Michael FOJ

Michael FOJ Teaching and Preaching the Demonstrated Gospel of Grace, Truth & Glory with Manifestation of Holy Spirit ( John 1:14,16-17 ).

  KILE NILICHOJARIBIWA NACHOKuna nyakati kwenye maisha Mungu hutaka tujifunze na kuhubiri sio kile tukisikiacho au tukis...
15/08/2026

KILE NILICHOJARIBIWA NACHO

Kuna nyakati kwenye maisha Mungu hutaka tujifunze na kuhubiri sio kile tukisikiacho au tukisomacho tu, Bali kile ambacho tumekiishi au tunakiishi - experienced - ( Ayubu 42:5 ).

Leo ni jumapili, ndugu Mchungaji twende tukahubiri alichotupa "Baba wa mianga" hata k**a unaona Bado hakijatokea kwako wewe hubiri; ndio ! kila MTU ANA MAJIRA YAKE; tambua tu kuwa, Kuna mtu Hilo neno litamsaidia kwa kuwa litakutana na majira yake, yaani leo ndio majira yake ya kukutana na Bwana kwa neno hilo.

Hubiri uzima hata k**a unahisi ugonjwa ndani yako, hubiri kuinuka hata k**a huoni dalili yoyote ya kutoka hapo ulipo, hubiri nasema tena hubiri wakati ukufaao na wakati usio kufaa ( 2 Timotheo 4:2 ).

Mtume Paulo katika barua ya Wagalatia ( 4:14 ) anaonesha kuwa alikuwa katika jaribu la kiafya, lakini katika nyaraka zake, tunaona Mungu akimtumia katika karama , vipawa na madhihirisho mengi ya roho mtakatifu ( 1 Wakorintho 2:1-5 ).

Kuna wakati utapewa neno la faraja wakati wewe mwenyewe una huzuni kuu, Kuna wakati utapewa neno la Imani wakati hofu imetawala moyo wako, ndio Kuna wakati utapewa neno la uponyaji wakati ukiwa hauwezi ( wewe hubiri ).

Kuna nyakati nilifundisha kuwa Mungu anajibu maombi walakini nikiwa na Mimi nasubiri niliyoomba yajibiwe,

Kuna wakati nilifundisha Kusamehe lakini wakati huo na Mimi natamani kuwa na moyo wa msamaha,

Kuna wakati nilifundisha utoaji katikati ya vipindi ambavyo nilipambana na roho mtakatifu mara anioneshapo mahali pa kupeleka hazina yangu,

Kuna nyakati nilihubiri kuhusu maombi lakini Mimi pia nikiwa na struggle ili niwe na maisha ya maombi ( nazikumbuka nyakati hizo ).

Katika mambo yote nimejifunza, kuhubiri ni jambo Moja ila kuhubiri ulichokiishi ni jambo lingine. Na kila mhubiri ni lazima apite kwenye kipimo Cha kupimwa katika Yale anayohubiri.

Waebrania 4 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁵ Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.
¹⁶ Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

____________
Michael FOJ
T.A.G - Valley Of Blessing - BLB
Mwanza, Tanzania.
+255 (0) 757 129 776.

"K**A ULIVYO MKUBWA MTANDAONI, PAMBANA KUWA MKUBWA KANISANI KWAKO"Hii kauli niliisikia Mchungaji mmoja pahala fulani aki...
13/08/2026

"K**A ULIVYO MKUBWA MTANDAONI, PAMBANA KUWA MKUBWA KANISANI KWAKO"

Hii kauli niliisikia Mchungaji mmoja pahala fulani akiwaambia wachungaji wengine ( katika namna ya masimango na majigambo ). Nikakumbuka kauli moja ya Mchungaji X ambaye alikuwa rafiki yangu sana tena sana wapekee miaka kadhaa nyuma.

Mchungaji X aliwahi mtembelea Mchungaji Y kwenye moja ya ibada kanisani; mara baada ya ibada Mchungaji Y akamkaribisha Mchungaji X nyumbani kwake ( kwa upendo tu ).

Mchungaji X alipofika nyumbani kwa Mchungaji Y ( kumbe alikuwa ana agenda ya kuchunguza maisha ya Mchungaju Y ). Alipoondoka tu, akanipigia simu,

Mchungaji X : Hello FOJ,

Mimi : Hello Mkuu, za siku ?

Mchungaji X : Nzuri Aisee..............,
( Akaanza kutafuta namna ya kuleta habari za Mchungaji Y kwangu ) na niliona anavyohangaika...

Mchungaji X : FOJ tusiogope ukubwa wa Jina la mtu mitandaoni aisee...! watu wana maisha ya maigizo sana !

