Kainos Creation Church - Felician Makarios Ministries

Kainos Creation Church - Felician Makarios Ministries Kainos Creation Church is a Church Ministry. Our Vision is to train believers in the work of the ministry in an atmosphere of love, fellowship, faith and power.

We equip believers with the Word to the intent that the same is grounded and able to teach

03/06/2026

SHERIA, NEEMA NA WAHUBIRI

The fact kwamba anayehubiri Haki Ipatikanayo mbali na matendo (wokovu kwa neema) bado Ana changamoto za kitabia,

Haifuti ukweli kwamba Yesu Alichukua Dhambi juu ya mti ili Waaminio Wahesabiwe Haki BURE KATIKA Yeye!

Injili au Kazi ya Yesu haiko qualified na tabia au Hali ya anayehubiri! K**a bado tuna akili Njema!

Inajitegemea, hata tusipoamini Yeye Hudumu WA kuaminiwa!

Ni ujinga kusema usihubiri Neema mana Watu watatenda Dhambi sana! Khaa!

Kwa hio tuseme uongo!? Kwamba hakufa! Hakufufuka!?

Unafikiri ukiwambia uongo ndiyo wataacha Dhambi?

My friend, kwa Nini kumsaidia Mungu Kazi!? Yeye aliyeanzisha ndiye atakayeimaliza mioyoni mwao!

Wewe unayekemea Dhambi mwenyewe watenda dhambi!

Mbona una uchungu na Watu Kutenda Dhambi kuliko Mtendwa dhambi mwenyewe!

Kweli, Wahubiri wananishangaza! Yeye kasema imekwisha, wewe unasema mh mh not yet! Hawa Watu watakua huru sana!

Ok, amejifunua katika Kristo k**a mwenye neema na rehema milele! Wewe Hapana, bado kuwatisha Watu na ghadhabu ambayo haipo Eti Bila Hivyo watatenda dhambi sana. Real!?

Hebu tufikiri!

Ikiwa Yesu alikufa ili Watu wasitende dhambi,

Basi alikufa BURE, mana bado Watu wanatenda- walio kanisani na ambao hawako kanisani.

Wanaohubiri Haki Ipatikanayo kwa matendo nao wanafanya Dhambi

Ukiwambia aisee bado mnatenda Dhambi na mshahara wake NI mauti wanasema huwa wakitenda Dhambi wanatubu!

Ok! K**a Dhambi inaondolewa na toba, basi Yesu alikufa BURE!

Tungeendelea kuonywa na manabii K**a zamani Kisha tunatubu na kusamehewa!

Haihitaji Mungu, ndiyo, Mungu Kuja duniani kuchukua mwili Kisha kuwafia Watu wake wakati inawezekana tu kuungama na kusamehewa!

Ninyi mnaotegemea matendo yenu na toba- Kristo hawafaidii kitu!

Mmeanguka kutoka kwenye Hali ya neema!

Na Hilo ndio anguko KUU!

Let love lead,

- Kainos Creation


03/06/2026

Maisha ya maombi ya Mwamini au huduma ya maombi ya mwamini lazima ijengwe katika upendo wa Mungu kwa wengine, Inapokua dua/sala au kuomba kwa ajili ya wengine itakua na mguso wa Moyo, uendelevu, pasipo kukoma, usiku na mchana.

Kainos Creation


03/06/2026

Kwa waamini wanao “fall in love” na wenye dhambi!

Wanaojifanya kuwaelewa sana wasioamini!

Upendo wa kipuuzi, upendo usio wa Mungu.

Je, unafikiri wasioamini hawajui wewe ni Mkristo dhaifu?

Unafikiri shetani haoni? Hajui?

Anajua hatampokea Yesu lakini anajua wewe mwenyewe ni mwamini dhaifu, anaanza kukuvuta kwa mapenzi na kujali!

Unaanza kulewa, kwa ujinga unasema; “Lakini yeye ni mtu mzuri. Lakini ananitunza, lakini familia yao ni nzuri.”

Hisia zako zimekuwa mungu wako!

Unaendeshwa na vichocheo vya kimwili na sio Roho wa Mungu’

Kwa nini unataka kuoa au kuolewa?

Yesu hayuko kabisa katika mpango wako?

Unataka kuoa kwa mapenzi yako mwenyewe ya kipuuzi kisha uanze kumwomba mchungaji ushauri (counselling)

Sifanyi ushauri wa kipuuzi.

Ukilivagamia, libebe mwenyewe! Ishi nalo!

Usiseme: “Pastor naomba ufunge pamoja nami”

Niache mimi nipige maziwa fresh, ma oats porridge na mihogo safi!

Beba msalaba wako mwenyewe!

Eeh..

Kuna shirika gani kati ya hekalu na sanamu, nuru na giza, haki na uasi?

Ukiona unavutiwa kimapenzi na wasioamini - cheki tena k**a umeokoa au la!

Ikiwa umeokolewa, tafadhali uwe mwenye hekima!

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009

03/06/2026

Kwa wengi, Yesu hakuja kuwaokoa bali alikuja kuwaonyesha "namna ya kujiokoa" kwa hio wako bize kufuata nyayo zake ili kutimiza "haki yote"

Kainos Creation


02/06/2026

JE, KUNA UHAKIKA? (1)

Wokovu ni kazi ya Mungu pekee ambayo inapokelewa kwa kuamini tu katika kufa, kuzikwa na kufufuka kwa Yesu.

Ingawa matukio haya (kufa, kuzikwa na kufufuka kwake) yalitokea mara moja, matokeo yake ni ya milele kwa asili.

Kwa hiyo, ni jambo la msingi kwa mwamini kuwa na maarifa au ufahamu sahihi kuhusu kweli muhimu wa neno la Mungu unaompa uhakika juu ya wokovu wake.

Waefeso 4:13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; 14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.

Paulo mtume anawaelezea waamini ambao “wanatupwa huku na huku” k**a watoto , neno ambalo linamaanisha kitu ambacho hakijakua au kukomaa vizuri (immature); inahusiana na hali ya kiroho ya mwamini.

Wanachukuliwa na kila upepo wa elimu. Mtume Petro pia anafundisha kitu hicho hicho;

2 Petro 3:15 Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, k**a vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; 16 vile vile k**a katika Nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika Nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, k**a vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe. 17 Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. 18 Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.

Mwamini lazima ajue haki, nafasi na urithi alionao katika Kristo, anatakiwa kukua katika maarifa au ufahamu wote juu ya yote ambayo Kristo amefanya na maarifa haya yanaweza tu kutoka katika maandiko.

Lazima ataarifiwe kikamilifu juu ya ushahidi wa kushangaza mno kutoka kwenye maandiko ambao unamhakikishia wokovu wake katika Kristo.

Kwa hiyo, inakua ni jambo la msingi na muhimu kujifunza juu ya maneno ambayo yanamwelezea mwamini kutoka kwenye maandiko (hasa katika Nyaraka).

Haya ni maneno yanayoelezea utambulisho wa mwamini ndani ya Kristo ambao unapata msingi juu ya dhabihu ya Yesu kwa dhambi.

Hebu tuchunguze baadhi ya kweli hizo.

