Efatha Church Morogoro

Efatha Church Morogoro KARIBU KANISA LA EFATHA MOROGORO. Marko 7:34
"Akatazama mbinguni, akaugua, akamwambia, EFATHA, maana yake, Funguka."

☎️ 0787432654 I 0743672904

BAADA YA MAOMBI YA MFUNGO.MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKISOMO: TAMBUA MAJIRA NA NYAKATI ZA KUPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAKO. Mhubi...
02/06/2026

BAADA YA MAOMBI YA MFUNGO.
MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKI

SOMO: TAMBUA MAJIRA NA NYAKATI ZA KUPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAKO.

Mhubiri 3:1 "Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu."

Kuna wakati wa (1).Kuomba (2). Kujaribiwa na (3). Kupokea Majibu.

Wengi wanatarajia wakishamaliza Maombi kinachofuata ni kupokea Majibu ya Maombi yao, kiuhalisia ni kwamba, katikati ya Maombi na Majibu kuna kipindi cha Mpito, hichi ndicho kinachowatesa na kuwakatisha wengi Tamaa.

UFANYE NINI ILI UFIKIE NYAKATI ZA KUJIBIWA MAOMBI YAKO?

2️⃣LAZIMA UWE NA UVUMILIVU NA SUBIRA.

Ufunuo 2:3 "Tena ulikuwa na Subira na Kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka."

Ili uweze kuzifikia Nyakati za kupokea Majibu ya Maombi Yako lazima uwe na Uvumilivu na Subira, bila kuchoka.

Uvumilivu ni Tunda la Roho linalomwezesha mtu kustahimili mambo na kusimama imara huku akiendelea kukabili tatizo fulani. Ni hali ya kungojea jambo fulani litokee/litendeke pasipo kujali urefu wa muda, maumivu au mabadiliko ya kimazingira. Uvumilivu unahusisha akili na moyo wa mtu, namna unavyotenda unapokabiliana na Nyakati/hali ngumu.
Uvumilivu unafanya Jaribu kali sana lionekane kuwa jambo linaloleta Utukufu kwa sababu ingawa kuna maumivu makali, bado kuna 'Tumaini'. Mtu anayevumilia anaonyesha sifa ya ujasiri, uimara, na Ukomavu.

Ili uweze kupokea Majibu ya Maombi Yako lazima uwe na Uvumilivu/Subra kwasababu "Daraja la Maombi na Majibu" ni Majaribu, Majaribu ndiyo yanayokuvusha kuyaendea Majibu yako, ni uamuzi wako kuvuka ng'ambo au kubaki ulipo. Kipindi hiki cha Majaribu ni kigumu sana, kinakatisha tamaa na kuvunja moyo, huwezi kuvuka bila kuwa mvumilivu. Ndipo Yesu anatusisitiza;

Yakobo 1:12 "Heri mtu astahimiliye Majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima,..."

Kumbe Kanuni ya Kupokea Majibu ya Maombi yako (Taji) ni kustahimili (Kuvumilia) Majaribu na si kinyume chake.

Uvumilivu wako unapimwa wakati ambapo Mazingira sio rafiki kabisa. Kwa kukosa uvumilivu, wengi wameikana Imani yao, wamekata tamaa na kurudi nyuma kutafuta njia za mkato ili kupata wanachohitaji. Neno linatusisitiza kwamba;

Yakobo 1:4 "Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno."

Kumbe pasipo kuwa na Saburi (Uvumilivu) ni lazima utapungukiwa tu!, utapungukiwa Imani, utapungukiwa Pendo, utapungukiwa Tumaini. Ukipungukiwa na hivi vitu vitatu (3), huwezi kupokea Majibu ya Maombi yako.

Lakini pia, hauwezi kupokea majibu ya maombi yako bila kuwa na Uvumilivu kwasababu Nyakati na Majira ya Mungu siyo k**a Majira ya wanadamu, na Mawazo yake sio k**a yetu, tuko tofauti sana. Wakati wewe unatamani jambo fulani litokee, Mungu anaona muda bado, ndipo Ayubu anasema;

Ayubu 30:26 "Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya; Nami nilipongojea mwanga, likaja giza."

Unaona mawazo ya Mungu na Ayubu yanavyopishana!? ndivyo ilivyo hata leo, kwamba wakati wewe unatarajia mema, yanakuja mabaya, wakati unawaza 'Leo' Yeye anawaza 'Kesho', ni mpishano tu!, Bila kuwa na uvumilivu na Ufahamu wakutosha, utagombana na Mungu tu! hakuna utakachopokea.

Sio jambo rahisi kuahidiwa na Mungu ukadhani Ahadi hiyo itatokea kesho asubuhi, Mungu ana namna yake ya kutenda tofauti na wanadamu, ni lazima uwe mvumilivu ili upokee toka kwake. Anasema;

Habakuki 2:3 "Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; IJAPOKAWIA, INGOJEE; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia."

Kuna mambo unayoyataka leo, Mungu anasema bado ni "kwa Wakati ulioamriwa", haya si Majira yake, anaendelea kutusisitiza "Kuyangoja" Majibu yetu hata k**a "Yatakawia". Hauwezi kungojea kitu k**a huna uvumilivu ndani yako.

