ELCT Northern Diocese

ELCT Northern Diocese The ELCT - Northern Diocese has estimated membership strength of over 350,000 members. It has 164 parishes and over 300 pastors.

Mhe. Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo ameongoza ibada ya Jumapili Usharika wa Sawe iliyokuwa na matendo mbalimbali leo ta...
31/01/2021

Mhe. Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo ameongoza ibada ya Jumapili Usharika wa Sawe iliyokuwa na matendo mbalimbali leo tarehe 31.01.2021.

Kwanza alizindua shamba la miparachichi ambalo kwa mujibu wa risala iliyosomwa na Kiongozi wa Usharika Mch. Joseph Loti Shango lina ekari 3 na miti ya miparachichi zaidi ya 300.

Pili alifanya sala ya kuhamisha madhahabu ya kanisa la zamani ili kupisha ujenzi wa kanisa jipya.

Tatu aliweka wakfu kiti cha madhabahuni akaliacho kiongozi wa ibada.

Nne alihubiri Neno la Mungu toka Efe. 2:8-10 akisisitiza mambo yafuatayo:

Kwamba, neema ni kitu ambacho mtu anapewa bure bila kukitumikia, bila kukilipia na kinachompa nguvu ili asihangaike kujitafutia wokovu.

"Uhai tulionao, hewa tunayovuta, familia tuliyo nayo, na maendeleo tuliyo nayo tunawezeshwa na Mungu kwa neema yake tu sio kwa nguvu ama akili zetu. Hivyo, tuone umuhimu wa kumshukuru Mungu." Alisisitiza.

Wapo wanaoanza kazi lakini wasione matunda, wasifurahie matunda ya kazi yao. Yote inakuwa ubatili tu.

Tunapoanza kazi, kuona matunda, na kuyafurahia ni kwa Neema ya Mungu tu.

Neno linaeleza kuhusu wokovu tuliopata toka dhambi, mauti, laana, ufalme wa giza ama shetani, na toka hukumu ya milele ni kwa nguvu ya Mungu tu.

Tunapokea wokovu kwa njia ya imani kwa Yesu Kristo tu katika kumwendea kwa toba na kuamini kuwa kazi yake msalabani tunapokea wokovu.

Na hata kumwamini Yesu tunajaliwa na Mungu mwenyewe. Hatuna cho chote tunachoweza kuweka ili kupata wokovu.

Ni kweli kwamba hakuna wokovu kwa mwingine wala kingine ila kwa Yesu tu. Hivyo, asije mtu akajiisifu. Tunajenga kanisa, tunapiga tarambeta, na mambo mbalimbali, asije mtu akajisifu. Tunachotoa ni kumrudishia Mungu shukrani.

Waliopata wokovu, Wakristo, wanajua kumtegemea na kumtumikia Mungu kwa furaha.

Na hatupaswi kuwahukumu wengine bali tuwaombee na kumzalia Mungu matunda mema kwa kutumia vipawa tulivyojaliwa kufanya kazi ya Mungu, kutenda mema kwa jirani, shughuli za maendeleo ya jamii na kutunza uumbaji wa Mungu.

Tumeokolewa ili kutenda matendo mema, bali hatuokolewi kwa matendo hayo mema.

Alihitimisha kwa kupongeza washarika wa Sawe kwa kazi kubwa ya ujenzi wa kanisa jipya unaoendelea. Kazi hiyo ikiwa ni itikio lao la wokovu walioupata kwa neema tu. Ni kibali cha pekee ambacho sio vizazi vyote vinapata bahati hiyo.

Aliwaasa watu wote kuwa tunapita nyakati ambazo ni ngumu. Tusihofu kuendelea na kazi zetu, bali tuendelee kuomba na kuchukua tahadhari dhidi ya COVID-19.

Tano aliongoza harambee ya ujenzi wa kanisa jipya ambapo zilipatikana zaidi ya Tzs 62Milioni.

Mbali ya harambee hiyo ilitolewa shukrani maalumu ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya harambee iliyopita hadi kufikia harambee hii nyingine ya ujenzi wa kanisa jipya.

Mwenyekiti wa jengo alitoa taarifa kuwa awali makisio ya ujenzi yalikuwa Tzs 300Milioni bali kwa kupanda kwa gharama mpaka sasa zimeshatumika Tzs 700M. Aidha, lengo la harambee hii leo ni kupata Tzs 100M kuendeleza kazi ya ujenzi huo.

