Kainos Creation Church - Felician Makarios Ministries

Kainos Creation Church - Felician Makarios Ministries Kainos Creation Church is a Church Ministry. Our Vision is to train believers in the work of the ministry in an atmosphere of love, fellowship, faith and power.

We equip believers with the Word to the intent that the same is grounded and able to teach

04/09/2026

Nainuka asubuhi kwa furaha; nikiwa nimejaa shukrani kwa zawadi ya siku nyingine tena kufanya kazi na Baba! Natembea katika siku yangu na ujasiri nikijua siko peke yangu na haniachi kwa sababu yeyote ile. Nakabiri changamoto za siku kwa imani na kamwe siruhusu zizime furaha yangu ya milele: kujua kua nina Baba aliyenipenda upeo na kunisamehe kabla sijakosea! Hakuna nafasi ya hatia wala hukumu nafsini, na hivi ndivyo navyoweza kuishi nikipenda wengine, nikisamehe na kutenda katika “potential” zilizo ndani yangu! Kuchoka kuko mbali nami!

Kainos Creation

03/09/2026
03/09/2026

Wokovu ni wito! Umeokolewa kutoka utumwa wa dhambi kuja kumtumikia Mungu. Usisubiri wito maalumu kutumika na Mungu. Fact kwamba umeokolewa ndio umeshaitwa hivyo. Huwezi kutenganisha uanafunzi wa Kristo na huduma. K**a haupo hudumani; ina maana moja tu - unaishi katika kutokutii, si mwanafunzi mzuri wa Kristo! Unafanya nini katika kanisa lako la mahali? Amka!

Kainos Creation

Shalom!Nakusalimu kwa jina la Yesu. Mchugaji kiongozi wa makanisa ya Kainos Creation Church (KCC) Anakukaribisha katika ...
30/08/2026

Shalom!
Nakusalimu kwa jina la Yesu.
Mchugaji kiongozi wa makanisa ya Kainos Creation Church (KCC) Anakukaribisha katika "SAA YA UPONYAJI"

Yoyote mwenye shauku ya kupokea uponyaji wake au ndugu yake anaruhusiwa kuhudhuria kipindi hiki.

Njoo na matarajio ya kupokea kutoka kwa Bwana.

Muda: Saa 3:00 usiku
💻 Mahali: Online kupitia Google Meet
*Jiunge kupitia*
Link 🔗: https://meet.google.com/vbc-ztam-nnd

Ni miaka miwili sasa tumekuwa tunakusanyika na kufanya kambi ya waamini. Na Pastor Chris Segun Onayinka Baba yetu akiten...
29/08/2026

Ni miaka miwili sasa tumekuwa tunakusanyika na kufanya kambi ya waamini.

Na Pastor Chris Segun Onayinka Baba yetu akitenga muda mahususi kabisa kuja Tanzania. (East Africa).

Mwaka huu tena kambi inafanyika Dodoma.

Karibu tukutane wote Dodoma!

Itakuwa ni muda mzuri kujifunza, kuomba, kufanyia mazoezi tulichojifunza, kuwavuna wengi kwa Yesu na Yesu atatukuzwa!

Jiandikishe sasa!!

24/08/2026

WAAMINI WALIOANGUKA KATIKA NEEMA

Hawa ni waamini walio okolewa kwa neema, kwa kazi ya Kristo, lakini katika mwenendo wao wanatumainia matendo yao. Wakati fulani waliamini juu ya dhabihu ya Kristo kwa ajili ya maisha yao, hata hivyo, njiani umakini wao umehamishwa kutoka kwenye hio kwenda kuamini kazi zao au matendo yao lakini bado haibadilishi chochote kuhusiana na wokovu wao.

Wagalatia 5:1-4 Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa. 2 Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno. 3 Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote. 4 Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.

Neno “kuanguka” limetafsiriwa kutoka kwenye neno la Kigiriki “ekpipto” (to be driven out of one’s course) likimaanisha kuondolewa katika njia yako, kuwa asiye na ufanisi.

Hii sio kupotea kwa wokovu bali kuhamishwa kwenye lengo na umakini wao wa kuiamini kazi ya Kristo pekee kisha kuziamini kazi zao wenyewe.

Ni kwa namna gani wanatolewa katika mwelekeo/njia?

