PEFA Karansi Church

PEFA Karansi Church Mathayo 28:19 Basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi

Somo la 1: Mafundisho Ya Maandiko Matakatifu Kuhusu Maandiko YenyeweUtangulizi:Biblia nzima huitwa “Maandiko Matakatifu”...
23/05/2026

Somo la 1: Mafundisho Ya Maandiko Matakatifu Kuhusu Maandiko Yenyewe

Utangulizi:

Biblia nzima huitwa “Maandiko Matakatifu”, yaani Neno la Mungu pekee linalotoa habari za Mungu kwa ulimwengu. Tunasoma kwamba “Maandiko Matakatifu yote ni pumzi ya Mungu” (2 Timotheo 3:16). Maana yake ni kwamba Mungu aliwaongoza watu ambao waliyaandika. Maandiko Matakatifu yameandikwa katika vitabu 66. Vitabu 39 ni Agano la Kale, na 27 ni Agano Jipya. Bwana Yesu Kristo alisema:

“Maandiko (Matakatifu) hayawezi kutanguka,” (Yohana 10:35) kwa hiyo tuyafuate kwa moyo wote yaliyoandikwa k**a alivyofanya Yeye. Biblia ni kitabu chenye ukweli, miujiza, unabii na mashairi; tena ni kitabu chenye maadili na mafundisho ya kiroho. Watu wengi, tangu zamani na mpaka leo, wameichukia Biblia na kujaribu kuiharibu, lakini wameshindwa kwa sababu “Neno la Bwana hudumu hata milele” (1 Petro 1:25).

Agano La Kale:

Kitabu cha “Mwanzo”, ambacho ndicho cha kwanza katika Biblia, hutufunulia mwanzo wa vitu vyote, isipokuwa mwanzo wa Mungu peke yake, ambaye hana mwanzo wala mwisho. Mwanzo wa ulimwengu, maisha, watu, dhambi, wokovu, ndoa, jumuiya, mataifa, mashairi, nyimbo, maarifa, na mwanzo wa kila kitu tukijuacho, umefunuliwa katika kitabu hiki cha ajabu.

Vitabu 16 vinavyofuata, kuanzia kitabu cha “Kutoka” mpaka “Esta”, hueleza kikamilifu juu ya Waisraeli. Vitabu 5 kuanzia “Ayubu” mpaka “Wimbo Ulio Bora” vimejaa mashairi na nyimbo. Vitabu 17 vinavyobakia tangu “Isaya” mpaka “Malaki” vimejaa habari za Mungu kwa Waisraeli; na unabii wa nyakati zijazo. Agano la kale huungana na Agano Jipya katika kutimizwa kwa unabii huo.

Agano Jipya:

Agano Jipya limegawanyika katika sehemu kuu nne: “Injili”, “Matendo ya Mitume”, “Nyaraka” ishirini na moja, na “Ufunuo”.

Injili nne hueleza habari za maisha, kifo, kufufuka na kupaa kwake Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. Matendo ya Mitume hueleza habari za Wakristo wa kwanza. Nyaraka hutoa mafundisho kwa ushuhuda za maisha ya Kikristo, na Ufunuo hutupatia upeo wa mambo yatakayotokea ulimwenguni, mbinguni na katika jehanum kwa nyakati zijazo.

Mwisho:

Biblia ni “taa ya miguu yetu na mwanga wa njia zetu.” (Zaburi 119:105)

Biblia ni “k**a nyundo ivunjayo mawe vipande vipande” (Yeremia 23:29).

Ni “neno lenye uzima”. (1 Petro 1:23) na “upanga ukatao kuwili” (Waebrania 4:12).

Kwa hiyo tuiokee na kuamini kuwa ni Neno la Mungu pekee na tujifunze neno hilo kwa ajili ya maisha yetu.

12/04/2026

Praise and worship at PEFA KARANSI

05/04/2026
We had a great Easter Sunday many people gave their live to Christ
05/04/2026

We had a great Easter Sunday many people gave their live to Christ

22/02/2026

Praise and worship

Nafasi za Kazi
31/12/2025

Nafasi za Kazi

We had a great service in our church.
17/11/2025

We had a great service in our church.

09/11/2025

Address

S. L. P 98, Sanya Juu-Siha
Moshi
25403

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when PEFA Karansi Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category