Ushindi Miracle Centre

Ushindi Miracle Centre Mark 16:15

TANGAZOWITO WA MAOMBI MAALUM YA KANISA LA NCHI KWA AJILI YA JANGA LA KUENEA KWA VIRUSI VYA CORONA (COVID-19) DUNIANI, TA...
14/03/2020

TANGAZO

WITO WA MAOMBI MAALUM YA KANISA LA NCHI KWA AJILI YA JANGA LA KUENEA KWA VIRUSI VYA CORONA (COVID-19) DUNIANI, TAREHE 16-22 MACHI 2020

IMARISHA NDOA YAKO SEHEMU YA ISHIRINI NA SITAKaribu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO, somo lililopita tu...
21/01/2020

IMARISHA NDOA YAKO SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

Karibu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO, somo lililopita tulianza sura ya TANO sehemu ya Ishirini na Tano yenye kichwa cha UMOJA UNAOIMARISHWA KWA MUME NA MKE KUWA SHIRIKA KATIKA FEDHA. Tuliishia kwa kusema hakuna haja ya kutengeneza maswali ya kujiuliza jinsi gani wanandoa wanaweza kuwa na umoja katika eneo la fedha kwa sababu hili si suala la elimu, halihitaji mtu aingine darasani na kujifunza maswali ya nadharia juu ya utatuzi wa migogoro ya kifedha katika ndoa. Hili linahitaji maswali ya vitendo ambayo yanaibuliwa na maisha ya wanandoa hao. Ni lazima yaibuke na ni lazima yapatiwe majibu kwa vitendo. Leo tutaendelea kujifunza sehemu ya Ishirini na Sita katika Sura yaTano ya somo hili.

I. Bila shaka, msingi wa umoja fedha katika ndoa ni jambo la muhimu sana, limezingatiwa kikamilifu katika falsafa ya Biblia kuhusu fedha. Wanandoa wa Kikirsto lazima wakubaliane na falsafa ya Bibiblia kuhusu fedha, si kwa sababu inafanya kazi au kwa sababu inatengeneza umoja wa ndoa yao, bali kwa sababu Mungu anataka wafanye hivyo. Wanandoa wakiamua kwa dhati kuchukua Biblia na kusoma falsafa au mwongozo wa Mungu kuhusu mapato na matumizi ya fedha wanazopata, hakika ndoa zitadumu, umoja utaimarishwa na uhasama au migogoro ya kifedha pamoja na ubinafsi wa wanandoa hao utakoma. Migogoro mingi ya kifedha katika ndoa inatokea kutokana na kukosekana kwa uelewa au elimu ya kiroho juu ya mapato na matumizi sahihi ya fedha, kila mmoja husoma biblia kwa kuangalia faida kwa upande wa maisha yake mwenyewe siyo kwa kuangalia maisha ya wote wawili (mume au mke).
Sasa hebu, tushiriki sote, mimi na wewe kujifunza msimamo wa Biblia (Mungu) kuhusu mapato na matumizi ya fedha, ili kanuni au falsafa hiyo itusaidie kumaliza tofauti zetu za mapato na matumizi ya fedha katika ndoa zetu;

A. Mungu ndiye aliyempa mtu uwezo wa kutengeneza fedha. Mungu ndiye anayempatia mtu utajiri na heshima, mume au mke anatakiwa kujua kuwa fedha au mali alizonazo amepewa na Mungu na anatakiwa ashirikiane na mwenzi wake kupanga na kutumia pamoja kwa sababu wao ni mwili mmoja, wameunganishwa na Mungu mwenyewe. Soma; Kumbukumbu la Torati 8:18, 1 Nyakati 29:11-12, Mithali 10:22 na 1 Wakorintho 4:7? Mume au mke hatakiwi kujivunia fedha zake kwa mwenzake, kwa sababu amepewa na Mungu ili watumie katika ndoa yao.

