Good News Centre

Good News Centre Mark 16:15 Then he said, "Go into the world. Go everywhere and announce the Message of God's good news to one and all.

Jumapili, Mungu atahudumia watu wake.
01/05/2026

Jumapili, Mungu atahudumia watu wake.

Bwana Yesu Asifiwe, GOOD NEWS CENTRE ibada ya wiki hii tumeindaa kwaajili ya marafiki zetu, wewe k**a rafiki wa huduma h...
09/04/2026

Bwana Yesu Asifiwe,
GOOD NEWS CENTRE ibada ya wiki hii tumeindaa kwaajili ya marafiki zetu, wewe k**a rafiki wa huduma hii basi ibada ya Jumapili inakuhusu tuna habari njema kwaajili yako, wewe k**a ni rafiki wa Mchungaji au mshirika wa kanisa hili basi uonapo ujumbe huu TUNAKUSIHI JUMAPILI TUNA SURPRISE YAKO.

Sisi GOOD NEWS tunaamini hadi hapa tulipo ni kwasababu yako wewe rafiki yetu, ni kwasababu ya maombi yako, ni kwasababu ya sadaka zako, na kujitoa kwako kwaajili yetu.

JUMAPILI YA URAFIKI
12.04.2026


KARIBU SANA

Jumapili Tarehe 08.03.2026Wanawake wa GOOD NEWS CENTRE, wanajambo lao.Ninaomba nikukaribishe kushiriki pamoja nasi ibada...
04/03/2026

Jumapili Tarehe 08.03.2026
Wanawake wa GOOD NEWS CENTRE, wanajambo lao.
Ninaomba nikukaribishe kushiriki pamoja nasi ibada hii, ninaamini utabarikiwa MNOMNO.

Karibu
GOOD NEWS CENTRE
MKUNDI SHELI
MOROGORO

28/02/2026

SIRI YA KUFANIKIWA NI KUANZA MAPEMA
HII ITAKUPA NAFASI YA KUJISAHIHISHA UNAPOKOSEA

Sifa Saba (7) za Kiongozi:MUSA NI MMOJA KATI YA VIONGOZI WAKUBWA KATIKA BIBLIA AMBAO TUNAWEZA KUJIFUNZA MAMBO MENGI KUPI...
28/02/2026

Sifa Saba (7) za Kiongozi:

MUSA NI MMOJA KATI YA VIONGOZI WAKUBWA KATIKA BIBLIA AMBAO TUNAWEZA KUJIFUNZA MAMBO MENGI KUPITIA MAISHA YAKE.

ZIFUATAZO NI SIFA SABA KATI YA NYINGI ZA KIONGOZI TUNAZO-JIFUNZA TOKA KWA MUSA:

🔑Sifa ya Kwanza:
KIONGOZI AWEZE KUONA MAMBO AMBAYO WENGINE HAWAYAONI BADO (Foresight/Visionary):

💥HESABU 27:12; “BWANA akamwambia Musa, panda wewe juu ya mlima huu wa Abarimu, uitazame nchi niliyowapa wana wa Israeli.”
💥Mungu anamuonyesha KIONGOZI, Musa, nchi ya ahadi ambayo tayari amewapa wana wa Israeli.
💥Kiongozi anatakiwa kuwa na macho ya kuweza kuyaona mambo ambayo Mungu amewaandalia wale anao-waongoza hata kabla ya mambo hayo kuwa halisi.
✅ Ili Musa aone mbali ilimpasa APANDE KWENYE MLIMA; ili mimi na wewe tuone mbali, inatupasa tupande kwenye MLIMA WA MAOMBI, tuwe peke yetu na Mungu ili kupata maono ya kule tunapotakiwa kuwapeleka watu wetu.

🔑Sifa ya Pili:
KIONGOZI AWEZE KUYASEMA MAMBO YALE AMBAYO WENGINE HAWAYAONI AU KUYAAMINI... UKIRI WA KIONGOZI NI MUHIMU (Persuasive):

💥KUTOKA 3:15-17; “Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya… Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali.”
💥Mungu anamwagiza Musa awaambie Wazee wa Israeli na Taifa zima kile ambacho Mungu anakwenda kuwafanyia.
💥Itawezekanaje taifa moja la WATUMWA liteke ardhi ya MATAIFA SITA yenye nguvu?? Ukiri na ushawishi wa kiongozi unatakiwa hapo!
✅Kiongozi lazima uwe na ujasiri wa KUTAMKA yale ambayo Mungu amekuonyesha bila kuogopa ni magumu kiasi gani.

