Shiloh International Ministries Tanzania/Tanga Branch

Shiloh International Ministries Tanzania/Tanga Branch Kujifunza neno la Mungu na kumtangaza Yesu kwa mataifa yote

05/02/2018

MSINGI WA MAISHA YA MKRISTO NI NENO LA MUNGU

Msingi wa maisha ya mkristo ni neno la Mungu . Hauwezi ukasema umeokoka na unampenda Yesu ikiwa unasoma neno la Mungu kila jumapili na mama unasoma gazeti tena kwa mazoea . Ili uweze kukua katika kumjua Mungu (kukua kiroho) si kwa kwenda kanisani, si kwa kuwa na namba za watumishi mbalimbali si kujua kuombea na watu wanaanguka mapepo si kufanya au kuona miujiza mingi la hasha utaweza kukua kiroho k**a utasoma neno la Mungu, utalitafakari na kuliingiza ktk matendo. Mfano unaumwa na mauti imekuzunguka unaweza ukatumia andiko hili "SITAKUFA BALI NITAISHI "ukawa unalikiri mpaka linajengeka katika nafsi yako na mauti inauachia.

Ishi ndani ya neno la Mungu maana vitu vyote vitapita, fedha, magari, nyumba, miujiza na vingine vyote lakini neno la Mungu kamwe litabaki milele.

Mathayo 4:4
Yohana 10:35
1Koritho 1:18
Waefeso 6:17
Wakolosai 3:16
Waebrania 4:12 , 13:7

Ubarikiwe.

Mungu anazo njia(miujiza) mingi/nyingi za kukutunza usitegemee muujiza(njia) mmoja. Njia (muujiza) aliokutunza nao mwaka...
27/01/2018

Mungu anazo njia(miujiza) mingi/nyingi za kukutunza usitegemee muujiza(njia) mmoja. Njia (muujiza) aliokutunza nao mwaka jana ukategemea unaweza ukaendelee nao mwaka huu. Nabii Eliya alituzwa na kunguru kwa kulishwa mchana na usiku ila muda (majira) wa muujiza ulipoisha Mungu alimuinua mjane wa sarepta kumtunza, 1 Wafalme 17
Ondoa hofu kwa ajili ya jambo lililokuwa linakusapoti likaisha Mungu anainua mtu mwingine kwa ajili yako.
Pokea !

Karibu uvuke mwaka KinabiiPiga kwa maelezo zaidi 0782911515 0756450674Kutoka 14:13Musa akawaambia watu, Msiogope, simame...
21/12/2017

Karibu uvuke mwaka Kinabii
Piga kwa maelezo zaidi
0782911515
0756450674

Kutoka 14:13
Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.

Karibu uje uuone wokovu wa Bwana.

Yeremia 17:7Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.Kwahiyo kuna baraka  nyingine zipo  k...
17/12/2017

Yeremia 17:7
Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA,
Ambaye BWANA ni tumaini lake.

Kwahiyo kuna baraka nyingine zipo kwa wewe kumtegemea Bwana mfano: watoto wanataka fedha ya ada wewe unayofedha kidogo au huna kabisa, umejaribu kutafuta mahali umekosa unaamua kumwambia Bwana wewe ndio unajua ninachojua wanangu wataenda shule na watapokelewa, na unapowapeleka shule wanapokelewa bila tatizo huku ukiendelea kutafuta fedha taratibu
Anaposema "Bwana ni tumaini lake" maana yake kuna mahali utapita ,utakata tamaa lakini yeye atakutia moyo, atakufariji na kukuvusha kwenye hilo jaribu.

Jiulize Umemuweka nani tegemeo lako? Je ni akili zako, nguvu zako, fedha, biashara, kazi, mke/mume, watoto au chochote kile unachokiona bila hicho hauwezi kufika/kupata unachikitaka? ulishawahi kujiuliza k**a hivyo vyote utavikosa nini utafanya?

Badilika sasa mfanye Mungu kuwa wa kwanza na tumaini yeye katika maisha yako naye atakushindia.

Usiwe mwepesi kukata tamaa.Kila siku uione ni yenye Baraka na mafanikio kwako. Yeremia 29:11
13/12/2017

Usiwe mwepesi kukata tamaa.
Kila siku uione ni yenye Baraka na mafanikio kwako.

Yeremia 29:11

When your weak allow the Lord to be your strength.
08/12/2017

When your weak allow the Lord to be your strength.

UMUHIMU WA KUVUKA MWAKA KATIKA UWEPO WA BWANASehemu ya pili.Kwanini adui anavuruga majira na wakati badala ya kuvuruga K...
06/12/2017

UMUHIMU WA KUVUKA MWAKA KATIKA UWEPO WA BWANA

Sehemu ya pili.

Kwanini adui anavuruga majira na wakati badala ya kuvuruga Kusudi ni kwasababu Muda unapofungwa (unapovuruga) unashindwa kufanya mambo yako kwa wakati na unaishi nje ya kusudi la Mungu. Ukisoma katika Daniel 1:1-14. Utaona Mungu alimjibu Daniel toka siku ya kwanza lakini kutokana na Adui kuzuia kuleta majibu kwa wakati ilimlazimu aendelee kuomba tu.