B. Kila tulicho nacho ni mali ya Mungu. Sisi (mume na mke) ni mawakili wa mali za Mungu, wanandoa wanatakiwa watumie rasilimali za Mungu ambazo amewapatia kwa kuomba na kwa uangalifu na uaminifu k**a Mungu atakavyo. Wanandoa wawe shirika katika kila kitu maishani mwao mpaka kifo kiwatenganishe zikiwemo fedha (Soma Zaburi 24:1 na 1 Nyakati 29:11, 14).

C. Kuna vitu vingi ambavyo ni vya thamani kuliko dhahabu au fedha. Kwa hiyo, usiuze upendo wako kwa mkeo au mumeo kwa sababu ya fedha, usivunje ndoa yako kwa sababu ya kutokuwa tayari kuwa shirika na mumeo au mkeo katika fedha, kwa sababu kufanya hivyo unamkosea Mungu pamoja na mume au mkeo. Unajitengenezea njia ya uharibifu. Kuweka kipaumbele fedha kuliko maagizo ya Mungu ya kumpenda mkeo au kumtii mumeo na kuwa mwili mmoja hakuwezi kukupeleka mbinginu kwa sababu fedha na mali ni vitu vya muda mfupi tu, kuna wakati wa kupanda na wakati wa kushuka kiuchumi lakini kwenye suala la upendo au umoja wa ndoa hakuna nyakati hizo za kuongeza upendo na kupunguza upendo au kuwa mwili mmoja (Soma vitabu hivi kwa msaada zaidi wa kiroho; Mathayo 16:26; 6:19-20, Luka 12:15,20-21, Mithali 15:16-17; 22:1; 19:1; 31:10; 19:14 na Zaburi 127:3,5. Pia kukosekana kwa hofu ya Mungu kwa mume au mke kunasababisha pia waingie katika majaribu na kutapanya fedha katika mambo ya anasa; soma 1Timotheo 6:6-9; 6:17-19. Ukiona mume au mke yupo tayari kutumia fedha kwa ajili ya mambo ya anasa ikiwemo uasherati na uzinzi ujue rohoni mwake ameharibika, amevamiwa na Ibilishi.

D. Tamaa mbaya, kukosa kiasi (kutokuridhika) na mashaka/woga katika kufanya maamuzi sahihi ya mapato na matumizi ya familia (makubaliano ya kuwa shirika katika fedha) ni dhambi. Kuna baadhi ya waume kwa wake wanawaka tamaa juu ya fedha za mwenzi wake na yupo tayari kumuua ili arithi mali au fedha, mume yupo tayari kumpoteza mke kwa sababu ya fedha, hiyo ni tamaa mbaya na ni dhambi, umoja wa ndoa hauwezi kupatikana. Mume na mke mnatakiwa muwe na kiasi, ridhikeni na aminiana ninyi kwa ninyi katika fedha zenu na kuweni na bajeti ya pamoja (mpange mapato na matumizi ya familia). Kila mmoja wenu ajue mnaingiza kipato kiasi gani kwa siku, kwa wiki, kwa mwezi na kwa mwaka na matumizi yenu ni kiasi gani kwa siku, kwa wiki, kwa mwezi na kwa mwaka pamoja na kuweka vipaumbele vyenu kwa pamoja (Soma, Kutoka 20:17, Luka 12:15, Mathayo 6:25, 31, 34, Wakolosai 3:5 na Waebrania 13:5).

Namshukuru Mungu kwa leo naishia hapo lakini ni matumaini yangu umefurahia somo hili na nikuahidi Mungu akipenda kipindi kijacho tutaendelea kujifunza sehemu ya Ishirini na Saba katika Sura yaTano ya somo hili yenye kichwa cha UMOJA UNAOIMARISHWA KWA MUME NA MKE KUWA SHIRIKA KATIKA FEDHA.

