Efatha Church Same.

Efatha Church Same. EFATHA CHURCH SAME
🌏

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 27 TAREHE 27.5.2026 EFATHA SAMEMAOMBI: Wafilipi 4 6 1.Muombe Mungu huduma yako ikawe ...
27/05/2026

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 27 TAREHE 27.5.2026 EFATHA SAME

MAOMBI: Wafilipi 4 6

1.Muombe Mungu huduma yako ikawe ushuhuda na barua ya kusomeka vyema mbele za Mungu; uwe kivuitie kwa wengi kumjua Yesu bila hata kuwashuhudia.

2. Mwambie Mungu asante kwa ile milango iliyofunguliwa kwangu ndani ya mwezi huu na ile anayo endelea kuifungua kwako.

3. Shuhulikia Roho ya bahari(marine spirit) ni roho za majini mapepo wabaya ... Unakuta mtu ameokoka ila haoi aolewi na kaoa au kuolewa ndoa inasumbua au kuvunjika , kazi, uchumi, biashara vinayumba na huelewi chanzo, mwingine ana mume au mke wa kiroho kwahiyo damu na nyama kila kitu kwake kinakwama na aelewi tatizo lilipo usipo jua ni roho ipi inakutesa utateseka sana haribu roho za bahari majini mahaba , wanaume na wanawake wa kipepo wanaokujia kuharibu ibada yako na Mungu kuua ustawi n.k

4. Shuhulikia kila mfumo wa kishetani uliowekwa kati yako na Mungu unao ua ibada ya ndani na mfumo wa kuabudu kati yako na Mungu

5. Tapika, tema, ondoa kila mahali walipo weka sumu zao juu yako sumu za kichawi , kipepi, sumu za nyoka n.k kuua mamlaka au hatma yako, nguvu ya Mungu kwako

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 26 TAREHE 26.5.2026 EFATHA CHURCH SAME.MAOMBI1. 1 Wafalme 2:3-4Leo ni siku ya familia...
26/05/2026

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 26 TAREHE 26.5.2026 EFATHA CHURCH SAME.

MAOMBI
1. 1 Wafalme 2:3-4
Leo ni siku ya familia Muombe Mungu familia yako ya sasa na ile utakayo kuwa nayo(uzao, mke,mume), wamche Mungu na kumtumikia ili yeye awakumbuke siku zote na kuwa kwaajili yenu

2. Yeremia 29:13
Muombe Mungu akupe kiu ya ibada ndani yako na kumtafuta yeye. Kwamaana Bwana anatafuta wamuabuduo.,, yaani Muombe Mungu aweke akili yake kwako ili uweze kumtafuta usiku na mchana pasipo kukoma na kumuabudu katika roho na kweli.

3. Muombe Mungu atoe ile ibada yako ya nje (ibada ya kidunia), inayokufanya utamani kuonekana na wanadamu wakuone una abudu; hivyo azuie na kuondoa ile dhambi inayokuzuia kufanya ibada ya Mungu yenye utukufu wake.

4. Isaya 57 18 Mwambie Bwana leo rejesha ile faraja niliyo ikosa, niliyo ipoteza kwangu, kwa familia, uzao n.k wewe ndiye unayejua faraja ipi haipo hapo mkumbushe msihi Mungu umesema utarejeza hiyo faraja kwangu na kwa wanaonilili wapo watu wanaumia kwa kile napitia rejesha Bwana.

5. Isaya 57 19 Bwana Mungu wangu na Baba yangu umesema nawe utaniponya , naomba uniponye majeraha ya ndani niliyo nayo ya toka nazaliwa niliyopitia mpaka kufika hapa nipe kuponyeka ili haya yanayo ninyima amani yaniondoke naruhusu kuponyeka kwangu sawa na Neno lako.

6. Fukuza kila uadui uliyowekwa katikati yako wewe na ile ibada yako na Mungu.

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 25 TAREHE 25.5.2026 EFATHA CHURCH SAME.MAOMBIIsaya 57 18  Nimeziona njia zake; nami n...
26/05/2026

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 25 TAREHE 25.5.2026 EFATHA CHURCH SAME.

