18/12/2025
> * KUWA NA TARAJIO *
Maisha yetu yamejengwa katika msingi wa matarajio.
Unachokitarajia ndicho kinaamua utendaji wako wa kila siku,
Wengi tunaenda kazini kwasababu tunatarajia mwisho wa Mwezi kuna kitu tutapata kazini._
Tunaamua kuoa kwasababu kuna mambo tunatarajia kuyapata kwenye ndoa,
Tunaenda kanisani kwa sababu kuna mambo tunatarajia kupata kanisani,
Tunaanza biashara kwasababu kuna faida tunaitarajia kwenye biashara.
Kwahiyo kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya matarajio yako na utendaji wako wa kila siku .
Na hapo ndipo hatari inapoanzia kwani,
ukitarajia madogo utatenda kwa udogo_
na kinyume chake ukitarajia makubwa basi hata juhudi yako kwenye hili jambo inakua ya tofauti sana .
Waaamini wengi tumejikuta waanga wa kufanya mambo madogo madogo kwasababu ya kushindwa kutumia vizuri uwezo mkubwa tulionao, kuwaza mambo makubwa badala yake tumejikuta tunatarajia mambo madogo madogo .
*Kumbuka:*
_Mungu hakatai mwanzo mdogo, ila anakataa kidumu kwenye udogo. Utukufu mkubwa wa Mungu ni matokeo ya matarajio ya makubwa yaliozaa imani kubwa .
Jizoeze kutarajia mambo makubwa utende makubwa.
Warumi 4
18 : Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, k**a ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
Msitari unamzungumza mzalendo wa imani katika biblia yaani baba wa imani Ibrahimu alikua na matarajio makubwa kiwango ambacho yameitwa yasioweza kutarajiwa .
Ni maombi yangu kwa Mungu ujaze mambo makubwa akili yako ambayo watu wanaokuzunguka watakushangaa yakitimia hata wewe utajishangaa yakikamilika .
Mungu akubariki sana