Mimi : Kwa nini mkuu ? ( Nikiwa na mshangao moyo, like why this now ...)

Mchungaji X : Aisee, ndugu yetu Mchungaji Y ana maisha ya kawaida kuliko unavyojua, nimefika kwake hana hata Sofa sebuleni, tulikaa Chini kwenye mkeka ( Huku anaendelea kuleta khabari....)

Mimi : Ooooh ( Nikaanza kuwaza, wakati huo huo moyo uliuma sana....like k**a anaweza mtangaza Mchungaji Y kwangu, basi kuna siku atanitangaza na mimi kwa Mchungaji C, A na B ).... Ndani yangu nikasikia maswali mengi yanazunguka sana....

Mchungaji X : FOJ , kuna hili na hili na hili na hili....,

Mimi : Nikamwambia, ndugu kuanzia leo wewe sio rafiki yangu, nikakata simu ( nikajiambia moyoni , atabaki kuwa Mchungaji mwenzangu ila sio mtu wangu wa karibu tena )

"Tusichunguzane ili kusemana"; Okay anyway turudi pale juu. Kwa umri mdogo nilionao nimejifunza kuwa Maisha , huduma na kila maendeleo aliyonayo mtumishi wa Mungu ni Neema tu; na hauhitaji kushindana na mtu yeyote yule.

Kuna mtumishi mmoja anaitwa Pastor Fred Msungu aliwahi Sema , kuna wachungaji wanajua kufundisha, wenye vipawa hadi ukiwasikia unatamani uwe wao ila hawajapata "Neema" ambazo wengine wanazo; hivyo tuzidi kuwa wanyenyekevu... ( k**a nitakuwa nimekumbuka vyema maneno yake ).

NB : Moja ya mambo ambayo nimekuwa namwomba Mungu atusaidie wachungaji wa kizazi hiki, ni :-

1:- Kutokuwa na mioyo yenye ushindani.
2:- Kutokuwa na mioyo yenye chuki wala kufurahia anguko la mtumishi yeyote.
3:- Kutokuwa na mioyo yenye kutosamehe.
4:- Kuwa na mioyo yenye Nia ya Kristo
( Wafilipi 2:1-10 )
5:- Kuwa na wasaa wa kupambanua na kujitathimini wapi tumetoka, neema tulizoziomba na sasa tumezipata.
6:- Kutotumia mafanikio ya leo k**a fimbo kwa watu wengine ambao bado wana mngoja Bwana awafanikishe.
7:- Kutokusahau AKILI NA NJIA ZA MUNGU ( Isaya 55:7-8 ).

NB : Huduma sio kupambana sana kwa sababu kuna watu wanapambana mno, wala maendeleo sio kupambana tu ni wakati na bahati ambao huwapata wote ( Mhubiri 9:11 ). Hivyo k**a yeye alivyo maarufu mtandaoni na hana matokeo yako, kadhalika wewe ambaye una matokeo na hauna umaarufu mtandaoni alionao yeye ( hivyo tu ).

Utumishi unahitaji kutiana moyo, kuheshimu nafasi na neema juu ya watu ( ukizingatia sio wote watakuwa wakimataifa etc ), utumishi unahitaji kuelimishana kwa upendo bila kujifanya Mungu mwenye kujua kesho za watu hata k**a unahisi hawawezi fika mbali. Tubaki wanyenyekevu, tubaki kusaidiana sana na sio kuhukumiana sisi kwa sisi.


________________
Michael FOJ
T.A.G - Valley Of Blessing - BLB
Mwanza, Tanzania.
+255 (0) 757 129 776.

 "Ukitaka kuwa tajiri kwa haraka sana basi fungua kanisa, utapiga mihela mnoo ", tafuta tu, k**a milioni 10 za kununua v...
12/08/2026



"Ukitaka kuwa tajiri kwa haraka sana basi fungua kanisa, utapiga mihela mnoo ", tafuta tu, k**a milioni 10 za kununua vyombo vya Mziki, alafu kiwanja utakodi ( k**a rahisi vile ), uwe na sauti kubwa kubwa, alafu utaona, yaani baada ya muda tu utakuwa tajiri sana; alisikika mtu mwenye kuongozwa na hisia mgando, asiyejua namna ya kupambanua mambo akisema hizi kauli, as if wachungaji wote ni wachumia tumbo ( 2 Wakoritho 4:2 & Tito 1:7 ) .

