The Christians Bible Church of Tanzania

The Christians Bible Church of Tanzania Only for religious matters and the major concern is for Christianity
God bless everyone

Mtu wa Mungu ujihadhari na vishawishi vya mpnga Kristo, hizi ni nyakati za mwisho.
24/09/2023

Mtu wa Mungu ujihadhari na vishawishi vya mpnga Kristo, hizi ni nyakati za mwisho.

Pasaka njema
09/04/2023

Pasaka njema

Tunawatakia wakristo wote Ibada njema ya kumbukizi ya kuteswa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
07/04/2023

Tunawatakia wakristo wote Ibada njema ya kumbukizi ya kuteswa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

KUNA VITA KWA VIJANA📌Maamuzi mabaya yanayo fanywa mapema katika maisha yaweza kuwa vigumu kurekebishwa hapo baadae katik...
20/03/2023

KUNA VITA KWA VIJANA

📌Maamuzi mabaya yanayo fanywa mapema katika maisha yaweza kuwa vigumu kurekebishwa hapo baadae katika kuishi kwetu. ( Ujana ni fahari na unathamani kubwa sana)

📌Ujana unakuja maramoja tu katika kipindi cha maisha ya mwanadamu
(Hakuna mtu anayeweza kuwa kijana zaidi ya maramoja)

📌Vita vinaendelea kupiganwa katika ulimwengu huu kuhusu vijana, ni vita vyenye ushawishi kwa vijana kuweza kufanya maamuzi ( Maamuzi ya kuweka alama kwa ukuu na utukufu ambao unatengenezwa wakati wa ujana)

📌Maamuzi tunayo yafanya wakati wa ujana ni maamuzi yasiyoweza kutenduliwa.

📌Unapokuwa kijana ni muda wa kuanzisha msingi wa maisha ya badae/ maranyingi matokeo ya maisha ya badae atakavyoishi mtu msingiwake hujengwa wakati wa ujana wake.

📌Wakati wa ujana wetu ni wakati wa vita ( Ambapo utachagua ni "Mungu" au 'shetani' atawale maisha yako )

📌Usijijengee msingi wa dosari katika maisha yako k**a kijana.

📌Kuna vita vyenye maumivu makali vinapiganwa upande wetu sisi vijana kati ya Mungu na shetani.

📌Huwezi amini pale unapo kubali --NDIYO kwa Mungu maana yake inakuwa - HAPANA kwa shetani na kutofanya maamuzi kwa Mungu sawasawa na kumruhusu adui anaye panga nani wa kummeza.

📌Shetani anafahamu vyema kesho yako iliyo nzuri inaanzia ungali kijana leo. Ndiyomana kunawakati kijana ukiwa una songa mbele katika maisha unakumbana na Majaribu, migogoro na shida. ( shetani ana akili, lengo lake ni kukutumia wewe na kukufanya kuwa mjinga katika maisha haya )

📌Mungu anafahamu kwamba katika umri wetu wa ujana ni wakati mzuri wa kuwekeza kwaajili ya kesho na ndiyomaana anatutaka tufahamu tumfuate, tumfuate yeye na tujiandae kwa kesho yenye utukufu.

📌Maisha yako huwezi ukayaishi kwa maranyingine tena. ( Dunia inapita )

📌Hakuna namna yakufuta au kuyageuza yaliyopita ( yaliyopita ni historia isiyo badirika utabadirika wewe )

Kuna hatua tatu anazozipitia kila mwanadamu nazo ni:

📍Wakati wa ufundishwaji, katika kipindi hiki unakuwa bado mtoto/mchanga yote unayohitaji kufanya yanafanywa na wazazi au walezi, huna maamuzi ya kutenda jambo au wajibu wa kulibeba lolote.