Jina langu naitwa Steward Dominicus Mkisi, a.k.a Baba Jebediah S. Mkisi na k**a una maswali, maoni au ushauri usisite kunitafuta kwa njia ya baruapepe [email protected] au nipigie kupitia simu ya mkononi +255764539949 au +255692485203
Mungu wa Mbinguni akubariki na tukutane Mungu akipenda kipindi kijacho, kwa herini na uwe na siku njema

Somo: KAZI YA ROHO MTAKATIFUMahali: TAG USHINDI MIRACLE CENTER ISYESYE MBEYAMhubiri: Rev. Sondasi SigallaTarehe: 15/12/2...
15/12/2019

Somo: KAZI YA ROHO MTAKATIFU
Mahali: TAG USHINDI MIRACLE CENTER ISYESYE MBEYA
Mhubiri: Rev. Sondasi Sigalla
Tarehe: 15/12/2019

1. Hutoa kazi ya kufanya kwa mwamini.

2. Huwezesha mwamini kuomba kwa muda mrefu bila kuchoka.

3. Yeye hurahisisha na kufanya kazi ya Mungu iwe nyepesi.

4. Huleta ramani za kimaongozi ya kimungu ili kumuongoza mwamini kutekeleza kusudi la Mungu. MATENDO 10:9-20.

5. Humwongoza mwamini aifuate kweli na kumpasha habari za mambo yajayo ambayo Mungu amwambie ayaseme. YOHANA 16:13 & 14. Ili Roho Mtakatifu aweze kufanya kazi zake kwa mwamini ni lazima mwamini awe na muda wa maombi.

6. Humpa mwamini ujasiri wa kulinena Neno la Mungu na kulitangaza mahali po pote. MATENDO 4:29-31. Mwamini huweza kusimama kwa ujasiri na kukemea maovu, kukaripia, kuonya na kutangaza habari njema za Yesu Kristo

7. Huwapa uwezo wa mwamini kuhubiri injili bila woga wo wote mbele ya vitisho na bila kujali gharama za maisha yake. Roho Mtakatifu humwezesha mwamini kuhimili mikimiki ya maisha ya kumtumikia na kutimiza kusudi la Mungu. MATENDO 4:18-20; 8:17-23; 5:41

8. Roho Mtakatifu hutoa nguvu na uwezo wa kusahau mambo yao ya kila siku na kuweka kipaumbele mambo ya Mungu. Roho Mtakatifu humwezesha mwamini kutambua kuwa kazi ya Mungu ni bora kuliko kazi aliyonayo mwamini na pia humwezesha mwamini asipate hasara kwa kumtumikia Mungu.

IMARISHA NDOA YAKO SEHEMU YA ISHIRINIKaribu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO leo tunaendelea Sura ya NNE...
06/12/2019

IMARISHA NDOA YAKO SEHEMU YA ISHIRINI

Karibu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO leo tunaendelea Sura ya NNE sehemu ya Ishirini, kichwa cha somo ni UMOJA UNAOIMARISHWA NA MAWASILIANO MAZURI YA MUME NA MKE. Somo lililopita tulieshia namba 2(e) kwa kuangalia mfano halisi wa mume na mke ambao walikaa miaka zaidi ya nane bila kufurahisa ndoa yako kwa sababu ya kukosa mawasiliano mazuri ndani ya ndoa yao na leo tunaendelea namba tatu,