Rafiki sio rahisi k**a udhaniavyo, na sio rahisi k**a vile maadui wa kanisa wasemavyo. "Chunga tamaa mbaya" aliimba mmoja wa watunzi wa mashairi wa Tanzania ( Matendo 17:28b ). Ndugu hakuna cha Mungu chenye kupatikana bila mchakato, na hata wale uwaonao kuwa ni matajiri kwa sababu ya "KANISA" hawakuwa matajiri kwa usiku mmoja, wana historia, tena yenye maumivu na subira kuu.

Siku moja nilisema na mtu mmoja kwa sababu ya kauli hii, kuwa ; "msukumo wa ndani huweka kila kitu bayana ni suala la muda tu", kwa sababu mchakato haudanganyi kabisa.

Kwanza kuanza huduma sio tu suala la kuwa na vyombo, sauti kubwa ( in fact hata makondakta wanazo hizo sauti ), sio suala la eneo kwa sababu yapo makanisa yalianza chini ya mti; huduma ni wito mkuu kutoka kwa Boss mkuu , Yesu. Wito huu ndio msukumo wenye kumfanya aliyeitwa aache vyote na azidi kusonga mbele katika misimu yote ya kimchakato ( 2 Timotheo 4:2 ), trust me ! k**a hauna au hujawahi sikia hii sauti ya Boss huwezi toboa kamwe.

Mtume Paulo anasema ;

Matendo ya Mitume 22
⁶ Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote. ⁷ Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi? ⁹ Na wale waliokuwa pamoja nami waliiona ile nuru, lakini hawakuisikia ile sauti ya yule aliyesema nami. ¹⁴ Akasema, Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe upate kujua mapenzi yake, na kumwona yule Mwenye haki, na kuisikia sauti itokayo katika kinywa chake.

NB : Zingatia ! "wale watu waliona nuru Bali hawakuisikia ile sauti". Hii sauti ndio hutufanya kuzidi sana katika kuitenda kazi ya Mungu, wengine huona matokeo ila sio kusikia sauti. Sauti hutupa kusonga mbele hata pale dunia inapokuwa kinyume nasi, hata pale tuliowaamini wanapotutupa ili tuwe kicheko, hata pale tuliowapenda wanapotusema kwa ubaya, hata pale mchana na usiku vinapokuwa sawa kwa kukosa usingizi; hii sauti hutupa nguvu ya kwenda mbele. Hivyo ukiona Mchungaji amefanikiwa, kabla ya kuona mafanikio, jitahidi kurudi na kutazama mchakato kwanza ( Waebrania 13:7 ).

Mimi natamani sana makanisa mengi yafunguliwe, watu wengi wasikie habari za Yesu; ila usije kwenye hii kazi kwa sababu ya msukumo wa kupiga "Mihelaa" , trust me hautakuwa na mwisho mwema, kwa “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”
— 1 Timotheo 6:10 (Biblia Takatifu)


_________________
Rabi Michael Foj
T.A.G - Valley Of Blessing - BLB
Mwanza , Tanzania.
+255 (0) 757 129 776.

BEHIND THE SCENES Siku nilipojua namna movie ya Titanic ilivyotengenezwa ,nilijicheka sana, nikakumbuka miaka ile nilivy...
23/07/2026

BEHIND THE SCENES

Siku nilipojua namna movie ya Titanic ilivyotengenezwa ,nilijicheka sana, nikakumbuka miaka ile nilivyolia wakati Jack amefariki mbele ya macho ya Rose; na nilijicheka namna nilivyoaminishwa na director mahiri James Cameron, nikakumbuka namna niliyohukumu na kujua ile ndio ilikuwa "KWELI", kumbe ulikuwa "UONGO" uliofanywa "UHALISIA" nyuma ya Kamera, nilijifyonya kwa kujihurumia.

Nilijicheka sana, nilijiambia, ooh kumbe hivyo ndivyo ilivyokuwa, kumbe lile halikuwa bahari, wala hakuna aliyezama na kufa kwa barafu ?, Nikatamani utoto wangu unge-jump leo, alafu ningejua namna ya kuitazama ile movie na kuitolea "HUKUMU SAHIHI" bila kuathiriwa na matumizi ya "HISIA" zangu katika "KUTOA HUKUMU" kati "UKWELI NA UONGO".

Sometimes kwenye maisha huwa tunatekewa na uzuri wa mambo tusiojua uhalisia wake nyuma ya pazia, Na kuna wakati tunayapa mambo majina mabaya pia kwa sababu hatujui the scene. Ubaya au Uzuri unaweza"pikwa" kabisa. Ndio ! k**a vile movie nyingine ambavyo hutengenezwa, kadhalika kuna mambo bado yamefichika sana mbele ya macho yetu ( hapa nasema na wenye uwezo wa kusikia na kuona ).

