Neno la Kristo

  • Home
  • Neno la Kristo

Neno la Kristo Karibu tujifunze Neno la Kristo pamoja

28/04/2026

MWANAUME

Ukiacha haya utakua mtu hatari zaidi (kiakili, kifedha, na hata kiroho).

1. Punyeto

Hii inakuondolea nguvu ya ndani bila wewe kujua. Unapoteza hamasa ya kufanya kazi, unakuwa mlegevu kiakili na kimwili. Ukiacha, utaona nguvu zako zinarudi, focus inaongezeka, na unaanza kuwa na control juu ya nafsi yako. Hakuna mpiga nyeto aliyefanikiwa kwa chochote



2. P**n (video za ngono)

Hii inaharibu ubongo wako taratibu. Unaanza kuzoea raha ya haraka isiyo na effort, na maisha ya kawaida yanaanza kukuonekana boring.

Ukiacha, utaanza kufurahia vitu halisi vya maisha na kupata hamasa ya kufanya kazi na kujenga maisha yako.



3. Kuishi bila direction

K**a hujui unataka nini, utatumia nguvu zako zote vibaya. Unakuwa busy lakini hauendi popote. Mwanaume anahitaji direction, iwe ni pesa, afya, au malengo ya maisha. Bila hivyo, miaka inaenda tu bila mabadiliko.



4. Marafiki wasiokuwa na malengo

Watu unaokaa nao wanaathiri maisha yako moja kwa moja. K**a kila siku ni stori za mipira, udaku, madem, starehe na hakuna anayekusukuma kuwa bora au kukuconnect kwenye fursa utaishia kuwa k**a wao.

Ukibadilisha mazingira, hata mindset yako inabadilika.



5. Kupoteza muda kwenye social media

Unatumia muda mwingi kuangalia maisha ya wengine kuliko kujenga maisha yako. Taratibu unapoteza focus na muda unaenda bila faida. Ukipunguza matumizi, utapata muda wa kufikiri, kujifunza, kufanya kazi, na kuongeza kipato.



6. Kukimbilia raha kuliko majukumu

Ukizoea kuchagua vitu rahisi, maisha yatakuwa magumu. Ukijifunza kuchagua vitu vigumu vinavyokujenga, maisha yanakuwa rahisi baadaye. Discipline ndiyo inatengeneza mwanaume imara.



7. Betting (k**ari)

Inakufanya utegemee bahati badala ya kazi. Unapoteza focus kwenye kazi au biashara. Ukiacha, unajenga pesa halisi......

Mabadiliko ya mwanaume hayawezi kuja kwa bahati. Yanakuja kwa kuacha vitu vinavyomrudisha nyuma na kuchagua vitu vinavyomjenga.

Ukidhibiti akili yako, muda wako, na tabia zako maisha yako yote

16/04/2026

TOFAUTI KATI YA KUTOA KWA UFUNUO NA KUTOA KWA MSUKUMO WA NJE

1. Utangulizi
Katika maisha ya kiroho, watu wengi huchanganya kati ya:
kufanya jambo jema (kutoa, kusaidia)
na kufanya jambo kwa uongozi wa Mungu
Wengi hutoa wakitegemea matokeo fulani, lakini si kila kutoa kunatokana na ufunuo.
Hivyo, ni muhimu kuelewa chanzo cha kile kinachotusukuma kutoa.

2. Maana ya “Kutoa kwa Ufunuo”
Kutoa kwa ufunuo ni:
kufanya tendo la kutoa baada ya kuongozwa na Roho Mtakatifu, ukiwa na amani ya ndani na imani ya kweli.

Sifa zake:
Kuna amani ya ndani
Hakuna presha kutoka kwa watu
Huna masharti kwa Mungu
Unakuwa tayari hata k**a matokeo hayaji haraka
Unafanya kwa utii, sio kwa biashara

3. Maana ya “Kutoa kwa Msukumo wa Nje”
Hii ni kutoa kunakotokana na:
kusikia shuhuda za wengine
presha ya mazingira
au tamaa ya kupata matokeo fulani

Sifa zake:
Unafanya kwa kufuata mkumbo
Ndani kuna matarajio makubwa ya matokeo
Unataka Mungu ajibu kwa haraka
Matokeo yakichelewa, unaanza kulalamika

4. Chanzo cha Tatizo
Watu wengi wanachanganyikiwa kwa sababu:
Wanachukua imani ya wengine na kuifanya yao bila ufunuo binafsi
Wanageuza kutoa kuwa k**a biashara na Mungu
Hawajifunzi kusikiliza sauti ya ndani