MAOMBI

Isaya 57 18
Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia.

Isaya 57 19
Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema BWANA; nami nitamponya.

1. Mwambie Baba nashukuru kwa kuniona huu mfungo na kwanzia sasa nitaongozwa na wewe.

NOTE: Mambo hayawezi kwenda kwako k**a huna faraja ile Amani ikiondoka kwako basi tumaini nalo haliwezi baki kwani Faraja inakupa kutumaini upya na hapo Amani inakaa unaanza kuona uponyaji, ustawi, imani inajaa ynaona kuna kwenda mbele, hivyo lazima uishi maisha marefu maana tumaini lipo na unaye mtumaini ndiye anaye ruhusu faraja.

Mtu akiondokewa na faraja nini hutokea?
Maumivu
Uchungu
Magonjwa yasiyotibika haraka
Huzuni na unyonge, unakosa changamko kwahiyo ni lazima kupoteza kila ufanyacho hata uhai wako.

2. Mwambie Bwana leo rejesha ile faraja niliyo ikosa, niliyo ipoteza kwangu, kwa familia, uzao n.k wewe ndiye unayejua faraja ipi haipo hapo mkumbushe msihi Mungu umesema utarejeza hiyo faraja kwangu na kwa wanaonilili wapo watu wanaumia kwa kile napitia rejesha Bwana.

3. Bwana Mungu wangu na Baba yangu umesema nawe utaniponya , naomba uniponye majeraha ya ndani niliyo nayo ya toka nazaliwa niliyopitia mpaka kufika hapa nipe kuponyeka ili haya yanayo ninyima amani yaniondoke naruhusu kuponyeka kwangu sawa na Neno lako.

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

IBADA YA JUMAPILI 24/5/2026 KANISA LA EFATHA SAMEMATUKIO MBALI MBALI KWENYE IBADAMsomee jirani yako ZABURI 23:1 Zaburi 2...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI 24/5/2026 KANISA LA EFATHA SAME

MATUKIO MBALI MBALI KWENYE IBADA

Msomee jirani yako ZABURI 23:1 Zaburi 23 1
BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
Sasa MUULIZE jirani yako k**a BWANA ndiye mchungaji wako kwanini umepungukiwa?

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

UKIRI1. Kwakuwa Bwana wa Mabwana ni Bwana wangu yeye ameondoa ile nira iliyokuwa inanitesa imevunjwa na kuondolewa , kwa...
24/05/2026

UKIRI
1. Kwakuwa Bwana wa Mabwana ni Bwana wangu yeye ameondoa ile nira iliyokuwa inanitesa imevunjwa na kuondolewa , kwanzia leo hakuna Nira yoyote mabegani mwangu mimi fulani niko huru.

2. Kila kifungo kilichokuwa kimenifunga nakutangazia umepasuliwa, vifungo vya laana, magonjwa, kurithi, vya kipepo, kichawi , mizimu havipo tena kwangu kwani NENO LAKE limenihakikishia amenifungua kwanzia sasa niko huru kwa jina la Yesu

3. Natangaza hakuna wageni watakao nitumikisha tena kwanzia sasa, kila adui , mchawi mapepo yaliyokuwa yakinitumikisha hayatarudi tena, nakutangazia wewe ugonjwa, umaskini hutonitumikisha tena , Bwana amesema juu yangu wageni hawatanitumikisha tena.

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 24/5/2026 KANISA LA EFATHA SAMESOMO: TEMBEA NA UKIRI WA NGUVU MPAKA UNAONA MAMBO YAMETOKEA Nidh...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 24/5/2026 KANISA LA EFATHA SAME

SOMO: TEMBEA NA UKIRI WA NGUVU MPAKA UNAONA MAMBO YAMETOKEA

Nidhamu ya ibada ni pamoja na kufuata utaratibu wa ibada, udhiirisho wa Roho Mtakatifu ni pale unapo pangilia utaratibu wa kanisa, familia, utumishi wako mbele za Mungu.

