11/01/2026
MAOMBI YA KUOMBA LEO JUMA PILI NA MWAKAKA MZIMA
Neno la Mungu linasema, Ikawa aliporudisha mkono wake, tazama, ndugu yake akatoka. Akasema, Mbona umepita kwa nguvu wewe? MAMBO YA NGUVU NA YAKUANDAME. Kwa hiyo jina lake likaitwa Peresi.Mwanzo 38:29.
1). Ingia KUOMBA SEMA, katika Jina la Yesu Kristo natangaza kutokeza kwa Nguvu mwaka huu na mwezi huu kiuchumi, kikibari, kimaendeleo na kimafanikio, sitafungwa Wala kuzuiliwa na mikono ya wachawi, waganga na washirikina kwa jina la Yesu Kristo aliye hai.
2). Ingia KUOMBA SEMA, katika Jina la Yesu Kristo natangaza mwaka huu na mwezi huu MAMBO YA NGUVU yanifuate kwenye kila eneo la maisha yangu, nguvu ya kupata fedha, nguvu ya kujenga, nguvu ya kufanya maendeleo na nguvu ya kuongzeka.Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao. Kutoka 1:7
3). Ingia kutangaza kwa jina la Yesu Kristo kila mikono ya kichawi, kiganga na kishilikina kurudishwa kwao wenye na yasiwe kikwazo kwenye maisha. Ikawa aliporudisha mkono wake, pia ukisoma Neno la Mungu linasema,Na laana hizi zote Bwana, Mungu wako, atawatia adui zako na hao wakuchukiao, waliokuwa wakikutesa.
Kumbukumbu la Torati 30:7