Nabii Apolo

Nabii Apolo Mwangaza wa Injili – watumishi wa Mungu tusiofungamana na upande wowote, tukieneza Neno la Mungu kwa usafi na bila kupotoa.

Simama imara katika imani, ukimtumikia MUNGU kwa ukweli na upendo wa Mungu. ukiwezeshwa na Roho Mtakatifu, kutotikiswa na DuniaπŸ™

🎀Je, wewe ni *Mtakatifu* ?, Kwa nini?πŸ‘οΈ Em  tulitazame hili katika Ufalme na Mamlaka ya Kiungu( *Mungu Wa Mbinguni* ) *T...
29/06/2025

🎀
Je, wewe ni *Mtakatifu* ?, Kwa nini?
πŸ‘οΈ Em tulitazame hili katika Ufalme na Mamlaka ya Kiungu( *Mungu Wa Mbinguni* )

*TWENDE PAMOJA*
> Hadi Mwisho πŸ‘‡

πŸ§Žβ€β™‚οΈ *UTAKATIFU* ni ile hali ya Mtu au Kitu kuwekwa wakfu kwaajili ya kazi ya MUNGU tu. Na Neno *Wakfu* linamaanisha *kujitolea* . Hivyo kuwa Mtakatifu ni ile hali ya *kujitolea kwaajili* ya MUNGU.
Pia hali ya *kujitolea* ni vile Mtu anafanya kitu kwa kuipenda tu pasipo kuangalia anapata kitu kwa ukubwa gani sasa lakini kwa *matumaini makubwa ya kupata kitu kikubwa* baadae.

🌝 *SASA*
Kuwa *Mtakatifu* ni kujitolea kwa kazi ya MUNGU tu, yaani *kujitoa* ya kuwa wewe ni wa MUNGU na kila *ukifanyacho* au *kukiacha* ni kwaajili ya MUNGU tu na si vinginevyo.

πŸ‘€ *Tuangalie*
Mlima Mtakatifu, Hekalu Takatifu, Mtaktifu Yohana *n.k* ( _oh kumbe hekalu ni kwaajili ya BWANA, Mlima nao Kwa kazi ya BWANA na Yohana nae kwaajili ya BWANA tu, wewe Je? Yule je?_ )

Hii inamaanisha kila ukifanyacho au ukiachacho ni kwaajili ya MUNGU.
> Kwa asilimia 100 zote bila hata kupunguka hata 1% kila akifanyacho au akiachacho Mtu huyo aitwaye Mtakatifu ni kwasababu ya MUNGU. Nayo katika mawazo, utayari wa moyo na matendo ya kujitoaπŸ“Œ

> Nabii na Mtume_Apolo *Nathubutu kusema* ya kuwa ukisema wewe au yule ni *Mtakatifu*, inamaana yeye ni Wa MUNGU, Kwaajili ya kazi ya MUNGU πŸ“Œ

πŸ‘ *SIFA KUU YA MTAKATIFU*
> Kila Jambo analolifanya au kuliacha ni kwa ajili ya MUNGU tuπŸ“Œ
Na hii hali huthibitishwa na yeye mwenyewe *katika mawazo yake katika akili na utayari wa moyo pasipo huzuni* kisha huonekana kwa matendo ya kujitoa katika *mwili* kupitia macho ya *nyama* ambapo watu humuona.

πŸ“ŒCHANZO KIKUU CHA MATENDO YA UTAKATIFU NI KATIKA *MAWAZO MEMA* NA *UTAYARI WA MOYO* PASIPO HUZUNI

πŸ§Žβ€β™‚οΈ *HALI YA MTU MTAKATIFU*
> MAWAZO MEMA, UTAYARI WA MOYO(pasipo huzuni) MATENDO YA KUJITOA