3. Maandiko yanatuonya tusiwe na hasira inayotusababisha kutenda dhambi. Waefeso 4:26-27; “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi”. Hii inafaa kutumiwa na wandoa ni kweli kuna kuudhiana au kukosana, lakini kusisababishe ndoa zenu zikavunjika kwa sababu ya ninyi kushinda kuamua kukaa mezani na kujadiliana namna ya kumaliza tofauti zenu. Njia sahihi ya kumaliza tatizo ndani ya ndoa ni kusameheana, kwa kuainisha au kutambua tatizo na kuamua kusamehe kabisa (1Petro 4:8; Mithali 10:12; 1Wakorintho 13:5, 7). Na si kila neon au jambo linatakiwa litoke vinywani mwenu au ndani ya ndoa yenu kwa sababu k**a yakitoka na kusikiwa na watu wengine yaweza kusababisha aibu ndani ya ndoa yenu na kusema hivyo, simaanishi kwamba wanandoa lazima mpotezee au mnyamaziane kwa kila jambo. Maandiko yanatuonya kuwa kuna mambo mengine ni aibu kutoka vinywani mwetu (Waefeso 4:29; 5:3, 4; Mathayo 5:27, 28 na Wafilipi 4:8).
4. Kuna baadhi ya kanuni za kibiblia ambazo ni lazima zituongoze katika kudumisha uhusiano wetu hasa wa mume na mke na hata katika kuonyesha uwazi na uaminifu. Mume au mke kabla ya kuzungumza au kuwasiliana na mwenzako ni vema ujiulize maswali yafuatayo ambayo ni msingi wa kanuni za mawasiliano kibiblia;
i. Ni ukweli na uhakika? Jiulize k**a una sababu za msingi za kusema hayo unayotaka kumwambia mwenzako (Waefeso 4:29, Mithali 18:13).
ii. Je, ninalotaka kulisema lina faida? Jiulize kwanza k**a jambo unalotaka kusema litamsaidia mwenzako au litamuumiza, au litajenga au litabomoa (Mithali 20:15; Waefeso 4:29 na Warumi 15:1-3).
iii. Je, ni wakati mwafaka wa kulisema au itakuwa vizuri nisubiri wakati wake? (Mithali 15:23, 28; 25:11,12).
iv. Je, mtazamo wangu ni sahihi? Waefeso 4:15, 32; 1Wakorintho 16:14; Tito 3:1-2).
v. Nimeliombea jambo hili na nina imani na Mungu kuwa atanisaidia? (Mithali 3:5-6; Wakolosai 4:2-6 na Zaburi 19:14).
vi. Je, maneno nitakayoyatumia yatafaa kuwasilisha ujumbe niliokusudia? Ni vizuri ujiulize na maneno utakayotumia kuzungumza na mwenzako k**a yataleta afya katika mazungumzo (Mithali 12:25; 15:1, 23; 16:23 na Mhubiri 12:10).
K**a nilivyosema, mume na mke hawawezi kuwa mwili mmoja bila kuwa na uwazi na uaminifu katika mawasiliano. Wakati huo huo, lazima iwe njia au kanuni sahihi ya uwazi na uaminifu. Vinginevyo, itaharibu badala ya kuongeza au kuimarisha uhusiano mzuri. Maswali hayo yanaweza kukuongoza katika kuimarisha uwazi na uaminifu katika mawasiliano badala ya kuvunja na kuharibu mawasiliano mazuri ya mume na mke.
II. Kutokana na kile tulichojifunza kuhusiana na kuimarisha mawasiliano mazuri ya mume na mke, ni dhahiri kwamba kujidhibiti mwenyewe (self-control) ni hitaji muhimu sana katika mawasiliano ya aina yo yote ile. Ili mawasiliano yawe mazuri ni lazima kuwepo na kiasi au kujidhibiti wazungumzaji katika mazungumzo yao. Mzungumzaji anatakiwa azungumze kwa kiasi ili kutoa nafasi kwa wengine lakini pia kuepuka kuzungumza maneno ambayo yaweza kuchochea hasira badala ya kuimarisha uhusiano.
a. Biblia imesema mengi kuhusu nguvu za uharibifu wa hotuba mbaya au mazungumzo mabaya. Maandiko yanasema maneno yetu yanaweza kusababisha hatari na maumivu k**a mkuki mkali au upanga mkali. “Kuna anenaye bila kufikiri, k**a kuchoma kwa upanga” (1Wakorintho 15:33; Mithali 12:18; 16:17 na Yakobo 3:5-8). Maneno yetu ni zaidi ya upanga unaotumika kuulia watu, ni zaidi ya mkuki ni vema kujidhibiti wenyewe katika mazungumzo yetu ndani ya ndoa (mume na mke mweni na kiasi, mjidhibiti katika mazungumzo yenu, si kila jambo la kuzunguza, litamuumiza mwenzako).

