Charles Gida's Ministry

Charles Gida's Ministry Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Charles Gida's Ministry, Religious organisation, P O. BOX 8234, Mbeya.

Bwana Yesu Asifiwe! Habari za juma Pili? Ndugu zangu nawashukuru watu wa mbalizi na makanisa yote ya mbalizi kuhuzuria k...
05/04/2026

Bwana Yesu Asifiwe! Habari za juma Pili? Ndugu zangu nawashukuru watu wa mbalizi na makanisa yote ya mbalizi kuhuzuria kwenye semina ya Neno la Mungu iliyo fanyika kwenye kanisa la UINJILISTI MAKAO MAKUU YAANI USHIRIKA WA MBALIZI KWA REHNER Mungu awabariki wote na kwaya ZOTE na wachangiaji wetu na waombeaji wote Mungu awabariki sana SANA

19/03/2026
01/02/2026

Bwana Yesu Asifiwe! Karibu sana tuombe kwajiri ya Tanzania

31/01/2026

SHALOM! Naomba USIKOSE KWENYE MAOMBI haya

MAOMBI YA KUOMBEA LEO JUMA PILI NA MWAKA MZIMA Neno la Mungu linasema, Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mw...
18/01/2026

MAOMBI YA KUOMBEA LEO JUMA PILI NA MWAKA MZIMA
Neno la Mungu linasema, Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota.
1 Wakorintho 15:41
Hapa Pana maneno yanayosema, maana IKO TOFAUTI YA FAHARI HATA KATI YA NYOTA NA NYOTA.... Neno FAHARI.... Maana yake uzuri, thamani au ubora wa kitu... Kwa hiyo kwa lugha nyingine tungesena, maana IKO TOFAUTI YA UZURI,THAMANI AU UBORA HATA KATI YA NYOTA NA NYOTA.... Sasa kitu kilicho nisumbua kwa Nini alipo fika kwenye nyota anasema kunatofauti ya fahari kati nyota na nyota? Ndugu yangu Tambua kila mtu ana nyota yake na kila NYOTA Ina ubora au thamani yake. Kwa nakusihi omba namna hii ili maisha Yako yawe ya tofauti mwaka 2026.

1). Ingia KUOMBA SEMA, katika Jina la Yesu Kristo naitangazia nyota yangu iliyo fungwa, au kuchafuriwa au kutiwa Giza kwenye ulimwengu wa roho Leo nifunguliwe, na nisafishwe na kuanza kuangaza kuanzia Leo na mwaka mzima.

2). Ingia KUOMBA SEMA katika Jina la Yesu Kristo natangaza mwaka 2026 nyota yangu ikawe Nzuri na yenye ubora na uthamani kuliko nyota zingine zote katika ulimwengu huu.

3). Ingia KUOMBA SEMA, natangaza NYOTA yangu ikawe na MVUTO MKUBWA wa fedha, mafanikio, kazini kwangu, kusikilizwa na kuamini kwenye kila ENEO la maisha yangu.

Mungu akubariki sana sana Mimi MwL Charles Gida- 0757 115257

11/01/2026

MAOMBI YA KUOMBA LEO JUMA PILI NA MWAKAKA MZIMA
Neno la Mungu linasema, Ikawa aliporudisha mkono wake, tazama, ndugu yake akatoka. Akasema, Mbona umepita kwa nguvu wewe? MAMBO YA NGUVU NA YAKUANDAME. Kwa hiyo jina lake likaitwa Peresi.Mwanzo 38:29.

1). Ingia KUOMBA SEMA, katika Jina la Yesu Kristo natangaza kutokeza kwa Nguvu mwaka huu na mwezi huu kiuchumi, kikibari, kimaendeleo na kimafanikio, sitafungwa Wala kuzuiliwa na mikono ya wachawi, waganga na washirikina kwa jina la Yesu Kristo aliye hai.

2). Ingia KUOMBA SEMA, katika Jina la Yesu Kristo natangaza mwaka huu na mwezi huu MAMBO YA NGUVU yanifuate kwenye kila eneo la maisha yangu, nguvu ya kupata fedha, nguvu ya kujenga, nguvu ya kufanya maendeleo na nguvu ya kuongzeka.Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao. Kutoka 1:7

3). Ingia kutangaza kwa jina la Yesu Kristo kila mikono ya kichawi, kiganga na kishilikina kurudishwa kwao wenye na yasiwe kikwazo kwenye maisha. Ikawa aliporudisha mkono wake, pia ukisoma Neno la Mungu linasema,Na laana hizi zote Bwana, Mungu wako, atawatia adui zako na hao wakuchukiao, waliokuwa wakikutesa.
Kumbukumbu la Torati 30:7

Bwana Yesu Asifiwe! Ukisoma Neno la Mungu linasema, Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha...
01/01/2026

Bwana Yesu Asifiwe! Ukisoma Neno la Mungu linasema, Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, Bwana amewatendea mambo makuu.
Zaburi 126:2. Ukisoma hapa utaona maneno haya NDIPO KINYWA CHETU KILIJAA KICHEKO.... NA ULIMI WETU KELELE ZA FURAHA... Maana yake KINYWA na ULIMI vilikuwa vinatoa matokeo yaliyomo kwenye mioyo Yao. Kwa lugha nyingine mioyo Yao ilijaa furaha na kicheko kikubwa sana ndani yao, hiyo ikasababisha midomo na ULIMI wao kupiga kelele na kuonyesha furaha Yao. Swali kwa Nini wali furahia na kupiga kelele? Jibu liko pale mbele inasema biblia, BWANA AMEWATENDEA MAKUU... Furaha Yao na shangwe Yao ilikuwa kubwa mioyoni mwao kwasababu Bwana AMEWATENDEA MAKUU.