*Yaani*
1. Kutafuta kwake Pesa ili kutumika kwa kazi ya BWANA tu
2. Huzitazama Fursa au kazi kwa jicho la Kiungu tuπŸ“Œ yaani k**a hakutakuwa na nafasi ya MUNGU kutukuzwa au kazi ya MUNGU kutosonga mbele *kazi hiyo huiacha* hata k**a inafaida kubwa. Yaani MUNGU tu
3. Safari zake zote ni kwajili ya kazi ya MUNGU au kutimiza kusudi la MUNGU
3. Kutoa msaada kwaajili ya Utukufu wa MUNGU ( *Hakuna asilimia hata 1% ya kujitazama yeye bali 100 zote kwaajili ya BWANA MUNGU* )
4. Kula kwake ni kwaajili ya BWANA tu
5. Huduma yake ni kwaajili ya BWANA tu
6. Kusoma kwake ni kwaajili ya kutimiza kusudi la BWANA tu
7. Kutembea kwake hakuhariibu UTUKUFU wa BWANA tu
8. Kuvaa kwake hakuharibu Utukufu wa MUNGU tu
9. Mke au Mume ni kwaajili ya Kazi ya BWANA tu
10. Rafiki Kwaajili ya Kazi ya BWANA tu
11. Maombi yake ni kwaajili ya Kazi ya BWANA
12. Furaha yake au Huzuni yake juu ya kitu fulani ipo kwa jicho la kiungu tu( *liwe baya atafurahi k**a ni kwa Utukufu wa MUNGU, liwe zuri ataumia k**a linaharibu Utukufu Wa MUNGU*)
13. *YAANI NI MUNGU TU* πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“Œ
Huyo ndiye *Mtakatifu*, yaani hana nafasi yake yeye k**a yeye katika Jambo lolote lile, bali yote kwaajili ya MUNGU.

🧠 *KUMBUKA*
Inakubalika kuwa UTAKATIFU tu ndiyo ticketi ya kwenda Mbinguni.(Yaani *Walio watakatifu tu ndiyo warithi wa Nchi Mpya*)

❓ *MASWALI*
1. Je, wewe ni *Mtakatifu* ?
2. Ni kweli kila ukiwazacho ni kwajili ya MUNGU ?
3. Uhitaji wako ili ukamilishe kazi, kusudi au Utukufu wa MUNGU?
4. Ni kweli misaada unayotoa hautaki Kutambukika, umaarufu, uonekane unamoyo, umeguswa, haunashaka, hauna huzuni wala kutaka chochote??
5. Ni kweli umeacha kufanya Jambo fulani kwajili ya Utukufu wa MUNGU, na hakuna sababu zako binafsi k**a kuumia, au kupoteza pesa, au aibu au kudharaukika?
6. Ni kweli unaumia umekosa kitu fulani k**a pesa, au mke au ajira au kitu cha thamani kwa sababu kazi ya MUNGU itapunguka??
7. Ni kweli unamsifu mtu juu ya Jambo fulani kwasababu ya Utukufu wa MUNGU, *Pasipo kuangalia ni Rafiki, ndugu au anione* ?,
8. Je, Furaha na Huzuni yako iko katika MUNGU?
9. Je, ni una MAWAZO, UTAYARI WA KUFANYA JAMBO NA MATENDO YAKO YA KUJITOA *kwaajili ya MUNGU 100%*
10. N. Kadhalika
> πŸ‘†K**a ndivyo kwa 100% Basi wewe ni mmoja wa wale walionenwa yakuwa ni warithi wa nchi, na k**a unapunguka hata 1% basi hautaonja pepo wala hautakuwa mrithi wa Nchi. Kwakuwa warithi ni walio watakatifu tu . *Tafakari kuu ya Biblia na Nabii na Mtume_Apolo*

πŸ₯² *Kweli kwa macho na tafakari ya kawaida ni vigumu kabisa kukamilisha Yote hayo ili kuwa Mtakatifu, lakini ni rahisi sana kuupata Utakatifu na Kudumu katika Utakatifu huo*

✍️ *MAMBO YA KUZINGATIA ILI UWEZE KUWA MTAKATIFU*
> ( _yaani kuweza kudumu katika utakatifu na kuweza *kufanya mambo yote* katika hali ya utakatifu_)

1. Kujisafisha kwa Toba iliyo ya kweli,πŸ“Œ pale utakapanguka katika dhambi kwa bahati mbaya( *kuto kujua* )
2. Usifanye baadhi ya vitu kwa ugumu wa moyo
3. Usifanye kitu kwa huzuni, au kwa influence za mtu
4. Omba kabla ya kufanya
5. *K**A MOYO UNAKATAA ACHA HATA K**A NI JEMA, NA K**A MOYO UNAKUBALI FANYA HATA K**A BAYA*
> ilimradi tu Amani ya moyo iwepo, yaani sikiliza moyo tu, na si kwa kuangalia huruma ya mtu, au uhitaji wa mtu au utaonekanaje, au hadhi yako. Narudia tena k**a kukataa kataa hata k**a Jema, ilimradi moyo wako Amani haipungui
> πŸ‘† *Amesema Nabii na Mtume_Apolo*