Mwamini Amehesabiwa Haki Na Ni Mwenye Haki

Warumi 3:24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.

Neno “wanahesabiwa haki” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “dikaioo” linamaanisha kutamka (to pronounce) kuwa mwenye haki.

Limetumika zaidi ya mara 40 katika maandiko ya Agano Jipya la Biblia.

Kihistoria, lilitumiwa na mahakimu au majaji kwenye tamaduni ya Kigiriki wakati wanapotoa maamuzi au hukumu kuwa mtu “hana hatia”.

Ni tamko la jaji, kuona k**a ni haki, kuonesha haki, kutendea k**a ipasavyo haki, kutangaza k**a mwenye haki.

Hivyo mwamini amehesabiwa haki.

Mtume Paulo anamuelezea Ibrahimu k**a aliyehesabiwa haki.

Warumi 4:1 Basi, tusemeje juu ya Ibrahimu, baba yetu kwa jinsi ya mwili? 2 Kwa maana ikiwa Ibrahimu alihesabiwa haki kwa ajili ya matendo yake, analo la kujisifia; lakini si mbele za Mungu. 3 Maana maandiko yasemaje? Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa haki. 4 Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. 5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki.

Ibrahimu alihesabiwa haki na Mungu; akatangazwa kuwa yuko sawa, mwenye haki.

Haikutegemeana na kile amekifanya (matendo) bali alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa haki.

Kwa msingi wa imani katika Kristo, alihesabiwa haki na kuitwa mwenye haki.

Hii ni sawa kwa kila anayeamini katika Kristo Yesu.

Warumi 3:25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake, kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilizotangulia kufanywa. 26 apate kuonesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu.

Mwamini anahesabiwa haki kwa imani yake katika Kristo na hivyo anatangazwa mwenye haki.

Hivyo huku kuhesabiwa haki kumefanywa na Mungu.

Warumi 4:24 bali na kwa ajili yetu sisi mtakaohesabiwa vivyo hivyo, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu katika wafu; 25 ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuliwa ili mpate kuhesabiwa haki.

Neno “mtakaohesabiwa” (imputed -KJV) linamaanisha kufanya au kutoa hesabu ya; (to take account of), kuhesabia (to reckon with).

Hivyo mwamini anahesabiwa haki kwa kigezo cha imani yake katika ufufuo wa Kristo Yesu.

Pia, mwamini si kwamba tu anatangazwa mwenye haki, amefanywa haki ya Mungu katika Kristo.

2 Wakorintho 5:21 Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.

Neno “haki” linamaanisha ambayo ni sahihi au inayofaa (proper), -enye maadili, -enye kukubalika na –enye haki.

Limetumiwa na Paulo katika:

Warumi 3:22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti.

Wafilipi 3:9 tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani.

Ni haki ile ya Mungu; haki hii ni kwa imani.

Imani hapa ina maana ya kuamini kile ambacho Mungu amefanya katika Kristo, kukubali kile alichotupa.

Kumbuka kwamba, haki ya mwamini ni haki ya Yesu.

1 Wakorintho 1:30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi:

Haki hii ni zawadi tunayopokea katika Kristo.

Warumi 5:17 Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. 18 Basi tena, k**a kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima.

Hivyo, mwamini ni mwenye kuhesabiwa haki, anachukuliwa kuwa ni mwenye haki kwa imani tu (pekee) katika Injili.

Mwamini Ametakaswa Na Ni Mtakatifu

1 Wakorintho 6:11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

Neno “mlioshwa” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “apolouo” ambalo ni muunganiko wa maneno mawili “apo” yaani “mbali na” na neno “louo” –“osha”.

Hivyo, apolouo lina maana ya “kuosha mbali na-” (to wash away from).

Walioshwa mbali na nini?

1 Wakorintho 6:9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.

Tunaona Paulo akitaja mambo mengi.

Hata hivyo, lengo lake ni mstari wa 11.

Kifungu cha maneno “na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii;” kinaelezea hali yao ya awali (zingatia matumizi ya wakati uliopita, “-mli-”) ambayo amekwisha kutaja katika mistari ya nyuma na sasa anaweka msisitizo katika hali yao ya sasa yaani, “…mlioshwa, …mlitakaswa, …mlihesabiwa haki…”

Neno “mlitakaswa” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “hagiazo”.

Limetoka kwenye neno mzizi “hagion” au “hagios” ambalo lina maanisha kutenga, kuwekwa pembeni kwa kazi maalumu, kufanya takatifu, weka katika utakatifu au kuwekwa pembeni.

Linahusika sana na kuhifadhiwa/kutunzwa.

Paulo anatumia neno hilo pia katika Waefeso 5.

Waefeso 5:26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno.

1 Wathesalonike 5:23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

Kulingana na 1 Wathesalonike 5:23, Mungu ndiye anayetakasa, ushahidi ambao unaoneshwa na kuungwa mkono katika maandiko mengine pia.

Waebrania 2:11 Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja.

Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake.

Kwa kuzingatia muktadha, “yeye atakasaye” ni Yesu, hivyo bila kujalisha chochote, mwamini amekwisha kutakaswa.

Waebrania 10:14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

Waebrania 10:10 Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.

Dhabihu ya Yesu ilitolewa mara moja vivyo hivyo na utakaso wake.

Mwamini anatakaswa mara moja kwa toleo moja la Yesu, hiki ni kitu kinachofanyika mara moja na sio kitu endelevu.

1 Wakorintho 1:2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu.

1 Wakorintho 6:11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

Waebrania 3:1 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu.

Katika matumizi yake yote hapo juu, neno “takaswa” limetumika kwa mwamini likiwa katika wakati uliopita.

Tukirudi 1 Wathesalonike 5:23

Katika 1 Wathesalonike 5:23 Paulo alikua anaelezea utakaso wa Mungu kwa waamini kuwa ni kamilifu hasa.

Neno “kabisa” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “holoteisis”; linamaanisha kwa ukamilifu, kikamilifu, isiyo na mawaa (completely, perfectly).

Ni neno ambalo limetoholewa kutoka neno la Kigiriki “teleios” ambalo linamaanisha “kamili” (complete).

Hivyo neno “holoteisis” linamaanisha “iliyowekwa tabaka zote kikamilifu (fully layered)” au “iliyofanywa kikamilifu”.

Mungu anatakasa katika ukamilifu wake (mazima); kwa ujumla au kikamilifu.

Hafanyi kwa hatua.

Lazima izingatiwe kwamba, Paulo hakusema “… Mungu wa Amani (atawatakasa) kabisa”, lakini anasema “…Mungu wa Amani (awatakase (sanctify-KJV)) kabisa (kikamilifu).

Pia, hili linaweka msisitizo kuwa hakuwa anawaombea ili Mungu awatakase.

Mtume Petro pia:

1 Petro 2:9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.

Neno “takatifu” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “hagios” ambalo ni mzizi wa neno “hagiazo” lilotumika hapo juu likimaanisha kutambua kuwa ni takatifu (sacred) yaani “kutengwa au kuwekwa pembeni”.

Ni kutakasa, kuwekwa wakfu, tenga pembeni.