5. Madhara ya Kutoa kwa Matarajio
Kukata tamaa
Kumlaumu Mungu
Kupoteza imani polepole
Kufanya mambo ya kiroho kwa mazoea bila uhalisia

6. Faida ya Kutoa kwa Ufunuo
Huleta amani ya kweli
Hujenga imani ya ndani
Humfanya mtu awe na uhusiano wa karibu na Mungu
Hata bila matokeo ya haraka, mtu hubaki thabiti

7. Jinsi ya Kutofautisha (Practical Guide)
Jiulize maswali haya kabla ya kutoa:
Je, nina amani ndani yangu au ninaharakishwa?
Je, niko tayari hata nisipoona matokeo ya haraka?
Je, nafanya kwa kumtii Mungu au kwa kutaka faida?
Je, ningefanya hivi hata k**a hakuna anayejua?
K**a majibu yako yanaonyesha amani na utii → inawezekana ni ufunuo
K**a yanaonyesha presha na matarajio → huenda ni msukumo wa nje

23/03/2026

Mtu wa Mungu, adui mara nyingi 1. Anatumia dhambi ulizowai zitenda awali, 2. Asili au tabia wazazi na familia 3. Maisha ya ukuaji katika umri mdogo mfano shuleni, na yanadhihirika kupitia Ndoto, anatumia haya kukurudisha nyuma, kukufanya ufanye dhambi na nk, hakikisha unasimamia msimamo kuwa wewe ni kiumbe kipya ndani ya Kristo na umewekwa wakfu kwaajili ya kumtumikia Mungu.
Mungu akubariki sana

20/03/2026

UNAJIANDAAJE NA UNYAKUO

1. Tubu na uokoke
Tambua dhambi zako na uziache.
Mwamini Yesu Kristo k**a Bwana na Mwokozi wako.
(Soma: Yohana 3:16, Matendo 2:38)

2. Ishi maisha matakatifu
Epuka dhambi kwa makusudi.
Fuata mapenzi ya Mungu kila siku.
(Waebrania 12:14 – “tafuteni utakatifu…”)

3. Soma na kufuata Neno la Mungu
Soma Biblia kila siku.
Tii mafundisho yake.
Neno linakusaidia kubaki kwenye njia sahihi.

4. Omba bila kukoma
Kuwa na maombi ya kila siku.
Omba nguvu ya kushinda majaribu.
Dumisha uhusiano wa karibu na Mungu.

5. Kuwa macho na tayari kila wakati
Yesu alisema arudi ghafla (Mathayo 24:42–44).
Usiahirishe toba au kubadilika.

6. Penda na kusamehe wengine
Upendo ni alama ya Mkristo wa kweli.
Samehe k**a Mungu anavyokusamehe.

7. Shiriki katika ibada na ushirika
Nenda kanisani.
Jifunze na kukua pamoja na wengine kiroho.
Kwa ufupi:

Kujiandaa si tukio la siku moja—ni maisha ya kila siku ya kumfuata Mungu kwa uaminifu.

20/03/2026

Usikate tamaa kwa sababu ya mazingira magumu unayopitia sasa.
Usikae chini na kujihurumia kwa kutazama hali ngumu zinazokuzunguka.
Kumbuka: Baada ya mazingira haya magumu, kuna mazingira mazuri mbele yako ambayo Bwana amekuandalia.
SONGA MBELE KWA JINA LA BWANA MUNGU WA MAJESHI — WEWE NI SHUJAA!

"Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho."
Yeremia 29:11

20/03/2026

TAMAA

Iwe ni Tamaa ya fedha, zinaa, nafasi

Ukianza kuiona tamaa ndani yako ; hiyo ni ishara ya mambo ya mambo yafuatayo

1. Ni shambulio la kiroho ( it is an attack)

Mathayo 4:3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.

Ukiiona tamaa, ni k**a unashindwa kujizuia kabisa, ukimuona huyo binti, unakosa nguvu, ukimwona huyo kijana nguvu za kujizuia zinaishi, ujue umeshambuliwa; unaona kupenda fedha kusiko kawaida, ujue umeshambuliwa

2. Ni ishara kwamba mwili unakuendesha, roho yako haina nguvu

Wagalatia 5:16-17 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. [17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

Na hii ni ishara mbaya sana; Biblia inasema

Warumi 8:13 kwa maana k**a tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali k**a mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.