πŸ§‘β€πŸ¦― *WITO*
Kuwa Mtakatifu ni Jambo linalohitaji kujitoa sana na si jambo la kuliepuka kwakuwa ndilo Tiketi ya kuwa Mrithi wa Nchi Mpya.
Hivyo, pasipo kuwa Mtakatifu huwezi kuwa Mrithi wa Nchi mpya. Jitahidi sana kudumu katika Utamatifu kwa Kuomba *Toba mara kwa mara* katika moyo ule unaohitaji msamaha wa kweli, na *mawazo ya kuchochea kiu* ya kuutafuta Utakatifu kwa Moyo wote. Nawe utadumu katika Utakatifu kwa Neema Ya BWANA YESU
> Amesema Nabii na Mtume_Apolo

πŸ™Œ *MWISHO*
Utakatifu ni hali inayojengwa katika misingi hii
1. Mawazo mema
2. Utayari wa moyo
3. Matendo ya kujitoa
4. Kujikana kabisa
5. Toba, Sala na Maombi
6. Ibada takatifu
7. Na kadhalika
> Ameyasema: Nabii na Mtume_Apolo.
✊ *TAFUTA UTAKATIFU UWE MRITHI WA NCHI MPYA NA UFALME WA MUNGU UJAO ULIO WA MILELE*

🧠Hekima ya;
Nabii na *Mtume_Apolo*
> *_Nguvu Ya Mungu, Nuru Ya ulimwengu, Uamsho Wa Kiroho, Elimu Safi Ya Kimbingu, Na Ukombozi Wa Ulimwengu katika YESU_*

πŸ“ž *0613826135*

πŸ§Žβ€β™‚οΈ *TOBA, SALA NA IBADA TAKATIFU*
> ( _Misingi Ya Maisha Matakatifu_ )

*MATHAYO 5:3*

βœ… *ATUKUZWE MUNGU WA MBINGUNI, MUUMBA MBINGU NA NCHI NA ALIYE MTUKUFU KATIKA UTAKATIFU*

*AMINA!*
πŸ™πŸ™πŸ™

*__Soma na Mwenzako kwa kuwatumia wale uwezao kuwafikishia ujumbe huu_*_
πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚πŸ«‚

Facebook Nabii Apolo

*UAMSHO WA KIROHO* ( _ONDOA MAMLAKA ZA KIPEPO UKIWA MWENYEWE TUπŸ™_ )Mamlaka hizo huleta matunda hayaNayo ni , *uadui* , *...
26/06/2025

*UAMSHO WA KIROHO*
( _ONDOA MAMLAKA ZA KIPEPO UKIWA MWENYEWE TUπŸ™_ )

Mamlaka hizo huleta matunda haya

Nayo ni , *uadui* , *ugomvi* , *wivu* , *hasira* , *fitina* , *faraka* , *uzushi* ,*uasherati* , *uchafu* , *ufisadi* ,, *ushirikkna* na uchawi,
*husuda* , *ulevi* , na *ulafi* ,
( _Na, Nabii na *Mtume_Apolo*_)

*Sasa* "NJOO NIKUPATIE KIJITABU BURE" kisha Soma kitabu hiko kisha Jipeleleze. Nakusii *Usipingane* na Neno Lolote katika Kitabu hiki kisha chukua hatua.

*KUMBUKA* Nafsi zetu hazipo Huru( *hazipo free* ) zipo chini ya mmoja wapo kati ya uongozi wa Roho Wa Mungu au roho za giza

πŸ‘† *Hakuna anayefanya analolifanya kwa uamuzi wake mwenyewe, lazima ushawishi ufanywe na mmoja kati ya hao Roho* ✍️.
1. Mpango wa kuiba sio wewe hata
2. Chuki sio wewe hapta
3. Kupenda au kuchukia sio wewe hata
4. N.k(ni roho za giza au Roho wa MUNGU)
*JIPELELEZE KISHA CHUKUA HATUA* πŸ™Œ