Uvumilivu ni kipimo cha uthabiti wa Imani yako na Pendo lako kwa Mungu. Hatahivyo hatujiwezeshi wenyewe kwa nguvu zetu kuwa na Uvumilivu bali kwa uwezo wa Mungu, anasema;

Wakolosai 1:11 "Mkiwezeshwa kwa uwezo wote,...mpate kuwa na Saburi ya kila namna na Uvumilivu pamoja na furaha;"

Ukimjua unaye muamini kuwa si mwongo, na kwamba hujibu Maombi ya kila anayemuomba kwa Wakati na Majira sahihi, basi huwezi kukata tamaa bali utaendelea Kuvumilia mpaka Majibu yako yatokee.

UNADHANI UMESHAVUMILIA VYA KUTOSHA NA SASA UMECHOKA HUWEZI TENA KUVUMILIA!?
Kabla hujachoka kabisa, Hebu wafikirie hawa na wengine wengi.
Mfikirie Ayubu aliyepoteza kila kitu mpaka watoto wake, lakini bado alivumilia mpaka mwisho. Nuhu aliyevumilia dhihaka na maumivu ya kujenga Safina miaka mingi bila kukata tamaa. Ibrahimu na Sara waliovumilia mpaka uzeeni ahadi ya kupata mtoto, Yusufu aliyevumilia kukataliwa, kusingiziwa na kuhukumiwa lakini bado alivumilia hadi Nyakati na Majira ya Bwana yalipofika akawa Waziri mkuu. Fikiria wengineo wengi waliosubiri kwa muda mrefu kabla hawajaona ile Ahadi waliyoahidiwa ikitimia, kila mmoja aliendelea kusimama kwenye nafasi yake bila kuyumba, ndipo Bwana akawapa Majibu yao.
Hauko peke yako, wote waliotaka Kitu toka Mungu iliwapasa wavumilie kwanza.

Jenga tabia ya Subira na Uvumilivu. Kadri unavyoendelea kuvumilia katika kumngoja Bwana, ndivyo unavyoyavuta Majibu ya Maombi Yako karibu nawe.
Kumbuka mwenye Kuvumilia mpaka mwisho ndiye anayepata Tuzo, usichoke!

©️ MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKI

NAIBARIKI JUMANNE YANGU. Ee NGUVU zangu, nitakuimbia kwa furaha, Mimi na Familia yangu tumebarikiwa. YESU asante.
02/06/2026

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.

Ee NGUVU zangu, nitakuimbia kwa furaha, Mimi na Familia yangu tumebarikiwa.

YESU asante.

Hautabaki k**a ulivyokuwa  katika msimu huu mpya. Roho wa Bwana atakuongoza,  na  kukupa hekima ili ushinde katika kila ...
01/06/2026

Hautabaki k**a ulivyokuwa katika msimu huu mpya. Roho wa Bwana atakuongoza, na kukupa hekima ili ushinde katika kila jambo.

Furahia na ushangilie wokovu wako! Badala ya huzuni, sasa ni majira ya kicheko, Mungu anaenda kufanya makuu katika maisha yako.

Umebarikiwa!


BAADA YA MFUNGO NA MAOMBI.MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKISOMO: TAMBUA NYAKATI NA MAJIRA YA KUPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAKO.Mhubir...
01/06/2026

BAADA YA MFUNGO NA MAOMBI.

MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKI

SOMO: TAMBUA NYAKATI NA MAJIRA YA KUPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAKO.

Mhubiri 3:1 "Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu."

Nyakati ni kipindi cha muda kwa Kusudi fulani kutokea. Kwa Habari ya Maombi, kuna nyakati/vipindi vitatu (3):-
▪️ Kuna Nyakati za Kuomba.
▪️ Kuna Nyakati za Kujaribiwa kwa kile ulichoomba.
▪️ Kuna Nyakati za Kupokea Majibu ya Maombi Yako.

Hizi ni Nyakati/vipindi vitatu(3) tofauti, vina Sifa na Kanuni tofauti. Ili kuvuka Nyakati zote salama na kwa ushindi ni lazima uzingatie Kanuni za kila kipindi.

Wengi wanatarajia wakishatoka kwenye Maombi kinachofuata ni kupokea Majibu ya Maombi yao, wanasahau kwamba kabla ya kipindi cha Kupokea Majibu huwa kuna Kipindi cha Mpito cha "Majaribu", na hichi ndicho kinachowatesa na kuwakatisha wengi Tamaa.

Yesu, Daniel, Hanna, Ayubu, Daudi,...n.k wote hawa waliomba, na kabla hawajajibiwa walijaribiwa kwanza, wakashinda, ndipo wakapokea Majibu ya Maombi yao.

Ni utaratibu wa Ki-Ungu, kupitishwa kwenye chekecho na Majaribu kwa kile unachokiomba, kwahiyo Jipange maana Nyakati za Kupokea Majibu ya Maombi yako zinakuja baada ya kushinda Nyakati za Majaribu.