Namshukuru Mungu kwa leo naishia hapo lakini ni matumaini yangu umefurahia somo hili na nikuahidi Mungu akipenda kipindi kijacho tutaendelea kujifunza suehemu ya ishirini na moja katika Sura ya Nne ya somo hili yenye kichwa cha Umoja Kupitia Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Mume na Mke.

Jina langu naitwa Steward Dominicus Mkisi, a.k.a Baba Jebediah S. Mkisi na k**a una maswali, maoni au ushauri usisite kunitafuta kwa njia ya baruapepe [email protected] au nipigie kupitia simu ya mkononi +255764539949 au +255692485203
Mungu wa Mbinguni akubariki na tukutane Mungu akipenda kipindi kijacho, kwa herini na uwe na siku njema.

IMARISHA NDOA YAKO SEHEMU YA KUMIKaribu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO tupo katika kipengee cha UMOJA ...
31/10/2019

IMARISHA NDOA YAKO SEHEMU YA KUMI

Karibu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO tupo katika kipengee cha UMOJA WA NDOA UNAOIMARISHWA KWA KUFAHAMU VIZURI MAJUKUMU YA MKE KWA MUME. Somo lililopita tulijifunza juu ya dhana potofu ya mke mkutii mume. Leo tunaendelea na somo hili sehemu ya Kumi ya somo hili kwa kujifunza majukumu ya awali ya Mke Kwa Mume.
Utii wa mke kwa mume wake ni tendo lisilo na kikomo, linatakiwa kufanyika kila wakati, muda wo wote (asubuhi, mchana, jioni na usiku). Mke anatakiwa kumtii mume wake kwa kila kitu ilimradi hakipingani na Neno la Mungu. Mke anatakiwa kuwa msaidizi wa mume wake na siyo mpinzani wa mume wake (Soma Mwanzo 2:18).