🔑Sifa ya Tatu:
KIONGOZI AWE MTOA MATUMAINI (Encourager):

💥KUTOKA 14:13-14; “Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. 14 BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.”
💥Musa akawapa matumaini watu walipokata tamaa baada ya kuona hatari iliyo mbele yao.
✅ Kiongozi unapaswa kuwapa watu matumaini wanapokata tamaa.

🔑Sifa ya Nne
KIONGOZI AWEZE KULEA MTU AU WATU WATAKAOCHUKUA NAFASI YAKE (Mentorship):

💥HESABU 13:16; “Hayo ndiyo majina ya hao watu waliotumwa na Musa waende kuipeleleza nchi. Na huyo Hoshea mwana wa Nuni, Musa akamwita jina lake Yoshua.”
💥Musa aliona kitu cha tofauti ndani ya kijana HOSHEA; kisha akambadilisha jina na kumwita YOSHUA.
💥Musa alitumia muda wa kutosha kumfundisha Yoshua na AKAHAMISHIA mamlaka yake kwa YOSHUA hata kabla ya kufa (HESABU 27:18-20).
✅ Kiongozi, anza kuandaa mapema mtu au watu watakaoweza kusimama kwenye nafasi yako. Ukifa kabla ya kuandaa mtu/watu, UASI unaweza kutokea.

🔑Sifa ya Tano:
KIONGOZI AWEZE KUFANYA KAZI NA WATU WENGINE (Team Work):

💥KUTOKA 18:25; “Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi.”
💥Musa aliwahitaji watu wengine wafanye nae kazi ili aweze kulitimiza kusudi la Mungu katika uongozi wake.
💥Mungu humpa MAONO mtu mmoja; lakini maono ya KIUNGU hayawezi tekelezwa na MTU MMOJA; inahitajika TIMU (team) ili kutimiza maono.
💥Kabla ya YESU KRISTO kuanza kufanyia kazi maono yake ya kuukomboa ulimwengu, alianza kwa kuandaa TIMU ya wanafunzi 12.
✅ Kiongozi unahitaji TIMU ya watu ambao watayaelewa maono uliyonayo na wafanye kazi pamoja na wewe kuyatimiza maono.

🔑Sifa ya Sita:
KIONGOZI ANAPASWA KUWAJIBIKA MAMBO YANAPOHARIBIKA (Taking responsibility):

💥KUTOKA 32:30-32 (NEN); “Siku iliyofuata Musa akawaambia watu, “Mmefanya dhambi kubwa. Lakini sasa nitapanda juu kwa Bwana, labda nitaweza kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.” 31 Hivyo Musa akarudi kwa Bwana na kumwambia, “Lo! Hawa watu wamefanya dhambi kubwa namna gani! Wamejitengenezea miungu ya dhahabu. 32 Lakini sasa nakusihi, wasamehe dhambi yao; lakini k**a sivyo, basi nifute kutoka kwenye kitabu ulichoandika.”
💥Musa hakuwepo wakati Waisraeli walipomkosea Mungu na kujitengenezea ndama; Yeye alikuwa mlimani akipokea amri 10. Hata hivyo, MUSA anajitwika wajibu na anawaombea msamaha kwa Mungu na anaenda mbali zaidi kwa kumwambia MUNGU amfute kwenye kitabu chake endapo atakataa kuwasamehe.
✅ Kiongozi, hata watu wako wakikosea, wewe bado ni kiongozi wao na ni lazima uwajibike!

🔑Sifa ya Saba:
KIONGOZI AWE NA NGUVU YA KUSIMAMA PEKE YAKE (Autonomous):

💥HESABU 12:1; “Kisha Miriamu na Haruni wakamteta Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.”
💥Miriamu na Haruni walikuwa watu wa karibu na muhimu sana kwa Musa; lakini wakamgeuka.
💥Hata YESU KRISTO alipok**atwa, wanafunzi wake wote wakamkimbia, akabaki peke yake (Mathayo 26:56; Marko 14:50).
✅ Kiongozi, zipo nyakati katika uongozi ambapo hata watu wako wa karibu wanaweza kukugeuka au kukuacha. Katika nyakati k**a hizo, kiongozi unapaswa uwe na nguvu ya kusimama peke yako huku ukimtumaini Mungu.