Kwa hiyo, Petro anachukulia kweli hii kuwa kila mmoja katika taifa hili (analolizungumzia katika muktadha) amefanywa mtakatifu na kazi ya Yesu.

Hivyo utakatifu haimaanishi “kutokufanya makosa” bali ni “kutengwa kwa ajili ya Mungu au kutengwa kwa Mungu”.

Kwa hiyo waamini wamefanywa watakatifu.

1 Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 K**a mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.

Mwamini ametakaswa na amefanywa mtakatifu; kazi hiyo ya utakaso ilifanywa na Yesu.

Mwamini Ana Msamaha Wa Dhambi

Waefeso 1:7 Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.

Wakolosai 1:14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi.

Wakolosai 2:13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote.

Mwamini ana (sio atakuwa na) msamaha wa dhambi.

Katika Nyaraka kuna neno lililotumika kwa msamaha (nomino na kitenzi);

neno la Kigiriki “aphesis” ni nomino la neno “msamaha” linamaanisha “kuondoa, weka mbali” yaani ni kuweka dhambi mbali wakati kitenzi kilichotumika ni neno “aphiemi, au charizomai” linamaanisha kusamehe, yaani ni kitendo cha kusamehe.

Katika vitabu vya Injili.

Mathayo 26:28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

Luka 24:47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.

Neno “ondoleo” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “aphesis” lina maana sawa na neno lilitafsiriwa k**a msamaha katika Nyaraka.

Linamaanisha kuondoa, kufuta dhambi.

Neno “dhambi” lina maana ya kosa, au kukosa shabaha.

Msingi wa msamaha ni katika sadaka au dhabihu yaani damu ya Yesu.

1 Yohana 2:1 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na k**a mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.

Tazama:

Neno “tunaye” katika andiko hilo hapo juu lipo katika wakati wa sasa endelevu ambalo linamaanisha “umiliki”, yaani kitu ulichonacho tayari.

Hivyo haitegemeani na kitendo au mwitikio (reaction) wowote.

Dhabihu ya Yesu kwa ajili ya dhambi kutoka kwenye andiko hilo inaonesha kuwa ni kitu ambacho kimekwisha kukamilika.

Neno “kipatanisho” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki ‘hilasterion” ambalo ni nomino.

Linazungumzia toleo au sadaka yenyewe.

Limetokana na neno la Kigiriki “hilasmos” lenye maana ya toleo ama sadaka ambayo inaleta kuridhika (satisfaction).

Hivyo, Yesu ni toleo au sadaka kwa ajili ya dhambi za mwanadamu, alikuwa ni sadaka kwa ajili ya dhambi na katika sadaka yake kuna maridhisho (satisfaction), yaani imekidhi matakwa kwa ajili ya ondoleo la dhambi.

Sadaka ya Yesu imeleta ondoleo la dhambi, kwa hiyo mwamini ana msamaha wa dhambi ndani ya Kristo.

Mwandishi wa Waebrania anasema jambo k**a hili:

Waebrania 8:10 Maana hili ndilo Agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu. 11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao. 12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.

Mwandishi ananukuu kutoka Yeremia 31:33-34.

Yeremia 31:33 Bali Agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.

Tofauti na dhabihu kipindi cha torati au Agano la kale ambapo kulikuwa na kumbukumbu ya dhambi zao kila mwaka kwa damu ya wanyama waliyokuwa wanatoa;

Waebrania 10:3 Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka. 4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Dhabihu kwa ajili ya dhambi katika Agano Jipya ni kamilifu, imefanyika mara moja na kwa umilele.

Waebrania 10:14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

Kwa hiyo, dhambi zimesamehewa, zimeondolewa, zimewekwa mbali kwa dhabihu ya Yesu.

Mungu hana kumbukumbu (hahesabu) ya dhambi na uovu k**a ilivyoahidiwa chini ya Agano la Kale; hana hiyo kwa mwamini.

Kwa hiyo, msamaha wa dhambi si kitu ambacho Mungu atafanya; bali ni kitu ambacho Mungu amefanya ndani ya Kristo Yesu.

Kumbuka; katika Nyaraka, maneno (“aphiemi na charizomai”) yalitumika kuwakilisha kitenzi cha msamaha yaani kusamehe.

Sasa ni muhimu kuzingatia kua katika Nyaraka, inapozungumzwa kuhusu msamaha au kusamehewa na Mungu, wakati wote limekuwa likitumiwa katika wakati uliopita.

Lilifundishwa k**a zawadi au kipawa cha Mungu kilichotolewa bila vigezo.

Paulo

Waefeso 4:32 tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane k**a na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Warumi 4:7 Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao.

Wakolosai 2:13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote.

Yohana

1 Yohana 2:12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake.

Angalia katika maandiko hapo juu; msamaha haimaanishi kitu ambacho Mungu atafanya, au anachofanya, ni kile ambacho amekwisha kukifanya ndani ya Kristo au kwa sababu ya Kristo.

Hata hivyo, ni muhimu kukumbuka kuwa ni mtume Yakobo pekee aliyetumia msamaha (charizomai) katika wakati uliopo.

Yakobo 5:14 Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. 15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. 16 Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

Sasa, kumbuka

- Yakobo hakusema kuwa aungame dhambi zake kwa Mungu, bali alisema hata akiwa ametenda dhambi, atasamehewa.

- Pia, hakusema ungama makosa yako kwa Mungu, bali ninyi kwa ninyi.

- Hivyo Yakobo alikua anazungumzia kurejesha mahusiano kati ya waamini.

Kwa hiyo, msamaha sio kitu ambacho Mungu anakifanya bali ni kitu ambacho Mungu alishakifanya kwetu ndani ya Kristo.

Yeyote aliyekwisha kuiamini Injili amepokea na hivyo ana msamaha wa dhambi.

Pia, waamini wameokolewa kutoka katika ufahamu wa dhambi.

Waebrania 10:3 Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka. 4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Dhabihu za wanyama zilibakiza kumbukumbu au ufahamu wa dhambi, hali ya kujiona mwenye dhambi (sin consciousness) lakini dhabihu ya Yesu inaleta uhuru.

Warumi 8:2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.

Hivyo, mwamini lazima awe na uhakika kuwa ana msamaha wa dhambi.

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009


02/06/2026

Sio matendo yako ya dhambi yatakayo kupeleka motoni… ni kiburi chako cha kutokuamini katika dhabihu moja na ya milele kwa ajili ya ondoleo la dhambi; kutokuamini katika Jina la Yesu liokoalo.

Ukiamini leo, kuwa Yesu Kristo alitolewa kufa kwa ajili ya makosa yako na kufufuka kutoka katika wafu ili wewe uhesabiwe haki utaokoka.

Onjeni muone, Bwana ni mwema!

Kainos Creation
1 Jun 2024


02/06/2026

Injili ni uweza wa Mungu uokoao kwa kila aaminiye! Nguvu ya kuokoa ipo katika hio Injili; katika facts za Injili. Uweza wa kuokolewa haupo katika matendo ya mtu wala jitihada zake. Injili haihitaji visaidizi wala nyongeza nyingine ile kuokoa, Inajitosheleza yenyewe. Tusiongeze mbwembwe wala chumvi juu ya Neno la Msalaba (Injili).