Usipotee, kwa kuona ni wewe uuamuaye kufanya hayoπŸ₯²

*Mithali 29:18*

*KUMBUKA*
Pasipo kuona ishara yoyote kwenye maombi yako, ni k**a hujafanya kitu bado, *Lazima uone ishara ya kutisha* , tena ya kutisha SANA, na si jambo la kawaida ni zito sana
1. Oba kwa ufupi sana kabla ya kusoma kijitabu hiki,
2. Baada ya kusoma tafakari njia zako zote mbaya kisha reflect na yote ukiyoyasoma
3. Kisha Imba kwanza kwa muda mrefu sana nyimbo za kumtukuza MUNGU. Sikiliza audio huku ukiimba kwa hisia za kweli (audio uzipendazo)
*Ukiona unatetemeka anza maombi hapo hapo usichelewe*
4. Kisha ingia kwenye maombi kwa kufuata kanuni za kiungu, na katika kutafuta kilele cha maombi, chagua sehemu ya mwili ambayo utaipigapiga kwa kukemea au kutaja *Jina* *La Yesu* TU, ili usiondoke katika njia ya kutafuta kilele cha maombi ambako nguvu hizo za giza zinakutoka.
Hapo utasikia kelele kubwa sana na ya kutisha kutoka katika Mwili wako.( *Sio pepo* ,πŸ“Œ *kwakuwa haijashikwa na pepo laki upo chini ya uongozi wa shetani* ) utasikia kelele tu kali sana.
5. Ukiishiwa Nguvu fanya utakachojisikia k**a kulala lala, kwa maana mwili hufa ganzi kabisa( *GANZI YA KUTOKA* ) lakini usiache kuliita Jina La Yesu katika hali hiyo.
6. Baada ya kuamka, omba tena kwa kiwango kile kile, kisha utapokea Nguvu Mpya, kisha Mwili utakufa ganzi kabisa katika mikono au Miguu ( *GANZI YA KUINGIA* )
7. Baada ya hapo usijizuie kufanya utakachohisi kufanya, k**a kulia lia sana tu, kwani ni majuto tu, na k**a kujikwangua basi jikwangue, k**a kujinyoosha jinyooshe hadi hamu itakapokwisha kabisa.
8. Omba kwa unyenyekevu wa kuyajutia yote ulioyafanya kwani haukuwa wewe ni uongozi wa giza tu. Usijizuie kulia wala chochote katika maombi hayo ikiwemo sauti kubwa, hata usiipingee
9. Mshukuru MUNGU kwa maombi ya upole yeye kufuata kanuni za maombi ya kiungu
*NB:* *Tafuta mazingira mazuri na tukivu ambayo mtu hawezi kukuingilia hata kidogo maana ni jambo zito na kubwa mno* lenye kelele na sauti kubwa mno za maombi.
Maombi ya kukemea fanya kwa sauti kubwa sana ukipiga sehemu yoyote ya mwili k**a *Tumbo* au *kufua* kisha Taja Jina La Yesu Tu, hadi uhisi mabadiliko yanaanza kutokea yaani unaona mazingira yasiyo ya kawaida kisha kemea iwezavyo.

*MUNGU NI MWEMA ATATENDA HAKIKA,NAWE UTAYASIMULIA MATENDO YA BWANA NA MAISHA YAKO YATABADILIKA HAKIKA.*

Kwa *walio wagonjwa* kipo kitabu kinaandaliwa kwaajili ya kufanya kazi juu Yenu, mkiwa pekee yako pasipo msaada wa mtumishi, nitakileta Muda utakaofaa, hakika MUNGU hatawaacha.