Wagalatia 1:1-9 Paulo, mtume, (si mtume wa wanadamu, wala kutumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo, na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu), 2 na ndugu wote walio pamoja nami, kwa makanisa ya Galatia; 3 Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana wetu Yesu Kristo; 4 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya dhambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu iliyopo sasa, k**a alivyopenda Mungu, Baba yetu. 5 Utukufu una yeye milele na milele, Amina. 6 Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine. 7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo. 8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. 9 K**a tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe.

Mstari 6

”Walimuacha” yeye aliye waita katika neema ya Kristo na kugeukia injili ya namna nyingine

Neno “kuacha” lilitafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “metalithemi” (a turn, a change) likimaanisha hali ya kugeuka, au badiliko.

Neema ya Kristo katika kitabu cha Wagalatia linaongelea Injili au kile Kristo amefanya.

Neno ”nyingine” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “heteros” likimaanisha namna ya tofauti.

Maneno “injili nyingine” inamaanisha ujumbe tofauti au wa aina nyingine. Ina maana walisikia ujumbe tofauti na ule walio upokea.

Mstari wa 7

”…wala si nyingine”
Neno ”nyingine” katika mstari 6, ni neno tofauti na lile limetumika katika mstari wa 7.
Neno “nyingine” lilitafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “allos” likimaanisha iliyo sawa.
Kile walichosikia hakikuwa sawa na Injili. Hii ndio sababu Paulo akawaita ‘wajinga’

“...kuna wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo”

Neno “taabisha” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “tarasso” likimaanisha “kuamsha vurugu, kuleta usumbufu” (to stir, to agitate, to unsettle). Hii ni mwamini kukosa utulivu.

Neno “kuigeuza” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki ”metastrepho”(turn across, to transmute or to corrupt) likimaanisha kugeuza, kubadilisha au kuharibu.

Inamaanisha mwamini anaweza kupoteza ujasiri wake kupitia ujumbe uliogeuzwa, uliobadilishwa, ulioharibiwa au ujumbe tofauti.

Hivyo, Paulo anawaita wasio na akili na waliorogwa kwa sababu walihamisha mlengo wao kutoka katika neema kuendea kazi au matendo ya sheria.

Wagalatia 3:1 Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? 2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? 3 Je! mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?
Ni waumini “wasio na akili” kwa sababu:

• Walianza kwa roho na wakaanza kutafuta kufanywa wakamilifu kwa mwili, yaani kwa matendo ya mwili.
• Walitafuta kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria
• Ni waumini wasio furahia uhuru wao ndani ya Kristo

Wagalatia 2:16-21 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki. 17 Lakini ikiwa sisi wenyewe, kwa kutafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, tulionekana kuwa wenye dhambi, je! Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? Hasha! 18 Maana nikiyajenga tena yale niliyoyabomoa, naonyesha ya kuwa mimi mwenyewe ni mkosaji. 19 Maana mimi kwa njia ya sheria naliifia sheria ili nimwishie Mungu. 20 Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu. 21 Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure.

Mstari 21

“Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure”

Neno “batili” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki ‘”atheteo” lenye maana ‘kuweka kando’ yaani kuweka kando kile kilichokuwa kimetolewa au kimewekwa k**a msingi.

Neno “kubatilisha neema ya Mungu” linamaanisha kuweka kando kwa kujaribu kuhesabiwa haki kwa sheria.

Hii inamaanisha kuwa mwamini ambaye amekwisha hesabiwa haki kwa imani anaweza kutereza kwa kutafuta kuhesabiwa haki kwa matendo.

Maneno “kuanguka kutoka katika neema” na “kuibatilisha neema ya Mungu” k**a yalivyo tumika katika kitabu cha Wagalatia hayaongelei kupotea kwa wokovu.

Basi,

Usitoke nje ya msingi wako wa imani!

Dhabihu ya Yesu inatosha,

Relax

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009

Shalom!Nakusalimu kwa jina la Yesu. Mchugaji kiongozi wa makanisa ya Kainos Creation Church (KCC) Anakukaribisha katika ...
23/08/2026

Shalom!
Nakusalimu kwa jina la Yesu.
Mchugaji kiongozi wa makanisa ya Kainos Creation Church (KCC) Anakukaribisha katika "SAA YA UPONYAJI"

Yoyote mwenye shauku ya kupokea uponyaji wake au ndugu yake anaruhusiwa kuhudhuria kipindi hiki.

Njoo na matarajio ya kupokea kutoka kwa Bwana.

