29/10/2024
BALLON D'OR | Mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia ni kiungo Rodri , raia wa Hispania anayekipiga klabu ya Man City ya England.
Nafasi ya pili imekwenda kwa Vinicius Jr., na namba tatu ni Jude Bellingham, wote kutoka Real Madrid.
Timu bora upande wa klabu ni Real Madrid, kocha bora ni Carlo Anceloti wa Real Madrid na golikipa bora wa dunia ni yuleyule Emiliano Martinez wa Aston Villa.
Aliyechukua Ballon d'Or upande wa soka la wanawake ni Aitana Bonmati wa Barcelona.
Je, una la kusema??