NB: *_USIENDE KWA MTUMISHI YOYOTE FANYA UKIWA PEKEAKO NA USIOGOPE CHOCHOTE PALE UTAKAPOONA MABADILIKO YA NGUVU YANAKUJIA MAANA SI_* *_VITA YA KIMWILI BALI NI YA KIROHO TU.*_

```Tafuta mazingira tulivu Maana Roho Mtakatifu atakapokushukia hautajizuia kufanya lolote, hasa kelele isiyoya kawaidda``` πŸ™πŸ™πŸ™

( _Utashinda hakika na Mkono wa Bwana hautakuacha_ )

Bwana awaaangazie Nuru Ya Uso wake na Kuwaongoza

Ni, Nabii na *Mtume_Apolo*
( *_Uamsho Wa Kiroho, Nguvu Ya Mungu, Elimu Safi Ya Kimbingu, Na Ukombozi Wa Ulimwengu_* )

Mawasiliano
0613826135

πŸ‘† *CHUKUA HII KWA HALI YA UZITO KABISA*
( _Usiende kwa Mchungaji wala Mtumishi Yoyote maana sio pepo wamekuingia bali ni uongozi wa giza_ )
Hata k**a ukaogopa kwa nguvu utakayoiona, haiwezi kukudhuru kwani sio *pepo mchafu* πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ™Œ

Ni, Nabii na *Mtume_Apolo*

( *_Nguvu Ya Mungu, Nuru Ya ulimwengu, Uamsho Wa Kiroho, Elimu Safi Ya Kimbingu, Na Ukombozi Wa Ulimwengu katika YESU_* )

_Share na Kutuma kwa Watu wengine nao Wapate kujihudumia na kuondoa mamlaka hizo_

*JAMBO LA SERIOUS KABISA* πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ₯²
*MUNGU AKUANGAZIE NURU YA USO WAKE NA KUKUONGOZA*

MWONGOZO WA MAOMBI KATIKA UTAKATIFU {_@Uansho_Wa_Kiroho( Yakobo 4:8, 1 Yohana 1:9, Yeremia 29:13, Waefeso 6:11_) } _Hatu...
22/06/2025

MWONGOZO WA MAOMBI KATIKA UTAKATIFU
{_@Uansho_Wa_Kiroho( Yakobo 4:8, 1 Yohana 1:9, Yeremia 29:13, Waefeso 6:11_) }

_Hatua katika Mwongozo _
1. Anza kwa kutamka maneno yanye kumpa Mungu Wa Mbinguni sifa na utukufu. Yaani kumtambua ya kwamba yeye ndiye mkuu na Mungu wa miungu, hapana mwingine k**a yeye aliye Mbinguni.

Mfano
" _Asante Mungu Wa Mbinguni, Baba Wa Bwana wetu Yesu Kristo, Mungu ustahiliye kuabudiwa hapana mwingine astahiliye utukufu ila wewe tu iliye Mbinguni, hakika wewe ni Mkuu matendo yako ni..............."_ ( SIFA ZOTE KWA KADRI YA UFAHAMU NA UWEZO WAKO )

2. Kujitakasa kwa kuomba msamaha kwa moyo wa kweli pale ulipoanguka kwa kuona au kutokuona, kwa hiari au pasipo maono, au kwa kutotimiza yakupasayo kwa jinsi ya kibinadamu au kutimiza yasiyokupasa kwa jinsi ya kibinadamu. Hapa unajitakasa kwa unyenyekevu ili uzidi kuwa mtakatifu na umtikuze katika utakatifu. Kutoka 15

Mfano
" _Mungu Wangu uliyemkuu wa vyote, kwa unyenyekevu nomba unisamehe kwa yale niliyoyatenda na kuharbu utakatifu wangu katika Utukufu wako, kwa kuona au kutokuona, kwa hiari au kwa lazima katika hali ya ubinadamu......, nisamehe na kunisafisha kwa damu ya Yesu Kristo, ili nikutukuze wewe katika Utakatifu kisha nikupendeze we Ustahimiye UTUKUFU.........._ "

3. Kushukuru kwa wakati uliopita. Kwa kukuepusha na mengi pia kwa kukufanyia mengi.

Mfano;
" _Mungu wangu nashukuru kwa wakati uliopita, nashukuru kwa wema wako na kunivusha nikiwa hai, kwa mkono wako umeniepusha na ajari, matukano_ ............."

4. Kumshukuru Mungu Wa Mbinguni kwa wakati mwingine aliokupa wa kujiuliza tena, kujitakasa tena na pia kupata nafasi ya kumtukuza yeye katika utakatifu.

Mfano;
" _Mungu wangu mwenye nguvu, Nashukuru kwa wakati mwingine ulionipa kwa upendo wako kwangu ili niweze kujitakasa zaidi, na kukutukuza zaidi katika utakatifu, na kutafakari matendo yako na kulijua Neno lako katika ukamilifu wa Imani nami nikutukuze wewe katika Utakatifu uliyemuweza wa vyote..........._ .."

5. Omba ulicho lengea, k**a cha kukemea au maombi juu ya jambo fulani, kuombea safari, kuuweka mfungo mbele za Mungu Wa Mbinguni na maombi mengine.

Mfano;
" _Mungu wa Rehema na Neema, niko mbele zako kwa moyo wangu wote nikihitaji........._ .."
πŸ‘† Hapa utakuwa unaomba katika utamatifu. (Kwa kuwa hatua namba 2, umeikamilisha kisha kujitakasa)