Siku nilipojua kuwa; Kuna wakati ukweli niujuao kumbe ni uongo uliopikwa kwa makusudi ili niamini kuwa ndio kweli; basi ! nilitamani kujua kwa nini uongo nilioaminishwa sio "KWELI", ndio ilikuwa kweli niliyotakiwa kuijua.

“Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake,........”
— 1 Wakorintho 4:5 (Biblia Takatifu)

Nimewaza tu kuhusu


__________________
Michael FOJ
+255 (0) 757 129 776
Mwanza, Tanzania.

22/07/2026
 Moja ya Mbinu za ushindi katika vita ni kuharibu Ghala la silaha za Mpinzani wako; hii hufanyika Kabla ya kumuua au kum...
21/07/2026



Moja ya Mbinu za ushindi katika vita ni kuharibu Ghala la silaha za Mpinzani wako; hii hufanyika Kabla ya kumuua au kumteketeza kabisa adui wako. Na hii imenipa kusema "Mungu ana akili sana; na upumbavu wake una hekima kuliko hekima ya Mwanadamu."

Ni kweli kuwa adui bado anatenda kazi ile ile ya Kuiba, kuchinja na kuharibu ( Yoh. 10:10 ); ingawa, Adui huyu hawezi kufanya lolote kati ya hayo bila kutumia silaha kuu mbili, moja ni uongo na pili ni hofu/uwoga ( Yoh. 8:44 ) ambazo zipo kwenye ghala kuu liitwalo ufahamu hasi.

Imani ni matokeo ya ufahamu wenye taarifa njema zenye kumfunua mwokozi aitwaye Yesu aliyezaliwa, kufa, kufufuka; na hizi taarifa zimelenga kuiharibu kabisa ghala ya silaha la adui. Hizi taarifa hujulikana kwa neno moja tu "Injili".

Injili ni habari njema, habari zenye tumaini kuu, habari zenye kuinua walio chini, habari zenye kufufua matumaini ya mti uliokatwa. Hivyo kila asikiaye hizi habari na kuziamini ni LAZIMA AISHI MILELE.

Ni ajabu kuona kuwa ati watu wengi wasemao wamemwamini Yesu bado wanaishi wakiwa na hofu nyingi kila eneo la maisha yao. Tena hofu yenyewe ni kuwa “kuna siku naweza upoteza wokovu”, kuna siku Mungu atanikataa kwa sababu ya matendo yangu. Kuna siku Mungu atanikana kuwa hakunijua kwa sababu ya tabia zangu. Kuna siku Mungu atasema ondoka kwangu maana ulipomkiri Yesu kuwa ni Bwana na Mwokozi wako ,hukumaanisha ? KUMAANISHA !!!!

Trust me ! Maisha ya kila mwamini yalitakiwa kubadilishwa na nguvu ya upendo wa Mungu pekee, kwa sababu injili ni taarifa zilizobeba tafsiri ya pendo la Mungu. Pendo lenye kustiri wingi wa dhambi ( 1 Petro 4:8 ) , Pendo lenye kumpa mtu bidii katika kutenda mema ( 2 Wakorintho 5:14 ), Pendo lenye kuvumilia yote ( 1 Wakorintho 13:4-8 ), Naam ! Pendo lenye kuamini yote !

Sikia ! Fanya maamuzi leo ya kuharibu ghala la silaha la adui kwa kuruhusu uhalisia wa Injili kupenya ndani ya moyo wako. Ndio , ruhusu injili izame moyoni mwako kwa uhalisia wake hata k**a unaona hai - make sense kwa sasa, kwa sababu injili sio hisia ni ELIMU.

SIKIA NDUGU hata k**a unaona yasemwayo ni magumu kuyaelewa kwa akili ya kibinadamu, bado hiyo ndiyo kweli; kwa kuwa Mungu huwa hafanyi jambo kwa kuwa linaeleweka sana na watu, laah hasha; Injili ndio hiyo, na hiyo ndio silaha pekee yenye kulipua ghala la silaha za adui.

NB:- Mbinu hii ilinipa kuona kuwa hakuna imani nzuri kuliko zote duniani k**a imani iletwayo kwa neno la msalaba.Naam, neno la neema yake, neno la Kristo, Ndio ! habari za tumaini kuu. Na hii imevuka hekima ,akili , ufahamu na amani ya dunia hii.

Kubali leo masamaha ya dhambi ya milele ili uishi katika utimilifu wa Kristo Yesu. “Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.”
— Yohana 1:16 (Biblia Takatifu)



___________________________
Michael FOJ
+255 (0) 757 129 776
MWANZA , TANZANIA .

Address

Mwanza

Telephone

0757 129 776

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Michael FOJ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Michael FOJ:

Shortcuts

Share