Ibada ilihudhuriwa na Wana Sawe toka maeneo mbalimbali nchini na ilianza saa 4:00 asubuhi na kumalizika saa 11:45 jioni. Hizi ni baadhi ya picha za matukio hayo.

Jana tare 3 Januari 2021 ilikuwa siku ya kustaafishwa rasmi kwa Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mch. El...
04/01/2021

Jana tare 3 Januari 2021 ilikuwa siku ya kustaafishwa rasmi kwa Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mch. Elingaya Agostino Saria. Tendo hilo liliongozwa na Mhe Baba Askofu Dkt Fredrick Onael Shoo, Mkuu wa KKKT na Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini kwenye Kanisa Kuu la Usharika wa Moshi Mjini.
Msaidizi wa Askofu Mch. Saria amestaafishwa baada ya kulitumikia Kanisa kwa miaka 40 katika nafasi tofauti. Alitumika kana Mchungaji katika sharika mbali mbali za Dayosisi baadae k**a Mkuu wa Jimbo la Kilimanjaro Kati na hatimae k**a Msaidizi wa Askofu. Alikuwa Msaidizi wa Askofu kwa miaka sita kuanzia 2014 hadi 2020.
Alikuwa Mchungaji aliyeeneza Neno la Mungu katika sharika nyingi za Dayosisi ya Kaskazini, misioni ya Mpanda na Sumbawanga na hatimae maeneo ya Misionil katika Dayosisi ya Dodoma.
Aliyechukua nafasi ya Msaidizi wa Askofu Mch. Saria ni Mchungaji Deogratious Msanya aliyeingizwa Kazini rasmi tarehe 22 Novemba 2020.
Tunamshukuru Mungu kuwa ilikuwa ibada yenye utukufu wake iliyohudhuriwa na takriban 1500. Baadhi ya picha za matukio zinafuata hapa chini.

Jana tarehe 28/12/2020 ilikuwa siku ya Askofu na WanaDayosisi wa Dayosisi ya Kaskazini wanaoishi kwenye mikoa mingine. U...
29/12/2020

Jana tarehe 28/12/2020 ilikuwa siku ya Askofu na WanaDayosisi wa Dayosisi ya Kaskazini wanaoishi kwenye mikoa mingine. Utamaduni huu umekuwa ukifanyika kwa takriban miaka 27 sasa. Mahudhurio ya jana yalikuwa takriban watu 530. Mhe Baba Askofu alitoa taarifa ya maendeleo ya Dayosisi na mipango ya miaka ijayo. Aidha Askofu aliwashukuru sana Wanadayosisi kwa michango yao ya Mali na mawazo ya kuendeleza jamii na Kanisa la Bwana. Kwa mara ya kwanza kikao hicho kilifanyika kwenye Makao makuu ya Chuo chetu Cha Stefano Moshi Memorial University College (SMMUCo) kinachojengwa Makuru, Machame. Zifuatazo ni picha za matukio hayo ya jana.

Picha ya pamoja ya Uongozi wa Dayosisi ya Kaskazini, Baba Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini na Mkuu wa KKKT Dkt. Fred...
19/12/2020

Picha ya pamoja ya Uongozi wa Dayosisi ya Kaskazini, Baba Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini na Mkuu wa KKKT Dkt. Fredrick O. Shoo, Katibu Mkuu Bw. Arthur N. Shoo na Mtunza Hazina Bw. Munguatosha Makyao katika mkutano wa pamoja na Wataalam wa kilimo wa mradi wa Climate Smart, wasaidizi wao, waratibu, viongozi wa DIRVA na viongozi wa clusters za wakulima...leo tarehe 19/12/2020 Uhuru Hotel Moshi. Miradi hiyo ipo chini ya ufadhali wa Norwegian Church Aid (NCA).

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Fredrick Shoo amewataka viongozi na waumini wa kanisa hilo k...
23/11/2020

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Fredrick Shoo amewataka viongozi na waumini wa kanisa hilo kumtegemea Mungu bila kuingiza mambo ya kidunia pindi wanapokutana na changamoto za kimaisha.

Dk Shoo, ambaye pia ni Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa hilo, ametoa wito huo jana tarehe 22 Novemba 2020, katika usharika wa Moshi Mjini, wakati akihubiri kwenye ibada maalumu ya kumuingiza kazini Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi hiyo, Mchungaji Deogratius Msanya pamoja na kubariki wachungaji watano.

Mchungaji Msanya ambaye anakuwa msaidizi wa saba wa Askofu katika Dayosisi ya Kaskazini, alichaguliwa Tarehe 18 Agosti 2020 kwenye mkutano mkuu wa 36 wa dayosisi.

