Chapeo Ya Wokovu

Chapeo Ya Wokovu Karibu mafundisho ya NENO la Mungu ukue KIROHO. Jiunge na channel yetu ya WhatsApp=>>https://whatsapp.com/channel/0029VbCp7ho4SpkEtKlTHK2I

08/05/2026

UKIANZA KUISHI K**A MUNGU ANAVYOTAKA UTAANZA KUWASHANGAZA WATU WANAOKUJUA

Mt 13:54-55 SUV
[54] Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? [55] Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?

Badiliko la mtu la ndani linaanza pale anapomwamini Yesu Kristo, pale anapoanza kuliishi neno la Mungu, anaanza kuwa mtu wa tofauti kwenye ulimwengu huu.

Kuna maeneo watu walimjua mtu alivyo, wengine alikua nao, wengine alisoma nao, wengine ni ndugu zake, anapoanza kutembea katika kusudi la Mungu anakuwa mtu tofauti kabisa na wa kushangaza watu.

Utakuwa shahidi wa hili, kuna watu uliwazoea kwa namna fulani kutokana na vile unawafahamu siku nyingi, ila baadaye wanakuwa watu wenye utofauti mkubwa na kujitenga kabisa na maisha fulani.

Utofauti wa mtu unaletwa na Mungu mwenyewe, anapoanza kutembea na kuongozwa na Mungu katika maisha yake, anakuwa mtu wa tofauti kabisa.

Huwezi ukawa umeokoka, umejazwa na Roho Mtakatifu, umejaa neno, na maombi, ukawa mtu yule yule.

Utaanza kuleta sintofahamu kwa watu wako wa karibu, watu wanaokujua wewe ni mtoto wa fulani, utofauti huo unakuja baada ya Mungu kukubadilisha.

Tegemea kukutana na badiliko la kweli katika maisha yako baada ya kumpokea Yesu Kristo, baada ya kujazwa Roho Mtakatifu, na baada ya kujaa neno la Mungu.

Hutabaki k**a ulivyo, na unajiona upo k**a ulivyo, yaani huoni tofauti kabla ya kuokoka na baada ya kuokoka, basi jitafakari upya uone kipi kimepungua kwako.

Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana

04/05/2026

Nguvu Ya Neno La Mungu || Rebecca Samson

28/04/2026

Omba bila kukoma

27/04/2026

MJARIBU SHETANI HAMWOGOPI MWOMBAJI MZURI

Mt 4:3 SUV

[3] Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.

Yesu akiwa kwenye maombi ya siku 40 ya kufunga, alikutana na mjaribu shetani. Tukio ambalo linatupa mshangao na kushtuka kidogo, maana tulitegemea mtu akiwa kwenye maombi mazito namna hiyo asingeweza kusogelewa na Shetani.

Nataka ujifunze jambo hapa, hasa ukiwa mwombaji mzuri, baadhi hufikiri shetani hawezi kutusogelea na kutujaribu wakati tupo kwenye maombi makali.

Ukiwa mwombaji Sana, utakutana na mjaribu, tena wakati ambao upo karibu sana Mungu wako.

Kukutana na mjaribu shetani haimaanishi kuna mahali umekosea mbele za Mungu.

Mjaribu anakuja kwako ili umkosee Mungu wako, na si kana kwamba umekosea ndio maana amekusogelea.

Tunapata funzo kubwa sana hapa kuwa tunapaswa kujaa neno la Mungu, ndipo tutaweza kukabiliana na mjaribu.

Mt 4:4 SUV

[4] Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

Mtu asiye na neno la Mungu la kutosha, anaweza akaingia kwenye mtego wa mjaribu, na akiwa kwenye maombi yake.

Nasema hivyo kwa sababu sio ajabu ukamkuta mwombaji amenasa kwenye mtego wa dhambi.

Narudia shetani haogopi waombaji k**a unavyofikiri, anaogopa mwombaji mwenye neno, ambaye hawezi kumdanganya na kumwingiza kwenye mitego yake miovu.

