BITA BLOG YA AFYA

BITA BLOG YA AFYA AFYA YA MWILI NA AKILI

Yajue matibabu yanayotolewa  kumsaidia mtu asipate maambukizi ya VVU baada ya  tendo la ndoa.Tuseme leo umeshiriki tendo...
28/06/2026

Yajue matibabu yanayotolewa kumsaidia mtu asipate maambukizi ya VVU baada ya tendo la ndoa.

Tuseme leo umeshiriki tendo la ndoa halafu kondom ikapasuka au ikachomoka au umebakwa unafanya nini baada ya hapo? Kwa sasa k**a umetokewa na hali mojawapo kati ya hizo kuna tiba ya kusaidia kupunguza uwezekano wa kupata maambukizi ya VVU. Tiba hiyo ndio inaitwa PEP. Kuna tiba nyingine inayoitwa PrEP hii pia inasaidia kuzuia maambukizi ya VVU lakini yenyewe inatumika kabla ya tendo la ndoa kwa watu ambao wako kwenye hatari ya kupata maambukizi mfano wafanyabiashara za ngono (hii tutakuwa na somo lake siku nyingine)

Twende kwenye PEP sasa;
PEP kirefu chake ni Post-exposure prophylaxis. Hii ni tiba ambayo inatolewa kwa mtu ambaye ameshiriki tendo la ndoa ama kwa hiyari au kwa kubakwa ili kumsaidia asipate maambukizi ya virusi vya UKIMWI. Tiba hii inatolewa iwapo kulikuwa na mgusano wa moja kwa moja wa uke na uume kwa mfano kondom ilipasuka au ilichomoka au mtu alibakwa.

Unaipataje PEP
Iwapo umetokewa na hali yoyote kati ya hizo ama kondom imechomoka au imepasuka au umebakwa, nenda kwenye kituo cha afya cha karibu kabla masaa 72 hayajaisha. Dawa hizi zinatolewa na daktari. Daktari atachukua maelezo yako kwa kina juu ya afya yako kwa ujumla. Baada ya hapo atakuambia ufanye vipimo vya HIV na hapo kutakuwa na mambo matatu:-

Kwanza; k**a hautakubali kufanya vipimo vya HIV utaambiwa uondoke na hautapewa dawa za PEP.

Pili; ukipima ukakutwa na maambukizi utapelekwa clinic za kawaida za watu wanaoishi na VVU ili wakuanzishie dawa.

Tatu; ukipima ukakutwa hauna maambukizi ndipo unapewa dawa za PEP ili zikusaidie usipate maambukizi iwapo mtu uliyefanya nae ngono alikuwa na maambukizi.

Dawa za PEP zinatumiwa kwa muda wa siku 28. Lakini iwapo umeanza dawa na mwenzako akawa tayari kupimwa na akapimwa akawa hana maambukizi basi daktari anaweza kukuachisha dawa.

Dawa hizi zinatolewa ndani ya masaa 72. Iwapo masaa 72 yamepita utashauriwa upime baada ya wiki 6 na k**a utakuwa umepata maambukizi utaanza dawa za ARV .

Ukimaliza PEP utarudia vipimo baada ya wiki 6 na baadae miezi mitatu. Iwapo utakuwa hauna maambukizi hautafuatiliwa tena iwapo utakuwa na maambukizi utaanza matibabu ya ARV k**a wagonjwa wengine.

Wakati wote unapotumia PEP usichangie damu(ndani ya miezi 12) na usishiriki tendo la ndoa bila kutumia kondom.