Askofu Shoo amesema kunahitajika uhodari mkubwa, umakini, moyo mkuu na kuondokana na woga, katika kuwatumikia watu wa Mungu, kwa kuwa Mungu aliyewaita watu wake, huonyesha njia ya namna ya kutumika na kulifikia kusudi.

Amesema katika dunia zipo changamoto nyingi, ikiwemo za Kiuchumi, kifamilia na hata za kiimani lakini k**a viongozi walioitwa kuliongoza taifa la Mungu, wanapaswa kumtazama aliyewaita, ambaye ana majibu ya changamoto hizo.

"Msitishwe na changamoto za dunia hii, k**a za kiuchimi, kifamilia na hata za kiimani, tambueni yupo Mungu na mtakapomtegemea na kumuita, atawawezesha kuzivuka changamoto zote," amesema Askofu Shoo.

Aliongeza kuwa "Tumtegemee Mungu bila kuweka mchanganyo, maana wapo watu wakiwa kanisani anamkiri Yesu Kristo, akitoka anakwenda kutafuta mchanganyo mwingine. Tutubu na kumtazama Mungu maana hashindwi na jambo lolote".

Askofu Shoo amemtia moyo Mchungaji Msanya na kumsihi asiogope wala kufadhaika kutokana na wajibu aliokabidhiwa, badala yake amtegemee Mungu aliyemuita katika wajibu huo.

"Uwe hodari na moyo wa ushujaa, usiogope wala usifadhaike, kwa kuwa Bwana Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako, na fahamu hukuitwa na mtu bali Mungu mwenyewe na katika yeye utayaweza mambo yote"

Ibada hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Dini na Serikali, akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira. Zifuatazo ni baadhi ya picha za tukio hilo.

Jana tarehe 15 Novemba 2020 ilikuwa siku ya furaha na Shangwe kwa Usharika wa Lawate. Usharika huo ulihamia Kanisa jipya...
16/11/2020

Jana tarehe 15 Novemba 2020 ilikuwa siku ya furaha na Shangwe kwa Usharika wa Lawate. Usharika huo ulihamia Kanisa jipya na la kisasa lililojengwa kuanzia 2008. Aliye weka wakfu jengo hilo la Kanisa alikuwa Mhe. Baba Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo.

Usharika wa Lawate upo Jimbo la Siha kwenye Dayosisi yetu. Ni Usharika wenye wakristo 804. Ujenzi wa jengo hilo uligharimu Tsh 419,500,000/=. Picha zifuatazo inaonyesha baadhi ya matukio ya sherehe hiyo.

15/10/2020
The ELCT Northern Diocese constitution stipulates that the Diocese shall hold a General Assembly (Synod) every two years...
21/08/2020

The ELCT Northern Diocese constitution stipulates that the Diocese shall hold a General Assembly (Synod) every two years. This years’ Synod was held on 18th August 2020 at Uhuru Hotel and Conference Center, Moshi. The unique thing about this Assembly was that it was held for one day instead of three days as it was done in the past. Key issues discussed were the implementation of the goals set in the 2018 assembly and plans for the coming two years. All matters were well presented and discussed in the plenary and in groups and feedback given to the assembly.

The assembly was attended by 408 participants among them were 345 voting members. We also had leaders from other ELCT Dioceses and the Catholic Diocese. The retired Bishops and other senior retired officers of the Diocese. The chairperson of the meeting was Bishop Dr. Fredrick Onael Shoo the Bishop of the ELCT Northern Diocese and the Presiding Bishop of the Church.

Among other issues discussed in the Synod was election of Dean (Assistant to the Bishop). The current Dean Rev. Elingaya Saria finished his term of office in this assembly. The Dean Elect is Rev. Deogratius John Msanya. Please let us pray for him as he takes over this important position. Also pray for the entire leadership of the diocese and of the Church. It was a very successful meeting full of God's spirt.

Below are some of the photos of the participants.

On Wednesday 8th July 2020 ELCT Northern Diocese was visited by the new NCA Country Director Madam Pauliina Parhiala. Sh...
11/07/2020

On Wednesday 8th July 2020 ELCT Northern Diocese was visited by the new NCA Country Director Madam Pauliina Parhiala. She was on tour to familiarize herself with the NCA Tanzania partners and activities. In the tour she was accompanied by NCA Tanzania senior staff.