📍Hatua ya pili ni wakati wa ujana/wakati wa vita vya ujana, huu niwakati ambao mtu anakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi yanayo mpendeza yeye mwenyewe k**a ni kwa kumtegemea Mungu au shetani. Ni wakati wa kuwa na machaguo binafsi, migogoro ya nafsi, upinzani mkali wa akilini mwako, kuwa na misimamo kwa mambo mbalimbali na umakini.

📍 Hatua ya tatu ni sehemu muhimu ya maisha uliyokuwa nayo. Wakati umeuvuka ujana utuuzima unataka kuchukua nafasiyake kwako.

📌Yote ya yote unatakiwa kusimama, tambua makosa yote uliyoyafanya katika maisha yako ya nyuma hayata hesabika makosa isipokuwa pale utakapo endelea kuyafanya ( kutenda kosa si kosa ila kurudia kosa )

📌Yesu siyo mwizi anaye ruka kwenye madirisha ya nyumba za watu. Yeye yupo mlangoni anabisha hodi akisubiri wito wako aingie ndani

📌Tambua wito wako na umkaribishe muumbaji wako aingie nyumbani mwako akuokoe na magereza ya shetani ambako wengi wamesha fungwa humo ( kwenye ulevi, uhuni, ujambazi, magomvi, tamaa mbaya nk.) There's a battle for the young and it's about you.

 .  The Christians Bible Church of Tanzania
17/03/2023

. The Christians Bible Church of Tanzania

Bwana Yesu apewe sifa.Type Amen...K**a unampenda Yesu.
15/07/2022

Bwana Yesu apewe sifa.
Type Amen...
K**a unampenda Yesu.

Pumzika kwa amani, Mwendo umeumaliza. Mungu aiweke roho yako mahala pema peponi - Osinachi Nwachukwu. Amina 🙏.
10/04/2022

Pumzika kwa amani, Mwendo umeumaliza. Mungu aiweke roho yako mahala pema peponi - Osinachi Nwachukwu. Amina 🙏.

🔴NGUVU YA DHAMBI PT 1Na. Kweka Glory...✍️➡️ Ezekiel 18:26-27"Mwenye haki atakapoghairi na kuiacha haki yake na kutenda u...
10/04/2022

🔴NGUVU YA DHAMBI PT 1
Na. Kweka Glory...✍️

➡️ Ezekiel 18:26-27
"Mwenye haki atakapoghairi na kuiacha haki yake na kutenda uovu akafa katika uovu huo, katika uovu wake alioutenda atakufa.Tena mtu mwovu atakapoghairi na kuacha uovu wake alioutenda na kutenda yaliyo hualali na haki ataponya roho yake nayo itakuwa hai"

⏩ Kwahiyo kuna vitu viwili mbele yako lakini maamuzi ya mwisho niyakwako kwamba ufate kipi katika hivyo viwili..lakini kitu cha msingi nilichokuwa nataka uone kwenye huo mstari ni kuwa UZIMA unatanguliwa na matendo ya HAKI na UZIMA huo huo umebeba/ umefungamanishwa na BARAKA.

👉 na MAUTI imetanguliwa na DHAMBI na MAUTI hiyo hiyo imebeba LAANA au ADHABU kwasababu hakuna MAUTI k**a hakuna DHAMBI na hakuna LAANA k**a hakuna kosa lililotangulia .
👉Vivyohivyo hakuna UZIMA wa kiroho k**a hakuna MATENDO YA HAKI na hakuna BARAKA au MAFANIKIO ya kiroho k**a hakuna WEMA uliotangulia au matendo yaliotangulia na kusimama kwa KUITAFSIRI haki ya Mungu.

