VIWAWA JIMBO LA MUSOMA

VIWAWA JIMBO LA MUSOMA Viwawamusoma

TUMSIFU YESU KRISTO
HII NI KWA VIJANA WOTE VIJANA WENYE CHACHU YA UTUME VIJANA WAKATOLIKI
KAULI MBIU YETU NI
NENO LA MUNGU NI TAA YA MIGUU YANGU JUBILEI 2025 MAHUJAJI KATIKA MATUMAINI

03/04/2026

*Mambo 12 muhimu ya kutafakari leo katika mashtaka, mateso na hukumu ya kifo cha Yesu*"

1. *Mwamtafuta nani? Yesu Mnazareti- Ni Mimi*". Ujasiri wa kukiri na kujitambulisha wazi wazi hata kwa gharama ya maisha yetu. Je tuko tayari kukubali kuwa sisi ni Wakristo hata ikiwa tunatafutwa kuuawa au pengine tungekana k**a Petro, simjui mtu huyo, mimi si mkristo kabisa wala sijui kinachoendelea. "*Mkristo tambua cheo chako*
2. *"K**a mwanitafuta mimi waachieni hao waende zao*. Ujasiri wa kubeba msalaba peke yako bila kudai wengine au kutaka kufa na wengi wasio na hatia.
3. *"Rudisha Upanga alani kikombe alichonipa Baba sitokinywa*. Kukubali kuwajibika na kujitoa kwa ajili ya wengine bila kutafuta udhuru au kujihurumia. Mpokee mwenzio wa ndoa, watoto, wazazi, majirani na hata marafiki k**a dai la msingi la uwajibikaji na kujitoa sadaka kwa ajili yao.
4. *"Nimesema na watu waziwazi wala sikusema neno lolote kwa siri*. Je kuna tunayo yasema dhidi ya wenzetu kwa siri, masengenyo, fitina, majungu n.k
5. *"K**a nimesema vibaya, shuhudia ule ubaya, la sivyo kwanini wanipiga?* Wakati fulani kudai haki na uhuru wa kujitetea, usikubali kukaa kimya pale haki inapokurupushwa kwa kudhani ndiyo msamaha. Dunia huharabika pale watu wema wanapotambua kuwa ubaya unatendeka kisha wakakaa kimya na kuruhusu ubaya utamalaki
6. *"Wewe wasema kwa nafsi yako, au wengine wamekuambia habari zangu?* Tutoe nafasi ya kuwasikiliza watu na hata kuwafahamu kwa ukaribu na si kukurupuka na kutoa hukumu za mchongo.
7. "*Mimi nimekuja ili nishuhudie kweli na kila aliye wa kweli husikia sauti yangu*. Isivyo bahati dunia ya leo haitoi kabisa nafasi ya kutafuta, na kuujua ukweli na hata kushuhudia ukweli bali uongo na fitina vimechukua nafasi kubwa. Je unaamini katika kweli na kushuhudia kweli?
8. *"Wewe ungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu ungepewa toka juu,lakini ana dhambi kubwa zaidi aliyenitia mikononi mwako*. Je tunatumia vyeo, nafasi na vipato vyetu kuwanyanyasa wengine au ninakubali kitumiwa na wakubwa na matajiri kufanikisha uovu wao dhidi ya wengine?
9. "*Mama tazama mwanao, Mwana tazama mama yako*. Kumbuka hakuna mtu aishie kwa nafsi yake mwenyewe. Tunawajibika kwa wenzetu, tutambue utu wao, heshima yao, na mahitaji yao na tuwe tayari kuwasadia pale inapobidi
10. "*Naona Kiu*: Kiu ni dai au hamu ya jambo fulani muhimu au la lazima katika maisha. Nini kiu yako katika safari yako na hatima yake? Kukutana na Mungu au kuupata ulimwengu na fahari zake? Nafsi yangu inamuonea kiu Mungu, Mungu wangu aliye hai, k**a Ayala aoneavyao kiu nyua za maji, lini nitakapomuona Mungu? (Zab 42)
11."*Baba wasamehe kwa kuwa hawajui watendalo:* Msamaha ni tiba, kuachilia huponya maumivu, Upendo huvumilia yote, Upendo hauhesabu maovu, haulipi kisasi.
12. *"Yametimia*: Je natambua kuwa maisha ya hapa duniani yana mwisho, ninamalizaje safari hii? Mwisho wangu unanipa kibali cha kuishi na Mungu au yametimia katika upotofu na nimepoteza kila kitu. Itamfaidia nini mtu akiupata ulimwengu wote na kupata hasara ya nafsi yake?

