa zaidi!

03/20/2026

👉 KWA NINI UNASALI LAKINI MAISHA YAKO HAYABADILIKI?

Fikiria, Unasali kila siku…lakini hakuna kinachobadilika.

Ukweli mchungu ni huu: si kila sala inabadilisha maisha.

Watu wengi wanaongea na Mungu…lakini hawamsikilizi.

Unaomba baraka…lakini hubadilishi tabia.

Sasa jiulize:
Je, sala zako zinakubadilisha…au ni maneno tu?

K**a unapendezwa na mafundisho k**a haya, tafadhali, Share, like na ukoment hapa chini.

03/18/2026

Je, kweli unamfuata Mungu, au unajidanganya tu?

Unasema unampenda Mungu. Lakini je, unatii kile anachosema?

Watu wengi wanapenda hisia za dini…
lakini hawapendi ukweli wake.

Kumfuata Mungu si hisia. Ni uamuzi mgumu kila siku.

Sasa jiulize kwa uaminifu:
Unamfuata Mungu…au unafuata unachotaka?

03/17/2026

UNGEPENDA KUFAHAMU ZAIDI KUHUSU TUMAINI LETU? UNAWEZA KUTUTEMBELEA KANISANI AU KUTUANDIKIA PIA!

03/16/2026

USIMSAHAU MUNGU WAKO HATA K**A UNATESEKA

Adresse

1292 Rue Larocque
Sherbrooke, QC
J1H4R9

Heures d'ouverture

Mercredi 6pm - 7pm
Jeudi 6pm - 7pm
Vendredi 6pm - 7pm
Samedi 8am - 7pm
Dimanche 5pm - 7pm

Téléphone

+18193425331

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Ministère MPA publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Raccourcis

Partager