VIPENGELE MUHIMU KATIKA KUITAFSIRI NGUVU YA DHAMBI:

1️⃣ MAUTI KUPITIA DHAMBI INAKUONDOLEA SIFA ZA KUITWA MWENYE HAKI.👇

⏩2mambo ya nyakati 7:19-20
"Lakini mkigeuka na kuziacha sheria zangu na amri zangu nilizoweka mbele yenu mkienda na kuitumikia miungu mingine na kuoabudu ndipo nitawang'oa katika nchi yangu niliyowapa na nyumba hii mlioitakasa kwa jina langu nitaziondosha itoke mbele zangu nami nitaifanya kuwa mithali na tukano katikati ya watu"
👉Kwa tafsiri ya DHAMBI kufungua mlango wa MAUTI juu ya mtu..INAMAANISHA hivi MAREHEMU hanaga haki kwahiyo ukifa umepoteza SIFA ya kwanza ya kuwa mwanadamu na kwamaana hiyo hakuna namna unaweza kupata haki za kibinadamu wakati wewe sio mwanadamu tena,,hiyo ni kanuni ya kimwili lakini ipo ata kiroho 🤔
⏩ Ezekiel 18:27-
"Tena mtu muovu akighairi na kuacha uovu wake alioutenda na kutenda yaliyo halali na haki ataponya roho yake nayo itakuwa hai"

2️⃣ HAKI YA MTU UMEFUNGAMANISHWA KATIKA TOBA
(Hualali au utakatifu)

⏩ Matendo ya mitume 3:19
"Tubuni basi mrejee Ili DHAMBI zenu zifutwe zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana"

Soma tena 👇
⏩Isaya 1:18-20
"Aya njooni tusemezane asema Bwana dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana k**a damu zitakuwa nyeupe k**a theluji, zijapokuwa nyekundu k**a bendera zitakuwa k**a sufu,
K**a mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi bali k**a mkikataana kuasi mtaangamizwa kwa upanga maana kinywa cha Bwana kimenena haya"

Kwa leo tunaishia hapa naomba usikose muendelezo wa somo letu majaaliwa ya mwenyezi Mungu.

Jumapili njema.
06/03/2022

Jumapili njema.

HABARI NJEMA KUHUSU UFALME WA MBINGUNI.Watu wa Mungu nawasalimu kwa jina la Yesu, leo nataka kusema nanyi jambo moja nal...
01/03/2022

HABARI NJEMA KUHUSU UFALME WA MBINGUNI.
Watu wa Mungu nawasalimu kwa jina la Yesu, leo nataka kusema nanyi jambo moja nalo ni hili la kuhusu Ufalme wa Mbinguni.

Yawezekana umewahi kusikia watu wakitamka kuhusu ufalme wa Mbinguni au mara kadhaa umekutana na maandiko kwenye Biblia au machapisho mbalimbali. Basi, leo tuangazie Ufalme wa Mbinguni nini maana yake, je yupi mwenye kustahili kuurithi Ufalme wa Mbinguni?

▪️Ufalme wa Mbinguni (Ufalme wa Mungu); hii ni serikali halisi iliyo anzishwa na Mungu mwenyewe na inatawala kutoka Mbinguni. _Marko1:14,15.
>> Mungu amemteua Yesu kuwa mfalme katika serikali yake iliyo kuu kuliko serikali zote ulimwenguni. _Mathayo 28:16-18.

>>Chini ya mwongozo wa Mungu Yesu amechagua watu kutoka kwa mataifa yote ambao"watatawala wakiwa wafalme pamoja naye huko mbinguni" _Ufunuo 5:9-10.
Na ufalme huo hauta haribiwa.Uta dumu milele yote. _Danieli 2:44.

▪️Kati yetu mimi na wewe je, ni nani anaye stahili kuurithi ufalme wa Mbinguni (Ufalme wa Mungu)?
Biblia inajibu swali hili kwa uwazi mkubwa, mtu yeyote anayefanya mapenzi ya Mungu anaweza kuwa raia wa Ufalme wa Mungu, bila kujali anatokea familiya ya namna gani au mahali alipo zaliwa_Matendo 10:34,35: Warumi 2:7-11.

