14/03/2023
*KESHA LA ASUBUHI 2023*
JUMANNE, MACHI 14
*MUUMBAJI WA MBINGU NA NCHI.*
Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumba ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru.
— Warumi 1:20
✒️ "Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisaria aliyeitwa Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima." Japokuwa Kornelio alikuwa Mrumi, alikuwa amemfahamu Mungu wa kweli, na alikuwa ameachana na ibada ya sanamu. Alikuwa mtiifu kwa mapenzi ya Mungu, na alimwabudu kwa moyo mkunjufu. Hakuwa ameungana na Wayahudi, lakini aliifahamu na kuitii sheria ya maadili. Hakuwa ametahiriwa, wala kushiriki katika kutoa dhabifu ya kafara; kwa hiyo alihesabiwa na Wayahudi kuwa najisi. Yeye, hata hivyo, alidumisha asili ya Kiyahudi kwa kutoa sadaka za ukarimu, alijulikana pote kwa matendo yake ya hisani na ukarimu. Maisha yake ya uadilifu yalimfanya kuwa na sifa nzuri, miongoni mwa Wayahudi na Wamataifa.
✒️ Kornelio hakuwa na imani yenye ufahamu katika Kristo, ingawaje aliuamini unabii, na alikuwa akimtazamia Masihi aje. Kupitia kwa upendo na utiifu wake kwa Mungu, alivutwa karibu na Yeye, na alikuwa tayari kumpokea Mwokozi wakati atakapofunuliwa kwake. Hukumu huja kwa kuikataa nuru iliyotolewa. Yule akida alikuwa mtu wa familia adilifu, na alikuwa na cheo cha uaminifu na heshima kubwa; lakini hali hizi hazikuwa na mwelekeo wa kupindua sifa adilifu za tabia yake. Wema wa kweli na ukuu viliungana kumfanya kuwa mtu mwadilifu. Mvuto wake ulikuwa wa manufaa kwa wote ambao alikutana nao.
🔘 Alimwamini Mungu mmoja, Muumba wa Mbingu na Nchi. Alimheshimu, alikubali mamlaka Yake, na kutafuta ushauri Kwake katika shughuli zote za maisha yake. Alikuwa mwaminifu katika kazi zake za nyumbani na pia katika majukumu yake ya kiofisi, na alikuwa amesimamisha madhabahu ya Mungu katika familia yake. Hakuthubutu kutekeleza