24/08/2026
IBADA YA JUMAPILI KANISA LA EFATHA SAME 23/8/2026
SOMO: UNA NINI MKONONI
Hapa duniani hakuna kitu ambacho Mungu hajampa mtu.
Kila mtu anacho kitu kwaajili ya Mungu na maisha yetu hapa duniani
mfano, yule mwanamke aliulizwa una nini akajibu ana chupa ya mafuta.
mfano 2;YESU aliwauliza wanafunzi wake wana nini mkononi wakajibu mikate miwili na samaki.
NDIPO SASA TUNAULIZWA TUNA NINI MKONONI?
-Kuna wapiga vyombo
-waimbaji
-waombaji
-wanao jitoa kwa kazi ya kuujenga ufalme wa Mungu kwa njia mbali mbali.
Hicho ulicho nacho lazima kisaidie wengine, SWALI linakuja wewe una nini unachofanya kimeinua watu? Mfani Malkia Esther yeye alicho nacho kilikuwa kukomboa taifa zima alitumia hekima mpaka mambo kukaa vizuri.
Uthamani wako upo katiks kupanda, uthamani wa kile ulicho nacho wewe, hakuna kitu utafanya ambacho Mungu amekupa na ukafanya kazi usipate kitu.
Naongelea wewe unafanya nini hapa kanisani na kwa watu?
1 Petro 2 5
Ninyi nanyi, k**a mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.
Mimi ni dhabihu kamili, na neno lasema huwapa mema wampendao kwa sababu hiyo kila aliyekuwepo duniani Mungu amemkusudia awepo.
2 Timotheo 3 17
ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
Utakuwa kamili hapo utakapo fanya hicho ulichopewa.
Unapohubiri injili ya kristo mweleze mtu habari za Yesu sio habari ingine.
1 kolosai 1;29
©️MTUMISHI WA MUNGU TOGOLANI MJEMA