Muda: Saa 3:00 usiku
💻 Mahali: Online kupitia Google Meet
*Jiunge kupitia*
Link 🔗:https://meet.google.com/bcg-qumz-dvj

23/08/2026

DHANA YA DHAMBI K**A ILIVYOFUNDISHWA KATIKA MAANDIKO YA KIEBRANIA YA BIBLIA - 2

Mti Wa Uzima

Mwanzo 2:9 Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya. 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

Musa aliandika kuhusu miti miwili; mti wa uzima na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Musa alidokeza nini kwa ‘mti wa uzima na mti wa ujuzi wa mema na mabaya’?

Kumbuka kwamba Musa alitumia taswira na mifano kueleza ahadi ya Mungu na utofauti wake.

Adamu alipaswa kuchagua kula matunda ya mti wa uzima.

Hii inadokeza kwamba mwanadamu alipaswa kuamini na kupokea ahadi ya Mungu ya uzima.

Hata hivyo, Adamu alionyesha kutoamini ahadi ya Mungu ya uhai. Kwa hiyo, hakutii na kufanya dhambi.

Mwanzo 3:5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa k**a Mungu, mkijua mema na mabaya. 6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. 7 Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo. 8 Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone. 9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi? 10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha. 11 Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale? 12 Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala..

Usemi ‘mti wa uzima’ pia ulirejelewa katika sehemu nyingine za Biblia k**a ifuatavyo.

Mwanzo 2:9 Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Mwanzo 3:22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa k**a mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;

Mwanzo 3:24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.

Mithali 3:18 18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashik**anaye naye.

Mithali 11:30 Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima; Na mwenye hekima huvuta roho za watu.

Mithali 13:12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.

Mithali 15:4 4 Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.

Inaweza kuonwa kwamba neno ‘mti wa uzima’ lilirejelewa k**a taswira.

Kwa hiyo, katika kitabu cha Mwanzo, Musa alirejelea ‘mti wa uzima’ kuwa mfano wa kueleza ahadi ya Mungu ya uzima ambayo Adamu aliikosa, tofauti (contrast) kwa mti wa uzima katika maandishi ya Musa ilikuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Hadi sasa, yafuatayo yametambuliwa;

- Mbingu na nchi ambayo ni umoja (muunganiko) wa Mungu na mwanadamu katika uanadamu mmoja.

- Roho wa Mungu; ambayo pia inaelezea nuru ya Mungu na uzima wa Mungu.

- Mti wa uzima unaoelezea uzima /uhai wa Mungu kwa mwanadamu.

- Sura ya Mungu ambayo inaeleza ahadi ya Mungu, mtu wa Mungu, Adamu wa Mungu

- Starehe ya Mungu ambayo inaeleza ahadi ya Mungu kukaa ndani ya mwanadamu

Kwa hiyo, dhambi (neno la Kiebrania ‘chattah’) ni hasara, upungufu, kutokuwepo na kukosa ahadi ya Mungu; sura ya Mungu; roho ya Mungu; nuru ya Mungu; uzima wa Mungu; pumziko la Mungu.

Kutokuwepo huku ndiko Musa alieleza kwa mwanadamu kuwa ‘giza’, ‘ukiwa tena utupu’ (uharibifu, utupu), ‘mti wa ujuzi wa mema na mabaya’ na ‘mauti’.

Hivyo, Musa alitumia utofautishaji (contrasts) ili kueleza ahadi ya Mungu iliyofafanuliwa katika maneno na shughuli zake na kinyume cha ahadi ya Mungu.

Musa alirejelea maneno haya kwa lugha ya picha ili kufafanua hali ya wanadamu.

Inaonyesha hali ya mauti, uharibifu, kutokuwepo kwa nuru, kutokuwepo kwa roho ya Mungu.

Kiini cha maandishi ya Musa haikuwa tu kuonyesha au kutoa historia, badala yake, alitumia simulizi zinazojulikana za historia kuwasilisha au kufundisha kuhusu ahadi ya Mungu.

Aliandika na kutoa ufafanuzi wa ahadi ya Mungu kwa kutumia mifano, misemo, mafumbo, na viwasilishi vya alama/ishara.

Ikumbukwe pia kwamba Biblia sio kitabu pekee kinachotoa masimulizi ya kihistoria.