3. Ni ishara kwamba Kuna uharibifu au anguko liko mlangoni, liko tayari kukupata

2 Petro 1:4 Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.

Kila aina ya uharibifu ulioko duniani, uko ni kwasababu ya uwepo wa tamaa ; ukiiona tamaa ndani yako, ujue anguko lako limeiva

Unahitaji, ufunuo wa Neno la Mungu, Imani kwenye Neno la Mungu, Maombi ya mwendelezo, Maombi ya mifungo na Nidhamu kwenye kufanya kwako, unahitaji umakini wa rohoni, ili kuwa mbali na hili

God bless you

Pastor Ibrahim Amasi

19/03/2026
16/03/2026

USIKATE TAMAA

Wakati mwingine maisha huleta majaribu makubwa hadi moyo unahisi umechoka na tumaini linaonekana kupotea. Lakini kumbuka: Mungu hajakuacha.

Neno la Mungu linasema katika kitabu cha Isaya 41:10:
“Usiogope, maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia.”

K**a umefika mahali pa kukata tamaa, fahamu kwamba Mungu bado ana mpango mzuri juu ya maisha yako. Maumivu ya leo si mwisho wa hadithi yako. Mungu anaweza kubadilisha hali yako ghafla.

Zaburi 34:18 inatukumbusha kwamba Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.

Wiki hii chagua kufanya mambo haya matatu:
1. Muombe Mungu kila siku, hata k**a ni kwa maneno machache.
2. Soma Neno la Mungu ili moyo wako upate nguvu.
3. Kumbuka kuwa kila jaribu lina mwisho.

Usikate tamaa. Mungu bado anafanya kazi katika maisha yako. Tumaini lako halijapotea.

Pastor Diallo Andrew

13/03/2026

MAADUI WATANO NILIAMUA KUSHINDANA NAO HATA KUFA.
1. Tamaa ya mwili
2. Tamaa ya macho
3. Kiburi cha uzima
4. Umaskini
5. Ujinga ( Ukosefu wa maarifa )

Ukikubali mwili ukutawale, utamkosea Mungu na kuanguka dhambini, Pambana na madhaifu yako ya mwilini kila inapoitwa leo.

Usikubali tamaa ya macho ikuongoze, kataa kusikiliza na kuangalia Picha chafu, movie chafu, matendo machafu, nyimbo chafu kwani unachokisikiliza na kuangalia kunaujaza moyo wako ambao ni hekalu lako takatifu na kukutana na Mungu wako.

Nyenyekea, shinda majivuno, shinda kiburi, shinda uasi, kataa kuinuliwa, Siku zote tamani Yesu peke yake ainuliwe na kutambukika. Kiburi cha uzima kinapeleka watumishi wengi kuzimu, Kinaondoa majina ya watakatifu wengi kwenye kitabu cha uzima kwani siku zote Mungu huwapinga wenye kiburi na kuwapa neema wanyenyekevu wa Moyo.

Umaskini ni rafiki wa karibu wa machafu yote ya dunia hii, na ndio silaha ambayo shetani anaitumia kuwaondoa watu kanisani na kwenda kujiuza, kuabudu miungu mingine, kukata tamaa ya maisha na kujiua, Umaskini ni mbaya kuliko hata shetani mwenyewe.

Dhahabu na fedha ni mali ya baba yako aliye mbinguni, Amka mapema, jifunze, ishi kwa kanuni Fanya kazi, Fanya kazi kwa bidii, toa fungu la kumi, weka akiba, wekeza, zalisha, Endeleza kazi ya Mungu duniani, ihubiri injili ya Kristo bila kuchanganya na matatizo yako binafsi, Pay no attetion to the devil, preach & teach lile neno la Mungu lisilogoshiwa.

Neno la Mungu linasema "watu wangu wanaangamizwa KWA KUKOSA MAARIFA" Eneo lolote ulilopo, eneo la wito wako, eneo unalotaka kuona mpenyo, usitumie nguvu nyingi, Anza kujifunza, Soma vitabu, sikiliza mafundisho, tafuta mentor, wekeza ujinga ukutoke kichwani na kwa hakika utakuwa ISHARA NA MAAJABU Ndani ya familia yako na zaidi sana ndani kizazi hiki.

God bless you !!
Sauti ya Mungu
Emmanuel Mrema
12/03/2026

06/03/2026

Nimesukumwa tuu nikuulize.
1.Eti umewahi fikiria hapo Kanisani unapo abudu Umeme unanunuliwa na nani?
Siku mojamoja omba namba ya mita nunua.

2.Umewahi kujiuliza vyombo vikipata shida nani anaingiaga gharama za kutengeneza?