Kainos Creation


30/05/2026

Ikiwa mtu anakuonya au kukurekebisha ina maana tu una nafasi katika moyo wake. Unaweza kuwa ndugu wa kweli ama jamaa wa kufahamiana tu, unaweza kuwa mwana wa halali ama mwana wa haramu! Usichukie maonyo, kumbatia marekebisho - wapende wanaokuonya na kukurekebisha; watu hao ni adimu siku hizi! - Heb 12:5-11

Kainos Creation


30/05/2026

JE ROHO MTAKATIFU ANATUSAIDIA KUOMBA?

Katika kujifunza “sanaa ya maombi” k**a ilivyo kwa mada nyingine yeyote ya Maandiko, ni vema kuyaelewa na kuyatumia mafungu ya maandiko katika muktadha wake.

Kutofanya hivyo kutapelekea kuingiza mafundisho yasiyo sahihi na kuangukia katika matumikio yenye makosa.

Tunaangazia kauli “Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba ipasavyo”.

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Kabla ya kuangazia andiko hilo hapo juu ili kufanya uchambuzi wa kina kubaini maana na mlengo wa mwandishi katika maneno yake, kwanza turejee na kujiimarisha zaidi katika namna maombi yanafanyika katika Agano Jipya.

JINSI IPI YA KUOMBA KATIKA AGANO JIPYA

Tutembelee tena maelekezo ya Paulo katika barua yake kwa Waefeso.

Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

Kwanza kabisa, kumbuka kutoka Sura ya Kwanza hadi ile ya Saba, kauli “sala na maombi” haikumaanisha shughuli mbili tofauti, bali kitu kimoja.

Neno “na”, ambalo lilitafsiriwa kutoka katika neno la kiyunani “kai”, katika muktadha huu lilikua ni lenye kuelezea, na linaweza kubadilishwa na “hiyo ni” au “ambayo ni”.

Hivyo kile Paulo alikua akisema kinaweza kuwekwa namna hii....kwa sala zote ambayo ni maombi wakati wote katika Roho…

Ni muhimu pia kukumbuka kutoka Sura iliyopita, kwamba neno “sala” lina maana ya ombi lisilobadilika (fixed).

Hivyo neno “zote” k**a lilivyotumiwa na Paulo lilikuwa katika kuvumisha mahitaji (haja na maombi) yanayofanywa kwa ajili ya watakatifu wote (yote ambayo tumekwisha kuchunguza vyema katika Sura zilizopita).

Hivyo inaweza kuhitimishwa kutoka katika maelezo ya Paulo kwamba, hakuna aina tofauti tofauti za maombi, bali, kile ambacho Nyaraka hufundisha na kuelekeza ni mahitaji tofauti tofauti katika maombi.

Yaani ni kusema kwamba, MAOMBI NI MAOMBI, yawe ni kwa ajili yako au kwa ajili ya wengine (uongozi na ushirika), kinachobadilika ni kitu na mahitaji yanayoombwa.

Tabia na mtazamo ambao kwa huo tunaomba na namna tunaomba hubaki vile vile.

Sasa, ni muhimu kuangazia tena Paulo alimaanisha nini kwa kauli “mkisali kila wakati katika Roho”.

Kwakuwa, sala/dua ni kufanya ombi maalum, hivyo alichokieleza Paulo ni kwamba mahitaji yetu katika maombi yanapaswa kufanyika au kupelekwa katika Roho.

Paulo anafundisha namna ambavyo hili linafanyika katika waraka wake mwingine kwa kanisa la Korintho.

1 wakorintho 14:14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina Matunda. 15 Imekuaje, basi? Nitaomba kwa Roho tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa Roho, tena nitaimba kwa akili pia.

Nikiomba kwa lugha, Roho yangu huomba.

Alilizungumzia hili pia mapema katika mstari wa 2

1 Wakorintho 14:2 Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; Maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake.

Kwa wazi kabisa; kuomba kwa lugha mpya ni kuomba kwa Mungu (baba) katika roho! –kunena kwa lugha ni kusema katika roho.

Paulo mwenyewe aliomba kwa lugha kila mara, kwa uendelevu; yalikua ni maisha yake ya maombi namna hiyo.

1 Wakorintho 14:18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha Zaidi ya ninyi nyote

Hivyo, maagizo ya kitume ambayo tunayo katika Nyaraka kuhusu namna gani tunaomba ni kwamba, kila uhitaji na maombi yote yanapaswa yafanyike kwa lugha.

Mmoja atasema – lakini kuna wengine hawasemi kwa lugha mpya!

Jibu ni kwamba, kila mwamini ana uwezo wa kunena (omba) kwa lugha. Uwezo huu unakaa ndani ya kila mwamini tangu alipoamini.

1 Wakorintho 14:5 nami nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini Zaidi sana mpate kuhutubu: maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokua afasiri, ili kusudi kanisa lipate kujengwa…Mst 18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha Zaidi ya ninyi nyote;… 23 Haya! Ikiwa KANISA LOTE limekusanyika pamoja, na wote wanene kwa lugha, kisha ikawa wameingia watu wajinga au wasioamini, je! hawatasema kwamba mna wazimu? … 26 Basi ndugu imekuwaje? Mkutanapo pamoja, KILA MMOJA ANA zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga.

Huwezi kutoa maelekezo kua WOTE wanene kwa lugha ikiwa kuna wengine hawakujaaliwa.

Na Paulo asingeweza kusema kua wanapokutana pamoja KILA MMOJA ana lugha ikiwa wengine hawawezi kuwa na lugha.

Yesu pia alizungumza kuhusu hili katika ufufuo wake.

Marko 16:17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

Zitafuatana na hao waaminio, naam, kila mwamini.

Siyo kila Mchungaji au kila “nabii”.

Hao waaminio, WOTE.

Katika Sura ya Sita tuliona katika kitabu cha Matendo ya Mitume kua kila mara waamini walipoongelewa kujawa na Roho na kusema kwa lugha ilikua ni WOTE pasipo hata mmoja kutengwa.

Matendo ya Mitume 2:4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, k**a Roho alivyowajalia kutamka.

Matendo ya Mitume 10:44 Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliosikia lile neno. 45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. 46 kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,

Matendo ya Mitume 19:6 Na Paulo alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.

Na imeelezwa na Paulo kwa msisitizo katika Nyaraka.

1 Wakorintho 12:4 Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule… Mst 7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana… 10 Na wengine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha.

Neno “karama” limetafsiriwa kutoka katika neno linalomaanisha; uwekezaji wa kiroho (supernatural endowmnents); vitivo na uwezo usio wa asili.

Hivyo Karama zote (ikiwemo lugha), zinakaa ndani ya kila mwamini.

Hivyo Paulo aliposema “kwa sala zote ambayo ndiyo maombi katika Roho”, alirejea kusali au kuomba kwa ajili ya watakatifu katika Roho.

Yaani ni kuweka katika matamshi haja zetu kwajili ya watakatifu, wahudumu wa injili, kazi ya huduma, kwa Baba katika lugha.

Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi, mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

1 Wakorintho 14:2 Maana yeye anenaye kwa lugha hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika Roho yake… 14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda… 15 imekuwaje, basi? nitaomba kwa Roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba roho, tena nitaimba kwa akili pia.

Yuda pia aliwaelekeza waamini waombe katika Roho Mtakatifu.

Yuda 1:20 Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya Imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu.

Sasa, kumbuka kwamba Paulo pia aliandika katika barua hiyo hiyo kwamba aliwaombea (Waefeso) siku zote.

Waefeso 1:16 siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu; 17 Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima naya ufunuo katika kumjua yeye.

Kwa hiyo inatosha kusema kwamba, maombi ya Paulo katika barua zake zote, ni tafsiri ya maombi yake kwa ajili ya waamini ambayo aliyafanya kwa lugha.

1 Wakorintho 14:18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha Zaidi ya ninyi nyote;

Hivyo, aliwaagiza waamini waombe kila wakati kwa sala zote na maombi katika Roho.

Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi, mkisali kila wakati katika Roho , mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

Jinsi ya kuomba, k**a ilivyofundishwa na kuagizwa katika Nyaraka ni katika Roho- kwa kunena kwa lugha.

Maneno ya Paulo katika 1 wakorintho 14:18 husema mengi.

1 Wakorintho 14:18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote.

Kutoka katika maelezo yake katika mstari wa 14 hadi wa 17

1Wakorintho 14:14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. 15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; nitaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia. 16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo? 17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi

Kunena kwa lugha kunahusisha kuomba kwa lugha na kuimba kwa lugha.

Na k**a ilivyoelezwa hapo awali, hiki ndicho ambacho Paulo alielezea k**a “Sala na shukrani katika Roho”.

Hivyo Paulo aliposema “Nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote”, alimaanisha kwamba aliomba kuliko kanisa lote la mahali.

Mtazamo huu na bidii hii ya Paulo inaonyesha umuhimu wa kuomba katika Roho.

Tazama kwa umakini alichokisema katika Mstari wa 19

1 Wakoritho 14:19 Lakini katika kanisa napenda kunenan maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.

Kwa maneno mengine, Paulo aliposema “nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote”, alikua anarejelea maisha yake binafsi.

Hivyo, Paulo alitumia muda wa kutosha binafsi kuomba katika Roho.

Kwa maneno mengine maisha ya maombi ya mwamini hayatakiwi kuwa na tabia ya kuomba katika mikutano ya maombi inayofanyika katika kanisa la mahali peke yake.

Kwa undani, kila mwamini (kiongozi au mshirika) lazima awe
na maisha binafsi ya maombi!

Lazima katika siku atenge muda wa kutosha wa kuomba kwa lugha / katika Roho.

Kumbuka kwamba, Yesu alikua na maisha ya maombi.

Alikua na muda ambao aliutumia binafsi katika kuomba, alitupa muundo na kielelezo hiki katika maisha yake.

Marko 1:35 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali Pasipokuwa na watu, akaomba huko.

Hapa, aliondoka mapema sana alfajiri, kukiwa bado ni giza ili aombe katika mahali pasipokuwa na watu akiwa PEKE YAKE.

Mathayo 14:23 Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda Kuomba. Na kulipokuwa jioni alikuwako huko peke yake.

Hapa, Yesu alijitenga PEKE YAKE kuomba.

Mathayo aliandika kwamba aliomba usiku/jioni.

Luka 6:12 ikiwa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu.

Hapa, Luka ameandika kwamba Yesu aliomba PEKE YAKE usiku kucha.

Paulo pia alimwambia Timotheo kua anamuombea pasipo kukoma usiku na mchana.

2 Timotheo 1:3 Namshukuru Mungu, nimwabuduye kwa dhamiri safi tangu zamani za wazee wangu, k**a vile nikukumbukavyo wewe daima, katika kuomba kwangu usiku na mchana.

Paulo pia alisema kwa kanisa la Kolosai kwamba Epafra, katika maisha yake ya maombi, aliwaombea siku zote.

Wakolosai 4:12 Epafra aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kudhibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.

Kwa hiyo, hii inaelezea kwamba, zaidi ya mikutano ya maombi inayofanyika katika makanisa yetu ya mahali (ambayo ni muhimu pia), kila mwamini (kiongozi na mshirika) lazima awe na maisha ya maombi.

Na maisha haya ya maombi lazima yawe ya kudumu!.

Hivyo vivumishi vilivyotumika kuelezea maombi… mkidumu; dumuni, kila wakati; bila kukoma; siku zote, bidii.

Warumi 12:12 kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu;

Kwa maneno mengine, lazima kuwe na utaratibu maalumu (regularity) katika maisha yetu ya maombi (iwe binafsi au k**a kanisa la mahali).

Hivyo maombi hayapaswi kufanywa pasipo mpangilio.

Hii ina maana kwamba, iwe ni katika maisha yetu binafsi au katika kanisa la mahali, mahitaji ya maombi (prayer points) hubaki zile zile.

Maisha ya Paulo ya maombi yalikuwa kwa ajili ya wengine:

Waefeso 1:15 Kwa sababu hiyo mimi nami, tangu nilipopata habari za Imani yenu katika Bwana Yesu, na pendo lenu kwa watakatifu wote, 16 siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu, 17 Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima nay a ufunuo katika kumjua yeye;

Waefeso 3:14 Kwa hiyo nampigia Baba magoti, 15 ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa, 16 awajilieni kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake katika utu wa ndani.

Wafilipi 1:8 Maana Mungu ni shahidi wangu, jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote katika moyo wake Kristo Yesu. 9 Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote;

Wakolosai 1:9 Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni; 10 mwenende k**a ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu;

Wakolosai 4:12 Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu. 13 Maana namshuhudia kwamba ana juhudi nyingi kwa ajili ya hao walioko Hierapoli.

2 Wathesalonike 1:11 kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu, akatimiza kila haja ya wema na kila kazi yaa Imani kwa nguvu;

Filemoni 1:4 Namshukuru Mungu wangu siku zote, nikikukumbuka katika maombi yangu; 5 nikisikia habari za upendo wako na Imani uliyo nayo kwa Bwana Yesu na kwa watakatifu wote; 6 ili kwamba ushirika wa Imani yako ufanye kazi yake, katika ujuzi wa kila kitu chema kilicho kwetu, katika Kristo.

Hakuna kifungu katika Nyaraka zote ambapo Paulo au Mtume yeyote walijiombea wao wenyewe kwa kugusia mahitaji yao ya kimwili.

Mlengo wao ulikuwa ni kwa ajili ya wengine.

Hivyo, Paulo aliposema katika 1 Wakorintho 14:18

1 Wakorintho 14:18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha Zaidi ya ninyi nyote;

Alikua anarejea katika maombi yake (kwa lugha) kwa ajili ya wengine na hali inayozingira au kuhusiana na injili.

Hii inaonyesha upendo wake na kujitoa kwa ajili ya maisha ya wengine na kwa ajili ya kazi ya huduma.

Kimsingi moja ya ushahidi wa pendo letu na kujitoa kwa wengine ni katika kuwaombea.