Unapofanya mambo kwa utaratibu mzuri unaruhusu mbingu kutenda kazi na wewe, kamwe usifanye kazi ya Mungu kwa kulipua hutoona nguvu za Roho Mtakatifu kwako. Kwani Yesu anafurahia mpangilio unao mfanya akutazame kwa furaha.

Maandalizi unayo fanya kwenye huduma yako, familia, wito na kufanya mambo kwa utaratibu na mpangilio mbingu huruhusu Roho wake kukushika mkono. Kwanini unafanya kazi ya Mungu bila mpangilio? Chochotw unacho fanya bila kufuata itifaki hakitakuletea matokea mema hakina utukufu... Iwe kwenye ndoa yako, Elimu, wito fanya mambo kwa utaratibu.

Mfano umepewa dhamana ya kuongoza ibada je unaiongoza kwa utaratibu ili Roho afurike juu yako wengine waponyeke na kumuona MUNGU katika hiyo ibada.

Chochote chenye utaratibu mzuri linavutia wengine na Mungu hatokuacha fanya mambo kwa ubora mwana wa Mungu.

Tabia yako tunaiona kwa vile unavyo tenda je unatenda kwa ubora au juu juu, kamwe usipuuzie kazi ya Mungu.

Mungu akikuona unashangaza wengine anakufungua vifungo YEYE MWENYEWE

Yeremia 30 8
Na itakuwa katika siku ile, asema BWANA wa majeshi, nitaivunja nira yake itoke shingoni mwako, nami nitavipasua vifungo vyako; wala wageni hawatamtumikisha tena;

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 24/5/2026 KANISA LA EFATHA SAMEMATUKIO KATIKA PICHA, IBADA NI KUMUABUDU MUNGUYohana 4 23  Lakin...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 24/5/2026 KANISA LA EFATHA SAME

MATUKIO KATIKA PICHA, IBADA NI KUMUABUDU MUNGU

Yohana 4 23
Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu k**a hao wamwabudu.

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 22 TAREHE 22.5.2026MAOMBITENZI 551.Yeremia 31 17  Tena liko tumaini kwa siku zako za ...
22/05/2026

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 22 TAREHE 22.5.2026

MAOMBI
TENZI 55
1.Yeremia 31 17
Tena liko tumaini kwa siku zako za mwisho, asema BWANA; na watoto wako watarejea hata mpaka wao wenyewe.

Mwambie Mungu nirejeze pale napo takiwa kuwepo penye mpaka wangu, mimi na uzao wangu nisaidie Bwana turejeze tutoe ambapo atutakiwi kuwepo.

2. Yeremia 31 18
Hakika nimemsikia Efraimu, akijililia hivi, Umeniadhibu, nami nikaadhibika, k**a ndama asiyeizoelea nira; unigeuze, nami nitageuzwa; kwa maana wewe u BWANA, Mungu wangu.

Mwambie Bwana Yesu nigeuze nami nitageuka, maana wewe ndiwe uliye nichagua mimi, mimi ni mtumishi wako nigeuze kwako Bwana.

3.Yeremia 31:19-20
(19)Hakika baada ya kugeuzwa kwangu, nalitubu; na baada ya kufundishwa kwangu, nalijipiga pajani; nalitahayarika, naam, nalifadhaika, kwa sababu naliichukua aibu ya ujana wangu(20)............

Bwana , chochote nachopitia chenye Aibu, naomba Rehema zako ili kiondoke kwangu, ajalishi hii Aibu imesababishwa na dhambi yangu, au maovu ya wengine naomba rehema zako nitoke ktk maisha ya aibu(jambo lolote la kushindwa, linalokufadhaisha, kukuumiza, lililokinyume chako ni aibu), umeahidi utanirehemu.