3.Umewahi jiuliza yule kijana mfanya usafi yule binti mfanya usafi kila ukienda chooni unakuta kusafi unajisaidia unatoka,umewahi guswa kufanya chochote kwaajili yake?
Umewahi jiuliza analipwa na nani na kwanini isiwe wewe ufanye usafi.

4.Umewahi jiuliza mchungaji wako huyo ambaye hafanyi biashara hafanyi kazi anaishije?
Anakuombea usiku na mchana huachi kumpigia simu akuombee na hachoki kwaajili yako.

Umewahi waza anaishije?
Utasema anakula sadaka k**a wengi mnavyopenda kuongea,Je! Umewahi toa sadaka ya kumuwezesha kuishi na kuvaa k**a unavyoona anavaa.
Kwanini usiwe wewe muhudumia mchungaji wako.
Kuhakikisha kila mwezi unampelekea chochote nyumbani.
Najua utasema huwa mnamtegemeza kila baada ya miezi mitatu.
Ni kweli huwa mnafanya tegemezo la kumtosha hiyo miezi mitatu? K**a sio basi anza kumuhudumia mchungaji wako.

Siku moja moja ukiwa kwenye nyama choma ikumbuke nyumba ya mchungaji kwa kilo ya nyama,Sikukuu ikumbuke nyumba ya mchungaji.
Fanya wewe binafsi usingoje wito wa wamama na wababa.

Kuna baraka kutajwa jina kwenye maombi ya mchungaji wako,akisema kumbuka mwanangu fulani anavyonitunza mimi mchungaji wake lazima mbingu zijibu.

5.Umewahi waza kubadirisha zile pazia,zile Mic zinazochoka,Ile madhabahu iliyokaa kikiwa wakati mtoto wa Mungu upo tena Mungu amekubariki.

6.Umewahi waza hata siku moja kupeleka uniform za watoto kwa mchungaji wako?

Hagai 1:4" Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao,iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?"

Anza sasa,fanya sasa Roho Mtakatifu amekukumbusha leo.

05/03/2026

🧊MOYO WA MUOMBAJI.
💧kuna vitu k**a viwili kwenye moyo wa Muombaji

1.BIDII - kusoma Neno, kuomba, MIFUNGO, kutafuta mafundisho, kumjua MUNGU na kuliishi Neno (UTII).

2.UVUMILIVU - unyenyekevu, Upole ,kutafakari neno, kutafakari na MUNGU hapa ndipo unapata maelekezo kwenye uvumilivu.

BIDII INAENDA NA UVUMILIVU
Naongelea.👎
💧Moyo wako kukupeleka kwa Mungu na unajikuta una Omba. Na si mdomo wako..
Ufahamu wako ukikosa unachokisema. Umekosa kupata unachokisema. Mpka pale ambapo moyo wako (Ufahamu). Unajua unachokisema.
Mithali 23:7
7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

🤔Yaani maombi yako haya badilishi kitu mpka moyo wako uone sawa na unacho kiomba..
💧Maombi yako yanahitaji sana ufahamu wako. Yaani Maneno yako ni mawazo yaliyo pewa sauti. Hapo umehusiana na maombi yako..
💧Moyo wako ndio Madhabau yako ya Maombi. Usipoenda mbali kwenye moyo wako Huwezi kwenda mbali na MAOMBI yako. Moyo wako ndio utakao amua maisha yako ya MAOMBI. Kwa kuulinda .

Mithali 4:23
23. Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

💧Ndio Maana Mungu anauchunguza sana moyo wako kuliko kitu kingine Chochote.
Yeremia 17:9
9. Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

10. Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.
💧MAOMBI yako yasipo husiana na moyo wako huwezi. Pata kitu mpka pale ukawa na Moyo wa MAOMBI. YESU Anawambia wanafunzi wake.
Mathayo 5:8
8. Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.
💧Moja ya kitu kinacho fanya moyo kuwa safi ni MOYO WA MUOMBAJI. Ndo maan usipo kua na Kujua Neno la Mungu. Utakosa kua na MOYO WA MAOMBI.
Yaani usipokua na MOYO SAFI HUWEZI KUMUONA MUNGU.
🩸MTU MWENYE MOYO WA MAOMBI ANAUWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, UKIONA UNAPATA SHIDA KWENYE KUSHINDA DHAMBI NA UNAOMBA. ANGALIA VIZURI MOYO WAKO..

Br. SAIMON MDESSA

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno la Kristo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your place of worship to be the top-listed Place Of Worship?

Share