17/01/2026
PONGEZI ZA DHATI
Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kufanikisha Sinodi ya Kanisa la Moravian Tanzania – Jimbo la Mashariki. Tunawapongeza kwa dhati Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, na Katibu Mkuu wa Halmashauri Kuu ya Jimbo kwa kuchaguliwa kuwaongoza waumini kwa kipindi cha miaka minne ijayo.
Tunawaombea hekima, unyenyekevu na uongozi unaompendeza Mungu katika kulijenga Kanisa lake.
“Mkamtegemee Bwana kwa mioyo yenu yote…” (Mithali 3:5)