Hivyo ndugu yatupasa kujichunguza k**a tunaishi maisha ya kumpendeza Mungu, huko ndiko kufanya mapenzi ya Mungu. Yesu alisema "si kila atakaye mwambia bwana, ataingia katika Ufalme wa Mbinguni" na aka sisitiza ili tuingie katika Ufalme wa Mbinguni, yatupasa kusikiliza na kuyatenda yote anayo tufundisha__Mathayo 7:21-27.

>>Katika nyakati hizi za mwisho wengi hujikuta wameanguka kwenye dhambi, ondoa shaka kwani mambo hayo hayana budi kutokea kwakuwa yalitabiriwa kutukia . Tukiwa tu wenye dhambi Mungu anatutaka tu tubu dhambi zetu ili tuweze kuurithi Ufalme wa Mbinguni__Mathayo 3:1,2. : Marko 1:14-15.

Kwa kuhitimisha ujumbe waleo, Mungu anatutaka wote tuweze kuurithi Ufalme wa Mbinguni ulio andaliwa kwa watu wote. Kwa Mungu hakuna ubaguzi wala upendeleo ikiwa wote tunaishi maisha ya kumpendeza yeye. Hivyo hakuna mbingu ambayo watenda dhambi wataingia k**a hawata tubu na kuacha kutenda dhambi. Waebrania 12:14.

Ujumbe huu umetolewa na kanisa la
The Christians Bible Church of Tanzania.

S.L.P 11
Mang'ula. Simu: +255692-340 503
Morogoro.

JE, TUNAISHI MAISHA YA KUMPENDEZA MUNGU? __________________________Bwana Yesu asifiwe...Mpendwa nina ujumbe wa Mungu kwa...
13/02/2022

JE, TUNAISHI MAISHA YA KUMPENDEZA MUNGU?
__________________________
Bwana Yesu asifiwe...
Mpendwa nina ujumbe wa Mungu kwako jumapili ya leo. Leo hii roho mtakatifu amenituma kusema na wewe juu ya maisha yetu.

1Wathesalonike 4:4-5.
[4] Kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

[5] Si katika hali ya tamaa mbaya, k**a Mataifa wasio mjua Mungu.

Katika maandiko hapo juu tunaweza kuona k**a tunaishi maisha ya kumpendeza Mungu.

Ili tuishi maisha ya kumpendeza Mungu jambo moja tu na ndilo msingi kwa mtu wa imani ya Kristo tunatakiwa kuuweza mwili.

Kuuweza mwili maana yake nini?
Hapa kuuweza mwili maana yake ni kuepukana na kufanya yasiyo mpendeza Mungu ambayo ni matamanio ya mwili tu.

Jambo la kuzingatia ni kwamba kunakuwa na ushindani kati ya roho wa Mungu na nafsi ya mtu iliyo ingiliwa na roho chafu. Kuna wakati linaweza kukujia wazo la kufanya uzinzi, hilo linakuwa tamanio la kimwili lakini pia ukasikia sauti ikisema kuzini ni dhambi. Sasa ili uuweze mwili unachotakiwa ni kuitii sauti inayo kukumbusha kwamba kuzini si tendo safi mbele za Mungu. Kwakufanya hivyo unaendelea kumheshimu Mungu na kudumu katika utakatifu.

Mpendwa biblia inatuweka wazi kwamba tusiwe watu wenye tamaa mbaya k**a watu wa mataifa ( wasio okoka) . Mpendwa, tamaa zimegawanyika katika makundi mawili. Moja ni tamaa mbaya, yaani mtu kutamani kutenda maovu k**a ilivyo desturi za watu wa mataifa hujikita kwenye wizi, ujambazi, uasherati na ulevi nk. Lakini zipo tamaa zilizo nzuri k**a vile mtu kutamani kuhubiri neno la Mungu kwa watu wa mataifa, kutamani kuwasaidia watu wenye shida mbalimbali lakini huku akichunga mienendo yake asije aka mkosea Mungu wakati akiyafanya hayo.