Sasa, angalia kimuktadha, maelezo ya Paulo kuhusu faida za kuomba katika roho/kwa lugha.

1 Wakorintho 14:2 Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake. 3 Bali yeye ahutubuye asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo. 4 Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa.

Kwa Maneno mengine mwamini anapotumia muda wake mwingi kuomba kwa ajili ya wengine na hali inayozingira injili, kwa lugha, anakua anajijenga mwenyewe pia.

Neno “kujenga” limetafsiriwa kutoka katika neno la kiyunani “oikodomeo” lenye maana ya kujenga, kuimarisha.

Yuda alifundisha hivyo pia katika Nyaraka

Yuda I:20 Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu,

Hivyo kuomba kwa lugha hufanya kazi mbili

1. Kunabadilisha hali na mazingira na kutimiza mahitaji ya wengine/waamini wengine

2. Pia inamjenga yule anayeomba:

a. Anasikia sauti ya Roho kwa wepesi na uwazi zaidi

b. Uinjilisti wake unaimarishwa (namna anawasilisha ujumbe na kua na matokeo katika uvuvi wa roho za wa watu)

c. Vipawa vyake vinaamshwa na kua na utendaji zaidi

d. Ufunuo wa Roho unatiririka katika ufahamu wake kwa wepesi zaidi

e. Anakua imara zaidi dhidi ya majaribu

f. Kunakua na wepesi wa utendaji wa Neno na hivyo badiliko la tabia na mwenendo, anatembea tofauti na kusema tofauti (sawa na Neno)

g. Anaona miujiza zaidi, anatoa pepo wengi zaidi na kwa wepesi, anaponya wagonjwa kwa wepesi zaidi.

Inaweza ikaelezwa kutoka katika maelezo ya Paulo na Yuda kutoka katika vifungu hapo juu, kwamba, kiwango ambacho mwamini anaomba kwa lugha, ndiyo kiwango ambacho yeye (kiongozi/mshirika) anajijenga mwenyewe.

Hivyo mwamini (kiongozi/mshirika) hawezi kumudu kua na maisha ya maombi yasiyokuwa ya mfululizo au yasiyo ya kudumu!

K**a Paulo, kila siku, pasipo kuyumba na kwa kudumu; kila mwamini (kiongozi/mshirika) LAZIMA atumie muda wake mwingi KUOMBA katika Roho.

Sasa, ni muhimu kutambua kwamba sala/maombi katika Roho sio alichokielezea Paulo katika Warumi 8:26.

ROHO HUTUSAIDIA UDHAIFU WETU?

Sasa tuangazie kile ambacho Paulo anafundisha katika kitabu cha Warumi, mara nyingi inadhaniwa kuwa Paulo alikua anaongelea maombi, la hasha!

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Neno “kadhalika”limetafsiriwa kutoka katika neno lenye maana ya kwa namna hiyo hiyo.

Au kwa jinsi hiyo hiyo.

Hivyo, ili kuelewa alichokua anajadili Paulo lazima tusome mistari iliyotangulia.

Kwa kuwa huwezi kuibuka tu na kusema “kwa jinsi hiyo hiyo” ikiwa hakukua na jinsi au namna uliyoizungumza kabla.

Usomaji kwa muktadha hutusaidia kuelewa mtiririko wa mada ya mwandishi.

Paulo anasema “kadhalika Roho naye…”, je ni Roho yupi anayemwongelea? Tutembelee muktadha wake.

Tambua kwamba, Paulo alitumia neno “Roho” katika sura hiyo hiyo mara 16, na katika muktadha huo alikua anarejea kwa Roho wa Kristo / Roho wa Mungu / Roho wake / Roho, iliyopokelewa na kukaliwa na mwamini kwa Imani katika injili.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. 2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti…9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wa …11 Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.

Hivyo Paulo aliposema “Roho hutusaidia udhaifu wetu…”, Roho katika muktadha huu ilikuwa ni rejea kwa Roho ya /ndani ya/ inayomkalia mwamini.

Neno “hutusaidia”(Warumi 8:26) limetafsiriwa kutoka katika neno lenye maana ya kutoa msaada, kutenda kazi kwa pamoja dhidi ya-.

Ni neno hilo hilo pia lililotumika na Luka katika injili yake.

Luka 10:40 Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.

Kifungu hapo juu kinatuonesha kwamba kulikuwa na shughuli ambayo Martha alijihusisha nayo, shughuli ambayo ilimuhitaji Mariamu aje kumsaidia.

Hii inamaanisha kwamba Paulo alichoeleza (katika Warumi 8:26) ni kwamba Roho hushik**ana pamoja na mwamini dhidi ya udhaifu wetu.

Neno “wetu” linaonesha alichorejea Paulo k**a “udhaifu” ni kwa waamini wote.

Ni “udhaifu” gani aliokua anaongelea?

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Neno “udhaifu” hapa limetafsiriwa kutoka katika neno lenye maana ya upungufu (inadequacy); udhaifu.

Ni neno hilo hilo liliotumika hapo awali katika Sura ya sita.

Warumi 6:19 Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa miili yenu. Kwa kuwa k**a mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa.

Paulo alitumia neno hilo hilo katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho.

1 Wakorintho 2:3 Nami nalikuwako kwenu katika hali ya udhaifu na hofu na matetemeko mengi.

Hivyo Paulo alipotumia neno “astheneia” katika warumi 8:26, alikua hamaanishi vitu vingi k**a ilivyoelezewa katika tafsiri ya KJV (infirmities: madhaifu), bali alikua anarejea upungufu au udhaifu wa miili yetu.

Yaani, udhaifu wa mwili wa mwamini ambao bado ni wa kuharibika; ni wa kufa, wenye kupatikana na magonjwa na mauti, ambao utahuishwa na kutukuzwa katika siku ya ukombozi wa miili yetu.

Hiyo ndiyo sababu alieleza mapema katika mstari wa 11

Warumi 8:11 Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.

Ameuelezea mwili wa mwamini k**a ulio katika hali ya kufa na Roho imkaliayo mwamini k**a “uzima” (mstari wa 2 na wa 10).

Hata hivyo mwili huo wa kufa/kuharibika utahuishwa au kupewa uzima kwa Roho amkaliaye mwamini katika ukombozi wa miili au katika ufufuo (mstari wa 23)

Warumi 8:23 Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu

Turudi hapa:

Warumi 8:11 Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu

Tambua kwamba ametumia neno “ata” katika “ata~ihuisha”, kwanza, ili kuelezea kwamba, mtu anapookolewa hawi na mwili wa kutokufa/kutoharibika.

Pili, kwamba kuhuishwa kwa mwili wa mwamini ulio katika hali ya kufa hakujatokea bado bali kutatokea hapo baadae (mstari wa 23).

Warumi 8:23 Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu

Hii ina maana ni jambo la baadaye.

Sasa, tazama kwa umakini maelezo yake kwa muktadha kuanzia mstari wa 18 na kuendelea.

Warumi 8:18 Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu k**a utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.