6. Kushukuru kwaajili ya maombi uliyo yafanya na kuomba yapate kibali mbele za Mungu Wa Mbinguni kwa Imani iliyo Kuu.

Mfano:
" _Mungu wangu Baba wa wote, asante kwa wema wako na kunipa nafasi ya kusema nawe, katika ukshirika wangu nawe kupitia Roho Wako Mtakatifu nimesema nawe, naomba yape kibari maombi yangu kisha ukatende kwa mapenzi yako sawa na hitaji la Moyo wangu kwaajili ya Utukufu wako wewe ustahiliye Kutukuzwa........_ ."
7. Seme sala yoyote ile katika Imani ili kukamilisha maombi yako, ikiweomo Sala Ya BWANA, Neema au Kiri Imani ya Mitume.

Mfano;
" _Namwamini MUNGU BABA MWENYEZI Muumba Wa Mbingu Na Nchi, na Yesu Kristo Mwana wake wa pekee, BWANA wetu_ ............"

8. Mwisho wa Sala hiyo na kwa ukamilisho wa maombi hayo. Tamka " _Kwa Jina La Baba, Mwana na Roho Mtakatifu_ ". Nimeomba na kuamini kupitia Jina La Yesu Kristo na katika ushirika waangu nawe Mungu wa Mbinguni kupitia Roho Mtakatifu umetenda na muachilia yote kwa mapenzi yako sawa na hitaji la Moyo wangu kwa utukufu wako wewe pekee ustahiliye kuabuduwa.

"AMINA!"

Mwongozo huu ameuandaa;
Nabii na Mtume_Apolo
K**a mwongozo kwa watakatifu wote katika maombi yao ya kila siku. Mwongozo huu unalenga kuhamasisha waumini wote kuomba lolote kwa MUNGU WA MBINGUNI katika utakatifu, kwa kuanza na sifa, toba, shurani, maombi, shukrani na sala ya mwisho. ili maombi hayo yapate kibali mbele za Mungu Wa Mbinguni.

OMBA KWA KADRI UTAKAVYOONGOZWA, KWA KUFUATIA MWONGOZO HUU, KILA UTAKAPOINGIA KWENYE MAOMBI YAKO.

Yakobo 4:8
" Mkaribieni Mungu,
naye atawakaribia ninyi."
MUNGU WA MBINGUNI AKUBARIKI SANA

Ni,Nabii na Mtume_Apolo
0613826135

(_Nguvu Ya Mungu, Nuru Ya ulimwengu, Uamsho Wa Kiroho, Elimu Safi Ya Kimbingu, Na Ukombozi Wa Ulimwengu katika YESU_)

AMINA!
πŸ™πŸ™πŸ™

TOBA, SALA NA IBADA TAKATIFU
( _Maisha Matakatifu Kwa Utukufu Wa Mungu Wa Mbinguni_ )
πŸ§Žβ€β™‚οΈπŸ™πŸ“–

Facebook Nabii Apolo Apolo Nabii

Usisemeshwe usichokijua kwa kuwa unahitaji uponyaji, utaunganishwa na mikataba mizito ya kiroho. ikiwezekana uliza hii i...
17/06/2025

Usisemeshwe usichokijua kwa kuwa unahitaji uponyaji, utaunganishwa na mikataba mizito ya kiroho. ikiwezekana uliza hii inamaana gani na umeipata wapi.

Epuka majina usiyoyajua katika uwakilishi wa MUNGU, kuna majina yapo ndiyo lakini si sawa na *heshima* ya *Mungu Wa Mbinguni* . Dini batili ni nyingi sana.

Eti kunena kwa Lugha πŸ€”
*LIA PAMOJA NAMI JUU YA HILI*
😭😭😭

*1 Wakorintho 14:27*
"K**a mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri."
Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na *anyamaze* katika kanisa; *aseme na nafsi yake tena na Mungu.*

*"Hii ni Moja kati ya hekima za Nabii na Mtume_Apolo*"

Zipo hekima nyingi sana zitakazokufanya uwe mkamilifu katika Mungu Wa Mbinguni bila kuwa na shaka yoyote.

Nitazileta zikiwa tayari kwa aliyetayari.

*Free Deliverance*
πŸ“ŒπŸ“Œ πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“Œ

🧠 *Wisdom of Prophet and Apostle_Apolo*

(The Power of God, Light of the World, Spiritual Revival, Pure Heavenly Knowledge, and World Redemption through JESUS)

πŸ“ž 0613826135

*TOBA, SALA NA IBADA TAKATIFU*
( *MAISHA MATAKATIFU* )

*TUSOME BIBLIA, TUACHE KUSOMA MAWAZO YA WATU YATATUPOTEZA, BIBLIA IPO 100% KATIKA UKAMILIFU WA KUKUFANYA WEWE KUELEWA* .

πŸ‘†Kwanza utaongozwaje kusema kwenye maombi?, wewe mgonjwa? Au ubongo haufanyi kazi kufikiria nini cha kuomba??

Ndio kuharibiana formula tu. Na kuunganishwa na mikataba mizito ya kiroho na kudhani ndiye Mungu Wa kweli kumbe ni uongo mtupu.

Ndio maana wanawaruhusu hata muwe kinyume na maadili ya kiungu, na hawakemei hata kidogo kwa kuwa wanachowapa ni mlemle tu yaani ni *ushetani mtupu* .😒

Na kwa kuwa mmefungwa na ninyi, "AH"