Ndio maana upo Umuhimu wa kuvuka mwaka katika uwepo wa Mungu kwa maana unapovuka chini ya uwepo wake, moja unaweka AGANO na Mungu kupitia neno la Mwaka mzima ambalo Mtumishi anakuwa anapewa kutembea yeye pamoja na familia ya watoto wa kanisa hilo na kuwaongoza kimaombi hao watakaovuka pamoja naye.

Pili, unamkabidhi Mungu muda, siku na wiki zako zote Tangu January hadi December ili hata adui anapokuja kuharibu muda wako anakutana na AGANO uliloweka na Mungu.

Na faida za agano ni kwamba Mungu atakujibu sawasawa na agano mliloliweka na si nje ya agano, kwasababu upo utofauti kati ya Baraka zilizopo ndani ya agano na nje agano. Fahamu unapokuwa ndani ya agano hata k**a Mungu hataki kukujibu Agano litamlazimisha tu akujibu. Mwanzo 15, Mwanzo 17,Kutoka 2:24

Mungu akupe nafasi ya kuhudhuria kuvuka mwaka katika uwepo wake.

Kuna watu wapo k**a daraja kazi yao ni kuhakikisha wanawavukisha watu, usiumie unapoona kila anayepita mikononi mwako an...
25/11/2017

Kuna watu wapo k**a daraja kazi yao ni kuhakikisha wanawavukisha watu, usiumie unapoona kila anayepita mikononi mwako anafanikiwa na hakuumbuki.

Inawezaka hicho ni kipimo chako cha uaminifu katika kuwavusha na ndio baraka zako zilipo wanapofanikiwa wao. Wasipokukumbuka fahamu kuwa wao hawana package yako , package yako iko kwa aliyewataka uwavushe.

Kumbuka jambo lolote unalolifanya usifanye huku ukiangalia kurudishiwa fadhila na unayemfanyia Bali Fanya k**a sadaka kwa Bwana.

Neno la Mungu ni chakula cha roho yako, jinsi unavyolisoma na kulitafakari ndivyo unavyozidi kuishibisha roho yako. Imea...
29/10/2017

Neno la Mungu ni chakula cha roho yako, jinsi unavyolisoma na kulitafakari ndivyo unavyozidi kuishibisha roho yako.

Imeandiwa katika Wakolosai 3:16"Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu."

Soma neno la Mungu, litafakari neno la Mungu na ishi ndani ya neno la Mungu, utamuona Mungu katika maisha yako maana NENO LA MUNGU NI MUNGU MWENYEWE. Yohana 1:1

Ubarikiwe.

Waefeso 6:1-3 imeandikwa "Enyi watoto, WATIINI wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. WAHESHIMU BABA yako na MA...
20/10/2017

Waefeso 6:1-3 imeandikwa "Enyi watoto, WATIINI wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. WAHESHIMU BABA yako na MAMA yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye AHADI Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia"

Kuna sehemu ya maisha, mafanikio na umri mrefu kwa mtoto ikiwa utakuwa na UTII, HESHIMA kwa wazazi wako. Wapo watu wengi mambo yao hayaendi vizuri umesoma haupati kazi, magonjwa hayakuishi, familia yako haina amani na unajitahidi kufanya kila kitu ila hakuna kitu kinachoendelea, hakuna amani kabisa.

Mwanangu jichunguze uhusiano na wazazi/ mlezi wako ulikuaje? K**a ulikuwa ni mbaya rudi kwa magoti kaombe MSAMAHA ili BARAKA hizo ziambatane na wewe.

19/10/2017

Tabia ya Mungu ni upendo,
Yoh 3:16
Ukiongozwa na upendo hautoweza kujihesabia haki na kujiona wewe ni bora zaidi ya mwingine, hautoweza kukaa na kinyogo na kuhesabu makosa ya rafiki, ndugu, jamaa au mfanyakazi wako kwasababu Mungu ni Mungu mwenye rehema na sisi tunamkosea yeye kila saa zaburi 130:3-4
Sisi ni mwili mmoja na tunakamilishwa na mwili wa Kristo pamoja na Upendo wake, Hivyo jifunze kuongozwa na upendo wa Mungu katika maisha yako ili tabia ya ki-
Mungu ijenge ndani na iwe Katika maisha yako

Usikatishwe tamaa na mtu aliyeiba wazo (idea) yako katika jambo lolote, ukumbuke Musa alitengeneza nyoka na waganga wa f...
25/09/2017

Usikatishwe tamaa na mtu aliyeiba wazo (idea) yako katika jambo lolote, ukumbuke Musa alitengeneza nyoka na waganga wa farao wakatengeneza kwa njia ile aliyotengeneza Musa (kutumia fimbo na kuitupa chini soma Kutoka 7:8-13) ila nyoka wa Musa alikuwa na nguvu kuliko nyoka wa farao kwasababu wazo (idea) Ya kutengeneza nyoka hawakuinzisha wao bali waliiga na kutaka kujionyesha wanaweza mwisho wa siku walimezwa na nyoka wa Musa.

Watakachoweza kuiba ni wazo (idea) ila hawatajua maarifa na nguvu iliyo upande wako. Kwahiyo songa mbele hata k**a kutakuwa na biashara kumi zinazofanana ila jua ulichokianzisha wewe haikuwa wazo (idea) ya kwako bali ni Roho Mtakatifu ndio alikupa Wazo hilo .

Jumatatu njema yenye baraka na mafanikio.

Address

Pongwe City Near By MSD
Tanga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shiloh International Ministries Tanzania/Tanga Branch posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share