MUNGU ATUSAIDIE VIONGOZI.
(Dr. Zakayo Nzogere).

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.GOOD NEWS CENTRE MOROGORO +255 762 186 639(Whatsapp)SIKU YA AROBAINI(40)13.02.2026*H...
12/02/2026

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO
+255 762 186 639(Whatsapp)

SIKU YA AROBAINI(40)
13.02.2026

*Hongera!* Leo ni
Siku ya 40, kilele cha safari yetu ya maombi. Leo tarehe 13 Februari 2026 (ikiwa ulianza Januari 5), ni siku ya Shukurani, Sifa, na Kuweka Muhuri wa Ushindi. Siku hii si ya kuomba mahitaji tena, bali ni ya kumshukuru Mungu kwa imani kuwa amejibu kila hitaji uliloliwasilisha kwa siku 39 zilizopita.

*MAANDIKO YA KUSIMAMIA*

Soma mistari hii kwa sauti kuu ya furaha:
Zaburi 100:4-5 *Imeandikwa* "Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru, Nyuani mwake kwa kusifu. Mshukuruni, lihimidini jina lake. Kwa kuwa Bwana ni mwema, fadhili zake ni za milele."

Wafilipi 4:6 *Imeandikwa* "...bali katika kila neno kwa kusali na kuomba pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu."

Yohana 11:41 *Imeandikwa* "Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia."

*MAOMBI YA LEO*

1. *Mshukuru Mungu kwa Kukamilisha:* Mshukuru Mungu kwa kukupa afya, nguvu, na uvumilivu wa kumaliza siku zote 40 bila kuacha. Wengi walianza lakini hawakumbaliza, mshukuru kwa neema hiyo.

2. *Mshukuru Mungu kwakuwa amekusikia:* Tamka kwa imani: "Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia maombi yangu yote ya siku 40." (Yohana 11:41).

3. *Kuweka Muhuri wa Damu ya Yesu:* Omba Damu ya Yesu iweke muhuri juu ya majibu yako ili adui asije akaiba kile ambacho Mungu ameachilia leo.

4. *Sifa na Kuabudu (Worship):* Tumia muda mrefu leo (hata saa nzima) kusifu. Mwambie Mungu jinsi alivyo mkuu, mwaminifu, na mwenye nguvu. Sifa ndiyo inakamilisha ushindi.

5. *Tangaza Matokeo:* Jitamkie kuwa mwaka huu 2026 ni mwaka wa kicheko, mwaka wa kuinuliwa, na mwaka wa ushuhuda mkuu. Tangaza kuwa "Imekwisha" kwa kila tatizo lililokuwa linakutesa.

6. *Toa sadaka ya SHUKURANI*: Andaa sadaka yako ya pekee ya shukurani na kuipeleka madhabahuni (kanisani) k**a ishara ya kusema "Asante Bwana kwa kunivusha."

*OMBA*
"Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, naja mbele zako leo nikiwa na moyo uliojaa shukurani. Asante kwa kuniongoza katika safari hii ya siku 40. Leo, sitasema 'nipe', bali nasema 'ASANTE'. Asante kwa afya, asante kwa milango iliyofunguka, asante kwa vita ulivyopigana kwa ajili yangu mnamo 2026. Naweka muhuri wa ushindi huu kwa Damu ya Yesu. Maisha yangu hayatabaki k**a yalivyokuwa. Naingia katika msimu wa ushuhuda kuanzia sasa. Katika jina la Yesu Kristo, Amen"

*MAELEKEZO MUHIMU*
1. *Linda Majibu Yako:* Endelea kuishi maisha ya utakatifu na imani. Usirudie dhambi ulizozitubu.
2. *Soma Neno:* Usiache kusoma Biblia kila siku.
3. *Toa Ushuhuda:* Mungu akikutendea kile ulichoomba, usisite kutoa ushuhuda ili kumtukuza Yeye.
Bwana akubariki sana kwa kukamilisha safari hii. Mwaka 2026 ukawe wa baraka tele kwako.