ILI UFIKIE NYAKATI ZA KUJIBIWA MAOMBI YAKO, FANYA HAYA.

1️⃣ Yashinde Majaribu.
Unapoomba, lazima Imani yako Ijaribiwe. chochote unachoomba, kabla hujakipokea, kuna kanuni ya kujaribiwa katika hicho.
Mjaribu anakuja kukujaribu, kuna mtikisiko unatokea ili kupima Imani yako na kukuyumbisha utoke kwenye focus.

Ili Daniel awekwe kuwa Mkuu wa wenye Hekima, alijaribiwa kwa kutupwa kwenye tundu la Simba (Daniel 6-16), aliposhinda, Mungu wake akaabudiwa, nayeye akapandishwa kuwa mkuu wa wote wenye hekima.

Yesu alipomaliza Kuomba, mjaribu alimjia na kadhia nyingi. Yesu akamshinda, Mbingu zikajivunia Yeye, akaitenda kazi yake kwa Utukufu mkubwa.

Ukishaomba, kumbuka upande wa pili kuna Jaribu, kubali kujaribiwa na ulishinde hilo jaribu.

Jaribu halitoki nje ya kile ulichokiomba, linatokea palepale kwenye Ombi lako.
▪️Ukiomba Afya njema, utajaribiwa kwa Magonjwa, yaani unaweza hisi unakufa kesho!
▪️Ukiomba Uchumi Imara, utapata mtikisiko wa kifedha wa kupindukia. Utajikuta huna hata mia mfukoni.
▪️Ukiomba kuhusu Mahusiano mazuri, utaona vurugu kwenye ndoa, magomvi kwa ndugu na majirani, mpaka watoto wako mwenyewe utaona k**a wanakuzunguka.

Sasa ukiona hivyo usiyumbe, kuwa na Msimamo, usipoteze mwelekeo, shinda hilo ni jaribu, ukilishinda unapokea Majibu ya Maombi yako na mambo yote yanakaa sawa.

Ni hatari sana, unaposhindwa na majaribu baada ya Maombi yako.
Ibrahim, Baba wa Imani, aliomba, akatoa sadaka zake, jaribu la usingizi likaja, akalala, akashindwa kulishinda Jaribu la "Usingizi" akajikuta amekiingiza kizazi chake chote utumwani.

Ukiona umemaliza Maombi na Mtikisiko ni mkubwa, kuwa na msimamo, shinda, Imani yako inawekwa kwenye mizani, hakikisha unashinda hilo jaribu, Majibu Yako yako karibu kukufikia.

©️ MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKI

NAIBARIKI JUMATATU YANGU. Mimi nimebeba baraka za Bwana, hivyo nimebarikiwa niingiapo na nimebarikiwa nitokapo: hakuna y...
01/06/2026

NAIBARIKI JUMATATU YANGU.

Mimi nimebeba baraka za Bwana, hivyo nimebarikiwa niingiapo na nimebarikiwa nitokapo: hakuna yeyote, hakuna chochote wala lolote litakalopinga hilo.

Haleluya, Yesu ni Mfalme mkuu.

MATUKIO KATIKA PICHA
31/05/2026

MATUKIO KATIKA PICHA

MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
31/05/2026

MEZA YA BWANA

Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.

Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.

Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

MEZA YA BWANAYohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.  B...
31/05/2026

MEZA YA BWANA

Yohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.”

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”

Yohana 1:1-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”

Tunapokubaliana na neno tunakuwa tunapata uzima wa milele, tunaporuhusu Neno ndani yetu tunaruhusu Yesu akae ndani yetu, kwa maana Yesu ndiye uzima wetu. Tukikubali Neno tumemkubali Yesu, na hapo ndipo tunalinda imani yetu, ukiilinda imani yako itakupa kuponyeka, ukiamini kile unachokiamini mtu asikiondoe wala kukiharibu ndipo uponyaji unatokea kwako, Yusufu alilinda imani yake japokuwa alitupwa gereani lakini akaishia kuwa mtu mkuu, Daudi pia alilinda imani yake na akaishia kuwa mfalme. Imani ukiilinda unakuwa salama na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 128:1-4 “Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake, Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema…”

Yule amchaye Bwana atabarikiwa. Kumcha Bwana ni kulinda kile unachokiamini, unapolinda unachokiamini maisha yako yanaonekana yana mpangilio na ndipo Mungu anakufurahia, kwa maana unapolinda hicho unajiponya na mambo au ulimwengu huu na ndipo Mungu anakufurahia na kuruhusu mema yakujilie na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 126:6 “Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Tunapolinda imani kuna magumu, machungu kudharauliwa na kusukumwa lakini usiangalie yale yanayoendelea bali angalia kile unachokiamini ili kikupe kile unachokitaka, hakikisha unalinda kile unachokiamini na ndipo kwako kutakuwa kwema na Mungu atakushangaza na kila mtu atakushangaa.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA | 31.05.2026PICHA KATIKA MATUKIO
31/05/2026

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA | 31.05.2026

PICHA KATIKA MATUKIO

Address

607
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Morogoro posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Morogoro:

Share