II. Kwa hiyo kutokana na maandiko tunachoweza kusema ni kwamba jukumu la awali la mke ni kumsaidia mume wake (kuwa waziri Mkuu wa mume wake au mtendaji mkuu katika ndoa). Wakati Mungu alipomuumba Hawa kwa ajili ya Adamu alisema, si vema Adamu akaye pekee yake, nitamfanyia msaidizi wakufanana naye (Soma Mwanzo 2:18-22)
A. Kutokana na maandiko haya tunapata mambo matatu muhimu kuhusu uhusiano wa mke kwa mume wake:-
1. Mungu alimuumba mwanamke awe msaidizi wa mwanamume. Pasipo mwanamke, mwanamume hata hali ya ukamifu wake haijakamilika.
2. Mungu alimuumba mwanamke awe msaidizi mzuri wa mume: Hakuna mnyama ye yote k**a mwanamke ambaye angeweza kusaidia kutosheleza msaada au mahitaji ambayo mwanamume alikuwa anahitaji. Mwanamke pekee ndiye aliyeweza kutoa msaada aliyokuwa anauhitaji mwanamume. (Soma Mithali 18:22 na Mithali 31:10, 11).
3. Mungu alimuumba mwanamke ili kukamilisha kwa mwanamume: Mwanamke anafanana na mwanamume lakini wanatofautiana kimajukumu na hawapo sawa. Mwanamke anakamilisha mambo ambayo mwanamume peke yake hawezi kukamilisha, mwanamke ni sawa na mkanda katika kamera, kamera bila mkanda huwezi kupiga picha au kurekodi video (1Wakorintho 11:11).
B. Kulingana na maandiko mke aliumbwa ili kukamilisha mahitaji, mapungufu, uhaba kwa mume wake. Aliumbwa awe msaidizi wa tofauti kwa mume wake. Amtendee mambo mazuri siyo mabaya siku zote za maisha yake (Mithali 31:12). Awe k**a tunda zuri la nyumba ya mume wake (Zaburi 128:3). Ni mwili mmoja na mume wake, na hili linaweza kutimilika kwa yeye kukubali kutii na kutekeleza wajibu wa mke katika ndoa kwa mujibu wa Mwongozo wa Mungu kuhusu ndoa.
1. Hii haina maanishi kuwa kila jambo analofanya linatakiwa liwe na muunganiko wa moja kwa moja na mume wake. Hapana, haina maana hiyo ila hatakiwi kufanya jambo au kazi kwa ajili ya faida yake mwenyewe au kwa ajili ya faida ya wengine au hatakiwi kujishughulisha na shughuli yo yote au taasisi yo yote ambayo haina manufaa katika ndoa yake (Mithali 31:10-31).
2. Ina maana kwamba mke hatakiwi kufanya jambo lo lote ambalo linaweza kumdhalilisha au kumuumiza mume wake kwa sababu atakuwa amekwepa majukumu yake ya awali ya kuwa msaidizi wa mume wake (Mithali 31:10-31).
C. Sasa kwa kuhitimisha sehemu hii ya Umoja unaopatikana kwa kuelewa vizuri wajibu wa mke kwa mume wake, naweza kupendekeza mambo ambayo mke anaweza kufanya kwa ajili ya kumsaidia mume wake. Anaweza kumsaidia mume wake kwa kufanya yafuatayo:-
1. Kufanya nyumbani kuwa mahali salama kwa mume wake: mke anatakiwa kumfariji, kumtia moyo, kumuelewa na kumfanya mume aone nyumbani ndiyo mahali pa kukimbilia (Mithali 31:11, 20). Usitumie utani au mambo ya kuumiuza k**a sehemu ya utambulisho kwake. Usiendelee kumkumbusha mapungufu yake, makosa yake au kushindwa kwake. Msahihishe au mshauri kwa maneno ya hekima/busara pale inapobidi. Epuka kuruhusu hatari ya kufanya nyumba iwe mahali pa matembezi (shamble) na mahali palipojaa migogoro na matukano. Vile vile, epuka hatari ya kufanya nyumba ya maonyesho ambako kila kitu wakati wote kinakaa safi na katika hali ya mpangilio usiobadilika, yaani mume akiweka au akihamisha kiti tu unampigia kelele na kumtukana k**a mtoto mdogo. Mume anataka nyumba ya kuishi siyo nyumba ya maonyesho au mahali pa wageni kufanyia utalii.
2. Uwe mwaminifu na tegemeo (Mithali 31:11, 12).
3. Tunza hekima au busara (Jibu kwa hekima na hoji kwa busara) (Mithali 31, 26, 28-29; Yakobo 3:13-18 na Wafilipi 4:4).
4. Jadili mambo kwa upendo, uwazi na hekima (Waefeso 4:25).
5. Ridhika na cheo chake, mali zake, na majukumu yake pia (Wafilipi 4:6-13, Waebrania 13:5, 16).
6. Uwe mvumilivu, samehe na kuachilia (Waefeso 4:2, 31-32; Waakolosai 3:12-14).
7. Onyesha uhusika katika tatizo lake na saidiana naye kutatua tatizo alilolipata (Wafilipi 2:3-4).

Namshukuru Mungu kwa leo tuishie hapo sehemu ya Kumi ya somo hili, ni matumaini yangu umefurahia somo na nikuahidi Mungu akipenda kipindi kijacho tutaendelea kujifunza sehemu ya Kumi na Moja ya somo hili kwa kuendelea kuangalia majukumu ya awali ya Mke Kwa Mume yaliyosalia.

Jina langu naitwa Steward Dominicus Mkisi, a.k.a Baba Jebediah S. Mkisi na k**a una maswali, maoni au ushauri usisite kunitafuta kwa njia ya baruapepe [email protected] au nipigie kupitia simu ya mkononi +255764539949 au +255692485203
Mungu wa Mbinguni akubariki na tukutane Mungu akipenda somo lijalo, kwa herini na uwe na siku njema.

Karibu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO, somo lililopita tulijifunza kuwa mwanzilishi wa ndoa ni Mungu n...
12/10/2019

Karibu katika mfululizo wa masomo ya IMARISHA NDOA YAKO, somo lililopita tulijifunza kuwa mwanzilishi wa ndoa ni Mungu na leo tunaendelea na soma hilo na kiichwa cha somo ni HATUA TATU MUHIMU ZA KUZINGATIA KABLA YA KUINGIA KATIKA NDOA.

