21/08/2026
Hitaji la kiroho ndani ya mtu hujibiwa kupitia ujumbe kutoka kwa Mungu, unaopitishwa kupitia mtumishi wake k**a chombo cha Mungu. Ingawa Neno linalotolewa ni moja, linaweza kufanya kazi tofauti kwa kila mtu kulingana na hitaji, hali na msimu wa maisha yake. Mungu hutumia Neno lile lile kumgusa, kumfundisha, kumtia nguvu na kumjibu kila mtu kwa namna inayolingana na uhitaji wake.
“Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu...” — Waebrania 4:12
“Ndivyo litakavyokuwa neno langu litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure...” — Isaya 55:11
“Alituma neno lake, akawaponya, akawaokoa na uharibifu wao.” — Zaburi 107:20