Lijue tatizo la mwili kuwasha baada ya kuoga...!Kuna wakati baadhi ya watu huwa inatokea akimaliza kuoga mwili unaanza k...
21/06/2026

Lijue tatizo la mwili kuwasha baada ya kuoga...!
Kuna wakati baadhi ya watu huwa inatokea akimaliza kuoga mwili unaanza kuwasha. Hii hali ya kuwashwa mwili baada ya kugusana na maji kwa kitaalam inaitwa aquagenic pruritus. Hali hii inaweza kusababishwa na mambo mbalimbali, wakati mwingine sababu haijulikani. Miongoni mwa magonjwa yanayoweza kusababisha hii hali ni ugonjwa ambao kwa kitaalam unaitwa Polycythaemia rubra vera. Mtu mwenye ugonjwa huu akipima anakuta damu iko juu sana zaidi ya gramu 16/dl. Watu wenye ugonjwa ukiacha mwili kuwasha baada ya kuoga wanaweza kuwa na dalili nyingine k**a vile kizungu zungu,kukosa utulivu, masikio kupiga ngoma na kujaa mwili. Matibabu ya ugonjwa huu yanaweza kuhusisha mgonjwa kutumia Aspirin na kutoa damu mara kwa mara...!

Wanasayansi wamegundua seli asilia (stem cells) kwenye ovari za mwanamke ambazo zinaweza kuzalisha mayai ya uzazi (oocyt...
21/06/2026

Wanasayansi wamegundua seli asilia (stem cells) kwenye ovari za mwanamke ambazo zinaweza kuzalisha mayai ya uzazi (oocytes) kwa wingi. Kwa kawaida, mwanamke huzaliwa akiwa na akiba ya mayai ambayo hupungua kadri anavyozeeka hadi kufikia ukomo wa hedhi (menopause), jambo linalopunguza uwezo wa kupata ujauzito.

Katika utafiti uliofanywa katika hospitali ya Massachusetts, Marekani, watafiti waliweza kutenganisha seli hizi maabara na kuzitumia kutengeneza mayai yenye uwezo wa kurutubishwa. Wataalamu wanaamini ugunduzi huu unaweza kuleta mapinduzi katika matibabu ya ugumba na kuongeza muda ambao wanawake wanaweza kupata ujauzito.

Kwa wale wanaojipima HIV nyumbani, endapo majibu yatakuwa positive, ni muhimu kwenda hospitali au kituo cha afya kilicho...
15/06/2026

Kwa wale wanaojipima HIV nyumbani, endapo majibu yatakuwa positive, ni muhimu kwenda hospitali au kituo cha afya kilicho karibu kwa vipimo vya uthibitisho. Usianze kuhitimisha moja kwa moja kuwa una maambukizi bila uthibitisho wa kitaalamu.

Pia, matokeo ya negative hayamaanishi kila wakati kwamba huna maambukizi ya HIV. Baada ya kupata maambukizi, kuna kipindi kinachoitwa "window period" ambapo vipimo vinaweza visiweze kugundua virusi mara moja. Kwa watu wengi, vipimo vya kisasa huanza kugundua maambukizi ndani ya wiki chache baada ya kuambukizwa, lakini muda unaweza kutofautiana kulingana na aina ya kipimo na hali ya mtu.

Katika mahusiano mapya, ni vyema kutumia kondomu mara kwa mara hata k**a vipimo vya HIV vimeonyesha negative. Hii ni kwa sababu kondomu husaidia kujikinga dhidi ya HIV na magonjwa mengine ya zinaa. Aidha, mtu anaweza kuwa katika kipindi ambacho maambukizi bado hayajagundulika na kipimo, lakini bado anaweza kuambukiza wengine.

Kipimo pekee kinaweza kutoa majibu kuwa una vidonda vya tumbo ni Oesophago-Gastro-Duodenoscopy (OGD) hii  imetengenezwa ...
14/06/2026

Kipimo pekee kinaweza kutoa majibu kuwa una vidonda vya tumbo ni Oesophago-Gastro-Duodenoscopy (OGD) hii imetengenezwa kwa mfumo wa camera ambayo inaweza kuingia hadi ndani ya mwanzo mwa utumbo mwembamba na kuchunguza k**a kuna vidonda.

14/06/2026

Kuna wakati dawa huponya mwili, na imani huponya moyo. Kila siku tunapovaa koti jeupe, tunakumbuka kuwa nyuma ya kila uchunguzi, tiba na ushauri, kuna tumaini ambalo mgonjwa analihitaji.

Tunaamini katika sayansi, lakini pia tunaamini katika nguvu ya sala, matumaini na huruma.

Address

Ubungo
Mwanza

Telephone

0621777644

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BITA BLOG YA AFYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share