*K**A UPO MOROGORO, LEO SAA KUMI JIONI HADI SAA 12 JIONI TUNAKUTANA PALE KANISA LA GOOD NEWS CENTRE, MKUNDI SHELI, ILI KUMALIZA MAOMBI PAMOJA, HIVYO KARIBU SANASANA*

*PIA JUMAPILI TUTAKUWA NA IBADA YA SHUKURANI, KUMSHUKURU MUNGU KWA KUTUWEZESHA LAKINI PIA KUSHUHUDIA MATENDO YAKE MAKUU ALIYO TUTENDEA, PIA KARIBU SANA SANA*

*KITABU CHA MAOMBI HAYA KITAACHILIWA MWEZI WA TATU, KITAKUWA KIMEBEBA MAOMBI YOTE YA SIKU 40, AMBAYO YATAKUPA MWONGOZO UNAWEZA KUKITUMIA KUOMBA KULINGANA NA SIKU ULIZOJIWEKEA*

KWA SADAKA YAKO TIMIA NAMBA HIZI:
0650 455 888 Mixx By Yas
0693 455 888 Airtel Money

MUNGU AKUBARIKI SANA.
Pastor Bampele Nathanael
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.GOOD NEWS CENTRE MOROGORO +255 762 186 639SIKU YA THELATHINI NA TISA(39)12.02.2026Si...
11/02/2026

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO
+255 762 186 639

SIKU YA THELATHINI NA TISA(39)
12.02.2026

Siku ya thelathini na tisa ya maombi.
Maandalizi ya Kupokea Majibu na Kumiliki Nchi (Preparation for Possession). Leo tarehe 12 Februari 2026 (ikiwa ulianza tarehe 5 Januari), tunashughulika na utayari wa moyo. Ni siku ya kuondoa hofu ya mafanikio na kujiandaa kuvuna kile ulichokuwa unakiombea kwa siku 38 zilizopita.

*MAANDIKO YA KUSIMAMIA*

Yoshua 1:11 *Imeandikwa* "Piteni katikati ya kambi, mkawaamuru watu, mkasema, Jiandaeni posho; kwa maana baada ya siku tatu mtavuka huu mto Yordani, ili mwingie kuimiliki nchi..."

Hesabu 13:30 *Imeandikwa* "Kaleb akawatuliza watu... akasema, Na tupande mara moja, tukaimiliki; kwa maana twaweza kushinda bila shaka."

Yohana 11:40 *Imeandikwa* "Yesu akamwambia, Je! Sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?"

*MAOMBI YA LEO*

1. *Mshukuru Mungu kwa kukuwezesha:* Mshukuru Mungu kwa kukuwezesha kufika mlangoni mwa siku ya 40 leo tarehe 12 Februari 2026. Mtukuze kwa ajili ya ushindi ulioko mbele yako.

2. *Kuvuka Yordani:* Taja kila kizuizi cha mwisho kilichosimama kati yako na "Nchi ya Ahadi" yako ya 2026. Amuru mto Yordani uliopo mbele yako upishe njia sasa kwa jina la Yesu.

3. *Kukataa ripoti Mbaya:* Kataa sauti yoyote inayokwambia "huwezi" au "nchi ina majitu." Simama na imani ya Kalebu na tamka: "Naweza kushinda bila shaka"

4. *Kusafisha Vyombo vya Kupokelea:* Omba Roho Mtakatifu asafishe moyo wako na mikono yako ili uweze kushika baraka takatifu bila kuzichafua kwa kiburi au dhambi.

5. *Kuomba Ujasiri wa Kumiliki:* Mwombe Bwana akupe ujasiri wa kupiga hatua ya mwisho. Usiogope ukubwa wa baraka unayokwenda kuipokea.

*OMBA*
"Baba wa mbinguni, leo Siku ya 39 naja mbele zako nikiwa nimejiandaa kuvuka. Asante kwa kunileta mpaka mlangoni mwa siku yangu ya 40. Leo, naondoa kila hofu na kujiweka tayari kumiliki nchi uliyoniahidi mnamo 2026. Naamuru kila Yordani ipishe njia. Naamini kuwa kwa msaada wako, nitashinda bila shaka. Kesho naingia katika siku yangu ya shukurani nikiwa na matokeo mkononi. Katika jina la Yesu Kristo, Amen."