Ndugu yenu
Padre Benedict Muk**a Luzangi

🎶 *Wimbo: Pasaka ya Kweli*✍️ Mtunzi: Emil Shayo🎹 Organist: George Rumala🎥 Audio & Video: G-MEC Pro🎬 Director: Nguku JrKa...
31/03/2026

🎶 *Wimbo: Pasaka ya Kweli*
✍️ Mtunzi: Emil Shayo
🎹 Organist: George Rumala
🎥 Audio & Video: G-MEC Pro
🎬 Director: Nguku Jr

Karibu tusikilize na kutafakari ujumbe wa Pasaka 🙏
Mungu akubariki unaposhare na wengine ❤️

🔗

Karibu tusikilize kwa pamoja wimbo huu mzuri PASAKA YA KWELI utunzi wake mwl EMIL SHAYO. Tunakumbushwa kuyaacha maovu yetu na kutenda yaliyo mema na kufanana...

UTARATIBU WA MKRISTO MKATOLIKI KANISANI👇👇👇🙋 Ninapoingia kanisani nachovya maji ya baraka na kusema"Unitakase Ee Bwana mi...
11/02/2026

UTARATIBU WA MKRISTO MKATOLIKI KANISANI👇👇👇

🙋 Ninapoingia kanisani nachovya maji ya baraka na kusema

"Unitakase Ee Bwana mimi na uovu wangu wote, ili nipate kustahili kushiriki ibada takatifu' Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu" Amina!

🙋Ninapiga goti huku nikisema
"Mungu wangu na Bwana wangu"

🙋Nikiinuka nasema

"Nitakusifu na kukuabudu katika Ekaristi takatifu"

🙋Naenda mpaka kwenye bench, napiga magoti au nakaa nikiwa mimeinamisha kichwa (k**a mabenchi yameisha nabaki nimejisimamia) huku nikitoa nia yangu ya kusali misa siku hiyo, mfano

"Ee Mungu, ninaungana nawe na jeshi lote la mbinguni, pamoja na Mama Bikira Maria, nikiwa na nia ya kumwombea mama yangu ambaye ni mgonjwa, jirani yangu ambaye mpaka sasa hatuelewani na pia familia yetu ambayo haina amani, Mungu kupitia misa hii rejesha hali ya mama yangu, rejesha uelewano na jirani yangu, na pia rejesha amani ya familia yetu pamoja na familia zote ambazo hazina amani"

🙋Ninaendelea na misa na Kushiriki litrujia kikamilifu

🙋Wakati wa komunyo nikikumbuka kuwa nina dhambi kubwa huwa nakominika kwa sala ya tamaa wala siendi mbele, huwa najikalia tu kwenye bench naangalia wenye moyo safi wanaenda mbele kumpokea Yesu (Kweli huwa najisikia wivu sana, itanibidi katikati ya wiki nifanye kitubio ili nisikae tena)"

🙋Mwisho wakati wa kuondoka nachovya maji ya baraka nikisema

"Unilinde Ee Mwenyezi Mungu, nikapate kuwa mfano katika jamii yangu, na nikushuhudie katika matendo yangu"
(Hapo nachovya maji ya baraka na kufanya ishara ya msalaba) "Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, amina"

Je, huwa tunafanya hivi wote?

JE IMANI AU MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI YANAPATIKANA KATIKA BIBLIA?

1) KUOMBEA MAREHEMU:

Tob 4:17

2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
2Fal 3:20-21
Hes. 21:8-9
K*t. 25:17-22
Kol. 1:20, 2:14
Yn. 12:32
Mt. 19:11-12

3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI K**A CHANZO CHA IMANI
2 The 2:15
2 Kor. 10:10-11
Yn 21-25
2 Yoh. 1:12
3 Yoh. 1:13

4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO).... Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
Ufu 1:10
Mdo 20:7
Mt 28:1-8
Lk. 24:1-7
Lk. 24:13ff
1 Kor. 16:1-2
Yn. 20:1-22

5) MAMLAKA YA PAPA K**A MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
Yn. 21:15-17
Mt 16:18-19
W 2:1-14

6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
Mwa 17:4
Yer. 7:7
Hes. 12:14
Yn. 6:49
Mt 23:30
Lk. 1:73

7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
Efe. 4:11-13
1Tim 5:17-25
1Tim 3:1-7,8-18

8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
Isa 35:8, 52:1
Zek 13:1-2
1Kor 3:15
Lk 12:47-48, 58-59
Ufu 21:27
Ebr 12:22-23
Ayu 14:13-17