Kuna maandishi mengine ya kihistoria ambayo yalikuwepo katika vitabu vingine na ukweli wao wa pekee, matukio, hekaya na historia ingawa yana matukio yanayofanana na yale ya Biblia.

Kwa hivyo sababu ya kuandikwa na Musa kwa ukweli huu wa kihistoria lazima ifafanuliwe.

Mtunga Zaburi alirejelea jinsi Musa alivyoandika;

Zaburi 103:7 Alimjulisha Musa njia zake, Wana wa Israeli matendo yake.

Neno ‘julisha’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘yada’ ambalo linamaanisha ukaribu, kujuana.

Neno ‘njia’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘derek’ ambalo linamaanisha umbali, njia au safari.

Neno ‘derek’ lilitokana na neno la Kiebrania ‘darak’ ni kuelezea kile unacholenga au kupanga kufanya.

Kwa hiyo, maandishi ya Musa yalikuwa na usuli wa kutafakari kwa mbele (kabla ya wakati) ahadi ya Mungu na hivyo alieleza kwa ustadi mambo aliyojua akitumia maneno na mifano (imageries) yake mwenyewe.

Mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Kumbuka kwamba kutokana na mistari iliyo hapo juu, imefafanuliwa kwamba Musa aliandika kuhusu ahadi ya Mungu iliyofafanuliwa k**a sura ya Mungu, roho ya Mungu, nuru na uzima wa Mungu ndani ya mwanadamu.

Kwa hiyo, dhambi ni kutokuwepo na kupoteza ahadi ya Mungu, hali iliyoelezwa k**a giza na mauti.

Kumbuka kwamba kitabu cha Mwanzo ndicho msingi wa maandishi mengine yote ya Musa.

Kwa hiyo, katika kuelewa kitabu cha Mwanzo, kuna haja ya kuelewa matumizi ya neno au maneno ya mwandishi na mpangilio au muundo wake wa kuwasilisha ahadi ya Mungu.

Kumbuka kutoka sehemu iliyotangulia ya kitabu hiki, tulipojifunza kuhusu maandiko, mada zinapaswa kuanzia katika kitabu cha Mwanzo.

Hili litatuleta kutazama mkazo wa kitabu cha Mwanzo kutoka sura ya 1-3 k**a bora na kamilifu ya Mungu (yaani, ahadi yake ya kumleta mwanadamu mahali ambapo mwanadamu amekosa kupafikia (missed the mark).

Swali linalokuja akilini juu ya mada ya dhambi; ni kipi kilicho bora na kamilifu cha Mungu kwa mwanadamu ambacho mwanadamu alikikosa; akaenda kando; akaondoka kutoka kwa hicho na ikaleta dhambi na matokeo yake; mauti, kwa mwanadamu?

Sura Na Mfano Wa Mungu

Mwanzo 1:26-27 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

Kishazi ‘na tum~’ (let is –KJV) katika maneno ‘na tumfanye’ katika Kiebrania cha Kale kilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘asah’ ambalo linaongelea nia, kusudio (an intention).

Kumbuka, neno ‘Mungu’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘elohiym’ linalozungumza juu ya mungu.

Ingawa neno 'sura' lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania 'tselem' ambalo lina maana ya mfanano au uwakilishi wa kile kinachoundwa ili kuwakilisha kingine; mara nyingi hurejelewa kwa uwakilishi wa mtu au kitu.

Ilirejelewa katika kitabu hichohicho na mwandishi yuleyule (Musa) kwa ajili ya Adamu.

Mwanzo 5:3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.

Tazama maandishi ya maandiko ya hapo juu, yameelekeza kwa sura inayotofautiana na sura ya Mungu katika Mwanzo 1:26.

Kwa hiyo, Adamu hakuwa katika mfano wa Mungu.

Sethi alikuwa kiwakilishi kamili cha Adamu na sio sura ya Mungu katika sura ya kwanza.

Hayo hapo juu yanamaanisha mambo mawili:

1. Sura ya Mungu ilikuwa ni ahadi.

2. Sura ya Mungu itakuwa chaguo kwa Adamu (wanadamu) kufanya.

Kumbuka, Neno 'na tum~' linamaanisha nia au kusudio.

Hii ina maana kwamba, Musa anawasilisha nia ya Mungu kwa mwanadamu kwa namna ya ahadi; yaani mwanadamu anapaswa kuwa katika sura na mfano wa Mungu.

