Binti wa kiha

Binti wa kiha Karibu! injili, Ushuhuda, Stori & ushauri � # injili.� Binti wa kiha.

Tubu,MWAMINI YESU huu ni wakati wa neema mlango utafugwa na utakosa nafasi..changamka mapema..Evod Medson.
27/08/2026

Tubu,MWAMINI YESU huu ni wakati wa neema mlango utafugwa na utakosa nafasi..changamka mapema..
Evod Medson.

25/08/2026

With Binti wa kiha – I've just made it onto their weekly engagement list by being one of their top engagers!

YESU ndiye aliye waokowa watu hawa nafulaiii kuona bado wana mtumikia MUNGU japo ni mdaa lakini mbingu zime funguka juuu...
25/08/2026

YESU ndiye aliye waokowa watu hawa nafulaiii kuona bado wana mtumikia MUNGU japo ni mdaa lakini mbingu zime funguka juuu yaoo

UKIONA MUNGU NI K**A AMECHELEWA BASI UJUE ANATAKA KUJA KWA UKUBWALeo asubuhi wakati namtafakari Mungu nikajifunza jambo ...
18/08/2026

UKIONA MUNGU NI K**A AMECHELEWA BASI UJUE ANATAKA KUJA KWA UKUBWA

Leo asubuhi wakati namtafakari Mungu nikajifunza jambo kubwa kutoka kwa Mungu.
Mungu huwa anaombwa na huwa halizimishwi kujibu tunavyotaka.

Nikajikumbusha hata katika ofisi za kawaida tunazoenda kuomba kazi huwa kuna vigezo wanatazama na kupitia kabla ya kumpa majibu ya ndio au hapana mtu anapoomba kazi.

Na katika kuangalia vile vigezo k**a uzoefu wa kazi, ujuzi katika kazi husika na mengine mengi basi hufuatia hatua ya pili ya kuwaita watu kwenye usaili(interview) waliokidhi vigezo.

Na katika Usaili huwa vinaangiliwa vitu k**a uwezo wa kujieleza, nini unajua kuhusu kazi unayoomba na mengine mengi. Kupata A kwenye vyeti huwa sio kigezo pekee cha mtu kupatiwa kazi.

Hivyo pamoja na kuomba kazi hiyo, kuitwa kwenye Usaili, kuwa na A kwenye vyeti, uamuzi wa nani apewe hiyo kazi uko mikononi mwa mwajiri.Na hauwezi kumlazimisha eti kwasababu umeomba hiyo kazi lazima uipate wewe.

Unaweza kukosa hiyo nafasi/ kazi either kwasababu ujuzi wako juu ya hiyo kazi ni mdogo, au kazi hiyo ni ndogo kwako wanasubiri siku wakitangaza kazi kubwa wakuchukue.

Lakini wengi wetu kwa bahati mbaya ile kwamba mtu aliwahi kuomba kazi ofisi Fulani akakosa bila kujua sababu ya yeye kukosa anajikuta ameichukia hiyo ofisi, hataki hata kuwasikia na siku ikitangazwa kazi nzuri zaidi mtu anajisemea niliomba ile nikanyimwa , hii ndio siwezi tena kuomba, au anasema yaani ile ofisi tangu waninyime ile kazi sitaki tena kuwasikia wala siwezi kuomba kazi pale.

Kumbe ilikuwepo nafasi nzuri kubwa iliyokuwa reserved kwaajili yake.

NINI NATAKA KUSEMA

Ile kwamba Mungu hajakupa ile kazi uliyomuomba, ile kwamba Mungu hajaruhusu uolewe na huyo kijana, Ile kwamba Mungu hakumponya mgonjwa wako, ile kwamba kuna lolote kubwa ulilomwamini Mungu kwalo kwa imani kubwa sana, ukatoa sadaka kubwa lakini bado Mungu hakujibu k**a wewe ulivyotaka haimanishi kuwa Mungu hakupendi, huna haja ya kujiuliza kuwa labda kuna ulichomkosea.
Pastor Winnie.

Mtu yeyote asiyekubali  kumwamini Yesu  kuwa Bwana na muokozi wa maisha yake hawezi kuona uzima wamilele  mwanadamu  oko...
17/08/2026

Mtu yeyote asiyekubali kumwamini Yesu kuwa Bwana na muokozi wa maisha yake hawezi kuona uzima wamilele mwanadamu okoka acha dhambi Yesu anarudi YOHANA 3:3. YOJANA 3:36 BY PASTOR MUSA KILAMBA

MAISHA NI HADITHI,IANDIKE YAKO VIZURI. Kwa bahati mbaya ni kwamba,hakuna anayeijua siku yake ya kuondoka hapa duniani,na...
11/08/2026

MAISHA NI HADITHI,IANDIKE YAKO VIZURI.

