ZGA Mwanza

ZGA Mwanza Zion Gospel Assembly Church Tanzania

31/05/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI 31/05/2026

24/05/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI 24/05/2024

17/05/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI 17/05/2026

10/05/2026

IBADA YA JUMAPILI 10/05/2026

10/05/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI 10/05/2026

Ibada ya jumapili 15/03/2026Muhubiri : Pastor OkwalingaNdugu ameliasa kanisa ya kwamba Yesu anakuja kuchukua kanisa lisi...
21/03/2026

Ibada ya jumapili 15/03/2026
Muhubiri : Pastor Okwalinga

Ndugu ameliasa kanisa ya kwamba Yesu anakuja kuchukua kanisa lisilokua na madoa wala makunyanzi analisafisha kwa injili yake, Kwa neno lake ambalo ni YESU mwenyewe.
Kuokoka sio mwisho, baada ya kuokoka
tunatakiwa tuendelee kuishi katika injili ili tuendelee kubadilishwa kumfaa Kristo.

Ndugu amelitia moyo kanisa ya kwamba kuna maeneo mengi tunaweza kujaribiwa nayo ili kuonyesha hali ya mioyo yetu na hapo ndipo nguvu ya msalaba inapohitajika kuyafia mambo ili kuendelea kumfaa Kristo.

Ndugu ameendelea kulitia moyo kanisa kuukumbatia ujumbe wa msalaba kwasababu
ndiyo nguvu ya Mungu na haki ya Mungu inatupa changamoto ya kuishi kwa imani kwa kumtegemea yeye peke yake.
Mtume paulo anasema Hasha asione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana Yesu
Kristo.

Mwisho amemaliza kwa kusema sisi k**a waamini tudhamirie moyoni kwamba tusione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Yesu Kristo.

VITABU
1Yohana 2:15 || 2Wakorintho 4:3-11 || Wagalatia 6:14 || Warumi 1:16-17 || Waefeso 5:25 || Waebrania 4:12 || Mathayo 13:44-46 || 1Wakorintho17-18

Ibada ya jumapili : 25/01/26Muhubiri: Pastor Elia TambeMtumishi wa Mungu ametukumbusha kua siku ya mwisho kila mtu atato...
30/01/2026

Ibada ya jumapili : 25/01/26
Muhubiri: Pastor Elia Tambe

Mtumishi wa Mungu ametukumbusha kua siku ya mwisho kila mtu atatoa hesabu ya maisha yake mwenyewe, ametukumbusha ile kiu na shauku tuliyokua nayo kwajili ya Bwana na ule upendo wa kwanza uliokua ndani ya mioyo yetu.

Ndugu aamelitia moyo kanisa tujihadhali tusijekua k**a mafarisayo, kwa nje tunaonekana tunaendelea kumbe tumekwama na k**a tunataka kurudi kwenye unyoofu basi turudi kwenye Unyenyekevu, utiifu, hofu ya Mungu na kuweka maisha yetu chini, na k**a tukitaka kanisa lipate raha basi inatupasa wote turudi katika utaratibu wa kanisa, utaratibu wa Mungu.

Mwisho kabisa ndugu ametusihi ya kwamba sisi k**a wana wa kristo imetupasa tutembee na
tushik**ane k**a kanisa.

Math 22:34-46 || Luk 10:25-28 || Waebrani 10:32-36

IBADA YA JUMAPILI  28/09/2025MUHUBIRI : Mch. Boniphace MkamiNdugu ameongelea juu ya Maisha ya Yesu na vile alivyotenda, ...
28/09/2025

IBADA YA JUMAPILI 28/09/2025
MUHUBIRI : Mch. Boniphace Mkami

Ndugu ameongelea juu ya Maisha ya Yesu na vile alivyotenda, lakini Mungu akitazama duniani anawaona watakatifu na kua mtakatifu maana yake sio kua mkamilifu ila kua na shauku ya kutubu na kumsogelea Mungu kila tunapokosea.

Ndugu ametukumbusha juu ya ufalme wa Mbinguni yakwamba tujiulize k**a nikwęli tunaishi maisha ya kumpendeza Mungu, Ukristo ni kujikana na kubeba msalaba kitu ambacho sio rahisi bila kumsogelea Mungu, pale ambapo utatukanwa unyamaze, udharauliwe ukae kimya kuishi maisha ya ushindi kwaajili ya ufalme na kwamba kilichotushinda wakristo sio kuongea ila kilichotushinda ni kuishi Maisha ya kujikana na kubeba msalaba.

Ndugu amemalizia kwa kusema kuwa dhambi haiokolewi kwa hasira, dhambi inaondoka moyoni mwa mtu pale mtu amepata neema moyoni mwake, maana kila aliekoka ameokolewa kwa Neema.

Luka 2:41-49 || 1 Petro 2:20-23 || Yoh 8:31-35, 48-49

Ibada ya jumpili 14/09/2025mhubiri : Pastor FelixNdugu ameongea juu ya injili ya kweli ambayo inaumba sura ya Mungu ndan...
14/09/2025

Ibada ya jumpili 14/09/2025
mhubiri : Pastor Felix

Ndugu ameongea juu ya injili ya kweli ambayo inaumba sura ya Mungu ndani ya mkristo, na kuleta tabia za Mungu ndani yetu na kwamba hatuwezi mtofautisha Yesu na injili.

Ndugu amelitia moyo kanisa ya kwamba kila mmoja wetu ameitwa kushiriki tabia halisi ya Yesu kristo, k**a Yesu anaishi kwa tabia yake ndani yetu basi sio sisi tunaishi bali kristo aliye ndani yetu.
Ili tuweze kuwashirikisha matunda wengine ni lazima kufata kanuni ya msalaba yani kujikana na tunapokua na tabia za Mungu ndani yetu inaleta uhai hapo ndipo tabia zetu zinakufa.

Ndugu amemalizia kwa kushiriki kwamba mara nyingi tunapofanya mambo kanakwamba nisisi wenyewe mwisho wake ni kuchoka na kukata tamaa, hivyo yapasa kila huduma tunayofanya itokane na roho, sheria haina nguvu ya kuleta mabadiliko.

Address

Mwanza

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ZGA Mwanza posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share