01/07/2023
Yes...Mungu ni mwaminifu sana kwetu, tunamshukuru sana Mungu kwa kutuwezesha kufanikisha mkesha wa vijana, uliongozwa na Mch. Godwin Mselle-Mchungaji Kiongozi Usharika wa Sanya juu.
Na wakufunzi wetu walikuwa ni Mwl. Frank Mdoe kutoka Arusha pamoja na Mwl. Atukuzwe Mmari kutoka Bomang'ombe.
Mada ilikuwa ni: Kijana Mkristo na malengo ya maisha, katika maeneo ya kiroho, kielimu, kijamii na kiuchumi.
Maombi na maombezi yalifanyika. Mungu awabariki sana.