13/04/2023
Kwa sababu ya MUNGU chochote kitakachojaribu kusimama kinyume chako hakitafanikiwa kwa jina la Yesu...!
Kwa sababu ya MUNGU kila mipango ya siri inayopangwa na adui zako, kila mipango ya siri inayopangwa na kuzimu ili ikudhoofishe kiroho, kimwili, ki-akili, ki-uchumi haitafanikiwa kwa jina la Yesu...!
Kwa sababu ya MUNGU kila mishale iliyoelekezwa kwako kujeruhi na kushambulia nafsi, moyo, mwili, familia yako, ndoa yako, uchumi wako, mahusiano yako, elimu yako, taaluma yako n.k ....INARUDI KWA ALIYEITUMA KWA JINA LA YESU...!
Kwa sababu ya MUNGU utaishi kutimiza kusudi lake na lako hapa duniani...Maisha yako hayatakatishwa kabla ya kutimiza kusudi lake na lako.
Kwa sababu ya MUNGU utafika walikosema hutafika na Mungu atakupa hatua kubwa za kiroho na kimwili ambazo hawakutarajia....
Kwa sababu ya MUNGU UTASHINDA VITA VYOTE...Haijalishi ni vita ya kiroho au ya kimwili,...UTASHINDA KWA KISHINDO kwa jina la YESU...!
USIOGOPE....INUA KICHWA CHAKO NA TEMBEA KWA UJASIRI UTIMIZE NDOTO YAKO, MAANA MUNGU YU PAMOJA NAWE KUKUSAIDIA...🙏🙏!
●Kumbukumbu la Torati 28:7,"BWANA atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba."
●Zaburi 7:15-16,"Amechimba shimo, amelichimba chini sana, akatumbukia katika handaki aliyoifanya.Madhara yake yatamrejea kichwani pake, na dhuluma yake itamshukia utosini."
●Isaya 54:17,"Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa..."
Isaiah