Mjue Mungu unayemwomba na kumwamini kupitia neno lake, ili ajapo mjaribu asiweze kukutoa kwenye mstari wa ki-Mungu.

Soma neno ukue kiroho

Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari

Mungu akubariki sana

27/04/2026

Vita si yako

Soma neno ukue kiroho
27/04/2026

Soma neno ukue kiroho

Usimsikilize 📌
18/04/2026

Usimsikilize 📌

10/04/2026

MUNGU AMEAZIMIA KUFANYA JAMBO JEMA KWAKO

Zek 8:15 SUV
[15] vivyo hivyo nimeazimia katika siku hizi kuutendea Yerusalemu mema, na nyumba ya Yuda pia; msiogope.

Kila mmoja anahitaji kufanyiwa jambo jema na Mungu, jambo la kuonekana kwenye maisha yake, awe na jambo la kujivunia ukuu wa Mungu.

Ikiwa Yerusalemu uliazimiwa na Mungu kutendewa mambo mema, inatupa kuelewa kuwa Mungu anatuwazia mema wanadamu au watoto wake.

Mungu anaweza kuazimia kutenda jambo jema kwetu, ila lipo sharti la kutenda hilo jema, tunatendewa bure ila lazima tufuate vile Mungu anataka tuishi.

Mungu anatutaka tuwe watu wa kweli, watu wa haki, watu wasiowaza mabaya juu ya watu wengine, watu waaminifu mbele zake, ndipo tutaweza kuona matendo makubwa ya ki-Mungu kwetu.

Zek 8:16-17 SUV
[16] Haya ndiyo mtakayoyatenda; kila mtu na aseme kweli na jirani yake; hukumuni kweli na hukumu ya amani malangoni mwenu; [17] wala mtu wa kwenu asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala msipende kiapo cha uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema BWANA.

Ukitenda yaliyo machukizo mbele za Mungu, alafu ukataka Mungu atende mambo mema kwako, unaweza kupishana na hizo baraka.

Mungu ataka atubariki tukiwa ndani yake, tukiishi maisha anayoyataka tuishi au aliyotuamuru tuyaishi, ametupa mwongozo mzuri kupitia neno lake.

Kuna baraka tutazipata tukiwa ndani ya Yesu, zingine tutazipata tukiishi maisha yanayompendeza Mungu, na kujiweka mbali na yaliyo machukizo mbele zake.

Ahadi za Mungu ni za kweli, sio hivyo tu, Mungu yupo wazi, ukitaka kumwona akihusika moja kwa moja kwako unahitaji kukaa katika njia yake. Ili kesho ukifanikiwa usiseme nguvu zako, akili zako, na uwezo wako wa kifedha umekusaidia.

Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana

Ukidharau mwanzo mdogo hata ule mkubwa unaoutaka unaweza usiufikie, ilikuwa safari ya siku tatu kusoma na kutafakari kit...
26/03/2026

Ukidharau mwanzo mdogo hata ule mkubwa unaoutaka unaweza usiufikie, ilikuwa safari ya siku tatu kusoma na kutafakari kitabu cha Habakuki, leo tunahitimisha safari hii, na kesho tunaanza safari mpya ya kusoma na kutafakari kitabu kingine cha Sefania.

25/03/2026

Zaburi 7
15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!

16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.

24/03/2026

‼️Usidharau hatua hizi tunazoenda nazo za usomaji wa biblia na kutafakari, hatua hizi zinatufanya tuweke moyoni neno la Mungu, na zinatufanya tuisome biblia yote katika maisha yetu yote bila shida yeyote.
Leo tunaanza kitabu cha Habakuki, jana tumehitimisha kitabu cha Nahumu.

Address

Pembe
Singida

Opening Hours

Monday 09:00 - 18:00
Tuesday 09:00 - 18:00
Wednesday 09:00 - 18:00
Thursday 09:00 - 18:00
Friday 09:00 - 18:00
Saturday 09:00 - 18:00
Sunday 00:30 - 18:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chapeo Ya Wokovu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Chapeo Ya Wokovu:

Share