Tumefuka mwaka 2026 natumaini Leo unakicheko na furaha kwasababu hakika Bwana amekutendea MAKUU sana sana utasema kivipi mtumishi Charles Gida? Ukisoma Neno la Mungu linasema,
nayo ni nchi itunzwayo na Bwana, Mungu wako; macho ya Bwana Mungu wako, ya juu yake, tangu mwanzo wa mwaka hata mwisho wa mwaka. Kumbukumbu la Torati 11:12. Ukisoma hapa Kuna maneno yasemayo, Nchi itunzwayo na Bwana, Mungu wako yangu mwanzo wa mwaka hata MWISHO wa mwaka... Kwa lugha nyingine Kuna msaada wa Mungu, malezi ya Mungu yamehusika kwenye maisha ya watu wanao Kaa kwenye nchi hiyo. Mfano chakula, mavazi, kutatua mahitaji na mambo mengine mengi. La Pili Neno la Mungu linasema, macho ya Bwana Mungu wako ya juu yake mwanzo wa mwaka hata MWISHO wa mwaka... Kwa lugha nyingine ulinzi, uangalizi wa maamzi Yako na hatuja zako zote Bwana Mungu wako amehusika kuzitazama kwa ukaribu sana. Ndugu yangu ukweri Mungu amekutendea MAKUU sana Hadi ADUI ZAKO WANAKILI YA KUWA BWANA MUNGU WAKO AMEKUTETE. Inuka KUMSHUKURU MUNGU Sana Sana kwa kukufanya ufike 2026. Niwatakie MWAKA MPYA NJEMA TENA UWE NA KIBARI NA NYOTA YENYE MVUTO MKUBWA KATIKA JINA LA YESU KRISTO.

Bwana Yesu Asifiwe! Ukweri nimeona niwashukuru sana sana viongozi wa Huduma na wanamaombi wote mlioshiriki kutoa NGUO kw...
31/12/2025

Bwana Yesu Asifiwe! Ukweri nimeona niwashukuru sana sana viongozi wa Huduma na wanamaombi wote mlioshiriki kutoa NGUO kwajiri ya ndugu zetu hakika tumemwona MUNGU kweri kweri.
Pia ninayo sababu ya kuushukuru uongo wa selikari ya kijiji Cha bomba MBILI kwa kutusanyia ndugu zetu walio shiriki baraka za mavazi walio toa watu wa Mungu kwajiri Yao. Neno la Mungu linasema, Ikawa alipokuwa akisema maneno hayo, mwanamke mmoja katika mkutano alipaza sauti yake, akamwambia, HERI TUMBO lililokuzaa, na matiti uliyonyonya. Luka 11:27
Hakika Ribarikiwe TUMBO na maziwa yalio kunyonyesha.... Kwa lugha nyingine kuzaliwa kwako ni faida kwenye maisha ya watu WENGINE. Kweri Mungu akubariki sana sana ndugu yangu
Pia Neno la Mungu linasema, Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao. Warumi 12:15. Ndugu zangu kweri Mungu awabariki sana sana

Bwana Yesu Asifiwe! Leo naomba nishilikishe Neno la Mungu lisemavyo kwenye Luka 2:9-10,14...Malaika wa Bwana akawatokea ...
23/12/2025

Bwana Yesu Asifiwe! Leo naomba nishilikishe Neno la Mungu lisemavyo kwenye Luka 2:9-10,14...Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.
Ukisoma hapa utaona hiki ni pindi ambacho Yesu Kristo amezaliwa na malaika walitumwa na Mungu kutoa taarifa ya kuzaliwa Yesu. Lakini Hawa wachungaji walikuwa wanapitia Hali zifuatazo
1). HOFU Kuu... Hii ni Hali waliyo kuwa nayo kulingana na majukumu mengi ya maisha mfano wa Sasa kila mtu kipindi hiki ana hofu Kuu juu namna atavyosherekea sikukuu hii namna atavyo kula, nguo za watoto, kodi za nyumba, madeni n.k ndiyo maana walipoona mwangaza hofu Kuu ikawatanda sunajua unapokuwa na jambo Lenye kukupa wasiwasi kila kitacho tokea mbele unahisi chenye kuogofya. Je na wewe kipindi hiki umekamtwa na HOFU Kuu?
2). Watu walikosa FURAHA mioyoni mwao kabisa. Ukisoma kwenye Luka 2:10...Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote. Hapa anasema nimewaletea furaha Kuu... Kwa lugha nyingine furaha ilikuwa haipo kwao ndiyo maana malaika akasema nimewaletea furaha Kuu. Unajua kwenye kipindi hiki furaha kwenye ndoa, familia na vikundi mbali mbali inakuwa haipo kabisa kwa sababu mbali mbali za kimaisha.
3). Watu waligubikwa na mioyo iliyo kosa AMANI ndani yao. Ukisoma pale kwenye Luka 2:14... Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Hapa Pana maneno Na duniani IWE AMANI... Ikiwa na maana kuwa amani haikuwepo kwasababu asinge SEMA IWE.. maana yake haikuwepo Sasa iwepo.
Ndugu zangu nawasihi kusudi la Yesu kuja duniani ni kuleta Furaha Kuu na AMANI na kuondoa HOFU Kuu.
Ukweli kabisa Yesu ndiyo Amani yetu k**a Neno la Mungu lisemavyo kwenye Waefeso 2:14.. Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga. Mungu akubariki na nikutakie Christmas njema