Mtu ambaye ni:

- K**a Mungu

- Mmoja na Mungu (katika muungano na Mungu). - Atakayejaza, kutiisha na kutawala.

Swali linalokuja akilini litakuwa: Kwa nini Adamu hakuwa katika sura na mfano wa Mungu?

Mwanzo 1:1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

Maneno ‘Mbingu na nchi’ k**a yalivyofafanuliwa kutoka sehemu zilizotangulia za somo hili yalirejelewa na Musa katika sura ya kwanza na ya pili ya kitabu cha Mwanzo.

Mwanzo 1:2 …Mbingu na chi…

Mwanzo 1:6 …Na liwe anga…

Mwanzo 1:8 …Mungu akaliita lile anga Mbingu…

Mwanzo 1:9 …ili pakavu paonekane; ikawa hivyo…

Mwanzo 2:1 …mbingu na nchi zik**alizika, na jeshi lake lote…

Mwanzo 2:4 …vizazi vya mbingu na nchi…

Angalia marejeo ya ‘Mbingu’ kutoka kwenye Mistari ya 6-8 ilikuwa ni anga-hewa (atmospheric heaven) anga (the sky); na “pakavu” inaashiria nchi.

Ingawa, katika Mwanzo 1:1 maneno ‘mbingu na nchi’ yataeleweka kwa maneno yanayoendelea.

Neno ‘Roho ya Mungu’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘Elohiym Ruach’.

Neno ‘ruach’ linamaanisha upepo; pumzi.

Musa alifundisha vivyo hivyo katika sura ya 3.

Mwanzo 3:8 Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone.

Maneno ‘jua kupunga’ yalitafsiriwa kutoka kwa neno lilelile la Kiebrania ‘ruach’.

Maneno ‘sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga’ ni sawa na ‘roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji’

kwa hiyo, matumizi ya Musa ya visawe hivyo hapo juu yalikuwa ni kumwasilisha Mungu akihusiana na mwanadamu.

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009

22/08/2026

DHANA YA DHAMBI K**A ILIVYOFUNDISHWA KATIKA MAANDIKO YA KIEBRANIA YA BIBLIA - 1

Musa alieleza jinsi Adamu hakuamini neno la Mungu ambalo aliambiwa na hivi ndivyo dhambi iliingia katika shughuli za mwanadamu.

Hii ilionyeshwa k**a kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Hata hivyo, neno ‘dhambi’ lilitumiwa kwa mara ya kwanza kuelezea tendo la mwanadamu katika Mwanzo 4.

Mwanzo 4:7 K**a ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Neno ‘dhambi’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘chattah’ . Muundo wa kitenzi cha neno ‘chattah’ ni neno ‘chata’ linalomaanisha kukosa, hasara, kupungukiwa au kutokuwepo.

Marejeleo ya neno ‘chattah’.

Mwanzo 20:6 Mungu akamwambia katika ndoto, Nami nimejua ya kwamba kwa ukamilifu wa moyo wako umefanya hivi, ndipo nami nikakuzuia usinitendee dhambi, kwa hiyo sikukuacha umguse.

Mwanzo 20:9 Kisha Abimeleki akamwita Ibrahimu, akamwambia, Umetutenda nini? Nimekukosa nini, hata ukaleta juu yangu na juu ya ufalme wangu dhambi kuu? Umenitenda matendo yasiyotendeka.

Mwanzo 31:39 Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea, mimi mwenyewe nimetwaa hasara yake, wewe umekidai katika mkono wangu, ikiwa kilichukuliwa mchana, au ikiwa kilichukuliwa usiku.

Neno ‘hasara’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘chata’ (muundo wa kitenzi cha neno ‘chattah’) ambalo hudokeza ukosefu, au kitu kilichokosekana au kutokuwepo.

Neno ‘chattah’ lilitafsiriwa kuwa ‘dhambi’ katika maandiko yafuatayo;

Mwanzo 18:20 Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha S***ma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,

Mwanzo 31:36 Yakobo akakasirika, akagombana na Labani. Yakobo akajibu, akamwambia Labani, N'nini hatia yangu? Nayo ni nini dhambi yangu, hata ukanifuatia namna hii?

Mwanzo 50:17 Mwambieni Yusufu hivi, Naomba uwaachilie ndugu zako kosa lao na dhambi yao, maana walikutenda mabaya; sasa twakuomba utuachilie kosa la watumwa wa Mungu wa baba yako. Yusufu akalia waliposema naye.