Asante,
Imechapishwa na, Kanisa la Wakristo wa biblia Tanzania.

.
Morogoro, kisawasawa.

29/01/2022

SILAHA ANAYOTUMIA SHETANI.
Na, ADAM .J. NYAMINYA...✍️

Biblia inasema

Yohana 10:10

"Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele".

Shetani ana majukumu matatu anayotekeleza Kwenye maisha ya wanadamu ili kuwapoteza wasiingie Kwenye Ufalme wa Mungu duniani na Mbinguni. Kazi hizo ni

1: Kuiba
2: Kuchinja
3: Kuharibu

👉 Shetani huiba utakatifu wa watu ili kuwaondoa katika Safari ya Kumuona Mungu.

Waebrania 12:14
[14]Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;

✍️Utasikia anainua mtu, anakuambia wewe inaonekana hauna Nguvu za kiume.
✍️Unajifanya mama mchungaji sana.
✍️Una sali sana utakufa maskini wewe.
UKISIKIA KAULI HIZO UJUE shetani yupo kazini.

✍️Shetani anachinja na kuharibu maono makubwa ya watu.

Atakuletea wazo la kujiona wewe hufai kwa sababu ya hali ya maisha unayopitia.
✍️Atakuambia wewe ni mbuzi wa maskini, yaani huwezi kutimiza ndoto na maono yako kwa sababu ya changamoto unazopitia.

UKIONA HIVYO ujue tayari ameanza kuharibu na Kuchinja maono yako.

👉Atakuletea Hali ya kutojiamini
👉Atainua watu wakukatae na kukudharirisha
👉Atakuinulia maadui kila kona, Lengo kubwa ni kuiba, kuharibu na Kuchinja ndoto zako.

🗣️Na Silaha yake kubwa ni UONGO
Yohana 8:44
[44]Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.

✍️Shetani kwa kupitia uongo wake, ameua, ameiba, ameharibu na Kuchinja watu kiroho na kimwili.

👉Watumishi wengi wameanguka kwa sababu ya uongo wa shetani.
👉Maono ya wengi yamekufa kwa sababu ya uongo wa shetani.

Yuda Iskariote alijikuta ameanguka Kwenye utume wake kwa sababu ya uongo wa Shetani.

Adamu na Eva wakijikuta wanafukuzwa Edeni kwa sababu ya uongo wa shetani.

Biblia inasema "Mtu huanza kujaribiwa na tamaa yake huku akivutwa na kudanganywa na shetani............".

Yakobo 1:14-15
[14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
[15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

😥Dhambi ndio chanzo Cha matatizo yote kwa mwanadamu, lakini shetani ndio kichocheo kikubwa kinachopelekea watu wengi washindwe kutii amri za Mungu na kujikuta wameingia Mautini.

🗣️Tuna njia moja ya kumshinda shetani, nayo ni KUMKARIBIA MUNGU

Yakobo 4:7-8
[7]Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
[8]Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

🗣️The moment mwanadamu anapoamua kuacha Dhambi na kumkaribia Mungu kwa sala na utakatifu ndipo shetani humkimbia mtu huyo Kwenye maisha yake.

We cure sin, by using Obedience antidote.

Kumbuka kuwa, Silaha ya shetani ni UONGO au Udanganyifu ambao huzaa dhambi. Na hutumia Dhambi K**a chombo Cha kumuongoza mwanadamu ili waende naye jehanamu akijua kuwa muda wake uliobakia ni mchache sana.

Ufunuo wa Yohana 12:12
[12]Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.

MKARIBIE MUNGU akusaidie kuteka nyara kila wazo linalokuja kwako kinyume na injili ya KRISTO, hapo utaweza kumshinda shetani.

2 Wakorintho 10:3-5
[3]Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;
[4](maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
[5]tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

Be blessed 🙏
.

Address

Mang'ula
Morogoro
P.O.BOX11MANG'ULA

Telephone

+255692340503

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Christians Bible Church of Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share