Alizungumzia vitu viwili hapa:

- Mateso ya wakati wa sasa

- Utukufu utakaofunuliwa kwetu

Kwa wazi, “mateso” ya wakati huu ilikuwa ina rejelea hali ya kuharibika au ya kufa kwa mwili wa mwamini,

wakati “utukufu utakaofunuliwa kwetu (waamini) ”anarejelea kuinuliwa au kufufuliwa kwa miili kutoka wafu, ambayo ni kuhuishwa mwili kwa Roho / Roho wa Mungu / Roho wa uzima katika Kristo; Roho anayetukalia.

Hii ndiyo sababu alieleza katika mstari wa 19 kwamba, “utukufu utakaofunuliwa kwetu” ni “kufunuliwa kwa wana wa Mungu”.

Hata hivyo, alitumia neno “vinatazamia” kuonesha kwamba “ufunuo” huu ambao ndio kutukuzwa, kuhuishwa, kukombolewa kwa miili ya waamini ni kitendo cha baaade.

Alieleza hili zaidi katika mstari wa 22 na wa 23.

Warumi 8:22 Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa. 23 Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.

Neno “vinaugua” na neno “tunaugua” katika mstari wa 22 na wa 23 kwa pamoja vimetafsiriwa kutoka katika neno lenye maana ya kulalamika au kusumbuka.

Tambua kwamba alitofautisha kati ya kuugua kwa uumbaji wote (mstari wa 22) na kuugua kwa mwamini (aliyekaliwa na Roho).

Paulo alitumia neno hilo hilo “kuugua” (stenazo) katika mstari wa 26

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Hivyo aliposema katika mstari wa 26 kwamba “Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa”, alikua anarejea katika kitu kile kile alichoeleza katika mstari wa 23.

Hivyo kuugua ni kutoka ndani ya mwili wa mwamini ambao bado haujatukuzwa/kombolewa/kuhuishwa.

Paulo alitumia neno hilo hilo katika barua ya pili kwa Wakorintho.

2 Wakorintho 5:1 Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni. 2 Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

Kwa mara nyingine, anarejea katika kitu kile kile:

“kuugua” au kusumbuka kwa mwili wa mwamini ambao bado haujavikwa nyumba itokayo mbinguni.

Ndiyo maana Paulo kwa mfululizo katika mstari wa 24 na 25 alirejea katika ukombozi wa mwili (ufufuo) wa mwamini k**a taraja, ambalo tunalisubiri kwa saburi.

Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho? 25 Bali tukikitarajia kitu tusichokiona, twakingojea kwa saburi.

Kwa ushahidi, wokovu huu (“tuliokolewa”) katika muktadha ni ule wa mwili wa mwamini ambao ni wa kutokea baadae.

Hii ndiyo sababu alielezea mapema katika mstari wa 15 kwamba tumepokea Roho ya kufanywa wana.

Warumi 8:15 Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.

Kwa Maneno mengine, mwamini anasubiria kwa saburi ukombozi wa / kuhuishwa / hali ya kutokufa ya mwili huu upatikanao na mauti.

Hivyo, matumizi ya “tuliokolewa” (mstari wa 24), ukombozi (mstari wa 23) na kufanywa wana (mstari wa 23) ni kwa mwili wa mwamini, ambao sasa uko katika hali ya kuharibika.

Ni kitu hicho hicho ambacho alikielezea k**a mateso ya wakati huu (katika mstari wa 18).

Kwa maneno mengine, “udhaifu wetu” ambao Paulo aliuzungumzia katika mstari wa 26, kwa uwazi ni hali ya kufa/kuharibika, upungufu wa mwili wa kila mwamini, ambao utatukuzwa; katika ukombozi au ufufuo wa miili yetu.

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Hivyo swali la kuuliza ni: K**a Paulo alieleza kwamba katika ukombozi wa mwili, mwili wa mwamini upatikanao na mauti utahuishwa (kufanywa hai) kwa Roho wake aliemfufua Kristo katika wafu, amkaliaye mwamini,

kwa nini Paulo alitumia neno “kuomba” (pray –KJV) kwa mwamini na “hutuombea” (Intercession –KJV) kwa Roho Mtakatifu?

Kumbuka kwamba neno “kuugua” limetumika kwa mfululizo na Paulo (katika mstari wa 23) kuelezea kusumbuka au mateso au upungufu au udhaifu au hali ya kufa ya mwili wa mwamini unaokaliwa na Roho wa Mungu,

hivyo kusema kwamba anatuombea sisi kwa kusumbuka au mateso ambayo hayawezi kutamkwa itakua sio sahihi kwa melezo yake kimuktadha.

Paulo alikua wazi katika maelezo yake:

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Sentensi “kusikoweza kutamkwa” imetafsiriwa kutoka katika neno la kiyunani “alaletos”, ni neno la muunganiko lililotoholewa kutoka katika maneno mawili:

- “Letos” - limetoholewa kutoka katika neno la Kigiriki “laleo” linalomaanisha kuzungumza, kutamka.

- “a”- neno “a” kwa kawaida ni kiambishi au neno awali linalotumika katika sarufi ya Kigiriki k**a kikanushi.

Hivyo, neno “alaletos” linaeleza kwamba hakuna maneno; yaani hakuna kilichotamkwa.

Hivyo basi sentensi hii inamaanisha kwamba mwili wa mwamini upo katika hali ya kutokutamka, unalalamika.

“Kuugua” kunatokana na hali ya mwili na hakuna maneno yanahusika.

Na hii ni kinyume cha kuomba -kupeleka haja kwa Baba k**a tulivyojifunza kua maombi yanahusisha kuyapa mahitaji matamshi.

Neno “kuomba” katika andiko hilo limetafsiriwa kutoka neno “proseuchomai”.

Ni neno la muunganiko linalotokana na maneno mawili ya sarufi ya Kigiriki “pro” linalomaanisha “kwa”/ “wakati” na “euchomai” lenye maana ya “shauku”/ “ombi”.

Paulo alitumia neno “euchomai” kwenye kitabu hicho hicho katika mstari wa tisa

Warumi 9:3 Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili;

Katika tukio hili, Paulo hakua anaomba kwa Baba, bali, alikua anadhihirisha shauku (ambayo ni kitu alichokihitaji).

Luka aliandika kwamba Paulo alitumia neno “euchomai” mara mbili katika kitabu cha matendo.

Tazama tafsiri zote SUV na KJV.

Matendo ya Mitume 26:29 Paulo akamjibu, Namwomba Mungu kwamba, ikiwa kwa machache au ikiwa kwa mengi, si wewe tu ila na hao wote wanaonisikia leo wawe k**a mimi, isipokuwa vifungo hivi…..

Acts 26:29 And Paul said, I would to God, that not only thou, but also all that hear me this day, were both almost, and altogether such as I am, except these bonds.

Matendo 27:29 Wakachelea tusije tukapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne za tezi, wakaomba kuche.

Acts 27:29 Then fearing lest we should have fallen upon rocks, they cast four anchors out of the stern, and wished for the day)

Yohana pia alilitumia katika Waraka wake wa tatu.

3 Yohana 1:2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo….

3 Yohana 1:2 Beloved, I wish above all things that thou mayest prosper and be in health, even as thy soul prospereth.)

Katika maandiko haya neno “kuomba” lilikuwa katika kuongelea shauku (wish, desire) sio maombi katika namna ya kawaida kuomba kufikisha mahitaji kwa Baba.