9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
K*t 30:34-37
Hes 16:6-7
Law 16:12-13
Lk 1:10
Ufu 8:3

10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
Lk 1:28
Lk 1:42

11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
2Fal 2:19-22
Yn 5:1-18
Yn 7:37
Hes 19:1-22

12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
Mit 15:8, 15:29
Ayu 42:8
Yak 5:16
Mt 16:19

13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
2Fal 13:20-21

14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
Mt 16:19,1-20
Yak 5:15-16

15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
Mdo 16:15-33
Mdo 18:8
Mt 28:19
Mdo 10:47-48

16) KUSIMIKWA KWA UTUME
K*t 28:4-43

17) RANGI ZA KANISA
K*t 27:9-29

18) MATUMIZI YA MISHUMAA
K*t 25:31-40; 27:20-21
Hes 8:1-4

19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
K*t 30:22-32

20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
Yak 5:14-15

Roho wa Bwana awe nawe.

Fuatilia kituo cha KILINGENI kwenye WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029VbBK1DyAInPleGrQw71X

Follow KILINGENI's WhatsApp Channel. Kituo hiki kimeundwa mahususi kukuletea taarifa sahihi na za haraka kuhusu Soka, Teknolojia, Biashara, Habari za Kimataifa]. Lengo letu ni kukupa maarifa, habari, na vidokezo muhimu moja kwa moja kwenye simu yako. Jiunge nasi na uwe wa kwanza kujua kinachoendelea!. Join 150 followers for the latest updates.

Mhashamu Almachius Vincent Rweyongeza, Askofu wa Jimbo Katoliki la Kayanga, ametoa onyo kali dhidi ya kile alichokiita "...
10/02/2026

Mhashamu Almachius Vincent Rweyongeza, Askofu wa Jimbo Katoliki la Kayanga, ametoa onyo kali dhidi ya kile alichokiita "ujinga na maigizo" ya baadhi ya viongozi wanaojaribu kuingiza siasa ndani ya Kanisa Katoliki.

Akizungumza kwa ukali kuhusu taratibu za kikanisa, Askofu Rweyongeza amewashangaa watu wanaoruka ngazi za uongozi na kwenda kumshtaki Askofu au Baraza la Maaskofu moja kwa moja kwa Baba Mtakatifu (Papa) bila kufuata utaratibu.

Askofu ameeleza kuwa Kanisa lina mifumo madhubuti ya kisheria na kikanisa ambayo haiongozwi kwa kukurupuka au shinikizo la kisiasa. Amebainisha kuwa Kanisa Katoliki ni taasisi kongwe ambayo imehimili dhoruba za kihistoria kwa zaidi ya miaka elfu mbili, na hakuna jitihada za kibinadamu zinazoweza kuliangusha.

Fuatilia kituo cha KILINGENI kwenye WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029VbBK1DyAInPleGrQw71X

https://youtu.be/56EZR_ILgS4?feature=shared

Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

💥🔥🔥🔥NEW RELEASE🔥🔥🔥💥📰WIMBO: NI NANI ANGESIMAMA?📰WAIMBAJI: G-MEC - MUSOMA📰MTUNZI; P.S.MAISA📰AUDIO: INNO PRODUCTION 📰DIRECT...
01/02/2026

💥🔥🔥🔥NEW RELEASE🔥🔥🔥💥
📰WIMBO: NI NANI ANGESIMAMA?
📰WAIMBAJI: G-MEC - MUSOMA
📰MTUNZI; P.S.MAISA
📰AUDIO: INNO PRODUCTION
📰DIRECTOR: NGUKU JR
📰ORGANIST: GEORGE LUMALA
Please kindly Subscribe, like, comment and share.
Tafakari njema iwafikie wote

Wimbo huu unatupa tafakari ya kina zaidi na kutukumbusha kuwa Mungu yuu nasi wakati wote. Karibu tutafakari kwa pamoja katika wimbo huu.

KUMBUKUMBU YA MIAKA 18 TANGU KUWEKWA WAKFU KATIKA DARAJA YA UASKOFU - ASKOFU MICHAEL GEORGE MSONGANZILA▪ ︎Karibu umtakie...
20/01/2026

KUMBUKUMBU YA MIAKA 18 TANGU KUWEKWA WAKFU KATIKA DARAJA YA UASKOFU - ASKOFU MICHAEL GEORGE MSONGANZILA

▪ ︎Karibu umtakie neno la Baraka na matashi mema Mhashamu Michael George Msonganzila, Askofu wa Jimbo Katoliki Musoma, leo hii anafanya Kumbukumbu ya Miaka 18 tangu alipowekwa wakfu katika Daraja Takatifu ya Uaskofu.