SHALOM! Zimebaki siku NNE tuende tukawaone WAHITAJI nakuomba sana sana tusaidie NGUO, gauni, VIATU,au FEDHA na kitu choc...
20/12/2025

SHALOM! Zimebaki siku NNE tuende tukawaone WAHITAJI nakuomba sana sana tusaidie NGUO, gauni, VIATU,au FEDHA na kitu chochote Mungu anakugusa moyoni mwako k**a Neno la Mungu lisemavyo kwenye Ayubu 31:19.. Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo, Au wahitaji kukosa mavazi. Ndugu yangu naomba Mungu akuguse na kusema nawe juu ya SADAKA hii maana Neno la Mungu pia linasema kwenye Yakobo 1:27..Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Bwana Yesu Asifiwe! Ndugu zangu tarehe 24/12/2025 Tutaenda kuwaona WAHITAJI. Kwa hiyo k**a mtumishi ninaomba k**a una VI...
19/12/2025

Bwana Yesu Asifiwe! Ndugu zangu tarehe 24/12/2025 Tutaenda kuwaona WAHITAJI.
Kwa hiyo k**a mtumishi ninaomba k**a una VIATU, NGUO AMBAZO UMEACHA KUVAA AU KUTUMIA mwingine akipa kwake atafurahi hata kutoa machozi na KUMSHUKURU MUNGU Sana pai hata k**a una SABUNI MAHINDI AU FEDHA tunapoke waweza Peleka kwa MwL mwankenja mwenye namba hii 0763183472. KUMBUKA KUNA FAIDA ZA kuwaona WAHITAJI na wenye changamoto nazo ni;

FAIDA YA KUWAJARI WAHITAJI.
Ukisoma kwenye Zaburi 41:1..Heri amkumbukaye mnyonge; Bwana atamwokoa siku ya taabu.
Bwana atamlinda na kumhifadhi hai, Naye atafanikiwa katika nchi; Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake.
1). Mungu atakuwa mwepesi kukusaidia siku ya shida au tabu Yako.
2). Mungu atauhifadhi Uhai wako uwe salama.
3).Mungu atakupa nguvu ya kufanikiwa kwenye kila eneo la chanzo chako Cha uchumi.
4). Atakuepusha na laana za ADUI zako

Pia ni KUMBUKA: unapotoa kwa wenye changamoto au maisha ya Uhitaji
1). Unabarikiwa na Mungu wako aliye hai
2). Unaandaa mahari pako pa kuketi yaani uzima wa milele soma kwenye Mathayo 25:34... Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu. Lakini hayo yote yatotekea k**a tutafanya kwa Hawa: Mathayo 25:40... Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

Bwana Yesu Asifiwe! Ndugu zangu na wapendwa wa Mimi MwL. Charles Gida Pamoja huduma YETU ya KUFANIKIWA KIROHO NA KIMWILI...
13/10/2025

Bwana Yesu Asifiwe! Ndugu zangu na wapendwa wa Mimi MwL. Charles Gida Pamoja huduma YETU ya KUFANIKIWA KIROHO NA KIMWILI TANZANIA nimeona niwashukuru sana kwa MAOMBI YENU NA SADAKA ZENU kwenye HUDUMA YA VWAWA MJINI MBOZI MKOA WA SONGWE iliyo Anza TAREHE 6-10/10/2025 Jana KWERI SINA CHA KUWAPATIA Ila Mungu afanye k**a alivyosema kwenye Mwanzo 28:3...Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mkutano wa makabila. PIA NAWASIHII KUSIKILIZA VIPINDI VYA MAFUNDISHO KWA NJIA RADIO HIZI:
@-REDIO BARAKA 107.7 FM KILA IJUMAA SAA TATU KAMILI USIKU
DREAM 91.3 FM KILA JUMA MOSI SAA TATU NA NUSU USIKU LABDA RATIBA YA MPIRA WANAWEZA PELEKA MBELE MUNGU AWABARIKI SANA SANA

Address

P O. BOX 8234
Mbeya

Telephone

+255757115257

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Charles Gida's Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Charles Gida's Ministry:

Share