Unafundishwa kunena kwa lugha, haujui inamaana gani kisha ukiomba unapokea unadhani ni MUNGU WA KWELI kumbe ni Mungu Wa Mizimu na Mapepo. Kisha kuendelea nae hata kufa katika MUNGU huyo. Mwisho hukumu tu.

*Mungu wa dunia hii anamaguvu sana* πŸ˜­πŸ“Œ

*Mithali 4:13*
"Mk**ate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako."

SOMA SANA BIBLIA CHINI YA UONGOZI WA ROHO MTAKATIFU.

πŸ‘‰Na maanisha baada ya maombi ya *Jasho na damu* ndipo ufungue biblia. Tofauti na hapo acha kabisa.

Ni *Mtume Apolo* πŸ˜­πŸ€”
0613826135

*Wasichukue nafasi ya Roho Mtakatifu kwako, watakupoteza*
πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“Œ

*WANA WA UOVU , WATEULE WA MUNGU, DHAMBI YA UMAUTI NA UTAKATIFU*  *WANA WA UOVU*Kwanza si kila mtu aliyepo duniani ameku...
26/04/2025

*WANA WA UOVU , WATEULE WA MUNGU, DHAMBI YA UMAUTI NA UTAKATIFU*

*WANA WA UOVU*
Kwanza si kila mtu aliyepo duniani amekusudiwa kuwa mrithi wa uzima wa milele(mteule). Wapo watu ambao kwa sababu ya chaguo lao la asili yao ya ndani, wamekuwa wana wa uovu na ni wale ambao wamekosa ratiba ya Mungu ya wokovu tangu kuumbwa kwa dunia(hawana nafasi ya kuokoka), wana waliokwisha kuhukumiwa na wetengwa tayari kwa hukumu, wanatumika kwa uasi na mwisho wao umeandikwa toka zamani, hawasikii sauti ya toba tena, na wana wa ibilisi katika kazi zao (mawakala wa ibilisi)

Pia, Watu hawa waliohukumiwa hata kabla ya kuingia duniani, na haiwezekani kuwafanya upya kwa toba na wapo waliokaribu na nuru lakini wanaikataa kwa makusudi, na kwao haitabaki tena nafasi ya wokovu (hawatapata wokovu kamwe labda kujifanya tu), humdhihaki Mungu, baadhi hawajifichi kutenda dhambi, huonja nuru lakini bado huikataa kabisa

Hawa ni wale waliotajwa katika maandiko k**a:
Magugu katika shamba (Mathayo 13:38), Vyombo vya ghadhabu (Warumi 9:22), Watu waliokwisha kuhukumiwa (Yuda 1:4), Wana wa Ibilisi (Yohana 8:44)
Mfano wao (wachawi ambao uchawi wao ni wa asili sio kununua), pia tunaona sifa za mfanano wa watu wakaribu hasa ndugu k**a baba alikuwa mwizi mlevi asiyambilika na mtoto anafuata huko huko nae haambiliki hata kidogo na kuishika katika mwisho wa dhambi, na watu weng8 wafananao sifa hizo

*WATEULE WA MUNGU*
Ni wale wote walioitwa na Mungu kwajili ya kumtumikia Mungu, yaani wanazaliwa pasipo doa lolote la uovu. Hawa wapo kwaajili ya utukufu wa Mungu tu, na ni watu wote katika ulimwengu, mzima isipokuwa wana wa uovu.

Wateule wanaangukia katika vishawishi vya wana wa uovu na kunasa katika mitego yao na kufanya matendo yako kwa ushirika pale wanaopitia hali za kuwakatisha tamaa katika maisha mfano umasikin, maradhi, njaa au vishawishi vingine vinavyomfanya aangukie katika dhambi na kuwa katika kundi hilo kwa ushirika wao.

*UTAKATIFU*
Unakuja pale mteule wa Mungu anpofuata yaliyo mapenzi ya Mungu na kuyaishi kwa usahihi pasipo mawaa. Na hii haiwezi fanywa na wana wa Uovu kwa kuwa hawana nafasi ya utakatifu hata kidogo wao ni kwajili ya dhambi tu na uasi labda wajifanye tu k**a watakatifu nje lakini moyoni mwao ni uovu na hasira na chuki juu ya wanachokifanya kwa upande wa utakatu.

*DHAMBI YA UMAUTI*
Hii ipo kwa wateule tu ambao wanakubali kuifia dhambi hadi kufa pasipo kutubu au kuomba toba iliyo ya kweli. Na hutokana na ushawishi wa *wana wa uovu* katika matendo yao yaani uasherati, wivi na matendo mengine k**a ilivyooneshwa katika kitabu cha *Wagalatia 5:19-21*

*Mteule anaangukia katika dhambi sio kwa uasili wake bali ni kwa ushawishi wa wana wa uovu*

*Mfano:* kwa wana wa uovuYupo mchawi wa asili lakini kwa mteule anaweza akanunua kwa sababu zake binafsi. Au kijuhusisha na ushirikina ili apate mali au pesa n.k

