02/06/2026
BAADA YA MAOMBI YA MFUNGO.
MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKI
SOMO: TAMBUA MAJIRA NA NYAKATI ZA KUPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAKO.
Mhubiri 3:1 "Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu."
Kuna wakati wa (1).Kuomba (2). Kujaribiwa na (3). Kupokea Majibu.
Wengi wanatarajia wakishamaliza Maombi kinachofuata ni kupokea Majibu ya Maombi yao, kiuhalisia ni kwamba, katikati ya Maombi na Majibu kuna kipindi cha Mpito, hichi ndicho kinachowatesa na kuwakatisha wengi Tamaa.
UFANYE NINI ILI UFIKIE NYAKATI ZA KUJIBIWA MAOMBI YAKO?
2️⃣LAZIMA UWE NA UVUMILIVU NA SUBIRA.
Ufunuo 2:3 "Tena ulikuwa na Subira na Kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka."
Ili uweze kuzifikia Nyakati za kupokea Majibu ya Maombi Yako lazima uwe na Uvumilivu na Subira, bila kuchoka.
Uvumilivu ni Tunda la Roho linalomwezesha mtu kustahimili mambo na kusimama imara huku akiendelea kukabili tatizo fulani. Ni hali ya kungojea jambo fulani litokee/litendeke pasipo kujali urefu wa muda, maumivu au mabadiliko ya kimazingira. Uvumilivu unahusisha akili na moyo wa mtu, namna unavyotenda unapokabiliana na Nyakati/hali ngumu.
Uvumilivu unafanya Jaribu kali sana lionekane kuwa jambo linaloleta Utukufu kwa sababu ingawa kuna maumivu makali, bado kuna 'Tumaini'. Mtu anayevumilia anaonyesha sifa ya ujasiri, uimara, na Ukomavu.
Ili uweze kupokea Majibu ya Maombi Yako lazima uwe na Uvumilivu/Subra kwasababu "Daraja la Maombi na Majibu" ni Majaribu, Majaribu ndiyo yanayokuvusha kuyaendea Majibu yako, ni uamuzi wako kuvuka ng'ambo au kubaki ulipo. Kipindi hiki cha Majaribu ni kigumu sana, kinakatisha tamaa na kuvunja moyo, huwezi kuvuka bila kuwa mvumilivu. Ndipo Yesu anatusisitiza;
Yakobo 1:12 "Heri mtu astahimiliye Majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima,..."
Kumbe Kanuni ya Kupokea Majibu ya Maombi yako (Taji) ni kustahimili (Kuvumilia) Majaribu na si kinyume chake.
Uvumilivu wako unapimwa wakati ambapo Mazingira sio rafiki kabisa. Kwa kukosa uvumilivu, wengi wameikana Imani yao, wamekata tamaa na kurudi nyuma kutafuta njia za mkato ili kupata wanachohitaji. Neno linatusisitiza kwamba;
Yakobo 1:4 "Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno."
Kumbe pasipo kuwa na Saburi (Uvumilivu) ni lazima utapungukiwa tu!, utapungukiwa Imani, utapungukiwa Pendo, utapungukiwa Tumaini. Ukipungukiwa na hivi vitu vitatu (3), huwezi kupokea Majibu ya Maombi yako.
Lakini pia, hauwezi kupokea majibu ya maombi yako bila kuwa na Uvumilivu kwasababu Nyakati na Majira ya Mungu siyo k**a Majira ya wanadamu, na Mawazo yake sio k**a yetu, tuko tofauti sana. Wakati wewe unatamani jambo fulani litokee, Mungu anaona muda bado, ndipo Ayubu anasema;
Ayubu 30:26 "Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya; Nami nilipongojea mwanga, likaja giza."
Unaona mawazo ya Mungu na Ayubu yanavyopishana!? ndivyo ilivyo hata leo, kwamba wakati wewe unatarajia mema, yanakuja mabaya, wakati unawaza 'Leo' Yeye anawaza 'Kesho', ni mpishano tu!, Bila kuwa na uvumilivu na Ufahamu wakutosha, utagombana na Mungu tu! hakuna utakachopokea.
Sio jambo rahisi kuahidiwa na Mungu ukadhani Ahadi hiyo itatokea kesho asubuhi, Mungu ana namna yake ya kutenda tofauti na wanadamu, ni lazima uwe mvumilivu ili upokee toka kwake. Anasema;
Habakuki 2:3 "Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; IJAPOKAWIA, INGOJEE; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia."
Kuna mambo unayoyataka leo, Mungu anasema bado ni "kwa Wakati ulioamriwa", haya si Majira yake, anaendelea kutusisitiza "Kuyangoja" Majibu yetu hata k**a "Yatakawia". Hauwezi kungojea kitu k**a huna uvumilivu ndani yako.
Uvumilivu ni kipimo cha uthabiti wa Imani yako na Pendo lako kwa Mungu. Hatahivyo hatujiwezeshi wenyewe kwa nguvu zetu kuwa na Uvumilivu bali kwa uwezo wa Mungu, anasema;
Wakolosai 1:11 "Mkiwezeshwa kwa uwezo wote,...mpate kuwa na Saburi ya kila namna na Uvumilivu pamoja na furaha;"
Ukimjua unaye muamini kuwa si mwongo, na kwamba hujibu Maombi ya kila anayemuomba kwa Wakati na Majira sahihi, basi huwezi kukata tamaa bali utaendelea Kuvumilia mpaka Majibu yako yatokee.
UNADHANI UMESHAVUMILIA VYA KUTOSHA NA SASA UMECHOKA HUWEZI TENA KUVUMILIA!?
Kabla hujachoka kabisa, Hebu wafikirie hawa na wengine wengi.
Mfikirie Ayubu aliyepoteza kila kitu mpaka watoto wake, lakini bado alivumilia mpaka mwisho. Nuhu aliyevumilia dhihaka na maumivu ya kujenga Safina miaka mingi bila kukata tamaa. Ibrahimu na Sara waliovumilia mpaka uzeeni ahadi ya kupata mtoto, Yusufu aliyevumilia kukataliwa, kusingiziwa na kuhukumiwa lakini bado alivumilia hadi Nyakati na Majira ya Bwana yalipofika akawa Waziri mkuu. Fikiria wengineo wengi waliosubiri kwa muda mrefu kabla hawajaona ile Ahadi waliyoahidiwa ikitimia, kila mmoja aliendelea kusimama kwenye nafasi yake bila kuyumba, ndipo Bwana akawapa Majibu yao.
Hauko peke yako, wote waliotaka Kitu toka Mungu iliwapasa wavumilie kwanza.
Jenga tabia ya Subira na Uvumilivu. Kadri unavyoendelea kuvumilia katika kumngoja Bwana, ndivyo unavyoyavuta Majibu ya Maombi Yako karibu nawe.
Kumbuka mwenye Kuvumilia mpaka mwisho ndiye anayepata Tuzo, usichoke!
©️ MCHUNGAJI ALLAN W. MLAKI