26/07/2026
Sikukuu ya Idara ya Uinjilisti – Kanisa la Moravian Zanzibar 🙏❤️
Leo tumeshiriki kwa furaha Ibada ya Sikukuu ya Idara ya Uinjilisti ya Kanisa la Moravian Zanzibar. Ibada iliongozwa na Mchungaji Onesmo Kasyama, huku Neno la Mungu likihubiriwa na Mama Mchungaji Japhet Mtafya, Mwenyekiti wa Eneo la Misheni Zanzibar, Mama yetu Chanda Ngwenya.
Mgeni rasmi wa maadhimisho haya alikuwa Ndugu Edgar Teacher, Mkurugenzi wa Tanzania Mwangaza, ambaye alituunga mkono na kushiriki nasi katika siku hii ya pekee.
Pia tulibahatika kutembelewa na Dada Bettina Nasgowitz kutoka HMH, jambo lililoongeza baraka na ushirika katika maadhimisho yetu.
Ujumbe mkuu wa siku ulitukumbusha kumtegemea Mungu pekee, kumwamini kwa moyo wote, na kutoweka tumaini letu kwa mwanadamu.
«"Amebarikiwa mtu yule anayemtumaini BWANA, ambaye tumaini lake ni BWANA." — Yeremia 17:7»
Tunamshukuru Mungu kwa siku hii yenye baraka, ushirika na mafundisho yenye kujenga imani. Mungu aendelee kuibariki Idara ya Uinjilisti, Kanisa la Moravian Zanzibar, na kila anayejitoa katika kuieneza Injili ya Kristo.