Tuungane na Mchungaji Mkuu wa Jimbo Katoliki la Musoma, Askofu Michael Msonganzila, leo anapofanya kumbukumbu ya miaka 4...
02/12/2025

Tuungane na Mchungaji Mkuu wa Jimbo Katoliki la Musoma, Askofu Michael Msonganzila, leo anapofanya kumbukumbu ya miaka 41 ya tangu alipopadrishwa, tarehe 02 Disemba 1984

Tumwombe Mungu amjalie, afya njema na utume mwema.

24/11/2025

Historia ya Kanisa Katoliki Kabla na Baada ya Kristo (muhtasari)

1. Kabla ya Kristo:
Kanisa Katoliki halikuwepo k**a taasisi, lakini lina mizizi katika Agano la kale Imani ya Kiyahudi, ambayo ilimngojea Masiya.
Mungu aliingia agano na Abrahamu (Mwanzo 12), Musa (K*toka), na manabii walitoa ujumbe wa toba na tumaini.
Hekalu la Yerusalemu lilikuwa kitovu cha ibada.
Hii ndiyo ilikuwa maandalizi ya ujio wa Kristo.

2. Maisha ya Yesu Kristo (miaka 0–33 BK):
Yesu alizaliwa, akaishi, akahubiri habari za ufalme wa Mungu, akasulubiwa na kufufuka.

Aliteua mitume 12, akisema: “Jenga kanisa langu juu ya mwamba huu”(Mathayo 16:18).
Yesu ndiye msingi wa Kanisa Katoliki.

3. Baada ya Kristo:
Karne ya 1–4: Mitume walieneza injili. Mtume Petro (aliyekuwa papa wa kwanza) alihubiri Roma. Kanisa likakua licha ya mateso ya Warumi.

313 BK: Mfalme Constantine aliruhusu Ukristo, na Kanisa likaanza kuimarika rasmi.

325 BK: Mtaguso wa Nisea ulifafanua imani ya Kanisa (mfano: “Nasadiki kwa Mungu mmoja…”).

Karne ya 5–15:Kanisa lilikuwa kiini cha maisha ya kijamii na kisiasa Ulaya.

1054 BK: Mgawanyiko mkubwa (Schism) — Kanisa Katoliki (Magharibi) na Orthodox (Mashariki).- *1517 BK:* Marekebisho ya Luther Kanisa la Kiprotestanti likazaliwa.

1962–65:Mtaguso wa pili wa Vatikano ulileta mageuzi makubwa, ikiwemo misa kufanyika kwa lugha za watu.


Kanisa Katoliki linaongozwa na Papa (sasa Leo XIV), lina mamilioni ya waumini duniani, na linaendelea na utume wa kueneza injili, kutoa huduma na kuhubiri upendo.

Fuatilia kituo cha KILINGENI kwenye WhatsApp:

WAKRISTO MSHUKURUNI MWENYEZI MUNGU KWA ZAWADI YA IMANIWakristo Jimbo Kuu Katoliki Dodoma wamekumbushwa kumshukuru Mungu ...
10/08/2025

WAKRISTO MSHUKURUNI MWENYEZI MUNGU KWA ZAWADI YA IMANI

Wakristo Jimbo Kuu Katoliki Dodoma wamekumbushwa kumshukuru Mungu kwa zawadi ya Imani. Wito huo umetolewa leo Agosti 10, 2025 na Mhashamu Wilbroad Henry Kibozi, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu, Dominika ya 19 ya Mwaka C wa Kanisa katika Parokia ya Watakatifu Mashahidi wa Uganda Lumuma, Jimbo Kuu Katoliki Dodoma iliyoambatana na utolewaji wa Sakramenti ya Kipaimara.

Askofu Kibozi amewasistiza waamini kumuamini Mungu kila wakati kwa sababu hutenda miujiza kwa kila anayemwamini ambapo amemtaka kila Mkristo kuona umuhimu wa kumshukuru Mungu kwa zawadi hiyo ya Imani.

Pia amewataka waamini wa Parokia ya Lumuma kuithibitisha imani yao kwa majitoleo yao katika Kanisa ambapo amewasistaza kushiriki kikamilifu kumtolea Mungu moja ya kumi ya mpatao yao Kwani hiyo ni amri ya Mungu mwenyewe katika Maandiko Matakatifu. Akiendelea na Homilia yake pia amewataka wazazi na watoto wote kushiriki kikamilifu mikutano ya Jumuiya kwani kila wawili wakusanyikapo na Mungu anakuwepo kati yao.

