20/09/2024
π Kila Mama yangu akitaka kupika maharage, lakini kabla ya kupika maharage, alichagua maharage mabaya na yasiyofaa na kuyatupa nyuma ya nyumba iliko sehemu ya kuweka uchafu, huku akipika maharagwe mazuri.
π Lakini mvua iliponyesha maharage hayo mabaya ambayo hayafai kupikwa yaliota na kuwa mbegu na kukua na kuonekana nzuri tena.
π Baadaye mama akatushauri tuyapalilie vizuri na kwakuwa kwenye sehemu ya kutupia taka kuna mbolea maharage yalistawi na kutoa maua kisha mbegu ikakomaa
β
Katika maisha binadamu tunapitia mengi, wakati mwingine, yule mtu aliyetupwa na ndugu zake kwa kutokuona umuhimu wake wakati huo, Mungu humtunza kwa ajili ya wakati ambao thamani yake itarudi.
β
Kwenye pito huwa kuna kuchongwa na kuzongwazongwa, utalia machozi sana, utaona machungu mengi n.k lakini unatengenezwa ili thamani ya kuumbwa kwako ionekane.
β
Mama aliyatupa yale maharage kisha anatuagiza tuyapalilie, aliyezitupa anaanza kuzivuna. Anatambua kuwa maharage aliyoyatupa yana THAMANI.
β
Wakati Yusufu anatupwa shimoni na ndugu zake, wakati anauzwa na ndugu zake, hakuwa na thamani mbele zao, alikosa thamani alikuwa k**a maharage yasiyofaa kupikwa.
π Usilie watu WAKIKUTUPA NYUMA, usilie watu WALIKUKATAA, usilie huku wanakutazama chini.
π Yusufu alipitia mengi huko Misri, kufanya kazi kwa potifa,mke wa potifa kumtwenza, kufungwa gerezani, kutafsiri ndoto.......hadi kufikia cheo kikubwa kuaminiwa na Wamisri haikuwa kazi rahisi, ilihitaji Mungu kumchonga, ilihitaji uvumilivu, ilihitaji kujitunza kilichoko ndani.
π MVUA inakuja na watu hao hao WANAOKUKATAA leo wataomba KUKUVUNA kesho.
πNjaa ilipozuka ndugu zake Yusufu walimfuata Yusufu pasipo kujua k**a ndiye aliyeongeza thamani kubwa, yeye ndiye mwenye kutunza nafaka ya Misri na mataifa mengine yalihemea huko, siyo tena Yusufu waliyemuuza alikuwa tayari thamani yake imepanda sana hata kufikia kiwango cha kuogopwa sana, mtu mkubwa, mtu mwenye cheo kikubwa, mtu aliyebeba uhai wa watu, kumbuka chakula ni hitaji la msingi bila chakula hakuna uhai.
π Hii ni yako wewe uliyekosa thamani kwako mwenyewe, mbele wa watu, umejichokea, umekata tamaa, Inuka umsifu Bwana kwenye mazingira yako, lipo kusudi juu yako, kesho yako inaandaliwa, thamani yako inatengenezwa, nyakati ya kutengenezwa ni nyakati ya utulivu, ongeza furaha yako kwa Mungu, kwakuwa hata ukinuna haisaidii, ni vizuri ufurahi kwenye chagamoto yako.
Paulo na Silla walipotupwa gerezani, tungetumia tamaduni zetu wangenuna, wangekasirika kuonyesha hisia zao, lakini wao walibadili gia hewani wakaanza kumsifu Mungu, Mungu akashuka na milango ya magereza yakunguka, kufuli zikadondoka. Haleluyah raha kuntumikia Mungu hakika π οΈ
Barikiwa
Mwebrania Sulle
Highlights