Kwa bahati mbaya ni kwamba,hakuna anayeijua siku yake ya kuondoka hapa duniani,na hakuna anayejua mshale wake wa saa umebaki kuzunguka mara ngapi.

HIVYO

Nikusihi wakati ungali bado uko hai jitahidi kufanya mambo yafuatayo.

Jitahidi sana kuishi maisha ya Utakatifu kila saa na kila wakati wakati uwapo hapa duniani.Ishi maisha yaliyo bora binafsi kuanzia kiroho,
pata muda wako binafsi na Mungu wako,jishugulishe na mambo yatakayokufanya kuwa bora kiroho,ie soma neno,pata muda wa kushiriki ibada,pata muda wa kuongea na kumsikia Mungu,toa sadaka,shiriki matukio ya kiroho mahali unapoabudu.

Jitahidi kufunga,na ukifunga funga kweli yaani maanisha.

*Kimwili* jitahidi kujijali pata muda wako binafsi, pata muda wa kujijali k**a kupumzika,k**a hujafunga kula vizuri kwa kadri ya uwezo wako, jipende vaa vizuri,lala sehemu nzuri samehe watu(hii ni sehemu ya kujijali na kujipenda.

Kwa habari ya *familia* yako fanya chochote unachoweza kilicho ndani ya uwezo wako kwaajili ya familia yako,k**a ni wazazi fanya kitu kizuri kwao kilicho ndani ya uwezo wako,wajulie hali kila mara,watengenezee mazingira mazuri ya wao kufurahia uzazi wao kwako .

Ndugu zako wa damu na hata ndani ya familia be good to them pale unapoweza jitoe kwao kwenye mambo yao ya muhimu

K**a mke au mme jitahidi uwekeze kwa mwenza wako,mtengenezee mazingira bora ambayo hata kesho ukiondoka asihangaike,mpende na mwonyeshe upendo .

Watoto wako vilevile wekeza upendo wa dhati kwao,jitoe kwao wewe pekee ndiye utakayewapenda bila sababu, upendo wa watu wengine huja kwasababu lakini upendo wa mzazi ndiyo ule tunauita upendo wa Agape,usiwekeze kwa watu wa nje ukasahau watoto wako,wapende kwa kuwapa muda,kwa kuwa sikiliza na kuwafanyia vitu vilivyo ndani ya uwezo wako kwaajili ya kuwajenga na kuwafanya kuwa bora .

Siku utakayoondoka kila mtu aweza kukusahau lakini siyo watoto waliotoka kwenye tumbo/viuno vyako

Pastor Winnie

Wewe Unae Soma Post Hii Mungu Akuondolee Mzigo Mzito unao fanya Usiombe Mtumishi wa Mungu Dan Wema.
10/08/2026

Wewe Unae Soma Post Hii Mungu Akuondolee Mzigo Mzito unao fanya Usiombe
Mtumishi wa Mungu Dan Wema.

Wiki Hii Kila Silaha Itakayo Fanyika kinyume Chako Haitafanikiwa Muimbaji wa nyimbo za injili Jenipher Mgendi.
10/08/2026

Wiki Hii Kila Silaha Itakayo Fanyika kinyume Chako Haitafanikiwa
Muimbaji wa nyimbo za injili Jenipher Mgendi.

Usitoe tumaini lako hapo ulipoliweka,, ukiwa umemtumaini  Yesu Kristo pekee,  basi amini uko katika mikono salama  , end...
10/08/2026

Usitoe tumaini lako hapo ulipoliweka,, ukiwa umemtumaini Yesu Kristo pekee, basi amini uko katika mikono salama , endelea kumtazama na kukiishi kile alichokiweka ndani yako , hata k**a majira na nyakati haziruhusu , zisikufanye uache kumtazama na kumtumaini , endelea tu kwa kuwa kuna wakati na nyakati za utimilifu wa kile unachokiona , kuwa na -IMANI- ya kuona kana kwamba imeshakuwako. Nayo itakuwa / itatimia kwa majira yake. SHALOM.....
Prophet Happy.

Address

Njombe
Mwanza
59100

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Binti wa kiha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share