Kwenye Adhimisho hilo la Ekaristi Takatifu Wakristo wapatao Mia mbili na nane (208) kutoka Vigango kumi na mbili (12) vya Parokia hiyo wamepokea Sakramenti ya Kipaimara na Wakristo wawili (2) wamepokea Sakramenti ya Ekaristi Takatifu kwa mara ya kwanza.

Akihitimisha Homilia yake Askofu Kibozi amewahimiza Waamini wote kuendelea kujiimarisha zaidi kiimani kwa kushiriki kikamilifu Sala kwenye Mikutano ya Jumuiya, kupitia na kuisoma Katekisimu Katoliki na kitabu cha Mwelekeo wa Jimbo kinachotoa mwongozo wa masuala yote ya imani ya kanisa Katoliki hasa zaidi kwa wanaostahili kupokea Sakramenti Takatifu za Kanisa.

Na Geofrey Rweyunga, Radio Maria Tanzania (Dodoma)
www.radiomaria.co.tz




LEO JULAI 28, TUNAYAKUMBUKA MAISHA YA MTAKATIFU SAMSONI WA DOLI, ASKOFU (565)Taarifa ya utoto wa Mtakatifu huyu ni k**a ...
28/07/2025

LEO JULAI 28, TUNAYAKUMBUKA MAISHA YA MTAKATIFU SAMSONI WA DOLI, ASKOFU (565)

Taarifa ya utoto wa Mtakatifu huyu ni k**a ya watu wengine walio wengi.
Alizaliwa mwaka 485 nchini Wales (Uingereza).
Wazazi wake walimpeleka kwa Wamonaki akiwa na umri wa miaka mitano tu.
Waliamua kufanya hivyo k**a tendo la shukrani kwa mwenyezi Mungu kwa kuwa mama yake alimzaa baada ya kuwa tasa muda mrefu.

Alijiunga na Utawa akapewa Upadre, baada ya muda Abate alimruhusu kuhamia Monasteri ndogo iliyokuwa imejengwa katika kisiwa fulani apate kuishi zaidi maisha ya Sala na mwungamo wa kiroho na Mungu.
Abate wa Monasteri hiyo ndogo alipokufa, Padre Samsoni alichaguliwa kushika nafasi yake.

Japo alikuwa anaishi k**a mkaa pweke hata hivyo alikuwa na mamlaka sana juu ya Wamonaki wake na hatua kwa hatua aliwaongoza kukua katika nidhamu ya Kiroho na maisha ya Sala.
Baada ya kujitahidi hivyo kwa muda alijiuzulu na pamoja na Wamonaki watatu akaenda kuishi upwekeni kabisa.

Lakini hali hii tulivu haikudumu muda mrefu kwa sababu Wamonaki wa Monasteri nyingine walimwita awe Abate wao.
Hapa muda mfupi tu baadaye aliambiwa katika njozi kwamba alikuwa akihitajiwa katika nchi nyingine.
Basi akawekwa wakfu k**a Askofu na pamoja na kundi dogo la Wamonaki akapanda mashua akaelekea kwanza sehemu ya kusini kabisa ya Uingereza iitwayo Kornwali.
Askofu Samsoni akawa mjenga Makanisa na mhubiri hodari.
Toka hapo akapanda chomboni tena akaelekea Mlangobahari wa Uingereza, akatelemka pwani ya Ufaransa sehumu iitwayo Bretanye na mji wa Doli ukawa ndiyo makao yake.

Tangu hapo Askofu Samsoni alizidi kuwa Mchungaji stadi.
Toka Doli alienda kila upande kuhubiri Injili kujenga Makanisa na Monasteri na ionekanavyo alifanya miujiza mingi.
Mwishowe akiwa amedhoofishwa kabisa kwa shughuli zake nyingi za Kimisionari alifariki dunia kitulivu sana kati ya Wamonaki wake akiwa na umri wa miaka themanini.

Huo ulikuwa mwaka 565 hivi, Mtakatifu Askofu Samsoni wa Doli ni mmojawapo wa Maaskofu Wamisionari wa Kiingereza wa Karne ya sita wenye maana sana katika historia ya Kanisa nchini Ufaransa kwa ajili ya bidii zake za kuihubiri habari njema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

MTAKATIFU SAMSONI WA DOLI ASKOFU, UTUOMBEE.

Address

Mwembeni
Musoma
P.BOX.62

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when VIWAWA JIMBO LA MUSOMA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to VIWAWA JIMBO LA MUSOMA:

Share