At ELCT Northern Diocese she was received by Rt. Rev. Dr. Fredrick Shoo the Presiding Bishop of ELCT and the Diocesan Bishop accompanied by other senior leaders of the Diocese.

Welcome to Tanzania Madam Pauliina.

Jana tarehe 7 Julai 2020 Mhe. Baba Askofu Dkt Fredrick Shoo, Mkuu wa Kanisa (KKKT) na Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini alif...
08/07/2020

Jana tarehe 7 Julai 2020 Mhe. Baba Askofu Dkt Fredrick Shoo, Mkuu wa Kanisa (KKKT) na Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini alifungua semina ya viongozi wa dini mbalimbali (Interfaith) Uhuru Hotel. Semina hiyo iliangazia kutunza umoja wa dini ambapo kazi kubwa ni kuelimisha waumini kuwa na hofu ya Mungu na mambo mtambuka km Afya, maendeleo endelevu nk. Pili, Nafasi ya Viongozi wa Dini kuelekea Uchaguzi ujao katika kutunza amani na utulivu kwa Taifa. Tatu, Namna ya kukabiliana na mazingira mapya ya changamoto za virusi vya corona.
Viongozi wa dini waliohudhuria semina hiyo walikuwa wawakilishi wa Waislamu (Bakwata) Wakatoliki, Walutheri, Wapentekoste na Waangilikana. Semina hiyo iliratibishwa na Mch. Andrew Munisi Katibu wa Uwakili Dayosisi ya Kaskazini. Tunashukuru sana ndugu zetu wa NCA kwa kuwezesha Semina hiyo.

Jana Juni 21, 2020 ilikuwa siku ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). KKKT ilitimiza miaka 57.Mheshimiwa B...
22/06/2020

Jana Juni 21, 2020 ilikuwa siku ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). KKKT ilitimiza miaka 57.
Mheshimiwa Baba Askofu Dkt. Fredrick Shoo Mkuu wa Kanisa na Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini aliongoza ibada ya kukumbuka siku hiyo kwenye shule ya Sekondari ya Wasichana ya Masama Jimbo la Hai. Mahubiri yake yaliongozwa na neno kutoka Injili ya Yohana 17: 20-21 “Wote wewe na Umoja”
Katika mahubiri yake alisema kuwa KKKT ilizaliwa mwaka 1963 kutokana na makanisa ya Kilutheri 7 yaliyokuwepo Tanzania wakati huo. Baada ya Uhuru (1961) viongozi wa Makanisa hayo wakiongozwa na Roho Mtakatifu waliungana na kuwa Kanisa moja - KKKT. Wakati huo waumini wa Kanisa walikuwa 500,000 leo hii tupo zaidi ya milioni 8, Dayosisi 26 na maeneo mawili ya misioni.
Kanisa hili limeendelea kuhubiri Injili, kutunza watu kimwili - kutoa elimu, afya na udaikonia. Kanisa limeingia vizuri sana kutoa huduma kwa walemavu na wanaopatwa na majanga. Kanisa limeweza kufanya hayo kutokana na Umoja uliopo. Umoja huu unatanguliwa na neno moja “kukaa Ndani ya Yesu Kristo aliye Bwana wa Kanisa. Pasipo na Umoja baraka za mbinguni zinafungwa. Tuendelee kumwomba Bwana Yesu Kristo aimarishe Umoja wa Kanisa letu, Dayosisi zetu na vituo vyetu. Umoja uliojengwa ndani ya pendo la Yesu Kristo.
Ibada hiyo ilitanguliwa na tendo la kuzindua Bweni la wanafunzi. Aidha wanafunzi wa kidato cha sita walikabidhiwa vyeti vya kuhitimu masomo yao shuleni hapo. Baadhi ya picha za matukio ziko hapa.

ELCT Northern Diocese this afternoon (4 June 2020) distributed eleven motorcycles to the ELCT ND / NCA field workers. Th...
04/06/2020

ELCT Northern Diocese this afternoon (4 June 2020) distributed eleven motorcycles to the ELCT ND / NCA field workers. The motorcycles are essential tools to increase efficiency of these workers in the field given their wide geographical area they cover. These field officers work with people at grassroots to build their capacity in vegetable production, IRVicoba, poultry, paralegal awareness and interfaith issues. We are grateful to Norwegian Church Aid (NCA Tanzania) for funding this project to improve the well-being of our people. The following are some of the photo taken during the handover of the motorcycles.

Address

Market Street
Moshi

Telephone

+255272754359

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELCT Northern Diocese posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share