Mungu ametoa Mwongozo wa ndoa ambao una hatua tatu amabazo zinatakiwa zizingatiwe na zifuatwe kwa utaratibu huo. Hatua hizo ni; i} Kuacha, ii} Kuambatana na iii} Kuwa mwili mmoja.
Kila hatua ina mambo mengi ambayo yanatakiwa yafanyike na yatekelezwe kwa kufuata utaratibu pia wa jamii husika bila kuathiri Mwongo wa Mungu kuhusu ndoa ili ndoa hiyo ikubalike mbele za Mungu. Hatua hizo naweza kuzielezea moja baada ya nyingine k**a zilivyokaa kwa mpangilio katika vitabu vyote vinne katika Biblia Takatifu k**a ifuatavyo:-
I. Kuacha Wazazi: - Mwongozo wa Mungu kuhusu ndoa unamtaka mwanamume na mwanamke wawaache wazazi wao (baba na mama wawaache peke yao).
A. Ina maana gani kuacha wazazi wako?
1. Haina maana kwamba uwaache wazazi wako wajihangaikie wenyewe na maisha yao wala usiwasaidie cho chote. (Linganisha Kutoka 20:12; Marko 7:9-13 na 1Timotheo 5:8)
2. Haina maana kwamba uhame eneo au mahali ambako wazazi wako kijiografia wanaishi uende ukaishi maisha ya ndoa mahali kwingine au sehemu ambayo wazazi wako ni vigumu kufika. Kuishi karibu sana na wazazi wakati wa kuanza maisha ya ndoa kunaweza kukuwia vigumu kuwaacha wazazi wako, lakini pia unaweza ukawaacha wazazi wako huku unaishi mlango wa pili kutoka kwa wazazi wako. Kinyume chake, unaweza ukaishi mbali sana na wazazi wako ambako hawawezi kufika baada ya kuoa au kuolewa lakini ukawa bado hujawaacha wazazi wako. Ki ukweli, unaweza usiwaache wazazi wako hata k**a walikwisha fariki dunia miaka mingi iliyopita.
B. Kuacha Wazazi wako inamaanisha kuwa uhusiano wako na wazazi wako lazima ubadilike sana:-
1. Ina maaana kwamba unaanzisha uhusiano wa utu uzima na wao (wazazi wako),
2. Ina maana kwamba lazima usikilize zaidi mawazo, ushauri na matendo ya mke wako kuliko wazazi wako na wakati mwingine unapuuzia mbali ushauri na mawazo ya wazazi wako.
3. Ina maana kwamba ni lazima uache utegemezi kutoka kwa wazazi wako wa kumpenda mkeo au mumeo, kuidhinisha, kusaidia na ushauri wa namna ya kuishi katika ndoa yako.
4. Ina maana kwamba lazima uondoe na kupinga waziwazi vikwazo vyote vinavyowekwa na wazazi wako katika ndoa yenu, mihemko ya wazazi wako bila kujali umbali uliopo kati yako na wazazi pamoja na kupinga mitazamo mibaya au hasi ya wazazi wako kwa mkeo au mumeo.
5. Inamaanisha kuwa unatakiwa uzuie majaribio yote ya wazazi ya kukutaka kukuondolea upendo wako kwa mwenzi wako kwa sababu ya yeye alivyo, mfano mwonekano wake hauwavutii wazazi (sura au maumbile yake hayawaridhishi wazazi).
6. Inamaanisha kuwa unafanya uhusiano wa mume na mke kuwa kipaumbele chako cha uhusiano wa kibinadamu;-