*TUNAPOELEKEA KUMALIZA MAOMBI, TUMEKUANDALIA KITABU AMBACHO KIMEBEBA MAOMBI YA YOTE YA SIKU 40 TUTAKIACHIA HIVI KARIBUNI TUTATOA UTARATIBU WA NAMNA KITAPATIKANA KWAKE*

*KWA SADAKA YAKO:*
0650 455 888 Mixx By Yas
0693 455 888 Airtel Money
Jina: Nathaniel Richard Bampele

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.GOOD NEWS CENTRE MOROGORO +255 762 186 639SIKU YA THELATHINI NA NANE(38)11.02.2026Si...
10/02/2026

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO
+255 762 186 639

SIKU YA THELATHINI NA NANE(38)
11.02.2026

Siku ya thelathini na nane ya maombi.
Kuhakikisha Ushindi Dhidi ya Maadui na Fitina (Victory over Oppression and Conspiracy). Leo tarehe 6 Januari 2026, tunashughulika na watu au nguvu zinazopanga njama kwa siri ili kukuangusha au kuzuia hatua zako za mwisho za mafanikio. Ni siku ya kuomba Mungu awe ngao yako dhidi ya kila hila ya siri.

*MAANDIKO YA KUSIMAMIA*

Isaya 8:10: "Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatika; semeni neno, nalo halitasimama; kwa maana Mungu yu pamoja nasi."

Zaburi 21:11: "Kwa maana walinuia kukufanyia mabaya; Waliwaza hila wasizoweza kuzitekeleza."

Mithali 26:27: "Achimbaye shimo ataumbuka mwenyewe; Na abingirishaye jiwe litamrudia."

*MAOMBI YA LEO*

1. *Mshukuru Mungu kwaajili Ulinzi:* Mshukuru Mungu kwa kukulinda na mitego mingi ya adui ambayo hukuijua tangu mwaka 2026 uanze. Mtukuze Yeye afichuaye siri za gizani.

2. *Kutibua Mashauri ya Siri:* Omba dhidi ya kila kikundi cha watu (kazini, kwenye biashara, au kwenye ukoo) kinachokaa vikao vya siri kwa ajili ya kukuharibia sifa au kuzuia maendeleo yako. Tamka: "Shauri lenu halitasimama!"

3. *Kugeuza Mashimo kwa Adui:* Simama juu ya Mithali 26:27. Omba kila shimo lililochimbwa kwa ajili yako (shimo la aibu, kufukuzwa kazi, au kufilisika) liwe shimo la mchimbaji mwenyewe.

4. *Kuharibu Hila za Maneno:* Omba dhidi ya fitina, masengenyo, na uongo unaosambazwa ili kukuchafua. Omba Mungu akunenee mema mbele ya watu wenye mamlaka.

5. *Aibu kwa Wanaotafuta Nafsi Yako:* Mwombe Bwana awafedheheshe wale wanaofurahia kuona unashindwa. Omba Mungu akuinue mbele yao ili wajue kuwa Yeye yu pamoja nawe.

6. *Kuomba Malaika wa Mlinzi:* Omba malaika wa Mungu wafunike kila hatua unayopiga ili usijikwae kwenye mtego uliotegwa kwa siri njiani mwako.

*OMBA*
"Baba wa mbinguni, leo Siku ya 38 naja mbele zako ukiwa ngao yangu. Kila shauri lililofanywa gizani dhidi ya hatima yangu mwaka huu 2026, ninalibatilisha kupitia jina la Yesu. Kila shimo lililochimbwa kwa ajili yangu liwe kaburi la aliyelichimba. Bwana, fanya hila za maadui zangu kuwa bure na unifiche katika siri ya hema yako. Asante kwa sababu hakuna silaha itakayofanyika juu yangu itakayofanikiwa. Amen."

Usiogope vitisho vya wanadamu. Kaa katika utulivu ukijua kuwa aliye upande wako ni mkuu. Soma Zaburi 35 ili kuona jinsi Daudi alivyoomba dhidi ya maadui.

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.GOOD NEWS CENTRE MOROGORO +255 762 186 639SIKU YA THELATHINI NA SABA(37)10.02.2026Si...
09/02/2026

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO
+255 762 186 639

SIKU YA THELATHINI NA SABA(37)
10.02.2026

Siku ya thelathini na saba ya maombi.
Kuharibu roho ya Kurudi Nyuma na Kukata Tamaa (Victory over Backsliding and Discouragement). Leo tarehe 10 Januari 2026, tunashughulika na hali ya kiroho na kisaikolojia inayomfanya mtu atake kuacha safari akiwa amebakiza hatua chache kuimaliza/kufika mwisho. Ni siku ya kuomba neema ya uvumilivu.

*MAANDIKO YA KUSIMAMIA*

Wagalatia 6:9 *Imeandikwa* "Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia mioyo."