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

Mwana Wa Mungu Ruhusi vitu vitoke ndani yako ili vipya viingie kataa kubaki hapo ulipo, ifanye mbingu ijivunie maombi ya...
21/05/2026

Mwana Wa Mungu Ruhusi vitu vitoke ndani yako ili vipya viingie kataa kubaki hapo ulipo, ifanye mbingu ijivunie maombi yako, uwepo wako.

Kile unacho kitangaza kiende sambamba na unachowaza na ukiishi hivyo, k**a unaamini Mungu anaweza kukuinua basi anza wewe kuinuka k**a ulikuwa hufanyi biashara anzisha kitu cha kufanya ili akuinulie apo, km ulikuwa humtolei Yeye inuka anza kumtolea ili abariki zaidi kazi ya Mikono yako.

Wengi hawaoni majibu sababu imani yako inakinzana na matendo yako. Unamtumikia Mungu lakini huuoni mkono wake sababu na yeye haoni mkono wako kwake . Jichunguze wapi unakwama.

1. Ombi; Mwambie Mungu , nashukuru umeikuza ahadi yako kwangu kuliko jina lako nisaidie kutembea vile ambavyo nitakutana na ahadi yako.

2.Nipe kunyooka mbele zako ili nikutane na wema wa Bwana nijalie kuwa muaminifu , mtii na kujitoa.

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

Kwanini mambo hayatokei ni sababu unatangaza ukubwa wa matatizo yako na sio ukuu wa Mungu na uwezo wake juu ya changamot...
21/05/2026

Kwanini mambo hayatokei ni sababu unatangaza ukubwa wa matatizo yako na sio ukuu wa Mungu na uwezo wake juu ya changamoto zako,,, utaona mtu anasema Maumivu nayo pitia Mungu ndio anajua teali amekuza ukubwa wa tatizo na sio Mungu anayeweza tatua tatizo.

ZABURI 138:2
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, Nitalishukuru jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako, Kwa maana umeikuza ahadi yako, Kuliko jina lako lote.

Yeye Mungu kaikuza ahadi yake kuliko jina lake ni kiasi gani anakupenda anakuheshimu, anakuwazia mema sasa kwanini wewe unakuza magumu yako, maadui zako kuliko jina la Mungu wako?

UKIRI
Yaambie matatizo yako niache maana Bwana ana nguvu, lazima nimtumikie yeye, nakustopisha wewe shida flani huna nguvu juu yangu kwani YESU kaniponya,mimi ni mshindi, sitakufa masikini

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 21 TAREHE 21.5.2026 EFATHA SAMESOMO: NENO LA MUNGU LINANGUVU JUU YA MAOMBI YAKO.YEREM...
21/05/2026

IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA 21 TAREHE 21.5.2026 EFATHA SAME

SOMO: NENO LA MUNGU LINANGUVU JUU YA MAOMBI YAKO.

YEREMIA 31: 12 -13
Nao watakuja, na kuimba katika mlima Sayuni, wataukimbilia wema wa BWANA, nafaka, na divai, na mafuta, na wachanga wa kondoo na wa ng’ombe; na roho zao zitakuwa k**a bustani iliyotiwa maji; wala hawatahuzunika tena kabisa........

Mungu anasema anatuwazia mema. Ni mpango wa Mungu wewe ufurahi, na kuuona wema wa Bwana
Unapo pitia huzuni , Maumivu, kukosa changamko kaa chini Tafakari usiwe na haraka kuomba chochote Tafakari wema wake kwenye maisha yako, angalia yale mazuri Mungu kayafanya kwako hata k**a ni jambo dogo sana alafu mwambie BABA nina hili na hili najua wewe unaweza kwani unaniwazia mema unanipenda

Wakati mwingine ukiwa unapitia gumu na hali ya sintofahamu ktk maisha yako, chukua biblia unapo kutana na neno linaloongelea Wema wa Mungu juu yako, ahadi ya Mungu juu yako ndio wakati unatakakiwa kuongea kinyume na hali unayo pitia na kuutangaza wema wa Mungu juu yako.

©️MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

Address

Same Saba Saba
Same
301

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Same. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share