a. Ndiyo, unatakiwa kufikiria kuhusu kuwa kijana mzuri/bora au binti mzuri/bora au mama au baba, lakini unatakiwa kufikiria zaidi kuwa mume bora/mzuri au mke bora/mzuri kuliko kuwa kijana mzuri au binti mzuri au baba mzuri au mama mzuri. Watoto hawahitaji wazazi wenye kutia moyo ambao hawapendani wao kwa wao hawajaliani, kila mmoja yupo kivyake. Watoto wanahitaji wazazi ambao wataonyesha jinsi ya kukabiliana na kutatua shida. Watoto wanahitaji wazazi ambao watawaonyesha jinsi ya kuwa waume na wake wazuri, jinsi ya kuhusishwa au kushirikiana na watu wengine.
b. K**a ninyi ni wazazi, malengo yenu yanapaswa kuwa ni kuwaandalia watoto mazingira ya kuondoka na siyo kukaa nanyi. Wazazi hamtakiwi kuwalea watoto kwa mfumo wa kuandaa mazingira ya maishi yenu kuwategemea watoto wenu au mnaandaa mazingira ya kuendelea kuishi na watoto wenu, kwa sababu kufanya hivyo mnaweza kuwasababishia watoto wenu wakawa walemavu kifikra au kimawazo.
c. Wazazi mnatakiwa kujiandalia mazingira mazuri mapema ili siku watoto wenu wakiondoa hakuna kitakacho punguza upendo wenu wa awali na kutegemeana ninyi kwa ninyi.
d. Watoto wenu wakioa au wakiolewa, hamtakiwi kuingilia mfumo wao wa maisha wala kuwawekea vikwazo maishani mwao. Wazazi mnatakiwa muwaachie uhuru wanandoa hao wapya waume na wake hao waanze maisha yao mapya ya ndoa wenyewe, wafanye maamuzi, waidhinishe na kila mmoja awajibike kwa mwenzi wake bila kuingiliwa na wazazi. Mnatakiwa kuwafundisha na kuwahamasisha watoto wenu (mabinti na vijana wenu) kujitegemea wenyewe (kutegemea wenzi wao) na siyo kujivunia malezi yenu, msaada wenu, upendo wenu na mshik**ano wenu.
Katika hatua hii ya kwanza ya kuacha wazazi, mambo mojawapo ambayo hufanyika ni pamoja na kutambulishana kwa wazee wa kanisa, wachungaji, wazazi, kulipa mahari, kutangaza uchumba pamoja na kuvalishana pete ya uchumba au kupeana kitu cha kuashiri wamechumbiana, kuaga wazazi (send-off) pamoja na ununuzi wa vyombo vya kuanzia maisha bila kusahau ujenzi wa nyumba ya kuishi au kupanga nyumba nzuri k**a muoaji hana nyumba.
Hatua hii ya kwanza, maandalizi ya mahali pa kuwapelekwa wanandoa watarajiwa hufanyika kwa ajili ya fungate ya ndoa (honeymoon), vikao vya harusi hukaliwa au k**ati za harusi hufanyika, ununuzi wa pete za harusi na pamoja na semina za ndoa kwa watarajiwa hao hufanyika.

Kwa leo somo litaishia hapo, tukutane katika somo lijalo ambapo nitafundisha hatua ya pili katika hatua za kuingia katika ndoa ambayo ni Kuambatana.

Kwa maoni, ushauri, maswali wasiliana nami kupitia mawasiliano yangu hapo chini, Mungu akubariki kwa kuwa pamoja nami katika kujifunza namna ya kuimarisha ndoa yako.

Mwandishi: STEWARD DOMINICUS MKISI.
MAHALI: KANISA LA TAG USHINDI MIRACLE CENTER. ISYESYE MBEYA.
SIMU Na. +255764539949
BARUA PEPE: [email protected]
TAREHE: 12/10/2019

Address

Vingunguti
Mbeya
53127

Opening Hours

Monday 16:00 - 18:00
Tuesday 09:00 - 18:00
Wednesday 16:00 - 18:00
Thursday 16:00 - 18:00
Friday 16:00 - 18:00
Saturday 16:00 - 13:00
Sunday 16:00 - 13:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ushindi Miracle Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share