Wafilipi 3:13-14 *Imeandikwa*
"13. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; 14. nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu."

Wafilipi 3:13-14 *Imeandikwa* "...nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele, nakaza mwendo niifikilie fadhili ya dhawabu..."

Isaya 40:31 *Imeandikwa* "Bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa k**a tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia."

*MAOMBI YA LEO*

1. *Mshukuru Mungu kwa Neema ya uvumilivu:* Mshukuru Mungu kwa kukuwezesha kufika siku ya 37. Ni neema yake pekee iliyokushika mkono tangu Siku ya 1 hadi leo tarehe 10 Januari 2026.

2. *Kukataa roho ya Kuchoka:* Kwa jina la Yesu, vunja kila roho ya uchovu wa rohoni na mwilini. Kataa sauti inayokuambia unapoteza muda au maombi haya hutapata majibu.

3. *Kusahau Yaliyo Nyuma:* Omba Mungu akusaidie kuacha kabisa kumbukumbu za kushindwa kwa miaka iliyopita. Tamka: "Sitaangalia nyuma tena, ninakaza mwendo kuelekea ushindi wa 2026!"

4. *Omba Nguvu Mpya:* Mwombe Bwana akufanye upya k**a tai. Omba "upako wa uvumilivu" (endurance) ili umalize siku hizi 40 zilizobaki kwa kishindo na kuanza mwaka kwa kishindo.

5. *Kuharibu roho ya Kurudi Nyuma (Backsliding):* Omba dhidi ya majaribu yanayoweza kukurudisha kwenye dhambi au tabia za kale ulizozicha. Omba Mungu akutie nguvu ya kusimama imara.

6. *Kuvuna kwa Wakati Wake:* Simama juu ya ahadi ya Wagalatia 6:9. Tangaza kuwa wakati wako wa kuvuna matunda ya maombi haya umewadia na hautapita.

*OMBA*
"Mungu Mwenyezi, leo Siku ya 37 naja mbele zako nikitafuta nguvu mpya. Nakataa roho ya kukata tamaa na kuzimia moyo. Asante kwa neno lako linalosema nitavuna nisipozimia moyo. Mwaka huu 2026, sitarudi nyuma; nitasonga mbele hadi nishike taji yangu. Nifanye upya k**a tai ili nipige mbio bila kuchoka. Asante Bwana kwa kunipa ushindi mlangoni mwa kilele cha maombi haya. Amen."

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.GOOD NEWS CENTRE MOROGORO +255 762 186 639SIKU YA THELATHINI NA SITA(36)09.02.2026Si...
08/02/2026

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO
+255 762 186 639

SIKU YA THELATHINI NA SITA(36)
09.02.2026

Siku ya thelathini na sita ya maombi.
Leo tutaomba kwaajili ya Nchi, Viongozi, haki na Amani katika nchi. Leo tarehe 6 Januari 2026, tunatoka nje ya mahitaji yetu binafsi na kuombea Taifa letu. Biblia inasema kuwa amani ya nchi ndiyo inayotupa sisi nafasi ya kufurahia baraka zetu kwa utulivu.

*MAANDIKO YA KUSIMAMIA*

1 Timotheo 2:1-2: "Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote; kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tupate kuishi maisha ya utulivu na amani..."

Yeremia 29:7: "Tafuteni amani ya mji ule... mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake ninyi mtapata amani."

2 Mambo ya Nyakati 7:14: "Ikiwa watu wangu... watajitokeza na kuomba... nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao."

*MAOMBI YA LEO*

1. *Mshukuru Mungu kwajiki ya Nchi yako:*
Mwambie Mungu ahsante kwa kuruhusu nizaliwe katika Taifa hili, ninaamini sikuzaliwa kwa bahati mbaya, ninajivunia Nchi yangu.

2. *Kuombea Viongozi:* Omba Mungu awape hekima viongozi wa Nchi (Rais, Mawaziri, na viongozi wote) katika maamuzi yanayo husu Taifa.

3. *Amani Katika Mazingira Yako:* Omba amani ya Mungu itawale mtaa wako na kijiji chako. Kataa roho za ujambazi, wizi, na fujo ambazo zinaweza kuvuruga utulivu wako na biashara zako.

4. *Uponyaji wa Nchi:* Omba dhidi ya magonjwa ya mlipuko, ukame, au majanga ya asili mwaka huu 2026. Mwombe Bwana aiponye nchi na kuifanya iwe na rutuba na utele.

