30/04/2026
SOMO: ANGUKO LA KANISA
Msingi wa Biblia: Ufunuo 2–3, Mathayo 24:4–13, 2 Timotheo 4:3–4
Utangulizi
Kanisa ni mwili wa Kristo (Waefeso 1:22–23), lakini Biblia inaonyesha wazi kuwa kanisa linaweza kuanguka kiroho hata k**a lina majengo, waumini wengi na shughuli nyingi.
Yesu mwenyewe alionya makanisa saba ya Asia Ndogo juu ya hatari ya anguko.
1. Maana ya Anguko la Kanisa
Anguko la kanisa si kufungwa kwa jengo, bali ni:
Kupoteza Nguvu ya Mungu,
Kukosa radha ya ibada, upendo kupungua sana na ibada za maigizo au (sanaa madhabahuni) kanisani (Ufunuo 2:4)
Kuacha kweli ya Neno la Mungu
Kuongozwa na mapokeo, tamaa na dunia na kutotambua nafasi ya Roho mtakatifu ndani ya kanisa .
👉 Kanisa linaweza kuonekana hai, lakini mbele za Mungu likawa limekufa ibada mufu (Ufunuo 3:1).
2. Sababu Kuu za Anguko la Kanisa
(a) Kuacha Neno la Mungu
“Watajiepusha na kuisikiliza kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.”
— 2 Timotheo 4:4
Mahubiri ya kuburudisha badala ya kuonya
Wachungaji kuogopa kupoteza washirika kwa sababu ya maonyo
Mavazi machafu huwezi tofautisha kahaba na alieko kanisani.
Injili ya baraka bila toba
Kuchagua maandiko yanayopendeza masikio
(b) Upendo wa Dunia
“Mtu ye yote akiupenda ulimwengu, kumpenda Baba hakumo ndani yake.”
— 1 Yohana 2:15
Fedha kuwa lengo kuu
Umaarufu kuliko utakatifu
Kanisa kuwa biashara