Kutoka 10:17 Basi sasa, nawasihi, nisameheni dhambi yangu mara hii moja tu, mkamwombe Bwana, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki tu.

Mambo ya walawi 4:3 k**a kuhani aliyetiwa mafuta akifanya dhambi, hata analeta hatia juu ya watu; ndipo na atoe kwa ajili ya dhambi yake aliyoifanya, na kumsongeza kwa Bwana ng'ombe mume mchanga mkamilifu, kuwa ni sadaka ya dhambi …23 akijulishwa hiyo dhambi yake aliyoifanya, ataleta mbuzi awe matoleo yake, mume, mkamilifu;

Mambo ya walawi 26:18 Tena ikiwa baada ya hayo hamtaki kunisikiza, ndipo nitawaadhibu zaidi mara saba kwa ajili ya dhambi zenu… 21 Nanyi ikiwa mwaenenda kinyume changu, wala hamtaki kunisikiza; nitaleta mapigo mara saba zaidi juu yenu, k**a dhambi zenu zilivyo.

Hesabu 5:6 Uwaambie wana wa Israeli, Mtu mume au mke atakapofanya dhambi yo yote, ifanywayo na binadamu, kumwasi Bwana, na mtu huyo akawa na hatia;

Hesabu 12:11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi.

Mika 6:13 Basi, kwa ajili ya hayo, mimi nami nimekupiga kwa pigo liumizalo sana; nimekufanya kuwa ukiwa, kwa sababu ya dhambi zako.

Neno ‘chattah’ lilitafsiriwa kuwa ‘adhabu’ katika andiko lifuatalo.

Zakaria 14:19 Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa yote, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda.

Vivyo hivyo tafsiri ya KJV inatafsiri neno hilo k**a adhabu (punishment) katika andiko hili chini japokua tafsiri ya Kiswahili inachagua kubaki na neno “dhambi”.

Lamentations 4:6 For the punishment of the iniquity of the daughter of my people is greater than the punishment of the sin of S***m, that was overthrown as in a moment, and no hands stayed on her. (KJV)

Isaya katika maandiko yake alieleza hali ya dhambi kuwa ‘ugonjwa’ katika maneno yake ili kumaanisha upungufu, yaani, kitu kilichokosekana au kutokuwepo.

Isaya 29:18 Na katika siku hiyo viziwi watasikia maneno ya hicho chuo, na macho ya vipofu yataona katika upofu na katika giza.

Isaya 32:3 Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.

Isaya 35:5 Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. 6 Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka k**a kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba; maana katika nyika maji yatabubujika; na vijito jangwani.?

Isaya 42:7 kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.

Isaya 53:4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. (5) Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona..

Nabii Isaya anahusianisha ugonjwa na hali ya kiroho ya mwanadamu katika dhambi.

Alitaja dhambi kuwa ni uziwi, upofu na giza.

Kwa maneno mengine, dhambi ina maana ya kasoro, kushindwa, upungufu, kutokuwepo au hasara.

Kwa hiyo, alifafanua wokovu kuwa ‘uponyaji’ wa hali ya kiroho ya mwanadamu katika dhambi.

Swali linalokuja kichwani ni hili; Ni nini kilikosekana au kutokuwepo au kupungua?

Acha tuchunguze maandishi ya Musa ili tuone yaliyotukia hapo mwanzo;

Mwanzo 1:1 1Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. 4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza. 5 Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.

Kumbuka kwamba katika Mstari wa 1, kulikuwa na rejea ya maneno ‘mbingu na nchi’.

Mbingu Na Nchi*

Kumbuka kwamba neno 'mwanzo' lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania 'reshiyth' ambalo linamaanisha ‘ya kwanza’, ‘bora’; au ‘iliyo kuu’.

Inarejelewa kwa mpangilio, wakati au cheo (rank).

Neno ‘mbingu’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘shamayim shayem’ ambalo linamaanisha anga.

Linarejelewa kuelezea ambapo maumbo ya angani (celestial bodies) yanazunguka.

Hata hivyo, neno ‘mbingu’ pia lilitumiwa kufafanua makao ya Mungu.

Hii inaweza kuzingatiwa na kuonekana katika maandishi ya Musa.

Mwanzo 28:17 17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha k**a nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. 18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha k**a nguzo, na kumimina mafuta juu yake. 19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu. 20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae; 21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu. 22 Na jiwe hili nililolisimamisha k**a nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.