5. *Kuombea Uchumi wa Nchi:* Omba milango ya biashara na uwekezaji ifunguke katika nchi yako ili vijana wapate ajira na umaskini upungue.

6. *Amani ya Kanisa na Huduma:* Omba kwa ajili ya viongozi wa dini na makanisa ili waendelee kuhubiri neno la kweli na kuliombea taifa kwa uaminifu.

*OMBA*
"Mungu wa mbinguni, leo Siku ya 36 ninakuja mbele zako nikiiombea nchi yangu. Wape viongozi wetu hekima ya Sulemani ili watu wako waishi kwa utulivu. Naagiza amani katika mitaa yetu na kukataa kila roho ya fujo mnamo 2026. Bwana, iponye nchi yetu na uibariki kazi ya mikono ya kila raia. Asante kwa sababu katika amani ya nchi hii, mimi na familia yangu tutapata amani. Amen."

Leo, unapopita mitaani au unapoona bendera ya nchi yako, itamkie baraka kimoyomoyo.

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.GOOD NEWS CENTRE MOROGORO +255 762 186 639SIKU YA THELATHINI NA TANO(35)08.02.2026Si...
07/02/2026

MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU 40.
GOOD NEWS CENTRE
MOROGORO
+255 762 186 639

SIKU YA THELATHINI NA TANO(35)
08.02.2026

Siku ya thelathini na tano ya maombi.
Leo tutaomba Nguvu ya Roho Mtakatifu na Upako wa Kufanya Makubwa. Leo tarehe 8 Januari 2026, tunaomba Mungu akujaze nguvu itakayokutoa katika hali ya kawaida na kukuingiza katika kiwango cha kiungu (Supernatural). Mwaka huu unahitaji mafuta mapya ili usichoke njiani.

*MAANDIKO YA KUSIMAMIA*

Matendo 1:8 *Imeandikwa* "Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu... hata mwisho wa nchi."

Zaburi 92:10 *Imeandikwa* "Bali pembe yangu umeitukuza k**a pembe ya nyati; Nimepakwa mafuta mabichi."

Isaya 10:27 *Imeandikwa* "...nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya upako."

*MAOMBI YA LEO*
1. *Mshukuru Roho Mtakatifu:* Mshukuru Mungu kwa kukupatia Roho Mtakatifu kuwa Msaidizi na Mfariji wako. Mshukuru kwa neema ya kufika siku hii ya 35 leo tarehe 8 Januari 2026.

2. *Omba Upako Mpya (Fresh Anointing):* Mwombe Bwana akupake mafuta mabichi kwa ajili ya huduma yako, kazi yako, na biashara yako. Tamka: "Leo napokea upako mpya wa kufanya mambo makubwa mwaka huu 2026!"

3. *Haribu Nira kwa Upako:* Omba upako wa Mungu uharibu kila nira (mzigo au kizuizi) ambayo imekuwa ikikutesa. Nira ya umaskini, nira ya magonjwa, na nira ya kushindwa na ivunjike sasa.

4. *Kupokea Nguvu ya Ushuhuda:* Mwombe Roho Mtakatifu akupe nguvu itakayokufanya uwe ushuhuda kwa wengine. Omba maisha yako yaonyeshe utukufu wa Mungu kupitia mafanikio yako.

5. *Kuongozwa na Roho:* Omba usifanye maamuzi kwa akili zako mwenyewe, bali uongozwe na sauti ya Roho Mtakatifu katika kila hatua unayopiga mwaka huu.

6. *Kufufua Karama Zilizolala:* Omba Mungu afufue karama na vipaji alivyoweka ndani yako ambavyo vilikuwa vimezimika au kusahaulika.

*OMBA*
"Baba katika jina la Yesu Kristo, leo Siku ya 35 nakuomba unijaze kwa upya na Roho wako Mtakatifu. Nipake mafuta mabichi yatakayonipa nguvu ya kushinda kila jaribu na kufanikiwa katika kila jambo nitalogusa. Mwaka huu 2026, nitatembea katika mamlaka na si kwa unyonge. Kila nira iliyokuwa imenifunga na ivunjike kwa sababu ya upako huu. Asante Bwana kwa kunipa nguvu ya kufanya makubwa. Amen."

Address

Morogoro

Telephone

+255762186639

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Good News Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share