Vivyo hivyo Paulo hakua anazungumzia maombi katika Warumi 8:26 k**a inavyoonekana katika muktadha wa maelezo yake,

hivyo kifungu hicho kitaeleweka vyema k**a neno “kuomba” lingebadilishwa na neno “shauku” (wish or desire).

Hivyo ni :

“… kwa maana hatujui nini tunatakiwa kuonea “shauku” k**a itupasavyo, ila roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa”.

Kimsingi, alichomaanisha ni hiki; shauku ya moyo wa mwamini ni ukombozi wa mwili au kuvikwa mwili wa mbinguni, kutokana na rejea ya kuugua au upungufu wa mwili wake.

Warumi 8:23 Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.

2 Wakorintho 5:2 Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

Sasa, Paulo alimaanisha nini kwa kusema “Roho hutusaidia udhaifu wetu” ?

Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Kwa kusoma kifungu cha hapo juu kwa umakini, ni dhahiri kwamba sentensi “roho hutusaidia udhifu wetu” ndicho alichoeleza Paulo k**a “Roho hutuombea”

hivyo, “hutuombea” ni kutusaidia katika upungufu wetu (udhaifu) kwa Roho wa uzima, Roho wake, Roho wa Mungu akaaye ndani yetu, katika Kristo.

Sasa kumbuka kwamba neno “hutusaidia” limetafsiriwa kutoka katika neno la muunganiko la kiyunani “sunantilambanomai” lenye maana ya kutoa msaada; kushik**ana pamoja dhidi ya-.

Hii inamaanisha kwamba Roho hushik**ana pamoja na sisi au hutoa msaada dhidi ya upungufu (udhaifu au kuugua) kwa mwili wa kufa wa mwamini, na sio kwamba Roho ndio inayougua au kulalamika.

Kwa maneno mengine Roho hutenda kazi kinyume na kulalamika au kusumbuka kwa mwili.

Roho hufanya hivi kwa namna gani?

Warumi 8:16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; 17 na k**a tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. 18 Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu k**a utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.

Hivyo, “kutuombea” katika muktadha (mstari wa 26) inaeleweka k**a ushahidi wa Roho ambao umearifiwa katika uaminifu wa Neno la Mungu kwamba miili yetu itatukuzwa katika ufufuo, na hii husaida kunyamazisha/kutuliza kuugua-na hili ndilo tumaini letu!.

Kwa maneno mengine, ushahidi wa Roho ni uthibitisho kwamba miili yetu itatukuzwa;

hivyo kutakua na kufunuliwa kwa wana (utukufu wa miili ya kufa ya wana wa Mungu kwa Roho akaaye ndani yetu).

Hivyo, wakati mwili upo katika hali ya kutokua na utulivu na kusumbuka, roho yetu ina shahidi.

Na hiki ndicho kinachotutenganisha na ubinadamu wa kawaida.

Tunakaliwa na Roho wake aliye mfufua Kristo kutoka wafu,

hivyo, tuna shahidi katika roho zetu; uthibitisho kwamba miili yetu itahuishwa /kombolewa/ fanyika wana/ tukuzwa/ fufuliwa.

Paulo alifundisha vivyo hivyo kwa mfululizo katika barua zake.

1 Wakorintho 15:35 Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?...39 Nyama yote si nyama moja; ila nyingine ni ya wanadamu, nyingine ya hayawani, nyingine ya ndege, nyingine ya samaki. 40 Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali. 41 Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota. 42 Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika; 43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu; 44 hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko. 45 Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha. 46 Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho. 47 Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni. 48 K**a alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na k**a alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni. 49 Na k**a tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni. 50 Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika. 51 Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, 52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika. 53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa. 54 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda. 55 Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

2 Wakorintho 4:10 siku zote twachukua katika mwili kuuawa kwake Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu. 11 Kwa maana sisi tulio hai, siku zote twatolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu ipatikanayo na mauti. 12 Basi hapo mauti hufanya kazi ndani yetu, bali uzima ndani yenu. 13 Lakini kwa kuwa tuna roho ile ile ya imani; k**a ilivyoandikwa, Naliamini, na kwa sababu hiyo nalinena; sisi nasi twaamini, na kwa sababu hiyo twanena; 14 tukijua ya kwamba yeye aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi nasi pamoja na Yesu, na kutuhudhurisha pamoja nanyi. 15 Kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ili neema hiyo ikiongezwa sana, kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu atukuzwe. 16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. 17 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; 18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.

2 Wakorintho 5:1 Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni. 2 Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni; 3 ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi. 4 Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twaugua, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.

Waefeso 1:13 Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu. 14 Ndiye aliye arabuni ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milki yake, kuwa sifa ya utukufu wake.

Wefeso 4:30 Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.

Petro pia alisema:

1 Petro 1:4 tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu. 5 Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho.

Yohana pia.

1 Yohana 3:2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona k**a alivyo.

Kimsingi, mwamini, ni mwana wa Mungu anaekaliwa na Roho (Warumi 8:9, 10, 11).

Hivyo kukaliwa na Roho ni uthibitisho kwamba miili yetu ya kufa itahuishwa katika ufufuo ( Warumi 8:11 & 18-23, 2 Wakorintho 4:10-18, 2 Wakorintho 5:1-4, Waefeso 1:14,4:30).

Hivyo, sentensi “Roho hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa”,

k**a ilivyoelezwa na Paulo katika muktadha inaweza kumaanisha kwamba maombi (intercession) ni dhidi ya kutokua na utulivu; kusumbuka au hali ya upungufu ya mwili wa mwamini ambao kwa sasa uko katika hali ya kufa (Warumi 8:23 & 26b).

Hivyo basi,

Warumi 8:26 sio kifungu ambacho Paulo alikitumia kufundisha maombi au kuugua katika Roho,

bali maelezo yake ni kuimarisha na kusisitiza kukaliwa na Roho ndani ya mwamini k**a arabuni ya kwamba mwili wa mwamini (ambao sasa uko katika hali ya kufa) utatukuzwa au kuhuishwa katika ufufuo.

Hivyo, “usaidizi wa Roho au Roho kutuombea” katika muktadha huo, ni muitikio wa Roho dhidi ya kuugua / upungufu / udhaifu wa mwili wa mwamini.

Hata hivyo Paulo alielezea kwa wazi alichomaanisha kwa kusema “kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho” katika barua yake kwa kanisa la Korintho.

Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote; 19 pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;

1 Wakorintho 14:2 Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake…..14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. 15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia.

Alikuwa anarejea katika kuomba sikuzote kwajili ya watakatifu kwa lugha.

Hivyo kila mwamini (kiongozi au mshirika) anapaswa kutumia muda wa kutosha katika maisha yake binafsi na hata katika makusanyiko ya maombi ya kanisa la mahali kuomba KILA WAKATI kwa ajili ya waamini wengine (viongozi na washirika) KWA LUGHA

Felician Makarios Phos
Kainos Creation Church (KCC)
0742107009


Address

Igoma Nyamagana
Mwanza
33000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kainos Creation Church - Felician Makarios Ministries posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share