*Nini cha kufanya k**a wewe mteule wa Mungu (Mtumishi halili wa Mungu au wewe muumini halali wa Mungu) ili uendelee katika utakatifi na usiangukie katika dhambi hata kufa*

1. Epuka kufunga nira pamoja nao wana wa uovu kwa kuoa au kuolewa, kutafuta mali pamoja au kiuchumi. na kushiriki katika mambo mengi ambayo yanaweza yakaingiza suala la uovu
2. n.k

*Je, tunaweza kuwatofautisha katika sifa zao kati ya SWANA WA UOVU NA WATEULE WA MUNGU ?*

Jibu ni *HAPANA*
Tunashindwa kuwatofautisha katika sifa hawa wana wa uovu na wateule wa Mungu kwa sababu mambo yao yanaingiliana yaani mteule katika uovu wapo pia katika utakatifu wapo na vivyo hivyo wana wa uovu katika uovu ndiko kwao pia katika utakatifu wapo kwa unafiki tu na sio kwa roho y kweli na wanaweza kuonesha k**a wanaimani kubwa lakini kwa unafiki tu.

*Kwanini MUNGU anaruhusu wawepo na kuharibu utukufu wake?*

*Jibu* : ili andiko litimie tu mfano Yuda iskariote(mwana wa uovu).
*Yohana 17:12* Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, *ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.*

*MWISHO*
Mteule uwe macho katika nyakati hizi, najua unajipeleleza mwenyewe tu kuwa ni mteule yaani umezaliwa pasip mawaa wala dosari ya kiovu na pengine ukazipata baada ya kuanza maisha katika dunia kwa kuvutiwa na kazi za wana wa uovu. Ipo nafasi ya kumrudia Mungu mwenye nguvu ya kushinda yote katika ulimwengu huu kwa kufanya toba ya kweli na kuendelea kuishi yaliyo mapenzi ya Mungu. Na wewe ambaye hujaasi basi endelea katika kumtukuza Mungu
( *AMINI MUNGU YUPO NA ANAISHI PIA ANATUTAKA TUISHI KATIKA UTAKATIFU)*

Haya ameandika: *Apolo Athanasio Mgalagala* , ambaye ni *Nabii Apolo* , katika utumishi mwema wa Mungu
( *0613826135 au 0760286135* )
Kwa upande wa mawasiliano

*HAKIKA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE MILELE NA HATA MILELE* AMINAπŸ™πŸ™

Facebook Facebook Security Nabii Apolo

Mkaribieni MUNGU kwa sala na maombi katika Juma Takatifu Yakobo 4:8"Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi..." Facebo...
14/04/2025

Mkaribieni MUNGU kwa sala na maombi katika Juma Takatifu

Yakobo 4:8
"Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi..." Facebook

Follow page hii Nabii Apolo  tuzidi kusemezana yaliyo mapenzi ya MUNGU na  hakika MUNGU atakubariki πŸ™ Facebook Facebook ...
27/03/2025

Follow page hii Nabii Apolo tuzidi kusemezana yaliyo mapenzi ya MUNGU na hakika MUNGU atakubariki πŸ™ Facebook Facebook Marketplace Community

Zaburi 50:15
Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.

AMEN πŸ™

Zaburi 27:14  "Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana"πŸ™
19/12/2024

Zaburi 27:14
"Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana"πŸ™

Sioni nafasi ya MUNGU tena katika hii dunia, jitahidi sana kumtumikia MUNGU kila wakati wewe k**a wewe, usiangalie wengi...
16/12/2024

Sioni nafasi ya MUNGU tena katika hii dunia, jitahidi sana kumtumikia MUNGU kila wakati wewe k**a wewe, usiangalie wengine. Shetan ana mbinu elfu na elf za kuzui watu kumuabudu mungu wa mbingn. Na sasa kwa kiasi kikubwa zimetawala dunia mambo hayo yafananayo na burudani za aina zote ukiangalia kwa jicho la kimbingu ni kumuabudu shetani mfano mambo yote machafu hufanywa kutokana na burudani zote ambazo shetani kazipamba kiaina yake hasa muziki, mpira na mengine yafananayo na hayo yenye kuipamba dunia vimekuwa vikichangia kusahaulisha watu kumtumikia MUNGU na vimeaambatana na ushetani ndani yake ikiwemo uasherati, ushirikina, ulevi, chuki na mengineyo. Pia tunaona mambo hayo yanaungana kwa kasi sasa kuiangamiza dunia. Tuwe makini sana πŸ™
Inaniuma sana ani dah 😭

Address

Apolomgala@gmail. Com
Kongwa

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nabii Apolo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share