Musa aliandika kuhusu kukutana kwa Yakobo na Mungu na akaeleza mbinguni kuwa ni nyumba ya Mungu.

Alifafanua zaidi mbinguni k**a mahali ambapo Mungu anakaa.

Kutoka 20:22 Bwana akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli hivi, Ninyi wenyewe mmeona ya kuwa nimenena nanyi kutoka mbinguni.

Kumbukumbu la Torati 4:36 Kutoka mbinguni amekusikizisha sauti yake, ili akufundishe; na juu ya nchi alikuonyesha moto wake mkuu; ukasikia maneno yake toka kati ya moto.

Musa alieleza mbinguni k**a mahali ambapo Mungu alisema kutokea hapo.

Kumbukumbu la Torati 26:15 Uangalie kutoka makazi yako matakatifu mbinguni, uwabarikie watu wako Israeli, na nchi uliyotupa k**a ulivyowaapia baba zetu, nchi imiminikayo maziwa na asali.

Vivyo hivyo, neno ‘nchi’ katika Mwanzo 1:1 lililotafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘erets’ linamaanisha shamba (field), nchi au ardhi.

Angalia jinsi lilivyorejelewa na Musa katika maandishi yake.

Mwanzo 1:26 26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. 29 Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu; 30 na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.

Mwanzo 6:6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. 7 Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya..

Mwanzo 11:1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.
Musa alielezea “nchi” k**a mahali ambapo mwanadamu hukaa, kuchunguza na kuratibu shughuli zake.

Kwa hiyo, matumizi ya neno “nchi” yanaeleza nafasi ya mwanadamu na shughuli zake ndani yake.

Kumbuka kwamba Musa alitumia maneno kufafanua mambo halisi ya kiroho kwa picha ya ahadi ya Mungu.

Maneno ‘mbingu na nchi’ yalirejelewa pamoja na Musa ili kueleza muungano wa Mungu na mwanadamu mahali pamoja (wanadamu).

Musa alizungumza juu ya ahadi ya Mungu ya kukaa ndani ya mwanadamu.

Alifafanua zaidi jambo hili katika Mwanzo 1 mstari wa 2 k**a roho ya Mungu juu ya uso wa maji.

Mwanzo 1:2 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. 4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.

Roho/Uzima/Nuru Ya Mungu

Kumbuka kwamba neno ‘ukiwa’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘tohu’ ambalo linamaanisha utupu, hakuna kitu, au upotevu.

Neno ‘giza’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘choshek’ ambalo linamaanisha kutojulikana, hakuna kitu kinachoonekana.

Linamaanisha ’bila nuru’.

Kishazi ‘uso wa vilindi’ ni sawa na kile Musa alichoeleza kuwa ‘uso wa maji’ katika mstari huo huo.

Neno ‘uso’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘paniym’ ambalo linamaanisha mwonekano (appearance).

Kwa hiyo neno ‘ukiwa tena utupu’ ndilo ambalo Musa alieleza kuwa ‘giza juu ya uso wa vilindi’.

Chunguza kwa karibu kauli zinazofuata;

…Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Mst 3 Mungu akasema, Iwe nuru, ikawa nuru.

Neno ‘roho ya Mungu’ lilitafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania ‘elohiym ruach’.

Neno la Kiebrania ‘ruach’ linamaanisha upepo, hewa au pumzi inayozungumzia uhai.

Hivyo, roho ya Mungu ni uhai (pumzi) ya Mungu.

Musa alielezea utendaji wa Mungu k**a uwepo wa roho ya Mungu juu ya uso wa maji.

Alifafanua zaidi k**a uwepo wa nuru yake.

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009

22/08/2026

Status ni maandalizi ya ibada kesho!
Tunajiandaa na kusanyiko bora kuliko yote duniani! Ni kusanyiko la watakatifu mahali mahali. Kuwepo kanisani kesho ndio iwe excuse ya kutokuwepo pengine popote! Unaweza kushiriki makusanyiko ya KCC mahali pengi Tanzania, nijie inbox kwa maelekezo wapi ndugu wanakusanyika! Usikae nyumbani - twende kanisani.

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009

Kainos Creation

Address

Igoma Nyamagana
Mwanza
33000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kainos Creation Church - Felician Makarios Ministries posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share